Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Mungu atusaide.....hivi kwa akili gani utasema Fisadi ndie anaefaa kuongoza watu mil zote hizi!! Yaani nchi hii imekuwa ya kupangiwa maraisi na magenge ya wezi!!!
 
Tatizo wengi humu wanampinga Lowasa hata hawajajiandikisha huko walipo na wengi hawatapiga kura.
Hata mtoa mada hajajiandikisha na hatajiandikisha na hata piga kura......
 
Mzee Mwanakijiji,

Ni vigumu sana kuwashawishi watu juu ya maadui zetu hawa watatu kipi kinatangulia. Kwa sababu wengi wao wanaokujibu tayari matumbo yao yameshiba na hii imetokea hadi nchi zilizoendelea wanashindwa kujua kwa nini watoto wa maskini hawataki shule, na hivyo kuhitimisha kuwa ni kosa lao wazazi ama watoto. ELIMU pasipo shibe hutapata wasomi hata siku moja utakuwa na darasa la watoro wa masomo ambao wameenda kutafuta japo riziki ya siku. ELIMU inatanguliwa na shibe, familia inayojiweza kuweka mlo mezani kama mzazi hawezi kukabiri mahitaji ya nyumbani basi watoto pia huingizwa katika utafutaji.

Kuna watu wengi sana leo hushangaa kwa nini mama zetu miaka ya 40s na 50s waliolewa wakiwa na miaka 13 hadi 14 wakati bado wadogo, hawa watu wasielewe kwamba mtoto wa Kike akisha vunja ungo na hakupata nafasi ya kuendelea mna masomo basi kilichofuatia ni kuozeshwa maana ilikuwa ndio njia pekee ya wakati ule kuepukana na Umalaya. Ukiwauliza wao wangefanya nini miaka hiyo hawana majibu isipokuwa fikra zao zimeganda katika haya walonayo mkononi.

Kwa hiyo watu wanatazama vitu katika dirisha walilopo na laukama wangekuwa katika hali hizo za umaskini wa kutupwa wangekuwa na majibu tofauti. Nakumbuka wakati wa Mwinyi au Mkapa alianzisha shule za msingi kulipia ada, ghafla idadi wa watoto walohudhuria mashuleni ikashuka hadi ikawa chini ya asilimia 50 madarasani, tena kwa kuponeshwa na mijini maana vijijini ndio ilikuwa patupu kabisa.

Ni vigumu sana kupanga mikakati ya Maendeleo na watu wasiokuwa katika mazingira hayo, sawa kabisa na navyopingana na msomi kutoka Ulaya anayekuja tupangia maendeleo nchini. Huyu mtu hakuwahi kupitia Umaskini maisha yake yote alichosoma ni pale nyenzo zote zipo kilichobakia ni utaalam tu wa kuzitumia na wakati gani. Kifupi yeye ndiye anakuja jifunza maisha yetu kesho akasimulie kwao na kuandika vitabu akauze kwao.

ELIMU ni muhimu sana wala haina hoja isipokuwa Umaskini unaweza kabisa kuathiri ELIMU kwa sababu nchi yeyote yenye Umaskini mkubwa hata ELIMU na AFYA zao hushuka vile vile. Ila zipo nchi zenye ELIMU kubwa lakini Umaskini ni mkubwa vile vile. Kwa hiyo, yote haya yanategemea nchi na nchi na Policies zake kwani Cuba na North Korea wana huduma za ELIMU na Afya bora zaidi ya nchi nyingine zilizoendelea lakini UMASKINI wameshindwa kuuondoa.
 
Kwa hoja zinazoendelea ambazo ni facts zaidi kuliko nguvu ya fedha ya lowasa, natabiri vijana ambao wamelipwa ili kuendelea kumtetea na kumsafisha fisadi papa na jambazi sugu lowasa watapotea km walivyopotea wale vijana waliolipwa ili washinde mitandaoni kutangaza chama cha kihuni cha act-wasaliti ikiwepo pia kazi ya kuponda hoja za upinzani hasa chadema
 
