Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Nani anafaa?

UKAWA hii nchi sio ya kupeana kama pipi watu wanawachukulia poa wananchi haya kama yeye hahusiki na richmond nani muhusika mpaka wakina karamagi nao wanasafishwa wacheni hizo sasa hivi kila mtu tunaaminishwa ni msafi utadanganya watu wawili kwa wakati mmoja lakini sio kumi kwa wakati mmoja tunataka mabadiliko.
 
Kwa kuwa marais masikini wameshatuongoza vya kutosha,na wametufikisha tulipo. Kwa nini tusimpe urais tajiri ili nae tuone atatupeleka mpaka wapi!? Akizingua si tunammwaga tu muda ukifika!
 
Mada za kumchafua EL zimekua nyingi sasa. Inanifanya nijue yy ni bora kwa jinsi mnavyokesha kumchafua
Mdau usipate hofu kabla ya kufika darajani. Pumba na mchele zitaeleweka badae. Let political analysts put things on silver plate. Nitashangaa kama EL hatsfuata na kuheshimu ilani na sera ya chama chake. Badala yake a invent za kwake.
 
Mwanakijiji mzee wa kanzi leo hii amegeuka mwanasiasa bila data; Unajulikana kuwa uko TIMU Membe, Unajulikana kuwa ww ni Vatican Mkereketwa, unajulikana kuwa Mzee Mwanakijiji anajaribu kupotosha ukweli ulio wazi kuwa Kilimo kwanza ililetwa na USA kupitia UN organs FAO, UNDP kwa maslahi ya Land Grabbers wa Dunia hii!!! Leo hii watanzania wanamiliki sehemu ndogo sana ya ardhi yao wakati makampuni makubwa ya kimarekani yakimiliki malaki ya hekari na mengine yanawakodishia wananchi!!!! Mzee Mwanakijiji anajua kuwa tatizo kubwa la nchi hii ni 1. EHM 2. EHM 3. EHM wanaolazimisha hata Gesi yetu ichukuliwe na wageni... MM anajua kuwa Richmond ni mradi wa Marekani, anajua kuwa Lowassa hakubaliani na ujinga wa kuwanufaisha wageni kwanza then wananchi wapewe makombo au kutumiwa kama vibarua!!! MM anadai kuwa hajui kuwa sasa hivi tunatazo la ajira lililosababishwa na watu wa Vatican kwa kiasi kikubwa ... Itoshe kusema Mzee Mwanakijiji na EHM wengine hamtaweza kumzuia Lowassa kuingia Ikulu this time ..
Hoja iliyo mezani ni je, Lowasa anatambua kuwa tatizo kubwa sana katika nchi yetu ni ufisadi uliokithiri? Yupo tayari kuupiga vita kwanza? Wewe acha kupiga kampeni za kitoto, jadili hoja kama msomi na kwa wasomi. Hatupo hapa kusikiliza upuuzi wako tunataka mjadala wa hoja na sio lamli zako dhidi ya Mzee Mwanakijiji.
 
Kujua au kufahamu kuwa lowasa hafai kuwa kiongozi wa nchi hakuhitaji kuvaa miwani ya kuona


Binafsi sipendi uchoyo au umimi. when you work as teamwork then kila mtu hulazimika kufanya juu chini kuhakikisha lengo linafanikiwa na sio nani kafanya nini. Watanzania hatuhitaji kumpa Edo nafasi nyingine ya kufanya! nasema hivi nikiwa na maana moja.

huyu mtu alikuwepo serikalini kwa muda mrefu, ameyaona matatizo ya taifa kwa jicho tofauti na wengine ambao hawajawahi kukaa juu huko. na ufumbuzi wa matatizo hayo anayosema/kujidai anayajua vyema ni kwa nini hakutoa ushirikiano kwa team yake (CCM) ku-overcome hayo matatizo?

Edo ni mchoyo, mbinafsi, ana umimi, ni jeuri. bora angekuwa na yote hayo huku anajua angalau tungesema anataka kutengeneza system yake afanye nayo kazi ila kiukweli hajui uongozi. Kiongozi hawi na sifa hizi. mabadiliko sio lazima uyalete kwa kukaa ikulu. hata huko nje ukiweza kuhamasisha usafi mtaani kwako ni mabadiliko! ukiwa na elimu ya kilimo ukawasaidia wanakijiji wa ulikozaliwa njia bora za kilimo tutasema unafanya mabadiliko! ukiweza kuongoza watu wakafikia lengo la kimaendeleo ni mabadiliko pia.

kwa atakaesema misaada makanisani na misikitini ni mabadiliko anakosea maana inagusa tabaka flani tu. naona ni kazi ya kueneza injili au uislamu.

