Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

hahahaha.. Nitawapeni hiyo scenario:

a. Kikwete anaamua kutokugombea mwakani kwa sababu x,y. WanaCCM wanaanza kumpigia kelele sana kuwa awe mgombea "pekee" lakini anazipuuzia na kuamua kuwa hataki tena mzigo huu wa urais kwani umejaa lawama sana (kumbuka JK hapendi kubebeshwa lawama na miaka hii mitano imekuwa mitamu na michungu). JK alitaka kuwa Rais kutimiza ndoto ya kuwa Rais. Period. Ameshaitimiza ndoto hiyo na milele ameingia kwenye historia. Sasa agombee tena 2010 ili kiwe nini? So, tu assume JK hatogombea 2010.

b. Nani ataweza kugombea ndani ya CCM zaidi ya Lowassa? HAKUNA. Hapa ndipo utaelewa "Agenda 21" ni ni nini (2010) ambayo niliielezea mwaka jana ilipoundwa tu na sasa iko full throtle. Kuna imani ya wabunge na viongozi wengi sana kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kukiongoza Chama na Taifa kwa uwezo mkubwa, kufanya maamuzi magumu n.k kama Lowassa. Wapo ambao wanamdharau kabisa JK na kumuita the "so called president". Hawa wanaelewa udhaifu wa JK kuliko mtu mwingine yeyote (ule wa kiongozi, msiende mbali...).

c. Lowassa anafuata ushauri wangu to the core kama nilivyoandika. Wengi labda hamjakumbuka kuwa wiki iliyopita alikuwa Mwanza na Rais ambako alishangiliwa na pole pole mtaona akirudi kwenye sura ya taifa na kilele chake cha kurudi rasmi na moto ulimini itakuwa Bungeni wiki chache zijazo. Ushauri mmoja ambao hatoufuata ni wa kuachana na kina Mwang'onda, Rostam na wengine. Hii kwake ni timu ya ushindi.

d. Atakapofanikiwa kuwa Rais au kumsaidia mtu wake (always ana plan b) kushinda basi tarajieni kisasi.

Ukiweza copy hii na iweke mahali fulani usije ukaanza kuitafuta huko mbeleni.
 
hahahaha.. Nitawapeni hiyo scenario:

a. Kikwete anaamua kutokugombea mwakani kwa sababu x,y. WanaCCM wanaanza kumpigia kelele sana kuwa awe mgombea "pekee" lakini anazipuuzia na kuamua kuwa hataki tena mzigo huu wa urais kwani umejaa lawama sana (kumbuka JK hapendi kubebeshwa lawama na miaka hii mitano imekuwa mitamu na michungu). JK alitaka kuwa Rais kutimiza ndoto ya kuwa Rais. Period. Ameshaitimiza ndoto hiyo na milele ameingia kwenye historia. Sasa agombee tena 2010 ili kiwe nini? So, tu assume JK hatogombea 2010.

b. Nani ataweza kugombea ndani ya CCM zaidi ya Lowassa? HAKUNA. Hapa ndipo utaelewa "Agenda 21" ni ni nini (2010) ambayo niliielezea mwaka jana ilipoundwa tu na sasa iko full throtle. Kuna imani ya wabunge na viongozi wengi sana kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kukiongoza Chama na Taifa kwa uwezo mkubwa, kufanya maamuzi magumu n.k kama Lowassa. Wapo ambao wanamdharau kabisa JK na kumuita the "so called president". Hawa wanaelewa udhaifu wa JK kuliko mtu mwingine yeyote (ule wa kiongozi, msiende mbali...).

c. Lowassa anafuata ushauri wangu to the core kama nilivyoandika. Wengi labda hamjakumbuka kuwa wiki iliyopita alikuwa Mwanza na Rais ambako alishangiliwa na pole pole mtaona akirudi kwenye sura ya taifa na kilele chake cha kurudi rasmi na moto ulimini itakuwa Bungeni wiki chache zijazo. Ushauri mmoja ambao hatoufuata ni wa kuachana na kina Mwang'onda, Rostam na wengine. Hii kwake ni timu ya ushindi.

d. Atakapofanikiwa kuwa Rais au kumsaidia mtu wake (always ana plan b) kushinda basi tarajieni kisasi.