Ndio nyie mkiambiwa mkewako malaya mnajitetea kwa kusema wanawakewote malaya. Ila siku ukiletewa ukimwi ndio unajuta.[/QU
Najua umethubutu kutoa mfano huu kwa sababu mtoa mada anamzungumzia lowasa. Lakini mtoa mada angekuwa anamzungumzia Mbowe hakika usingetoa mfano huu. Labda tu niseme kwamba, humu Jf kumekuwa na kasumba ya HOJA BORA NI KUSIFIA CHADEMA NA HOJA MBOVU NI KUONGELEA CCM(POSITIVELY)/KUONGELEA MADHAIFU YA CHADEMA
Naamini humu Jf 95℅ wanakubaliana na huu msemo HAKUNA BINADAMU ALIYE MKAMILIFU/BINADAMU SI MALAIKA. Lakini wakereketwa wa CHADEMA humu ndani wamekuwa wakileta hoja ambazo ni kama zinarasmisha kuwa viongozi wa CHADEMA ni malaika, hawana makosa na wala hawatafanya makosa. Viongozi & wabunge wa CHADEMA kila wanapopanda kwenye majukwaa ya siasa wanawasema CCM kuwa ni mafisadi,wafujaji wa Mali za umma na wapo kwa ajili ya kuwanyonya tu watanzania. Lakini wamewahi kujiuliza kwamba ni nani aliyemsafi ndani ya CHADEMA? Je, Mbowe/Slaa au wengine hawana elements za ufisadi, hawafuji Mali za chama au hawapo kwa ajili ya kuwatumia watu wengine(wafuasi wa CHADEMA) ili kujinufaisha wenyewe? Ninachotaka kusema ni kwamba tuwe wakweli juu ya hawa wanaowania uongozi wa nchi yetu, tuache kila mtu azungumze kile anachokifahamu juu ya hawa wagombea ili tuwaweke kwenye mzani tuone nani anatufaa watanzania. Mashabiki wa CHADEMA/ukawa msitumie maneno ya kejeli,dharau ,dhihaka na matusi kuwalinda viongozi wa CHADEMA/ukawa ambao nao hawana sofa za kushika hatamu kuongoza nchi yetu.

Muungwana hutafakari kwa kina na kujibu kwa hoja Bali mpumbavu hukurupuka na kulopoka bila kutafakari matokeo ya anachokizungumza. Hapo ndipo huuanika upumbavu wake kwa hadhara
 
Kuna swali wanajiuliza: kama kibwagizo ni Elimu Kwanza, je kimeingizwa/kitaingizwa kwenye ilani ya CCM? Kumbuka mwenyekiti wake ni Wasira! Lowasa is a nut!
 
dah watanzania mna kazi aisee kama hizi ndizo arguments zenu kumsupport Lowasa!

Huwezi hata kuona kuwa ni argument; wengine wanasema ni Bora Lowassa hata ukiuwaliza kwanini ni bora hawawezi kuelezea kwanini.
 
Kujua au kufahamu kuwa lowasa hafai kuwa kiongozi wa nchi hakuhitaji kuvaa miwani ya kuona

Heko kwa Mwanakijiji kwa mada nzuri. Story yako imenikumbusha ya mitaani, kwa zaidi ya mara 3 sasa tangu NEC ya CCM itoe taarifa yao fupi, Nimeshuhudia taflani mitaani kwenye vimeza vya Magazeti pale anapo jitokeza mtu Kumsifia Lowassa kwamba jamaa anafaa....... ehhhhhhhhh..... analaluliwa kama nini bwana!

Haya tusonge mbele na mada,

Sijawahi kusikia Mh Lowassa akisema jambo lolote linalo husu tatizo la wizi wa fedha za Wananchi (UFISADI)!

Tatizo letu kubwa Watanzania ni
1. UFISADI (Wizi wa fedha za wananchi)
2. RUSHWA (kutokupata haki na kusababisha hasara kwa wananchi na Watanzania kwa ujumla kama rushwa inahusisha miradi mikubwa ya Kitaifa)

Miaka ileeeee,, Nyerere alisema adui wakubwa kwa Watanzania ni
1. Maradhi
2. Ujinga
3. Umaskini

Kwa sasa idadi ya maadui imeongezeka na kubwa kuliko zote ni UFISADI. Hata hivyo, ili tuepuke na maadui hao nyenzo aliziona wakati ule na bado zinafaa, soma hapa chini

Ili Taifa lisonge mbele tunahitaji vitu vine
1. Watu; Kwa sasa watu tunao
2. Ardhi; Ardhi inazidi kuporwa na wachache
3. Uongozi Bora; Kwa sasa hatuna
4. Siasa Safi; Kwa sasa hili ni janga

Angenda ya kutokomeza ufisadi iwe namba moja na isiwe tu kuitaja! Bali anaye taka urais atuwekee yafuatayo
1. Plan and time frame(namna gani atashughulikia na kwa ratiba maalum)
2. Implementation strategies (atalitekeleza kwa taratibu zipi, yepi yatakayofanyika kukomesha UFISADI)
3. Monitoring and Evaluation (Namna gani atafanya tathimini ya mafanikio)

Yeyote anaye utaka Urais aje na agenda na utekelezaji wake kama nilivyo ainisha hapo juu, hakuna bla bla.... matumaini hewa ya Kikwete 2005 yanatosha! This time tuwe wazungu zaidi, hakuna Ubongo bongo!
 
  • Thanks
Reactions: MC
NJAA MBAYA ETI WATU WANAENDESHA BODABODA KUTOKA MBEY KWENDA DODOMA KUMUOMBA FISADI AWE RAIS:glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy: SHITI
 
Back
Top Bottom