Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Mada za kumchafua EL zimekua nyingi sasa. Inanifanya nijue yy ni bora kwa jinsi mnavyokesha kumchafua

Hoja ni UFISADI kama tatizo kubwa linaloliangamiza Taifa wewe unayesema Lowasa anachafuliwa unaweza kutuwekea hapa kauli yeyote ya Lowasa aliyoizungumza tangu azaliwe ambayo inaonyesha kukemea UFISADI au kuonyesha kuwa akiwa Rais atatatua tatizo hili la UFISADI?
tatizo lako hoja iliyoweka hapa ni nzito wewe unakurupuka na majibu mepesi ya kiudaku ambayo hayajengi zaidi yanabomoa na kukuweka katika kundi la watu wenye upeo mdogo sana wa kufikiri.
 
uamzi ulishafanyika na kwa sasa ni mwezi na nusu umepita......ajaye anafahamika miongoni mwetu.....hatuwezi kuwa na rais kisha baada ya miezi tisa tunachagua rais mwingine au makamu anashika nafasi hiyo!!....madhara yatokanayo na huyu akiingia ni makubwa kuliko wakat wowote ambao tumewahi kuwa nao katika nchi...tahadhari zote zimezingatiwa
 
Hapo hauna msaada kwa nchi yako. Yes Lowassa hafai lakini hujasema nani anafaa, ungeandika mengi ya kumsifia ANAYEFAA ungekuwa na msaada kuliko kumponda asiyefaa kwa maneno mengi bila kuonesha mbadala. Hii nchi ina matatizo makubwa kuliko tunavyodhani kama thinkers ndio nyie

Nadhani mleta mada amekusoma na amekuelewa.
 
1. marafiki wanamchangia ili nini?!! wana malengo gani, ni akina nani hao marafiki? wamepataje hizo pesa wanazomchangia? watazirudishaje? hawa wanaomchangia akishakuwa Rais wakimtaka jambo hata kama halina maslahi kwa Taifa atawakatalia vip? si ndo yale yale ya Mtandao wa 2005 haya?!!
2. Anasema anachukia umaskini, hivi kuna Mtanzania anaupenda umaskini?
Inajulikana kuwa Hakuna mtu anayemchukia tajiri bali tunamchukia tajiri ambaye ni kiongozi wa umma, tunamlipa mshahara, tunamtunza yeye na familia yake halafu bado anaiba na kufisadi mali za umma huo huo. Utajiri wa wizi na ufisadi hatuutaki. Amekuwa mtumishi wa Umma miaka yake yote hiyo biashara ya kujilundikia mali zote hizo kaifanya lini na wapi hasa ukizingatia viongozi na watendaji wa umma ni juzi tu wameanza kufanya biashara baada ya kuua azimio la Arusha? Huo utajiri huyu mtu kaukusanyakusanyaje kama si uwizi?
3. Kuuchukia umaskini si justification ya Kuiba na kiongozi wa umma kutokuwa fisadi haina maana kuwa kiongozi huyo ni maskini. Hivi kuna kiongozi au mtendaji wa Umma anauchukia umaskini wake binafsi na ule wa wananchi wenzie kuliko Mwalimu Nyerere? Je kwa standard ya nchi yetu Nyerere alikuwa maskini? Ukweli ni kuwa Nyerere hakuwa maskini lakini pia hakuwa tajiri wala fisadi. Kina Butiku, Salim, Warioba si matajiri lakini pia, kwa standard ya nchi yetu, huwezi kusema kuwa wao ni maskini. Maisha yao kama watumishi wa umma yanareflect standard ya maisha ya wananchi wa nchi hii. Tunachokataa si utajiri bali ni utajiri wa wizi na ufisadi
4. Kiongozi wa Umma unamiliki utajiri wa kutisha katikati ya wananchi maskini, ardhi kila mahali, majumba kila mahali mengine mpaka huko london, nchi yenyewe "maskini" hohehahe. Halafu unataka ukabidhiwe ofisi kuu ya nchi ukiwa unaongozana na kina rostam, karamagi chenge and the like....kweli?????!!!! haka kanchi si katajifia tu haka???!! katafisadiwa mpaka basi.