Ukiweza copy hii na iweke mahali fulani usije ukaanza kuitafuta huko mbeleni.

....pheeeeeeeeeeeeeeeewww! shukran MM. kuna watu hawakuamini humu, mie sina shaka na tabiri zako.
 
hahahaha.. Nitawapeni hiyo scenario:

a. Kikwete anaamua kutokugombea mwakani kwa sababu x,y. WanaCCM wanaanza kumpigia kelele sana kuwa awe mgombea "pekee" lakini anazipuuzia na kuamua kuwa hataki tena mzigo huu wa urais kwani umejaa lawama sana (kumbuka JK hapendi kubebeshwa lawama na miaka hii mitano imekuwa mitamu na michungu). JK alitaka kuwa Rais kutimiza ndoto ya kuwa Rais. Period. Ameshaitimiza ndoto hiyo na milele ameingia kwenye historia. Sasa agombee tena 2010 ili kiwe nini? So, tu assume JK hatogombea 2010.

b. Nani ataweza kugombea ndani ya CCM zaidi ya Lowassa? HAKUNA. Hapa ndipo utaelewa "Agenda 21" ni ni nini (2010) ambayo niliielezea mwaka jana ilipoundwa tu na sasa iko full throtle. Kuna imani ya wabunge na viongozi wengi sana kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kukiongoza Chama na Taifa kwa uwezo mkubwa, kufanya maamuzi magumu n.k kama Lowassa. Wapo ambao wanamdharau kabisa JK na kumuita the "so called president". Hawa wanaelewa udhaifu wa JK kuliko mtu mwingine yeyote (ule wa kiongozi, msiende mbali...).

c. Lowassa anafuata ushauri wangu to the core kama nilivyoandika. Wengi labda hamjakumbuka kuwa wiki iliyopita alikuwa Mwanza na Rais ambako alishangiliwa na pole pole mtaona akirudi kwenye sura ya taifa na kilele chake cha kurudi rasmi na moto ulimini itakuwa Bungeni wiki chache zijazo. Ushauri mmoja ambao hatoufuata ni wa kuachana na kina Mwang'onda, Rostam na wengine. Hii kwake ni timu ya ushindi.

d. Atakapofanikiwa kuwa Rais au kumsaidia mtu wake (always ana plan b) kushinda basi tarajieni kisasi.

Ukiweza copy hii na iweke mahali fulani usije ukaanza kuitafuta huko mbeleni.

Asante mkuu; Nashusha pumzi ,tuendako mmh!!!
 

Mimi, Edward Ngoyayi Lowassa, naapa kuwa:

Nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wangu wote, na kwamba nitaihifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Nitatenda kazi zangu za Urais kwa uaminifu na kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu, na kwamba nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Sheria, mila na desturi za Tanzania bila woga, upendeleo, huba wala chuki.

Nitatetea na kudumisha umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mungu nisaidie


How can we make this impossible?
 
Nchi inahitaji RAIS ambaye ni semi dikteta.

EL ni semi Dicteta. EL ameshakusanya mali. Inachobakia ni kuongoza nchi. Mimi nitampigia kampeni za nguvu 2015

Si kweli kuwa tajiri haitaji pesa zaidi. Kadiri mtu anavyokuwa na pesa nyingi, ndivyo anavyohitaji pesa nyingi zaidi.

Lililo la kweli zaidi ni kwamba, EL akipata nafasi ya kuwa Rais (au hata PM) atatumia muda mwingi zaidi kulipiza kisasi kuliko kufanya kazi za kimaendeleo.
 
Swali litakuwa ni kwanini Lowassa autake Urais wakati alishawahi kuwa Waziri Mkuu?
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu hiyo agenda 21, Kikwete sii mwanachama wala hana uhusiano..Na utabiri wako nina hakika hautatimia kwa sababu Kikwete sii Mtandao tena... Alikuwa...niamini kwa hilo.

Na nakuhakikishia kwamba Kikwete anaweza kuwa mjinga lakini sii mjinga Hivyo! kwa sababu hakuna rais hata mmoja duniani ambaye huingia Ikulu kwa sababu anataka kuwa ktk record ya kiti hicho bali wengi kama sii wote huvutwa na tamanio (ambiton), kama muuza Unga kamwe hatosheki..
Katika kupiga bao langu, Richmond na Dowans ni akiba imewekwa storage.. Itaibuka tu mara hawa jamaa watakapo potea maboya kuingia 2nd phase.. kwa sababu agenda 21 ilikuwa ktk hatua ya kuwamaliza wote wabunge wanaopingana na mtandao.. Toka Sitta, Mwayembe, Mama Kilango, Selukindo na wengineo wengi tu..