Edo is FAKE. he is just trying to use some guys kufanikisha malengo yake, kwanza abadilishe jamii yake,

cleardot.gif
 
Sipingani na hoja ya MWANAKIjiji well said ila tatizo ni hizi mada naona ni nyingi mno na ni kuhusu lowassa tu. Kwani c kunawengine walio onesha azma ya kutaka urais. Je nani ni bora mbadala wa Lowassa??. Ndo kitu watu wanataka kujua.
Hao wengine hawajaweka ajenda zao kama alivyofanya Lowasa. Kinachojadliwa hapa ni hizo ajenda zake, mbona hilo lipo wazi wala halihitaji diploma kulifahamu.
 
Chambua bila kuonesha upande,kweli yawezekana EL hafai lakini katika hawa wanaoonesha nia nani unadhani anafaaa?maana rais lazima atoke miongoni mwetu,ukimkataa huyu na ukamkubali yule,uo uhalali wa sisi kumkubali uyo mwingine ni wako si wa jumuiya...nasisitiza mimi binafsi ufisadi sio shida kuu! ELIMU ELIMU ELIMU,huu wimbo sahihi kwa waTanzania

Elimu bila kushughulikia ufisadi kutakuwa na tofauti gani na sasa? au unafikiria hawaweka mkazo kwenye elimu? si watakuonesha shule, vyuo na idadi mbalimbali "nyingi" tu? Hili la nani mwingine siyo hoja ya sasa wala haitusumbui sana; hakuna ambaye ameenda mbali katika kujinadi sana kama Lowassa. Hata kwa wenzetu US.. kwa demokrati anayefuatiliwa sana ni Hillary Clinton.. simply kwa sababu anaonekana ndiye mwenye uwezo wa kupitishwa kule... Hawaulizwi watu mbona wengine "hamwajadili"? labda hawana umuhimu kama wa Lowassa?
 
Kwa kuwa marais masikini wameshatuongoza vya kutosha,na wametufikisha tulipo. Kwa nini tusimpe urais tajiri ili nae tuone atatupeleka mpaka wapi!? Akizingua si tunammwaga tu muda ukifika!

yaani miaka mitano mingine au kumi baadaye? ukimwaga akatokea tajiri mwingine unafanyaje?
 
Binafsi sipendi uchoyo au umimi. when you work as teamwork then kila mtu hulazimika kufanya juu chini kuhakikisha lengo linafanikiwa na sio nani kafanya nini. Watanzania hatuhitaji kumpa Edo nafasi nyingine ya kufanya! nasema hivi nikiwa na maana moja. huyu mtu alikuwepo serikalini kwa muda mrefu, ameyaona matatizo ya taifa kwa jicho tofauti na wengine ambao hawajawahi kukaa juu huko. na ufumbuzi wa matatizo hayo anayosema/kujidai anayajua vyema ni kwa nini hakutoa ushirikiano kwa team yake (CCM) ku-overcome hayo matatizo?Edo ni mchoyo, mbinafsi, ana umimi, ni jeuri. bora angekuwa na yote hayo huku anajua angalau tungesema anataka kutengeneza system yake afanye nayo kazi ila kiukweli hajui uongozi. Kiongozi hawi na sifa hizi. mabadiliko sio lazima uyalete kwa kukaa ikulu. hata huko nje ukiweza kuhamasisha usafi mtaani kwako ni mabadiliko! ukiwa na elimu ya kilimo ukawasaidia wanakijiji wa ulikozaliwa njia bora za kilimo tutasema unafanya mabadiliko! ukiweza kuongoza watu wakafikia lengo la kimaendeleo ni mabadiliko pia.kwa atakaesema misaada makanisani na misikitini ni mabadiliko anakosea maana inagusa tabaka flani tu. naona ni kazi ya kueneza injili au uislamu. Edo is FAKE. he is just trying to use some guys kufanikisha malengo yake, kwanza abadilishe jamii yake,
cleardot.gif
Unclean candidate with support of unclean people will deliver unclean products.
 
