Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

kama tume ya mwakyembe imemuona EL ana hatia na ikamlazimika kujiuzulu kwa nini tena liundwe jopo la majaji kwa ajili ya kitu kile kile??

Bunge sio mahakama na wala sio jukumu letu kuamua kesi. Rushwa ni kosa la jinai. Tume ya Majaji itakayoundwa kwa mujibu wa Public Inquiry Act inaweza kumwelekeza DPP afungue kesi ya jinai dhidi ya mtu yeyote. Kamati ya Bunge haiwezi kuona mtu ana hatia maana sio mandate yake hiyo.

Hata hivyo nimesema, kama tunajiridhisha kuwa Mahakama itamsafisha Lowasa na wengineo katika kashfa mbaya kabisa ya Richmond basi wazo hili life. Maana iwapo tunaogopa mahakama kushughulikia suala hili baada ya Serikali na Bunge kugongana - basi kuna mashaka makubwa na 'hatia' ya Lowasa. Mimi ninaamini, kwa taarifa za kibunge kutoka kamati teule, Lowasa hasafishiki. Njia ya kumfikisha mahakamani ni Judicial Commission pekee. Bunge haliwezi kuamuru Lowasa kushtakiwa. HALIWEZI na halina nguvu hizo kikatiba. Mhimili wenye nguvu hizo ni mahakama na huko ndio haki hutendeka.
 
Mbunge pekee ambae ametoa wazo la kuunda jopo la majaji ni mimi. Hii inatokana na imani yangu ya kupata haki na ukweli. Sina sababu yeyote ile kumtetea Lowasa. Sina interest yeyote ile na Lowasa. Ndio kwanza nasikia kwako kuwa Jopo la Majaji laweza kumsafisha Lowasa. Nimetoa mawazo haya kwa nia njema kabisa nikiamini kuwa Serikali imelikosea Bunge kwa kutototekeleza maazimio na kusafisha wakosaji. Nikadhani kwamba, iwapo mihimili miwili ya Dola inagongana, mhimili wa Mahakama ndio utaweza kutenda haki.

Kumbe hili laweza kumsafisha Lowasa? Kwamba inawezekana kabisa mtu mwenye akili timamu akahisi kuwa mimi ninaweza kutumika kumsafisha Lowasa? Hata kwa mikakati ya kisiasa ya badae ni kosa kubwa mimi kutaka Lowasa atakate.

Mimi ninadhani huu mzimu wa Lowasa huu usizibe fikra huru. Haiwezekani hata kidogo watu tuache kufikiri kwa kumwogopa Lowasa. Ifahamike kuwa Maamuzi ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu Richmond ni maamuzi bora kabisa kufanywa na Bunge na ni maamuzi ambayo yamelipa Bunge heshima kubwa sana. Siwezi kuwa mmoja wa watu ambao wanataka heshima ya Bunge kuporomoka. Wazo la Jopo la Majaji sio Bahati mbaya. Bali ni hatua ambayo itaweka kila kitu wazi - kwani majopo haya hufanya kazi kwa uwazi kabisa na wakati mwingine kurushwa 'live'. Huoni jopo la Majaji litatufanye tujue yale ambayo Dokta Mwakyembe alisema hawakuyasema?

Hata hivyo, kama tunaamini kuwa jopo la majaji litamsafisha Lowasa, basi tusiunde! Nilidhani jopo la majaji ndio limwadhibu Lowasa na wengineo waliopanga kutuibia kupitia Mkataba wa Richmond.


Kama unaamini kuwa tume ya majaji itamsafisha Lowasa, uko tayari kufuta kauli na kutamka kwamba isiundwe? na je hili litafanyika lini?
 
Kama unaamini kuwa tume ya majaji itamsafisha Lowasa, uko tayari kufuta kauli na kutamka kwamba isiundwe? na je hili litafanyika lini?

Kuamini kuwa Mahakama itamsafisha Lowasa ni kitu cha ajabu sana. Ni ishara kuwa hatuna imani kabisa na Majaji na hivyo mfumo wa kutoa haki una matatizo makubwa.

