asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,039
Yaani huyu asipohamisha watu ccm na kuwaletea mpasuko atabakia na legacy ya ufisadi, Richmond na anakatwa basiiii.
CCM wenzake wamemdharau sana.
CCM wenzake wamemdharau sana.
Kwenye RED, Jana wakati naangalia TV ndo nilichoka kabisa timu yake yote ya Dar ilikuwa pale ikishindana kumshangilia Magufuli, yaani we acha tu. hata yule alomfananisha na Mtume alikuwepo akishangilia yaani hadi jino lake la 33 nililiona jana. Kweli sisi binadamu vinyonga, na unaweza toswa ndani ya muda mfupi tu. Ila Sophia Simba yeye sikumuona pale
Hajaongea tu hata kutoa shukrani?
Kimya kingi!!
Mkuu BRAND,
Hizo picha ni dalili mbaya sana kwa ccm mkoa wa Arusha. Kama wanataka kupona ni bora wakamsikiliza Mzee Kingunge alichowaambia leo. Wakidharau watakipata cha mtema kuni.. Hakuna cha Tingatinga wa Ninganinga.. Watapwerepwetwa vibaya sana.
BACK TANGANYIKA
Lowassa njoo UKAWA.
Kwa usalama wake abakie hukohuko ccm,maana akitoka harafu wakubwa wake waone mambo yanawaendea kombo lazima tu watam-KOLIMBA au pia wanaweza kum-MWANGOKA.
Alimaanisha nini,,?Ndugu EL katua jimboni kwake kujiandikisha kupiga kura Jana 15.07.15. Naona jimbo linaenda cdm kwa sababu msafara wake umepokelewa na bendera za chama hicho. Hakuongea chochote zaidi ya kusema endeleeni kuwa na imani na chama chenu kisha kuingia kwenye gari na kuondoka na kuwaacha watu wakiimba peoples power.