Nani anafaa?


mawazo yangu,nadhani tunaitaji rais aliyerizika,maana rais aliyekuwa masikini na akawajali masikini wenzake ni NYERERE tu baada ya hapo, maana kuanzia kwa wabunge wote wanaingia wakijidai masikini wenzetu wakifika huko wanafanya harakati za kuanga umasikini na kutusaau sisi masikini wakati sisi ndo tunawapereka bungeni,
 
Sipingani na hoja ya MWANAKIjiji well said ila tatizo ni hizi mada naona ni nyingi mno na ni kuhusu lowassa tu. Kwani c kunawengine walio onesha azma ya kutaka urais. Je nani ni bora mbadala wa Lowassa??. Ndo kitu watu wanataka kujua.

Kama kuna mtu mwingine anataka kujadili wengine si awajadili; ndio uhuru wa maoni. Kwani lazima mtu mmoja awajadili wote ili kuonesha aina fulani ya kuwa sawa? Tukisema huyu "hafai" kwani lazima tuseme "yule anafaa". Hizi siyo hesabu za 2 + 2 = 4...
 
Binafsi sipendi uchoyo au umimi. when you work as teamwork then kila mtu hulazimika kufanya juu chini kuhakikisha lengo linafanikiwa na sio nani kafanya nini. Watanzania hatuhitaji kumpa Edo nafasi nyingine ya kufanya! nasema hivi nikiwa na maana moja. huyu mtu alikuwepo serikalini kwa muda mrefu, ameyaona matatizo ya taifa kwa jicho tofauti na wengine ambao hawajawahi kukaa juu huko. na ufumbuzi wa matatizo hayo anayosema/kujidai anayajua vyema ni kwa nini hakutoa ushirikiano kwa team yake (CCM) ku-overcome hayo matatizo?Edo ni mchoyo, mbinafsi, ana umimi, ni jeuri. bora angekuwa na yote hayo huku anajua angalau tungesema anataka kutengeneza system yake afanye nayo kazi ila kiukweli hajui uongozi. Kiongozi hawi na sifa hizi. mabadiliko sio lazima uyalete kwa kukaa ikulu. hata huko nje ukiweza kuhamasisha usafi mtaani kwako ni mabadiliko! ukiwa na elimu ya kilimo ukawasaidia wanakijiji wa ulikozaliwa njia bora za kilimo tutasema unafanya mabadiliko! ukiweza kuongoza watu wakafikia lengo la kimaendeleo ni mabadiliko pia.kwa atakaesema misaada makanisani na misikitini ni mabadiliko anakosea maana inagusa tabaka flani tu. naona ni kazi ya kueneza injili au uislamu. Edo is FAKE. he is just trying to use some guys kufanikisha malengo yake, kwanza abadilishe jamii yake,
cleardot.gif
Yes, Unclean candidate with support of unclean people will deliver unclean products.
 
Kama hauwezi kusema nani anafaa ili anye ajadiliwe kama Lowasa hoja yako inakosa nguvu. Hakuna anayekataa ufisadi ni kitu kibaya, hata hivyo sekta nyingine zote haziwezi kusimama ili kupanambana na ufisadi. Sitaki kuamini kuwa unamchukia Lowasa hata hivyo kwa kutokuwaambia watanzania na wasomaji wa JF wazi kuwa kama Lowasa hafai, yupi unayedhani anafaa utakuwa hautendei haki Watanzania na JF kama jukwaa. Kinsingi ufisadi hauhitaji kuwa sera ya maendeleo ya nchi. To me kiongozi ambaye ana nia nzuri na nchi ni lazima awe na sera na mikakai imara inayolenga kuondoa umaskini na kuipelekea nchi yetu kwenye uchumi wa kati. Endapo kutakuwa na mifumo dhabiti na dhamira ya kweli kusimamia kila hatua na kuwajibishana ufisadi unakufa wenyewe na wala hauhitaji kuwa ndiyo kipaumbele cha kulikomboa Taifa kwenye Wimbi la umaskini. Kwangu mimi ufisadi unakosa dhamira tu ya kusimamia misingi. Imekuwa ni hulka kwa vijana wengi kukaa vijiweni asubuhi hadi jioni bila kijishughulisha, na pindi anapotokea mmoja wao akajishughulisha na kuwa na maisha tofauti basi hupewe jina ufisadi. Kwa mantiki hiyo siungi mkono matumizi ya neno ufisadi kwa waliwengi Tanzania kwa kuwa linatumiwa kukatisha tamaa kwa vijana kutumia ubunifu na rasimali ili kujiletea maendeleo kwa hofu ya kuambiwa wao ni mafisadi. Suala la ufisadi linahitaji maamuzi na nia na haliwezi kuwa ndiyo msingi wa ukombozi wa Mtanzania.
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it

 
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it


hadithi ndefuu kuonyesha upeo wako wa kufikiri ulivyo mdogo,umekurupuka but kukurupuka kwako kutakusaidia leo...

