Mkuu
Kukaa kimya Watanzania wakilishwa peremende badala ya mlo si kuwatendea haki.
Jana nilikuwa naangalia BBC nikaona mgao wa mafuta katika taifa mwanachama wa OPEC Nigeria.
Sababu kubwa ni kutokana na ufisadi ambao umefikia mahala pa kuiweka serikali mateka
Kwa wasioona wanaweza kudhani hilo lipo Nigeria na kwingine.
Guess what! anayedhani hivyo anahitaji msaada wa wataalamu wa macho, masikiona ubongo. Tatizo lipo nchini na linaimarika kila siku
Ukubwa wake nchini ni zaidi ya Nigeria. Kule Nigeria tunafahamu ufisadi na utapeli ni sehemu ya maisha (norm)
Hapa kwetu limeingia kwa kasi kiasi kwamba, mafisadi wananunua na kuchagua nani aende Ikulu nani awe nani
Katika mkutano wa juzi Lowassa amesaidia wasiomjua. Ameeleza, pesa anazopata zinatoka kwa marafiki zake.
Utaratibu wa nchi yetu vyama hudhamini watu wao na kuendesha kampeni kwa niaba ya mgombea wao.
Ndilo chimbuko la ruzuku za vyama vya siasa. Sasa Lowassa anapotuambia anachangiwa na marafiki zake, je huo ndio utaratibu wa CCM wa siku hizi? Kwanini hakusimama ili sheria ya mgombea binafasi kama yeye ipite? Marafiki zake ni akina nani, wanamchangia ili iweje?
Kuhusu suala la Elimu, akiwa mbunge hakuna kumbu kumbu zinazoonyesha kama aliwahi kupingana na chama chake ndani ya vikao kuhusu kilimo kwanza au elimu kwanza.
Pengine ushahidi mzuri ungekuwa yeye kujiuzulu nafasi za uongozi kupinga sera zisizo sahihi. Hakufanya hivyo. Leo anaingia na sera yake
Hapa anatuambia, anachotaka kufanya si sera za wana CCM bali ana zake.
Ukichanganya na hoja ya kuchangiwa na marafiki, hakuna shaka kuna 'kachama' kake pembeni kanakohitaji 'label' au logo ya CCM
Lakini pia, tunataka EL atuambie, anasimama vipi katika ufisadi ambao ni tatizo linalodumaza Kilimo kwanza na Elimu kwa upana wake?
Huwezi kufanikisha sera ya elimu akiwa umefungwa mikono na miguu na mafisadi waliowekeza kumpeleka Ikulu
Tuna mahali pa kuanzia na si kutekwa na wafanyakazi wake wanaoaminisha umma, anafaa bila kutueleza kivipi.