Lowassa: Kiongozi na wananchi wote wanalalamika

Lowassa: Kiongozi na wananchi wote wanalalamika

Curriculum Specialist

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2007
Posts
2,732
Reaction score
750
Mtuhumiwa Mashuhuri wa Richmond ataongea muda si mrefu bungeni, kumbukeni hii itakuwa ni Mara ya pili kuongea bungeni toka achaguliwe 2010!
Ni kauli aliyoitoa wakati akichangia bungeni na kutoa tahadhari kama viongozi hawawezi kufanya maamuzi na wao wakajiunga kwenye kundi la kulalamika, hali hii inaashiria kuwa na nchi ya malalamiko, viongozi wachukue hatua badala ya na wao kulalamika.

Kaongelea issue za ajira kwa vijana, Elimu na miundo mbinu; lakini hao aliowaambia wanaambilika?
Monday, November 4, 2013

1.jpg

Edward Lowassa.

Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.

Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.

Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.
 
Anapongeza Kila kitu, eti Kamati imefanya kazi nzuri, minafiki inashangilia km kawaida Yao, ma tanesco si wamekata umeme ghafla khaaaaaaaaaaa
 
Lowassa,najua una mambo ya msingi

Namkubali sana huyu jamaa,
Ni jasiri sana anapambana kiume hana ile ya "umemwaga ugali mimi nimwage Mboga" kwa manma issue ya richmond ilivyokuwa naamini wangekuwa vioongozi wengine wangetajana hadi wakome lakini jasiri amepambana kufa kupona hadi mwisho na 2015 lazima ataingia white house.

Pamoja na Membe kutumia mbinu ya kuwarubuni baadhi ya marais wa vyuo vikuu kuwapeleka china ili warudi na kutengeneza mtandao wake wa kufanikisha adhima ya kukaa Ikulu kwa Lowassa atangoja sana!
 
Back
Top Bottom