Ninaamini haki na ukweli vinapatikana mahakamani. Sitafuta kauli ya kupeleka suala hili la Richmond kwa majaji. Mimi ninaamini Judicial Commission itatoa haki na Taifa litafaidika zaidi kuliko kuendeleza kurushiana mpira kati ya serikali na Bunge juu ya jambo hili kwa miaka 2 sasa.
 
Kuamini kuwa Mahakama itamsafisha Lowasa ni kitu cha ajabu sana. Ni ishara kuwa hatuna imani kabisa na Majaji na hivyo mfumo wa kutoa haki una matatizo makubwa.

Ninaamini haki na ukweli vinapatikana mahakamani. Sitafuta kauli ya kupeleka suala hili la Richmond kwa majaji. Mimi ninaamini Judicial Commission itatoa haki na Taifa litafaidika zaidi kuliko kuendeleza kurushiana mpira kati ya serikali na Bunge juu ya jambo hili kwa miaka 2 sasa.

Ukiangalia idadi ya majaji walioteuliwa na JK unathani Lowasa atapona ? au ndo sabau ukataka hili liendae mahakamani?
 
Ukiangalia idadi ya majaji walioteuliwa na JK unathani Lowasa atapona ? au ndo sabau ukataka hili liendae mahakamani?

Sijaangalia hilo. Kumbe majaji walioteuliwa na JK wanaweza kumbeba? Justice ni ndoto Tanzania, eti? Asante kunikumbusha
 
La mafisadi bwana kwa kuteteana hiyo mihela na kutaka kututawala kwa lazima sijui kutawasaidia nine.Tanzania ipo ,itakuwepo nasi tutaicha..
 
Bunge sio mahakama na wala sio jukumu letu kuamua kesi. Rushwa ni kosa la jinai. Tume ya Majaji itakayoundwa kwa mujibu wa Public Inquiry Act inaweza kumwelekeza DPP afungue kesi ya jinai dhidi ya mtu yeyote. Kamati ya Bunge haiwezi kuona mtu ana hatia maana sio mandate yake hiyo.

Hata hivyo nimesema, kama tunajiridhisha kuwa Mahakama itamsafisha Lowasa na wengineo katika kashfa mbaya kabisa ya Richmond basi wazo hili life. Maana iwapo tunaogopa mahakama kushughulikia suala hili baada ya Serikali na Bunge kugongana - basi kuna mashaka makubwa na 'hatia' ya Lowasa. Mimi ninaamini, kwa taarifa za kibunge kutoka kamati teule, Lowasa hasafishiki. Njia ya kumfikisha mahakamani ni Judicial Commission pekee. Bunge haliwezi kuamuru Lowasa kushtakiwa. HALIWEZI na halina nguvu hizo kikatiba. Mhimili wenye nguvu hizo ni mahakama na huko ndio haki hutendeka.

nijuavyo mimi mtu yeyote(incl wabunge) yule anaweza akapeleka ushahidi kwa dpp, na dpp kutumia huo ushahidi kuwashitaki watuhumiwa provided huo ushahidi ni wa kweli???

kwanini huo ushahidi wa tume ya mwakyembe usitumike na kupeleka kwa DPP?

kama huo ushahidi wa mwakyembe ulimfanya lowasa ajiuzulu, kwa nini dpp ashindwe kuutumia huo ushahidi kumfungulia kosa la jinai?

bunge sio mahakama lakini bunge lina uwezo wa kupeleka uchunguzi wao kwa dpp na dpp kuufanyia kazi
 
Sijaangalia hilo. Kumbe majaji walioteuliwa na JK wanaweza kumbeba? Justice ni ndoto Tanzania, eti? Asante kunikumbusha

Majaji wamejitahidi kutenda haki mara nyingi angalau ndio watumishi pekee tutakao sema anagalau hawajaingiliwa sana mimi nadhani kwa uzoefu wako wa kuwa bunguni endelea na hoja yako kama watamsafisha halitakuwa jukumu lako tena lakini watanzania si wajinga tena watajua ukweli na huo utakuwa ushahidi tosha wakuwashitakia wananchi ,simamia taratibu zitto
 
Majaji wamejitahidi kutenda haki mara nyingi angalau ndio watumishi pekee tutakao sema anagalau hawajaingiliwa sana mimi nadhani kwa uzoefu wako wa kuwa bunguni endelea na hoja yako kama watamsafisha halitakuwa jukumu lako tena lakini watanzania si wajinga tena watajua ukweli na huo utakuwa ushahidi tosha wakuwashitakia wananchi ,simamia taratibu zitto

