Lowassa: Kiongozi na wananchi wote wanalalamika

Lowassa: Kiongozi na wananchi wote wanalalamika

Namkubali sana huyu jamaa,
Ni jasiri sana anapambana kiume hana ile ya "umemwaga ugali mimi nimwage Mboga" kwa manma issue ya richmond ilivyokuwa naamini wangekuwa vioongozi wengine wangetajana hadi wakome lakini jasiri amepambana kufa kupona hadi mwisho na 2015 lazima ataingia white house.

Pamoja na Membe kutumia mbinu ya kuwarubuni baadhi ya marais wa vyuo vikuu kuwapeleka china ili warudi na kutengeneza mtandao wake wa kufanikisha adhima ya kukaa Ikulu kwa Lowassa atangoja sana!

twilumba mbavu zangu membe alipeleka vijana china?why china?mwambie atangoja sana wa mdimu
 
Bunge ni kanisa la 20 kwa Lowasa, makinda ndiye Mchungaji, kwani akiamua toka nje unatoka!!!ahaaa, Lowasaaaa
 
MH Lowasa anaongea jambo la busara vijana tumuunge mkono sana mana ndio atakayoinua taifa la kesho la vijana ni kiongizo anaejitoa na ana msimamo katika maamuz yake.
 
Hana jipya na urais asahau,akale ile hela aliyoiba ya Richmond.Mbona alishaambiwa aachane na urais?
 
Hamna kiongozi mzuri na mwenye uthubutui kama lowassa. Huyu ndio rais wetu 2015.
 
Waulize watu wa shinyanga maji wanayotumia aliwapgania nani mpaka wakapata?
Kulikua na vikwazo vingi ikiwemo kutishiwa kupigwa na egypt lakin huyu bwana alisimama imara mpaka mpango ukakamilika.
Ana upungufu mkubwa sana,
ila si vema kusema hajafanya lolote.
Amepungukiwa kwenye suala la kuaminika toka sakata la richmond lakini ukweli utabaki kua ukweli,
Jamaa alikua mchapakazi sana.

Acha uongo swala la Maji alisimamia kwa makini zaidi DR.Pius Yasebasi Ng'wandu wakati huo akiwa waziri wa maji awamu ya kwanza ya mkapa.Kwa taarifa yenu mwaka 1995 wakati wa uchaguzi mkuu mji wa shinyanga yaani jimbo la shy town uliongoza kwa wingi wa kura zilizopigiwa kwa mkapa kwa Tanzania nzima.Na mkumbuke mrema na mkapa ilikuwa neck to neck kwa kura.Mkapa aliahidi mwenyewe wakati anatoa shukrani kwa wanashy kuwa atahakikisha anaupatia maji ya kudumu mji wa shy.Mzee LEONALD NEWE DEREFA MBUNGE mstaafu anaweza toa ushuhuda.WATU WASITAKE CHEAP POPULA.
 
Monday, November 4, 2013

1.jpg

Edward Lowassa.

Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.

Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.

Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.
 
Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.

Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.

Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.
 
Hapo inaonyesha LOWASSA anapenda kazi za John Pombe Magufuli zaidi ya WAZIRI MKUU anayemuingilia kwenye shughuli zake...

Conflict of Interests...???
 
Lowasa ana stress ndio maana mara nyingi hapendi kuongea ndani ya bunge kwa hofu ya kuchafua hali ya hewa ya huko.
 
Serikali isiyo na priorities siyo!!! haya tumekusoma mzee wa moduli -kaza buti 2015 si mbali.
 
amesema vyema ila jk foleni ni maendeleo maana watu wengi wana magari
 
Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.

Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.

Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.

Mkuu mbona haja nguruma chochote hapa ninacho kiona ni kwamba amerudia yaleyale wanayoyafanya wenzake hata BRN yao imejikita kwenye maeneo hayo hayo.Hiyo foleni iliyopungua Dar es Salaam ni ipi? lets be serious jamani hakuna kilichopungua adha ikopalepale as usual ila sema kwa kuanzisha treni la usafiri wa ndani amabalo halijaondoa adha ya usafiri bado ulikuwa ni ubunifu iwapo ungezingatiwa kwa kuweka Mtandao unao hudumia sehemu zote korofi.Kwa sasa ksema kwamba kunamtu kapunguza foleni aah hapana bado! bado sana.

Halafu sidhani kama kuna uchumi wowote unao haribika kwa watu kuchelewa barabarani kwasababu wote ni wauza Juice na matunda si ndo tume ambiwa na Profesa Muhongo .Uchumi uko kwenye gesi wengine wote wauza Juice na vitumbua na hawana umuhimu wowote kwa serikali hii.
 
Back
Top Bottom