Kama unakumbuka Mama kilango alipigwa vita hapa JF kama ile ile ya Mwakyembe.. neno kwa neno, hoja kwa hoja vitu vingi vilifanana.. Na kabla yao Spika Sitta pia alizungumziwa kama ni fisadi vile vile yakasemwa mengi sana..Kisha ikatokea hoja ya Kikwete kuwa mgomnbea pekee wa kiti cha Urais toka CCM ikapigwa vita sana hata kina Malecela wakaitwa majina...Wadanganyika wengi wanaamini Kikwete hafai tena kuwa rais mwaka 2010 wakati hawana sababu za kutosha zaidi ya hizo kesi ambazo zimewekwa chini ya mto makusudi..
Nina hakiika kabisa kabla ya Uchaguzi ndani ya chama CCM Ufisadi utakuwa somo namba moja na watachuana wenyewe kwa mzani wa Ufisadi..Just wait, utakuja nambia..

Na kwa sababu Kikwete alikuwa Mtandao na akapita chaguzi kwa nguvu ya Mtandao hawezi kabisa kuingilia vita hiyo ya Ufisadi... wapo keyplayers ambao watawafuata kina Lowassa na kundi lake kila wanapoingia.. Na Lowassa hatathubutu kusema lolote kuhusiana na JK kwa sababu wanajua watakuwa wamevunja yamini waliyokula..JK anasubiri tu wao waanze kumtumbukiza ktk Ufisadi kisha yeye atamaliza.. Hapatakalika tena CCM na hilo haliwezi kutokea...watauana....
Ndio maana hao Mtandao na hiyo agenda 21 wanataka kuingia phase ya Pili - Kujitangaza wao kwa kupitia jina la CCM..lakini wanashindwa mbinu za kumwondoa JK, zaidi ya kusema hafai tena..
Jamani kama Lowassa angekuwa waziri mkuu hadi leo hii ni kitu gani angekifanya?.. hizo mvua za sayansi? Je, kuna mtu angweza kuzuia Dowans kuuza mashine zile Tanesco wakati Lowass ni waziri mkuu! tazama mradi wa TRC na India kauweka yeye, Pinda kakuta mkataba tayari, haya itazame hiyo reli ya kati ianvyozidi kumomonyoka!. ATC imetoka South, Lowassa akiwa waziri mkuu kafanya nini kuboresha!.. Hakuna..Baada ya kuwafukuza Citywater kafanya kipi bora ktk usambazaji maji..Yaani huyu kaondoka katuachia mzigo mkubwa kama Mkapa kisha tunataka JK ayamalize madudu yote ya Lowassa ghafla bin vuuu.
Nasema hivi Lowassa hawezi kuwa rais mwaka 2010 wala 2015 hata kama atatumia mbinu ya mzee ruksa kwa sababu, Mwinyi hakuhusika na mauaji ya Shinyanga isipokuwa mauaji yale yalitokea under his watch..qakati Lowassa ni keyplayer wa mipango yote ya Richmond...Atakataa yote lakini moja ambalo nalikumbuka ni Ushahidi tosha kabisa kumweka hatiani.Aliposhauri Tanesco kama mkataba wa Richmond unaweza kuhamishiwa Dowans..Statement hiyo nakumbuka kuisoma hapahapa JF ktk makkala fulani...
Leo mnasema ati Lowassa atakuwa rais wa Tanzania!..afanye atakayo yafanya lakini hawezi kufanikiwa..Siku atakayo jaribu hilo basi huo ndio utakuwa mwisho wake..
 
yale yale ya MALECELA na laana za NYERERE sembuse Lowasa! wala msiogope JF tuko pamoja tutamuangusha kirahisi sana tumuombee mema ili aonje nguvu ya umma ikoje naona anaamini sana nguvu ya pesa

