Lowassa: Kiongozi na wananchi wote wanalalamika

Lowassa: Kiongozi na wananchi wote wanalalamika

Sijaona lolote la ajabu aliloongea hapo, nashangaa anavyorushwa utafikiri kaongea ishu sensitive sana.
 
Lowassa kawa mbunge na waziri miaka nenda rudi...je alifanya nini ambacho kwa hicho ndio ajitambishie kwa wenzake wa sasa??

Jibu ni kwamba HAKUNA, hayo aliyoongea bungeni ni porojo tu maana mtu yoyote anaweza akaongea hivyo kwa kuwa ni vitu dhahiri.
 
Kweli mzee kachoka aiseee ...CCM mnalo hili kunga make naona nyote mmeshikwa hamna la kujitetea,tunawaomba sana mtuachie huyo el alafu muone CDM tutakachomfanya 2015 ,atajuta kuifahamu CDM.
 
kwani yy alipokuwa waziri mkuu alifanya nn?
asitusumbue
 
jkama hayo aliyozungumza ndo kunguruma basi hana jipya hata akipata urais, kazi ya kwanza itakuwa kuwarudishia fadhira marafiki zake wanaompa fedha za kupeleka misikitini na makanisani. Tanzania ni nchi ya kulipa fadhira za viongozi.
 
Monday, November 4, 2013


Edward Lowassa.

Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.

Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.

Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabar ani badala ya kufanya kazi.

Lowassa akitaka apate Urais kiulaini atangaze sera yake moja tu !yaani atangaze Serikari itahamia Dodoma siku akiapishwa Kuwa Rais kwani kero number one Dsm ni foleni za magari na Rais pekee atakayeweza kuhamisha serikari jijini atakuwa shujaa wa kitaifa kwani Magari ya serikari yakihama jiji Pia magari Yao Binafsi yakahamia huko foleni zitakwisha na itakuwa history
 
Mwizi mkubwa!watanzania tunataka urudishe pesa ulizoiba kwenye Richmond,ha2wezi kumpa fisadi hili papa urais,anaota ndoto za mchana-pumbaf sana.
 
sijui Watanzania wanaogopa nini kuiweka ccm nzima likizo japo ya miaka mitano hili wajionee tofauti ya vitendo badala ya kulaghaiwa na watu wale wale kila kukicha!
The answer is simple!. Hawana mtu au chama ambacho ni zaidi ya CCM kukipa nchi.

Viongozi wenyewe wa upinzani and government "in waiting" wanataka kutoana macho kwa sababu tu ya sitting allowance, si ndiyo itakuwa ulafi zaidi ya baadhi ya viongozi wa CCM kwenye oil and gas kama wakipewa nchi kuiongoza na kutawala.

Angalizo la Watanzania linasema, bora zimwi likujualo angalau halikuli likakumaliza!.
 
hajaongea lolote jipya,sana sana kamzodoa Mtoto wa Mkulima jeuri kiaina flani hivi kuhusu utendaji wa Magufuli
 
Duh !!! Lowasa naye ?

Kwenda kumsifia Magufuli na Mwakyembe kwa kutimiza wajibu wao imekuwa binge la hotuba? Napata mshangao.
Angejitokeza na kuhoji kwa nini Kagasheki,Nchimbi na Nahodha wameagiza vijana wao wawatese,kuuawatu na mifugo, kupora mali za watu na mwisho nasikia kuchuna watu ngozi kwa kisingizio kuwa eti hao ni majangili ningesema kweli huyu Lowassa kazungumza kama mwakilishi wa Raia walioteseka wa Monduli na Tanzania nzima.
Kwangu mie hakuna kitu hapo.
 
It's fact. Wakati Mh. Lowassa akiwa Waziri Mkuu, serikali ya Rais Kikwete ilikuwa ina chapa kazi vizuri sana na kufanya maamuzi magumu. Everything start falling apart baada ya kukikalia kiti mtoto wa mkulima mwenye experiance ya ufugaji wa nyuki badala ya sheria kama alivyosomea.

Maamuzi yake kwa sasa niya kisiasa zaidi kumzidi hata Katibu Mkuu wa CCM. He's leading CCM government to the gutter for the taking.
 
Our next president bravo...! tukitoka Brazil tunakuja kukukabidhi nchi...!
 
Hii tunaita "self promotion by window dressing".

Lowasa anasema serikali iweke nguvu katika vipengele vichache kama ajiria, afya, elimu na miundo mbinu. Atuambie ni vipengele vipi ambavyo kwa sasa serikali inatia nguvu lakini tunaweza kuviacha, maana alivyoviacha kutaja vya msingi ni kama ifuatavyo, kwenye red;

1. Ajira
2. Afya
3. Elimu
4. Miundombinu
5. Nishati (umeme)
6. Maji
7. Kilimo
8. Madini

Kwa hiyo, aseme wazi, serikali iache nini kwa sasa, michezo na utamaduni?

Pili, Lowasa aidha hana ufahamu wa uchumi au alikuwa anaongea ili watu wasikie sauti yake. Ajira si kipengele ambacho serikali inaweza kushughulikia "in isolation". Ajira ni matokeo ya serikali kushughulikia sekta nyingine. Kwa hiyo kama ana busara kama anavyotaka tufikirie atuambie ajira zitaongezwa kwa kushughulikia nini, sio kwamba serikali ishughulikie ajira. Huko ni kujipendekeza kwa watu wasio na ajira. Kwa mfano ukisema shughulikia miundo mbinu au nishati tayari unashughulikia ajira. Hivyo asitoe maneno ya kuremberemba hapa, watu tuna akili zetu za kutosha japo hatujawahi kuwa Mawaziri Wakuu kama yeye.
Ni huyuhuyu amewahi kusema huwezi kuendelea bila ku-improve poverty. Huo ufahamu autoe wapi kilaza huyu ?
 
Back
Top Bottom