Alipokuwa anatangaza nia kule Arusha Lowassa alihutubia kwa dk 20. Juzi Mbeya kahutubia kwa dakika 16, Arusha Dakika 7 na Zanzibar Dakika 11. Hivi huyu Lowassa ataweza kuhutubia mikutano ya Kampeni zaidi ya minne kwa siku?
Ataweza kuzunguka nchi nzima kama alivyokuwa anafanya Dr Slaa? Mwisho ataweza kuhutubia Bunge kwa masaa mawili hadi matatu? Ataweza kukagua paredi ya kijeshi? Mhhhh naanza kupata mashaka.
So what!.....idiot!
ww jamaa lowassa alisha kuwaga mwanajeshi akapigana vita harafu leo eti ashindwe kura ugali we jamaa acha utaniSijawahi kumuona lOWASA akila hadharani. Nimesikia analishwa siku hizi. Hapo kwenye dhifa ya kitaifa akialikwa huko majuu iatakuwaje.. unaweza ukadhani nakashifu lakini just think critically.
Kama Lowasa akichaguliwa kua rais, atatuletea gharama za misiba na mazishi zisizokua na maana. Afya yake obviously ni choka mbaya
Huyo Rais anayestaafu alikuwa anatupotezea muda kwa kuhutubia muda mrefu mpaka tunashindwa kuelewa alilenga nini hasa. Yaani longolongo zinakuwa nyingi na maccm ndo mlivyo kwa kuwa na longolongo sana bila maamuzi.
Sisi tunadhani Lowassa anajali muda na anahutubia kwa malengo bila kuwapotezea wananchi muda wa kufanya mambo mengine ya maendeleo kwa taifa.
Maadam kichwa chake kiko poa na kinatoa mafikara ya maana, anafaa kuliongoza taifa. kumbuka Rais wa Algeria anatembelea wheelchair na alishinda uchaguzi katika wheelchair hiyohiyo, hivyo sidhani akili yako kama ni nzuri kiasi kwamba huwezi kutanabahisha ni kitu gani unataka kwa Rais unayemtarajia.
Kama ni maguvu mbona kila siku Kinana anabeba madumu ya maji na matofali ya kujengea katika sanaa za chama lakini amekuwa proved failure?
Ukikasirika shauri yako
Kuna jamaa siku ya kuhitimisha kampeni yaani kesho uchaguzi, alipiga mweleka wa hatari kwenye umati mkubwa jicho likageuka,ulimi nje,mwili mlenda. Watu tukajua safari imeiva lakini alichahuliwa na kadunda for ten years.
Kwa hiyo afya ya MTU anaijua mwenyewe na daktari wake.
Hata wewe mleta mada waweza jiona uko byeee kumbe ukifanya uchunguzi unakuta una tezi la kisasa
Mipango ya maendeleo inakuwa kwenye maandishi haiwi kichwani mwa rais mtu yeyote anaweza kuisoma. Kama ni kuugua Lowassa ni binadamu kila mtu huugua. Hata rais aliyepo Ikulu kwa sasa ni mgonjwa isipokuwa ana nafuu. Na mbona hata wakati wa kampeni alikuwa anaanguka majukwaani lakini mpaka sasa ni rais? Juzi juzi alikuwa amelazwa huko Marekani na kwa maneno yake alisema alikuwa anaumwa muda mrefu lakini alikuwa ameficha tena akasema alimficha hata nkewe! Hivyo hata sisi tunaonnyooshea vidole Lowassa inawezekana ni wagonjwa zaidi yake sema tu magonjwa yetu hayajajitokeza. Ya Mungu mengi huenda huyo tunayesema ni mgonjwa akahudhuria misiba yetu tutakapokuwa tumekufa. Wangapi walisemwa ni wagonjwa lakini mpaka sasa wako hai na wale waliosema wenzao ni wagonjwa wamekufa wao na tumeshaanza kuwasahau?Mipango ya maendeleo ya taifa ya miaka mitano itaelezwa kwa muda huo? Utendaji unahitaji muda pia! N ni dhahiri kwamba sio dakika ni miaka!