Jeuri wanayo kwa sababu wanajua watanzania wakisha pewa pilau na kanga uwezo wa kufikiri unakuwa umefikia kiwango chake.
pili wanajua kabisa kuwa mbinu za ccm na vyombo vya dola hakuna mwananchi wala nguvu ya wananchi iliyo na ubavu wa kuvipangua.
wanajua kabisa kuwa vyama vya siasa a.ka. vya uinzani vyote ni vyama vyua ubinafsi hakuna siku wamewahii kuamua kutetea mwananchi bali wana tetea masilahi yao kama ilivyo kwa chama tawala, kama wangetetea masilahi ya wananchi hawakuwa na sababu ya kushindana katika jimbo moja vyama lukuki badala ya kusimamisha mgombea mmoja kulingana na mwelekeo au mwanendo wa uchanguzi.
Kwa hivyo jeuri ya chama tawala itaendelea na wana uwezo wa kumweka wanayemtaka kwa kuzingatia uwezo wa pesa za walala hoi/walipa kodi na za wafanyabiashara wakuu wanaolinda mali zao/mafisadi.
 
Jeuri wanayo kwa sababu wanajua watanzania wakisha pewa pilau na kanga uwezo wa kufikiri unakuwa umefikia kiwango chake.
pili wanajua kabisa kuwa mbinu za ccm na vyombo vya dola hakuna mwananchi wala nguvu ya wananchi iliyo na ubavu wa kuvipangua.
wanajua kabisa kuwa vyama vya siasa a.ka. vya uinzani vyote ni vyama vyua ubinafsi hakuna siku wamewahii kuamua kutetea mwananchi bali wana tetea masilahi yao kama ilivyo kwa chama tawala, kama wangetetea masilahi ya wananchi hawakuwa na sababu ya kushindana katika jimbo moja vyama lukuki badala ya kusimamisha mgombea mmoja kulingana na mwelekeo au mwanendo wa uchanguzi.
Kwa hivyo jeuri ya chama tawala itaendelea na wana uwezo wa kumweka wanayemtaka kwa kuzingatia uwezo wa pesa za walala hoi/walipa kodi na za wafanyabiashara wakuu wanaolinda mali zao/mafisadi.


- Mkuu Kahinda, maneno mazito sana haya yaani hakuna cha kuongeza wala kupunguza, I am down! na habari nilizozipata kwenye dataz ni kwamba ni kweli mkuu el yumo mbioni kurudi tena kwa speed kali sana ila binafsi ninasema overmy-dead body haendi kokote mbio za ukingoni!

Respect.

FMEs!
 
politically EL is over.....

EL hawezi kuwa rais wa TZ 2010 or 2015 ana roho mbaya na chuki na watu wengi sana ndani na nje ya ccm.....

ukiangalia siku za usoni utaona JK anafuata nyayo za Kibaki
kibaki na Raila walishirikiana vizuri sana kuhakikisha kibaki anakuwa rais kwa madhumuni kwamba atakaa msimu mmoja na kumuachia raila. lakini kibaki alivyokuwa rais akanogewa na kikubwa alichokifanya ni kupatana na MOI na kumtenga raila ambaye alikuwa anataka kiti chake na mpaka leo uhasimu ni mkubwa sana
kwa upande wa JK na EL walivyochukua nchi kampeni of terror ikaanza ilikuwa ikiongozwa na EL kwa wale watu wote waliokuwa wanampinga EL baada ya muda EL akaanza kumkumbusha bwana mkubwa JK ile promise waliyowekeana nae, JK alichofanya ni character assassination, akahakikisha EL anakwenda na richmond tangu siku hiyo wamekuwa wakicheka ki sinema, ingawa JK hana maamuzi lakini si mpumbavu kama watu mnavyomfikiria, bado kuna mawaziri kibao ambao wanawaabudu EL na RA kasoro watano.
kama unavyoangalia sasa hivi JK amerudisha uswahiba wake na BWM(MOI) na kumsifia hadharani na hii yote ni kuwahakikishia watu wa BWM wanaoteswa na watu EL na RA kuwa wako salama, na hii ni njia moja wapo ya kumtenga EL na kundi lake. EL atakapotangaza tu kugombea 2010 richmond ndiyo itakuwa jeneza lake.
Ni dhairi kabisa kwamba 2015 JK atampa mtoto wake mwenyewe wa damu (BERNARD MEMBE), hawezi kumpa EL kwa ajili anajua atapata sana mateso na EL hamwamini tena JK kwa ajili keshavunja ahadi ya kwanza na njia pekee aliyokuwa nayo EL ni kuanzisha vita 2010.
Na hii vita ni dhairi kwamba EL ataanguka vibaya
EL na RA pamoja na pesa zao hawawezi kununua ushindi 2010 or 2015 wanachukiwa sana ndani ya ccm na watu wengi