Elimu kwanza ndio msingi,,elimu inabeba dhana zote ambazo wewe unapinnga,,watu wakielimika vyema watafundishwa kujiajiri,,wakielimika vyema wataffundishwa namna bora ya kilimo,,wakifundishwa vyema watajua namna ya kusaka masoko na kushindana,,usipoelimika vyema huwezi jua hata kama unaibiwa na haki zako,elimu itasaidia kufuta ufisadi unaosema wewe
 
Lowassa alishapigwa chini Uraisi the moment amemaliza hotuba ya kujiuzuru
 
Huwa mara nyingi siungani na hoja za kaka yangu Mwanakijiji. Lakini katika hili umenena ipasavyo.

Lowasa is charming unemployed youth na issue ya ajira. Yaani huku mitaani vijana huwaambii kitu juu ya huyu jamaa.

Tumaini langu na wale wote wanaoliombea mema taifa letu ni CC ya CCM kutenda haki kutuletea mtu sahihi kwa nyakati hizi.
 
Zitto , alikuwa akiwalaghai tu , muulize kama zilikuwa haziendi kwenye Akaunti yake ......Kachukua posho zote kama atabisha tuweke nyaraka hapa.......Mlaghai tu Zitto......

mkuu uhakika zitto alikuwa achukui hizo hela, wengine wote hovyo tu walinikera sana,jiulize unataka ml 289 kwa utumishi wa miaka mitano na wengine hawafiki kwenye majimbo yao lkn hawapandishi posho za madakitali walimu ambao wanatunikia zaidi ya miaka 35 inaingia akilini kweli?
 
Elimu bila kushughulikia ufisadi kutakuwa na tofauti gani na sasa? au unafikiria hawaweka mkazo kwenye elimu? si watakuonesha shule, vyuo na idadi mbalimbali "nyingi" tu? Hili la nani mwingine siyo hoja ya sasa wala haitusumbui sana; hakuna ambaye ameenda mbali katika kujinadi sana kama Lowassa. Hata kwa wenzetu US.. kwa demokrati anayefuatiliwa sana ni Hillary Clinton.. simply kwa sababu anaonekana ndiye mwenye uwezo wa kupitishwa kule... Hawaulizwi watu mbona wengine "hamwajadili"? labda hawana umuhimu kama wa Lowassa?

Kwanza kaka mukubwa naomba katika mifano tumia mifano yenye uwiano! kufananisha siasa za US na TZ,hapo hapana...tuna level tofauti tena kubwa sana hasa katika siasa,still we have a long way to go....

Mimi nadhani labda unafikiri katika uchache,kwamba rasilimali za nchi ni kama nyumba yako au yangu au ya yule...angalia jiografia ya nchi ifikiri na kuielezea kwa upana uo,ni mpumbavu tu ndio ataingia hofu kwamba mafisadi wawili au mia au mia mbili watamaliza neema ya hii nchi,nasisitiza ni 'MPUMBAVU PEKEE'...tupo katika kipindi cha mpito kukua,kuna watu ao waTanzania wa baadae wataneemeka,tusisubiri mabadiriko kwamba lazima tuyaone sisi,sasa nguvu zetu zote,akili zetu zote,rasilimali zetu zote zijikite katika kupata ELIMU ya kiada na ziada.

Lowasa ana kitu (yaweza kuwa kibaya au kizuri) ndio kimecreate mvuto wetu wooote wa kumjadili...uoni hilo?usibeze,mbona atujamjadili mwingine?kwani hatufaham kwamba yupo nani na nani nao wanataka nafasi io?why EL?trust me,ana kitu...kilichovuta hisia zetu na za wengine.

Okay boss kazi,sina neno zaidi.
 
CCM inabidi waweke mtu mwenye very low profile lakini mkali na ana uwezo wa kukemea rushwa na hata akifanyiwa vetting atakuwa safi mpaka kwenye mirija ya moyo wake. Vinginevyo wajiandae kuwa wapinzani maana hakuna msafi kwenye list yao ya sasa hata mmoja.
Ufisadi kila kona kuanzia bandarini, richmond/iptl, serikali za mitaa, ujenzi, usafiri, mawasiliano, jumba jeupe sasa pamebaki wapi!!??
 
Back
Top Bottom