ashura munga
Member
- Sep 27, 2015
- 5
- 0
Baba kubaliana na matokeo
Hali ni tete ndani ya kituo cha ITV kufuatia kuvuja kwa video zinazomuonyesha mgombea wa Chadema Edward Lowassa akiwa kwenye hali ya udhoofu.
Mtoa taarifa ambaye ni mtangazaji wa ITV anasema, mmiliki wa kituo hicho Reginald Mengi baada ya kulalamikiwa na Lowassa juu ya video hizo ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii, alitaka wote waliohusika kwenye utayarishaji wake wawajibike.
Anasema uandaaji wa matangazo hayo ya Lowassa ambayo yameanza kurushwa na ITV, yalichukua muda mrefu kuyaandaa ambapo Lowassa kutokana na hali yake ilimlazimu kurudia kila mara na wakati mwingine alionekana kushindwa kuongea na kukohoa sana.
Video hizo ambazo alishindwa kuongea ndo zimesambazwa na kumkera Lowassa na kukosa imani na ITV kituo ambacho inaelezwa alianza kukilalamikia kwa kupunguza habari za mikutano yake.
Mtoa taarifa anasema tayari baadhi ya watendaji wamesimamishwa kazi kwa kitendo cha kusambaza video zinazomdhalilisha Lowassa na kuonyesha udhaifu wake ambao Chadema wanajitahidi kuuficha.
TUTAMPIGIA KURA EDWARD LOWASSA KESHOKUTWA,Hata iweje,nyie CCM endeleeni na huu uzushi wenu.
Ngoja niwawekee aina uongo Magamba
wanaoutengeneza na kuusambaza Facebook instargram na mitandao mbalimbali na ukweli wake
Magamba wanadhani bila Lowassa ndo watashinda
Thubutuuuu hata asingekuwepo Mwaka huu mtakoma
lisemwalo lipo na kama halipo laja
Jamani huwezi kuficha ugonjwa wako huo ni uonevu
Kiwanda cha uongo at its best!Hiyo clip iliyovuja kaiona nani?Lumumba mmechanganyikiwa nin?
Naomba huyu aliyetoa uzi huu awajibishwe sheria ya mtandao kama itadhibitika ni mchochezi.
Hakuna wa kututenganisha na lowassa coz ni chaguo letu.
Mtoa uzi huu tubu kwa Mungu ,hujafa hujaumbika ,
Unasema mwenzako mgonjwa,watu wanatangulia wanamwacha wanayemwita mgonjwa
Nakwambia tubu maana Mungu anajibu kwa moto.
Kumbuka sala ya sheikh pale Jangwani UKAWA walipozindua kampeni!
Usiseme tuta , sema uta. Wengine wengi wanajitambua sana na wala usudhani watanzania wote ni kama wewe. Sisi hatutoki kaskazini na wala si walutheri so hatutampigia ng'ooo!Hata iweje...TUTAMPIGIA KURA EDWARD LOWASSA.
Hata iweje...TUTAMPIGIA KURA EDWARD LOWASSA.
Ugonjwa wake ni wa kusahau hata jina lake siku hizi halikumbuki, utamsikia naomba kura zenu tu. Rais ndio symbol ya nchi, hatutakiwi kuwa na shaka shaka nae,usalama wa nchi yote uko kichwani kwake. Hatutaki tumchague lowasa aongoze Sumaye.
Pushup dk 5 hotuba lisaa na nusu non stop and without sitting or pee!!
kwa hiyo mawazo yako nini ndg yangu kwa nini waandae muda mrefu.acha siasa chafu za Lumumba
Vipi na kuhusu zile video za TBC zinazodaiwa zilizovuja zikimwonesha Lowassa akimkunja saba mama yako umeshazipata?
Ivi katika ulimwengu huu nani ni mzima?
Tutajionea kesho katika mdahalo, kama nikweli hawezi kuongea kwa 1hr
Wenzako wametangulia kabla yake, naona na wewe unamwita zrael kwa nguvu