watu wengi sana ni bora kikwete awe rais kwa ajili ana ubinadamu kuliko EL. EL rais na RA chief of staff sijui watu kama wakina mengi sijui watapitia wapi.....
kamwe EL hawezi kuiongoza TZ
 
Last edited:
politically EL is over.....

EL hawezi kuwa rais wa TZ 2010 or 2015 ana roho mbaya na chuki na watu wengi sana...............................................ni bora kikwete awe rais kwa ajili ana ubinadamu kuliko EL. EL rais na RA chief of staff sijui watu kama wakina mengi sijui watapitia wapi.....
kamwe EL hawezi kuiongoza TZ


ANAWEZA!
hao alionachuki nao ni tone tu la maji katika bahari (wadanganyika wapiga kura) anachojali yeye ni kupitishwa na CC na NEC ya ccm basi. wapiga kura hilo halina tatizo kabisa; wakipewa pipi , chumvi, sabuni na kanga za ccm watampa kura tu. just imagine mapokezi ya EL, RA na mzee wa vijisenti kule majimboni kwao yalikuwaje.
 
Last edited:
I see what is happening in Iran coming up here, we will know the real cost of freedom..
 
Tulikuwa tunashangaa story ya Iran, Wahenga walituambia, "ukiona mwenzako ananyolewa...."
 
Kwa muda sasa Taifa limekuwa likikumbana na mambo yanayotokea iwe ndani ama nje ya Bunge huku wengine wakiwa wanayaona kuwa ni mambo ya kawaida tuu bila kuhoji nini kinaendelea kutokea huku wengine wakihoji tena kwa vinywa vipana kabisa.

Nataka leo niwaambie kuwa tangu anguko la Lowassa mwaka 2007 , huyu Lowassa na wenzake hawajalala kwani walikuwa wanatengeneza mkakati wa jinsi ya kuweza kumsafisha na imekuwa ni operation maalum na inayofanywa kwa ustadi mkubwa sana na watu wengui sana .

Wengine wamekuwa wakijikuta wanaingizwa kwenye kufanya kazi hiyo hata bila ya kujua kama wapo kwenye operation maalum.

Yaliyotokea ni kama ifuatavyo;

1. Tangu mwaka 2007 Lowassa amezunguka kwa siri nchi nzima na amekuwa akikutana na viongozi mbalimbali wa dini kwa siri na alikuwa anafanya kazi moja tuu ya kuwaeleza kile alichokuwa anawaambia kuwa ni upande wa pili kuhusu Richmond .

2. Lowassa alifanya sherehe kubwa sana na kuwaalika wakuuu wa mikoa na wilaya karibia wote nyumbani kwake wakati wa mkewsha wa mwaka mpya mwaka 2009 ,na lengo likiwa ni kuwaeleza nini kilitokea japo alitumia kigezo kuwa anaenda kuwashukuru kwa kazi alizokuwa amefanya nao huku Rais wa Nchi akiwa hajaweza kufanya tukio kubwa tangu aingie madarakani baada ya lile la MAELEKEZO YA NGURUDOTO.

3.Kundi la Lowassa na lile la Mkapa wameungana na wanafanya mikakati ya pamoja ya jinsi ya kuweza kujisafisha na kurudi kwenye siasa upya.Makundi haya yameweza kuanza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani ripoti mbili zilizowasilishwa Bungeni hivi majuzi kuhusu Richmond na Kiwira ni matunda ya mkakati huo .

4.Wapo waandishi wa habari na wengine ni wahariri ambao mara nyingi walionekana kama ni watetezi wa Taifa lakini kwa sasa wanafanya jambo jingine , wengine wakiwa wanafikiri kuwa wanafanya kwa kushirikiana na ubalozi wa Iran kuandaa kijarida ambacho miongoni mwa wahariri wake ni dada Sakina Datoo na Hawra Shamte .