5. Ni kwa nini timu ya huyu mzee imejaa majoka ya makengeza tupu? hivi ccm mnatupeleka wapi? ccm kuna siku mtasababisha nchi hii itaingia katika vurugu kama nchi nyingine majirani. kwa sababu itafika mahali Vijana hatutakubali. Ni heri iwe mbwai tu. tunashangaa sana kuna baadhi ya wanaccm, wazee watu wazima, wamekuwa viongoz wa nchi hii halafu leo bila aibu wanamsapoti hadharani kabisa huyu jamaa eti aingie magogoni!!! hivi ccm mpoje nyie? yaan nchi hii apewe rostam na bashe?

ccm mnatia aibu sana. huyu hata ile kufikiria tu kuwa awe rais asingepaswa kufikiria. hivi Nyerere angekuwepo hawa wezi wangethubuti kututukana kiasi hiki hawa? CCM mngekuwa chama makini huyu bwana angepaswa awe ameshafukuzwa kutoka kwenye chama lakini hiki chama ufisadi umekipofusha.

ccm kuna siku mtalipa gharama ya kuasisi na kulea ufisadi. Mmejenga chama kwa Ufisadi na kwa sababu hiyo ni lazima Mtakiua chama kwa ufisadi huo huo....Msumari unapoingilia ndipo unapotokea na Ukiua kwa upanga na wewe au familia yako itakufa kwa upanga pia.

Time will Tell.
 
Kama tumepigwa upofu vile...! Sikuwaza hata mara moja toka scandals za Richmond kuwa EL angefikiri kuwa rais wa nchi hii. Kibaya zaidi mkumbo wa watanzania kutokuona nje ya box la mafisadi kuwa kunawanaoweza zaidi kuongoza Taifa.

Asante MM/kijiji kwa kutukumbusha ulivyomuona jk miaka iyo na akaonekana ulivyomuona miaka yote y utawala wake...sishangai kwa tabia yake akajifanya hamtaki EL na baadae kuungana naye kampeni za urais....kumbuka alivyompigia debe ubunge 2010...pamajo na ufisadi wote huo...
 
Think big! Utamalizaje ujinga bila nyenzo? Jibu ni huwezi. Hivyo yabidi uwe na nyenzo ndio uushinde ujinga! Fedha zilizopotea kwenye kashfa zote zilizotokea kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita (zilizojulikana na zisizojulikana) zingetumika kwenye elimu tungekuwa na shule bora kabisa. Wewe unaona logic, kwa mfano, ya kuongeza majimbo ya uchaguzi wakati hatuna shule za kuridhisha? Again think big!

naona ume-think big! congrats...kuna sehemu nimesema ni bora kuongeza majimbo ya uchaguzi?aya great thinker...good for you! ningekuwa wewe nisinge quote kisha nikafanya uchambuzi kama huo. Kama unadhani ufisadi ndio tatizo kuu la Tanzania endelea kuamini hivyo hivyo,waaminishe na watoto wako weka mbali ELIMU,umesikia great thinker?
 
naona ume-think big! congrats...kuna sehemu nimesema ni bora kuongeza majimbo ya uchaguzi?aya great thinker...good for you! ningekuwa wewe nisinge quote kisha nikafanya uchambuzi kama huo. Kama unadhani ufisadi ndio tatizo kuu la Tanzania endelea kuamini hivyo hivyo,waaminishe na watoto wako weka mbali ELIMU,umesikia great thinker?
Huwezi kuona connection iliyopo kati ya elimu na resources zinazotakiwa ku-establish hiyo elimu kwa sababu hata hiyo elimu uliyoipata haina ubora unaohitajika na uliaminishwa shule ni jengo. ie: ulihudhuria shule lakini hukupata elimu ya kiwango kinachostahili. Na ndio maana unasema unaweza kuboresha elimu kwenye nchi iliyotamalaki ufisadi! Sio kosa lako! Walau unajua kitu kinachoitwa vicious circle?
 
Lowasa uwezo wake wa falsafa ni wa darasa la pili. Mwalimu na usomi wake ailijua bila kilimo hakuna elimu kwanza kwani ili utoe elimu bora lazima government revenue iongezeke na productivity pia iongezeke. Angesema tutaimarisha uzalishaji wa kilimo, viwanda na sekta nyingine ili tuboreshe elimu yetu katika ngazi zote ningemwelewa. Narrow vision gives wrong results. We need a visionary leader who can pursue the nation's vision in a right way not Lowasa.
 
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it



Sasa naona Mzee Mwanakijiji umegeuka kuwa Kijana wa mjini!! dont jump the gun please! naona kama unajaribu kukataa ukweli kwamba ELIMU ndio ufunguo wa maendeleo; Elimu ndio Urithi endelevu! Elimu ndio STOCK IN TRADE ya watu walio wengi nchini mwetu na duniani kote! (msome hayati Lee kuan Yew; Founding father wa Island state ya Singapore; Hayati baba wa Taifa akiita Singapura!; Taifa Mama la dhana ya Matokeo makubwa Sasa;BRN inayowachanganya viongozi wetu wengi!)

