Ni kweli kabisa Mzee Mwanakijiji, Nigeria ina idadi kubwa zaidi ya wasomi wengi wa viwango vya Kimataifa, kuliko pengine nchi yoyote nyingine Afrika. Siyo hilo tu, kulingana na takwimu za 2014, Nigeria ndiyo nchi yenye uchumi mkubwa zaidi Afrika (GDP: $509.9b), ikifuatiwa na Afrika Kusini (GDP: $370.3b). Nigeria ndiyo nchi ya kwanza Afrika kwa uzalishaji wa mafuta, na ya kumi na moja, duniani. Kulingana na takwimu za Forbes 2014, tajiri NA.1 Afrika, anatoka Nigeria, na katika matajiri 50 walio matajiri zaidi Afrika, 13 kati yao wanatoka Nigeria! Pamoja na yote haya, Ufisadi Nigeria ni sehemu ya maisha!
Kwa sababu ya ufisadi uliokithiri Nigeria, hali ya kijumla ya maisha ya wananchi Nigeria inatisha, kwa mfano, siku za karibuni kumekuwa na uhaba wa mafuta uliosababisha foleni za kutisha na kugombea mafuta, kwa bei ya kulanguliwa! Bila kushughulika na ufisadi, yote ni bure! Nchi za mashariki anazozisema Lowassa siyo tu walitoa kipaumbele kwa elimu, lakini kipaumbele kikubwa zaidi kilikuwa, na hata sasa, ni vita kali dhidi ya ufisadi. Kwa mfano China, hukumu ya Ufisadi, ni kifo, na bila huruma, wameuawa matajiri na wenye vyeo vikubwa serikalini, kwa sababu ya ufisadi. Tatizo la Tanzania, ni ufisadi uliokithiri. Bila kiongozi anayechukia ufisadi, na mwenye dhamira ya kweli ya kuupiga vita ufisadi, Tanzania hatuwezi kutoka hapa tulipo. Je Lowassa na Meneja wake wa Kampeni, Rostam Aziz na wapambe wake akina Karamagi na Chenge, kweli, wana nia na uwezo wa kuupiga vita Ufisadi????? TUTAFAKARI!!!!!!