5.Kundi la Lowassa ndani ya CCM litakuja na mkakati ndani ya kikao kijacho cha kamati kuu kuitaka CCM itamke wazi kuwa Lowassa hakuhusika na ufisadi ila aliwajibika kutokana na nafasi yake , na huu utakuwa mwanzo wa Lowassa kujitokeza hadharani na kuanza kuzungumza.Kama ambavyo hivi punde Mkapa atajitokeza hadharani na kuanza kuzungumza.

6.Kundi la Lowassa limefanikiwa kuwakamata wanasiasa machachari wa Upinzani na mmoja wao ambaye bado uchunguzi unaendelea kama anafanya kwa bahati mbaya ama ni kwa kutumwa ni mbunge mmoja kijana ambaye anataka iundwe tume ya majaji kwa ajili ya kujadili masuala ya Richmond .Hii imekuwa ni mbinu ambayo imetumiwa na mafisadi wengi duniani katika kujisafisha kwani mwisho wa siku ni kuwa mahakama itatakiwa kupata ushahidi usiokuwa na shaka , kitu ambacho hakiwezekani kwani mpaka sasa serikali imeshasema kuwa maafisa wake waliohusika kuandaa mikataba hiyo hawakusika na ufisadi wowote ule. hivyo tume ya majaji kwa sababu itategemea ushahidi kutoka serikalini na serikali ushahidi wake ndio huo majibu yanajulikana kuwa majaji watasema nini.
Mbona hatusemi paundwe tume ikachunguze meremeta, Tangold,Kiwira,Deepgreen n.k?

7.Chama cha CUF kimejikuta kikiwa centre ya mapambano haya bila hata kujijua kuwa mwisho utakuwa nini na wao wameelekeza mashambulizi yao kwa kundi la JK na kuliacha kabisa kundi la Mkapa na Lowassa , na mifano iko mingi sana ukizingatia kuwa viongozi wa CUF hawajasikika hata siku moja wakitaka KAGODA apelekwe mahakamani, Rostam ashughulikiwe,Mramba achukuliwe hatua na sasa wameacha kabisa kumtaja Mkapa na kashfa zake.

8.Taarifa nyingi zinazotoka sasa na haswa kuhusiana na kundi la Spika Sitta na haswa wakimlenga yeye binafsi zina lengo moja tuu la kuhakikisha kuwa wanamnyongonyesha na mara baada ya hapo yeye na kundi linalojiita jeshi dhidi ya UFISADI litafifia na hivyo kulipa nguvu kundi la akina Lowassa kuweza kujitokeza , mifano angalia hotuba za mawaziri ni mawaziri gani walishambuliwa na walishambuliwa na makundi gani ama na watu gani utaweza kuona ninachokisema hapa.

Hivyo basi OPERESHENI SAFISHA LOWASSA ni ya kudumu na inatarajiwa kuendelea na mipango mingi inafanyika kuhakikisha kuwa wanatoka na kuweza kufikia malengo yao waliyojiwekea. KILA MMOJA ACHUKUE HATUA.

KILA LA KHERI , Ila kila mmoja wetu ajue kuwa anatakiwa kuanzia sasa kuonyesha yuko upande gani na kwa masilahi ya nani .
 
Last edited:
Ndugu mleta hoja,
Asante kwa maelezo yako matamu na marefu ambayo hayana uthibitisho.
Kwa upande wangu sijaona ufisadi wa Lowasa mpaka sasa. Lowasa alijiuzulu cheo chake tokana na kuwajibika na wala si vinginevyo. Tumeona toka mwanzo ilipoundwa tume ya Mwakyembe kuhusu Richmond haikumtendea haki Lowasa kwa kumnyima haki ya kujieleza mbele ya tume kwanini alitenda yale aliyoyatenda katika sakata la Richmond.
Ndugu mleta hoja, ni vyema kuangalia na kupima ukweli kabla ya kumuhukumu mtu. Usifuate mkondo wa watu wengi ama usiwe na upande wowote katika kuangalia haki. Unaposema Lowasa ni Fisadi na mwizi tafadhali njoo na vithibitisho vya kauli yako.