Ukimuhukumu EL na kujaribu kushawishi wana CCM; CC; NEC na mkutano mkuu wa CCM "wamchinjilie mbali EL" kisa tu hakutamka kwamba moja ya agenda zake pindi akiteuliwa na hatimaye kuwa rais wa tano wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ni "Kupambana na Ufisadi; Ufisadi na Ufisadi ni sawa na kutwambia kwamba "kutamka ni sawa na kutenda"!! aaaah wacha masihara Muzee; hiyo miujiza ni ya enzi za Nabii Issa Muzee mwanakijiji!! Wangapi wametamka na wakashindwa kufuatilia kauli zao kwa vitendo!! to talk is one thing; Mzee Mwana kijiji; BUT to walk the talk is quite a different creation Muzee wangu!!!

Hebu rejea kauli hizi: Ari mpya; Nguvu mpya na kasi mpya; tafsiri yake rahisi ni nini?!; Nina list ya Wauza mihadarati wote; wanapeta nje nje! Kinara wa ujangili yuko pale Arusha; lini alikamatwa?!; Tanzania bila Ukimwi inawezekana; Ukimwi uliisha lini?! Maisha bora kwa kila Mtanzania; yako wapi?! Kura ya maoni ya katiba pendekezwa ni April 2015; iko wapi?! Kura ya maoni iko pale pale; iko wapi?; tutakomesha mauaji ya watu wenye Albinism!; robo ya kwanza ya mwaka huu tumeshuhudia mauaji ya kutisha ya Albinos!

Nimetangulia kusema awali kwamba do not jump the gun! huyu EL ni wa kumsubiri kwenye campaign trail ikiwa atateuliwa kupeperusha bendera ya CCM: hapo abanwe kulia na kushoto kuhusu ufisadi na tuhuma mbali mbali za ufiadi zinazomzunguka yeye mwenyewe, wanahabari wacheze sehemu yao, wananchi kwenye mikutano ya kampeni; ndani ya midahalo na mitandao ya kijamii, atwambie kinaga ubaga agenda yake pana akiwa Rais; ufisadi included; mikakati ya utekelezaji wake na time frame.ni lazima pia atwambie mahusiano yake na watu wanaomzunguka ambao wana tuhuma lukuki za ufisadi pia na jinsi atakavyotnganisha kazi zake Ikulu na urafiki wakwe na watu hao!

tukifika mahali tukakubali as a nation mtu akatoa kauli tukashangilia tu kama mazuzu ili mradi katamka; bila kuhoji, kuuliza maswali magumu na kudai taarifa za utekelezaji na majibu husika tutakuwa tumekwisha kabisa na hilo ndilo lililotufikisha hapa tulipo!!

Elimu kwanza; yees! Elimu inajenga kujiamini kwa sababu mtu anakuwa anajua anachokisema kwa sababu amekifanyia kazi! anajua wapi kwa kupata taarifa sahihi; Elimu hiyo ndio itakayotuwezesha watu wetu kudai elimu ya uraia; kuhoji matumizi mabaya ya raslimali za umma; viongozi wetu kupenda starehe na kuishi nje ya uwezo wao (ostentation!); kudai nafasi yao sahihi katika uopngozi wa nchi yao; kukataa kufanywa watwana na viongozi wao; kusisitiza haki sawa kwa wanachi wote; kukemea usiginwaji wa haki za binadamu na demekrasia; watu wasio na elimu ya kutosha; elimu bora sio bora elimu katu hawawezi kuhoji ufisadi kwa sababu hawajiamini na hawana taarifa sahihi; kwa hiyo ni waoga ni rahisi kudanganywa na kukubali vizawadi zawadi vya kanga duni na fulani cheap na kazi yao ni kupiga makofi tuuu!

Muzee mwanakijiji; hebu vipange vipaumbele vyako vizuri zaidi, ufisadi ni mbaya ndio, EL huenda sio msafi ndio! lakini "wrong diagnosis leads to a wrong perscription"; dakitari akikosea kutambua ugonjwa lazima atatoa dawa ndivyo sivyo! mgonjwa atakufa mwana kijiji.
Mzee mwanakijiji; nina maoni mazito; (strong opinion) kwamba katika maswala nyeti ya nchi; You have your priorities TOP SIDE DOWN!!!!; hakuna kama elimu; it is second to none! Elimu hujenga kujitambua; kujiamini; kuweka vipaumbele sawasawa; kuwa na maono mapana kuhusu maisha na dunia kwa ujumla; not vice versa.
 
