OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
Kibaka yeyote angeweza kuongea hayo.Mimi ni Pro Membe tena?
Saa nane vipi ile issue ya kutaka kumuuwa zitto kabwe na sumu ilifikia wapi updates please
Kibaka yeyote angeweza kuongea hayo.Mimi ni Pro Membe tena?
Alishaielezea kuwa ni ya mkuu mwenyewe maana kila kitu walikuwa wanawasiliana naye. Si unakumbuka hata yule jamaa aliyekuja kudai kuwa ndiye mkurugenzi alifika mpaka ikulu akaonana na makamu na kumwachia salamu za mkuu wakati huo mkuu alikuwa majuu kama kawaida yake?Je kaelezea richmond ni ya nani?.
Namkubali sana huyu jamaa,
Ni jasiri sana anapambana kiume hana ile ya "umemwaga ugali mimi nimwage Mboga" kwa manma issue ya richmond ilivyokuwa naamini wangekuwa vioongozi wengine wangetajana hadi wakome lakini jasiri amepambana kufa kupona hadi mwisho na 2015 lazima ataingia white house.
Pamoja na Membe kutumia mbinu ya kuwarubuni baadhi ya marais wa vyuo vikuu kuwapeleka china ili warudi na kutengeneza mtandao wake wa kufanikisha adhima ya kukaa Ikulu kwa Lowassa atangoja sana!
Monday, November 4, 2013
Edward Lowassa.
Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.
Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.
Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.
Monday, November 4, 2013Edward Lowassa.
Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.
Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.
Je kaelezea richmond ni ya nani?.
Na wewe uko kwenye payroll yake?
Wewe ndio una stress pesa ipo uwezo wa kaz anao kwa nn awe na stress
Hii tunaita "self promotion by window dressing".
Lowasa anasema serikali iweke nguvu katika vipengele vichache kama ajiria, afya, elimu na miundo mbinu. Atuambie ni vipengele vipi ambavyo kwa sasa serikali inatia nguvu lakini tunaweza kuviacha, maana alivyoviacha kutaja vya msingi ni kama ifuatavyo, kwenye red;
1. Ajira
2. Afya
3. Elimu
4. Miundombinu
5. Nishati (umeme)
6. Maji
7. Kilimo
8. Madini
Kwa hiyo, aseme wazi, serikali iache nini kwa sasa, michezo na utamaduni?
Pili, Lowasa aidha hana ufahamu wa uchumi au alikuwa anaongea ili watu wasikie sauti yake. Ajira si kipengele ambacho serikali inaweza kushughulikia "in isolation". Ajira ni matokeo ya serikali kushughulikia sekta nyingine. Kwa hiyo kama ana busara kama anavyotaka tufikirie atuambie ajira zitaongezwa kwa kushughulikia nini, sio kwamba serikali ishughulikie ajira. Huko ni kujipendekeza kwa watu wasio na ajira. Kwa mfano ukisema shughulikia miundo mbinu au nishati tayari unashughulikia ajira. Hivyo asitoe maneno ya kuremberemba hapa, watu tuna akili zetu za kutosha japo hatujawahi kuwa Mawaziri Wakuu kama yeye.
el ni chuma cha pua,hakuna jembe kama hilo