Ningependa uelewe kwamba Lowasa alijiuzulu tokana na kuwajibika, na isitoshe aliepusha mambo makubwa sana kwani kama haki na ukweli ungefuatwa basi wa kujiuzulu hakuwa Lowasa.
 
6.Kundi la Lowassa limefanikiwa kuwakamata wanasiasa machachari wa Upinzani na mmoja wao ambaye bado uchunguzi unaendelea kama anafanya kwa bahati mbaya ama ni kwa kutumwa ni mbunge mmoja kijana ambaye anataka iundwe tume ya majaji kwa ajili ya kujadili masuala ya Richmond .Hii imekuwa ni mbinu ambayo imetumiwa na mafisadi wengi duniani katika kujisafisha kwani mwisho wa siku ni kuwa mahakama itatakiwa kupata ushahidi usiokuwa na shaka , kitu ambacho hakiwezekani kwani mpaka sasa serikali imeshasema kuwa maafisa wake waliohusika kuandaa mikataba hiyo hawakusika na ufisadi wowote ule. hivyo tume ya majaji kwa sababu itategemea ushahidi kutoka serikalini na serikali ushahidi wake ndio huo majibu yanajulikana kuwa majaji watasema nini.

Mbona hatusemi paundwe tume ikachunguze meremeta, Tangold,Kiwira,Deepgreen n.k?

.

Mbunge pekee ambae ametoa wazo la kuunda jopo la majaji ni mimi. Hii inatokana na imani yangu ya kupata haki na ukweli. Sina sababu yeyote ile kumtetea Lowasa. Sina interest yeyote ile na Lowasa. Ndio kwanza nasikia kwako kuwa Jopo la Majaji laweza kumsafisha Lowasa. Nimetoa mawazo haya kwa nia njema kabisa nikiamini kuwa Serikali imelikosea Bunge kwa kutototekeleza maazimio na kusafisha wakosaji. Nikadhani kwamba, iwapo mihimili miwili ya Dola inagongana, mhimili wa Mahakama ndio utaweza kutenda haki.

Kumbe hili laweza kumsafisha Lowasa? Kwamba inawezekana kabisa mtu mwenye akili timamu akahisi kuwa mimi ninaweza kutumika kumsafisha Lowasa? Hata kwa mikakati ya kisiasa ya badae ni kosa kubwa mimi kutaka Lowasa atakate.

Mimi ninadhani huu mzimu wa Lowasa huu usizibe fikra huru. Haiwezekani hata kidogo watu tuache kufikiri kwa kumwogopa Lowasa. Ifahamike kuwa Maamuzi ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu Richmond ni maamuzi bora kabisa kufanywa na Bunge na ni maamuzi ambayo yamelipa Bunge heshima kubwa sana. Siwezi kuwa mmoja wa watu ambao wanataka heshima ya Bunge kuporomoka. Wazo la Jopo la Majaji sio Bahati mbaya. Bali ni hatua ambayo itaweka kila kitu wazi - kwani majopo haya hufanya kazi kwa uwazi kabisa na wakati mwingine kurushwa 'live'. Huoni jopo la Majaji litatufanye tujue yale ambayo Dokta Mwakyembe alisema hawakuyasema?

Hata hivyo, kama tunaamini kuwa jopo la majaji litamsafisha Lowasa, basi tusiunde! Nilidhani jopo la majaji ndio limwadhibu Lowasa na wengineo waliopanga kutuibia kupitia Mkataba wa Richmond.
 
4.Wapo waandishi wa habari na wengine ni wahariri ambao mara nyingi walionekana kama ni watetezi wa Taifa lakini kwa sasa wanafanya jambo jingine , wengine wakiwa wanafikiri kuwa wanafanya kwa kushirikiana na ubalozi wa Iran kuandaa kijarida ambacho miongoni mwa wahariri wake ni dada Sakina Datoo na Hawra Shamte.

Mnamwonea sana Sakina. Uzalendo wa dada huyu hauna mashaka hata kidogo. Usafi wa Sakina hauna mawaa hata kidogo. Kumhusisha Sakina na mipango ya kifisadi ni kumwonea sana. Nina uhakika Mungu atalaani wote wanaowazushia watu wema. Sakina is Real! She has NO multiple faces! Kuacha kwake kazi IPPMEDIA kusitumike kumzushia. Alieandika haya anajua kuwa anamzushia Sakina.