Mwanakijiji

Mie nafikiri hoja yako haina mashiko, mie nashawishika kuamini kua wewe mwenyewe hulijui tatizo la Tanzania na kama unalifahamu basi correlation ya vimeng'enya vyake ume fail kwa nyuzi za juu kabisa katika mfumo wa mmeng'enyo wa uchambuzi wako.

Namba aushi ulizotabanaisha kwa kuzipigilia mstari kwamba ndo tatizo kuu, nafikiri hazina uwiono na tija murua ambazo kwayo zinaweza tumika ili kuuwezesha uchumi wa Tanzania kushika mchapuko chanya.

Nafikiri na pia naamini ungejielimisha tofauti ya root causes na outcomes/results. Na bado pia naamini unachoongelea yani ufisadi ni results yani ni matokeo. Sasa utayazuia vipi matokeo, ni kutafuta source yake yani root cause. Ehe na root cause ya ufisadi ni nini ni ELIMU MBOVU.

Ukiwa na Taifa la watu wenye elimu bora ufisadi unakufa BY DESIGN. Taifa lolote lenye ufisadi lina wananchi ambao wana elimu mbovu. KITUO KIKUBWA. Na taifa lenye elimu mbovu haliwezi kuondoka kwenye umasikini hata kama mna kiongozi Malaika. Mfano Mwl Nyerere alikuwa kiongozi safi sana sio fisadi na mkemea ufisadi, anaweza kuwa nambari moja ama mbili duniani kwa ubora, swali je mbona umasikini ulibaki palepale?

UFISADI linaweza pia kua kikwazo cha maendeleo, lakini pia linaweza kuwa sio kikwazo cha maendeleo utofauti unakuja ni je ufisadi unafanywa na mwenye elimu mbovu ama mwenye elimu nzuri. Mfano Wamarekani/Waingereza na wamagharibi wote wanafanya ufisadi kila sehemu mara Iraq, yemen, Tanzania, nk Je ufisadi wao huu umekuwa ni kikwazo cha maendeleo kwao? Wakoloni walifanya ufisadi sana je ilikuwa ni tatizo la maendeleo kwao? tofauti ni ELIMU.

Yes, Lowasa yuko sahihi, bila elimu bora ufisadi hauwezi kuisha na maendeleo hayawezi patikana.
 
Kaka mukubwa masikio sasa yanataka kuzidi kichwa...! sipo na wewe,pamoja na kwamba moja kwa moja sifungamani na EL mpaka pale utakapo tokea m'badala otherwise bora EL kwa asilimia zote! Kuliko hawa wengine waliotangaza nia au wenye viashiria vya kushika nafasi ya juu ndani ya chama chao.

Hakika hizo ni chuki kama si chuki naomba jiridhishe...kwanza Tanzania mbali na changamoto nyingine shida kuu sio 'UFISADI' kama ambavyo mimi binafsi unataka niamini...io analysis kwamba shida yetu kuu ni ufisadi umejiridhisha nayo? au nikujiona wewe ni bora katika kutafakari m'badala wa wengine? Bado naamini Ujinga ambao dawa yake ni Elimu ndio shida yetu kuu,kwanini? arithmetic nyepesi tu,uwiano wa mafisadi na rasilimali zetu ni tofauti kubwaaa saaana,wataona wanaiba lakini katu amini nakwambia hawawezi maliza,sasa kwa nini nasema bado naamini changamoto yetu kuu bado ni Elimu,watu wetu wanatakiwa kusoma na kupata maarifa...time is coming!

Chambua bila kuonesha upande,kweli yawezekana EL hafai lakini katika hawa wanaoonesha nia nani unadhani anafaaa?maana rais lazima atoke miongoni mwetu,ukimkataa huyu na ukamkubali yule,uo uhalali wa sisi kumkubali uyo mwingine ni wako si wa jumuiya...nasisitiza mimi binafsi ufisadi sio shida kuu! ELIMU ELIMU ELIMU,huu wimbo sahihi kwa waTanzania

kama mpaka leo hujuwi kama ufisadi ni tatizo hapa nchini utakuwa una matatizo ya ubongo kichwani kwako.kwa ushauri wa bure kesho asubuhi nenda ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali ukajionee ripoti za ufisadi.kama uko dar.
 
