Labda Tupeane za Uso humu JF, yaishie Humuhumu.. Bernard Kamilius Membe, mbaba wa miaka 59 sasa, ambaye 2015 atafikisha miaka miaka yake 62 hana Ndoto, wala hawazii kupania kugombea eti awe Rais.. Jambo Hilo Haliko moyoni mwake wala ndani ya Familia Yake.. mwenyewe haelewi ni lini au ni nani aliyepelekea yeye kuanza kuandikwa kwenye vyombo vya habari kwamba ana dalili za Kukabidhwa kijiti. Marafiki wake wa karibu wanamfariji kwamba labda ni kwa sababu amekikalia kiti cha Uwazili baada ya bahati kutokea kwa Asha Rose Migiro 2007 kuondoka ofisini hapo na yeye kuingia watu wanafikiri amewekwa hapo ili atengeneze mtandao wa siasa za nje kitu ambacho hakina mantik kabisa, Au kwa sababu mtangulizi wake naye alikikalia kiti hicho.
Yeye kama msomi wa" Maryland "kwenye fani ya Mahusiano ya Kimataifa kwenye chuo cha kifilosofia cha Yohana.. amejihusidha na masuala ya kiintelijensia kwa miaka Yake mingi ya Utumishi. Anakiri kwamba siasa kwake ilikuwa kama Mbeleko kwa sababu ya kuonekana msomi pekee wa kijiji kwenye Jimbo la Mtama Huko Lindi ingawa si mapenzi yake hasa kuwa mwanasiasa. Katika Shahada yake ya kwanza Chuo Kikuu DSM, hakuthubutu hata kukaimu wadhifa wa mtunza madaftari ya darasa. Alipoulizwa na marafiki zake Je kama Ukiteuliwa kugombea na Hatimae kuwa Rais alidiriki kusema uRAis ni kazi Kama Kazi Nyingine, ashirio kwamba ni mtu asiye na Jipya.
Lowasa Ngoyai Edward ambaye Umri wake sawa na Bernad Membe naye 2015 atakuwa na miaka 62, lakini kwa Mzee sita yeye kidogo 2015 atakuwa amesogeza umri wa miaka 66. Tofauti na Membe, Lowasa na Sita Hali zao kiafya ni mgogolo sana. Hakuna anayeombea magonjwa kwa binadam mwenzake, Lakini pia hakuna afichaye maradhi, Ukweli ambao hata wao wanaujua.. Wakifanyiwa rehersal ya Kuzungukia lau mkoa mmoja na wilaya zake kufanya kampeni ya aina yoyote asilani wakaimudu.. .
Jambo Lililopo ni Ubabe, kila mtu Myuma yake ana watu na hao watu wana "mtu" wao ambao wanataka yeye "AWE" kwa maslahi yao..Na Mbaya zaidi katika makundi haya SITA na la saba na nane linanukia Hakuna Mzanzibar Hata Mmoja anayetajwa. na kila Kundi Lina nguvu, ushawishi na dumna ambayo si tu hatari kwa kifo cha CCM bali pia amani ya nchi. Nchi ambayo Viongozi wake waandamizi kwenye vyombo vya Ulinzi na Usalama wameshasahau wajibu wao na kujikita kwenye siasa ni Hatari sana sana..
Kwa mtazamo huu, Kuna kampeni ambayo sitaki kuihukumu kwamba ni mbaya au nzuri inayoitwa SASA NI ZAMU YETE(ZANZIBAR). Kampeni hii ina malengo matatu. Kwanza ni kudhoofisha Nguvu ya makundi ambayo ni hatari kwa nchi, pili ni kuleteleza dhana ya Muungano na mazolea na tatu ni kukinusuru Chama. Kampeni hii inaokuja kwa Fujo imebeba sumu mbili ambazo ni hatari kulikoni makundi. Sumu ya kwanza ni Ubabe kwamba Zanzibar ni Nchi Huru yenye Mipaka yake Kisiasa, kiutamaduni, Kiuchumi na Kijeshi pia. Na kwa mantik hiyo Lazima ijitawale yenyewe(serikali ya mapinduzi ya Zanzibar) na Itawale bara (SJM) hi ni zumu ya kwanza ya wazi ambayo hawaipingi wanaihubiri waziwazi. Lakini sumu nyingine mbaya zaidi ni Udini..
My Take: Rais aliyeko madarakani namshauri ajiuzulu. Kwa hatua ya Makundi ilipofikia, haigusiki... haiwezekaniki kabisa kuyaondoa makundi kwa namna yoyote. Ulikuwepo uwezekano wa kufanya hivyo nyakati za nyuma ila sio sasa. Ameshailea hali hiyo na mtoto keshakua. Na kwa hatua ya Zanzibar vilevile si rahisi akaidhibiti.. Labda kwa sababu ya kuwa na washuri wabaya au maamuzi mabaya inchi imeshashindikana kuongozeka, kila mtu sasa ni Rais, anasema na kufanya anavyotaka. Basi ni Heshima yake akiachia ngazi, ili nchi iingie kwenye uchaguzi mwingine na yeye atakuwa na sifa yake. Uzalendo ni kukubali uelekeo wa upepo kabla nyumba haijaezuka mbele ya macho yako na kuwa aibu ya maisha.
Kukubali Kushindwa ni USHINDI!!