Hawra Shamte, binti wa Waziri Mkuu wa Kwanza na wa mwisho wa Zanzibar amekuwa mwandishi mwenye kuandika anachoamini. Uislam wake na mahusiano yake ya kidini na Jamhuri ya Iran visitumike kumpaka matope. Ninaamini Hawra hawezi kuingia katika mtego wa kutetea na kusafisha watu.
 
Wazo la Jopo la Majaji sio Bahati mbaya. Bali ni hatua ambayo itaweka kila kitu wazi - kwani majopo haya hufanya kazi kwa uwazi kabisa na wakati mwingine kurushwa 'live'. Huoni jopo la Majaji litatufanye tujue yale ambayo Dokta Mwakyembe alisema hawakuyasema?

kwani hao majaji wa sasa hivi si ndio watakao kuwa kwenye jopo la majaji??

kama tume ya mwakyembe imemuona EL ana hatia na ikamlazimika kujiuzulu kwa nini tena liundwe jopo la majaji kwa ajili ya kitu kile kile??

kwa nini usitumie muda kuwashinikiza wabunge wengine ili lowasa afikishwe mahakamani na badala yake unataka jopo la majaji ambalo linaweza kumsafisha???
 
Mbunge pekee ambae ametoa wazo la kuunda jopo la majaji ni mimi. Hii inatokana na imani yangu ya kupata haki na ukweli. Sina sababu yeyote ile kumtetea Lowasa. Sina interest yeyote ile na Lowasa. Ndio kwanza nasikia kwako kuwa Jopo la Majaji laweza kumsafisha Lowasa. Nimetoa mawazo haya kwa nia njema kabisa nikiamini kuwa Serikali imelikosea Bunge kwa kutototekeleza maazimio na kusafisha wakosaji. Nikadhani kwamba, iwapo mihimili miwili ya Dola inagongana, mhimili wa Mahakama ndio utaweza kutenda haki.

Kumbe hili laweza kumsafisha Lowasa? Kwamba inawezekana kabisa mtu mwenye akili timamu akahisi kuwa mimi ninaweza kutumika kumsafisha Lowasa? Hata kwa mikakati ya kisiasa ya badae ni kosa kubwa mimi kutaka Lowasa atakate.

Mimi ninadhani huu mzimu wa Lowasa huu usizibe fikra huru. Haiwezekani hata kidogo watu tuache kufikiri kwa kumwogopa Lowasa. Ifahamike kuwa Maamuzi ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu Richmond ni maamuzi bora kabisa kufanywa na Bunge na ni maamuzi ambayo yamelipa Bunge heshima kubwa sana. Siwezi kuwa mmoja wa watu ambao wanataka heshima ya Bunge kuporomoka. Wazo la Jopo la Majaji sio Bahati mbaya. Bali ni hatua ambayo itaweka kila kitu wazi - kwani majopo haya hufanya kazi kwa uwazi kabisa na wakati mwingine kurushwa 'live'. Huoni jopo la Majaji litatufanye tujue yale ambayo Dokta Mwakyembe alisema hawakuyasema?

Hata hivyo, kama tunaamini kuwa jopo la majaji litamsafisha Lowasa, basi tusiunde! Nilidhani jopo la majaji ndio limwadhibu Lowasa na wengineo waliopanga kutuibia kupitia Mkataba wa Richmond.
Mhe. Zitto, japo siungi mkono mkakati wowote wa unaoitwa wa kumsafisha Lowasa ila naomba tusimame kwenye haki.

Dr. Mwakiembe ni mwalimu wangu wa sheria pale UD somo la kwanza, siku ya kwanza ya kusoma sheria ni pamoja na the 1st principle of natural justice, "No one is condemned unheard" kwa nini Dr. Mwakiembe mwanasheria aliyebobea alimtenda hivi Lowassa?.

Kwa kuzingatia hili, Lowassa ana haki ya kutafuta haki yake. Kama kweli ni mchafu hana haja ya kujisafisa, lakini kwa sababu anayo version yake ya mambo hayo, ni haki yake akaiweka wazi halafu public ndio itajudge how clean he is. Let him come clean, ili ile ahadi ya boys II men iliyokuwa itimie 2010 sasa itatimia 2015.
 
Back
Top Bottom