Kwa kuwa marais masikini wameshatuongoza vya kutosha,na wametufikisha tulipo. Kwa nini tusimpe urais tajiri ili nae tuone atatupeleka mpaka wapi!? Akizingua si tunammwaga tu muda ukifika!

Angekuwa utajiri wake kaupata kwa jasho lake tungemchaguwa.lakini kwa sababu utajiri wake ni kutokana na wizi wa mali ya umma hatufai.akiingia ataendelea kuiba zaidi tutaendelea kuwa masikini.
 
kama mpaka leo hujuwi kama ufisadi ni tatizo hapa nchini utakuwa una matatizo ya ubongo kichwani kwako.kwa ushauri wa bure kesho asubuhi nenda ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali ukajionee ripoti za ufisadi.kama uko dar.

Duuu! Kweli hii ndio JF,boss kazi kabla ujakoment naomba japo ujaribu kupitia mtiririko wa mwanzo wa maongezi kabla ujachangia hoja katikati...hakuna anaye bisha juu ya changamoto ya ufisadi na hakuna bina Adam timamu yeyote atatetea UFISADI,hoja ni nini sasa? Kujaribu kuaminisha umma na mimi nikiwepo kwamba Tanzania ya leo shida kuu kama taifa ni UFISADI?kweli...? ufisadi ni changamoto kali lakini sio kuu,ELIMU (UJINGA) bado mimi nbinafsi naona ndio changamoto kuu ya TAIFA,hivyo lazima iwe kipaumbele cha kwanza coz kina mahusiano na matokeo ya ufisadi,maradhi n.k mengine aksante,sipo dar naomba nisaidie kwenda uko boss kisha unionesha ao wanao ona shida kuu Tanzania ni UFISADI.
 
Hivi Mzee Mwanakijiji ni kweli kuwa huyu Lowasa alikataliwa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa sababu ya kushiriki ten per cent katika uagizaji wa magari ya serikali akiwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais wa wakati huo akiwa John Malecela?
 
Watu wanatumia nguvu nyingi kuutafuta urais. kwa nini wananchi tusitumuie nguvu nyingi na akili nyingi kumtafuta rais?
Let us lay down the rules kama zile 17 za mpira wa miguu kisha tunamtafuta mtu atakyechezesha mchezo halafu tunampima kupitia zile rules., tumfukuzeee tumshtakiii!
Kosa letu ni kwamba tunamwacha kila mtu aje na rules zake halafu tumpe nafasi akasimamie rules alizotunga yeye. Hebu tunaoshabikia watu tuwe tunafikiri kiundani kwanza.
Mzee Mwanakijiji kuna kitu muhimu kwenye hii hoja yako.
 
EDUCATION S POWER,UKIONA MSOMI AMAIBA UJUE ELIMU YAKE NI HAFIFU MAANA MSOMI ANATAFUTA FULSA MBALIMBALI ZA KUMPA KIPATO PASIPO KUIBA, mf angalia nchi kama china idadi kubwa ya wasomi wako kwenye tafiti kujipatia kipato ndani na nje ya nchi,sisi hatuna wasomi.


Unajua huko chini kama kuna kitu hawakivumilii ni ufisadi. Unajua adhabu yao ni nini kwa mafisadi? Unafikiri wanaangalia hata sura zao?
 
Sipati picha endapo kweli mamvi atakuwa raisi!!!
Mwakyembe, Sitta, Nape,Kirango, mzee Malecela, Maropu etc Hawa lazima wahame nchi

Haya ndio mawazo muflisi; wahame nchi kwanini? kwani Lowassa atakuwa amenunua nchi kwa jumla (wholesale)?
 
Najiuliza hv kwa nn mtu huyu anaesemwa kila siku ni fisadi lkn bado watu wengi wanaendelea kumsapoti tu!?ni coincidence ama ni nn!???km bado ni mchafu na bado watu wanamkubali basi ndo chaguo la mungu hilo..na ana makusudi yake..jinsi alivyosemwa kwa miaka yote ilikua ni tosha kwa watu kumkataa lk ndo kwanza nyota inazidi kungara..poleni mnaoshindana na ukweli.

wewe hujuwi kwanini inasemwa lowasa anapendwa.? Huzioni harambee za kumwaga pesa? Huoni magazeti na media zikimnadi na kumuuliza maswali anayotaka kuulizwa? Yote hii ni sababu ya pesa.lowasa anapendwa kwa sababu ya noti zake.nguvu ya pesa.natumaini utakuwa umenielewa.
 
Back
Top Bottom