Majaji wangapi wanasimia haki? walijua la wanafunzi wa chuo cha ustawi wa Jamii walivyonyimwa haki yao sababu tu walitetewa na wakili mwenye itikadi ya Upinzani? na wajua kuwa katika kesi hiyo Jaji wa kwanza alijiuzulu kwa kutotaka kutumiwa? hii inammanisha ni Majaji wachache sana wanao simamia haki bila kuingiliwa na Serikali
 
Mkuu Zitto,

Ninakubaliana kabisa na mawazo yako kwamba jukumu ya kuona mtu ana hatia au la ni la mahakama tu. Ndiyo maana Bunge baada ya uchunguzi hupendekeza kwa serikali hatua za kuchukua. Ni juu ya serikali kuamua wafanye nini. Weakness ya mfumo huo ndiyo kama tulivyoona serikali haijaweza kuwachukulia hatua wale wote ambao Kamati ya Dr. Mwakyembe iliwaona wana makosa.

Je, Mahakama inaweza kutenda haki iwapo akina Lowassa na wenzake wanaweza kufikishwa kwenye Jopo la Majaji?

Hapa inategemeana na mambo 2. Moja, je, Idara ya Mahakama iko Huru? Hapa nina maanisha je serikali haina mkono katika ku-influence hukumu za kesi ambazo zina-impact kubwa kwa viongozi wa juu walio madarakani?

Jambo la pili, ni nani ambaye ataandaa mashitaka? Ni huyu DPP Feleshi ambaye mpaka leo anagwaya kufikisha baadhi ya watuhumiwa mahakamani? Je, ni huyu ambaye anasema KAGODA ni ngumu, kwa madai kuwa wakipeleka kesi mahakamani watawaonea wale waliotumika tu na wale waliowatuma wataachwa huru. Hivi kweli DPP huyo ndiyo utamwamini aandae mashitaka? Je, ni huyu DPP aliyeandaa kesi fake za EPA, Owner wa Richmond na kesi za kina Mramba, Yona na Mgonja?

Kwa kifupi ni kwamba the public imeishakosa confidence kwa Jeshi la Polisi na Idara ya Mahakama na ndiyo maana kuna watu wanajichukulia sheria mkononi mpaka wanachoma moto vituo vya polisi.

Uliona mwenendo wa kesi ya Marehemu Ditopile (RIP) na matukio ya pale Mahakama Kuu ya Tanzania mpaka mtuhumiwa anapitishwa kwenye mlango unaotumika majaji tu. Bado unataka wananchi wawe na imani na mahakama.

Kama kweli tunataka haki itendeke reform inatakiwa kuanzia Idara ya Mahakama, Ofisi ya DPP (ikiwa ni pamoja na kumpunguzia nguvu za ziada alizonazo za kuamua kupeleka kesi mahakamani ama kutopeleka kulingana na yeye "anavyojisikia" - nimetumia neno kujisikia kwa kuwa sidhani kama kuna kipengele kinambana kisheria kwamba ikibainika aligoma kupeleka case ambayo ni valid anachukuliwa hatua gani ama kuna taratibu zipi zinatumika), Jeshi la Polisi na PCCB. Ndio maana kila kukicha ni lawama kwamba Polisi wameonea mtu fulani na wamemwachia mtuhumiwa fulani.

Kwa hiyo hoja yako ni nzuri sana, lakini mimi na wananchi wengine (inawezekana hata na wewe mwenyewe) tumepoteza imani kwa Idara ya Mahakama, Jeshi la Polisi, PCCB na Ofisi ya DPP. Those are key players ili haki iweze kutendeka, lakini ikitokea mmoja kati yao akawa na kasoro basi mfumo mzima wa kudai na kutoa haki unaingia kasoro, na haki haiwezi kupatikana kamwe.
 
Majaji wamejitahidi kutenda haki mara nyingi angalau ndio watumishi pekee tutakao sema anagalau hawajaingiliwa sana mimi nadhani kwa uzoefu wako wa kuwa bunguni endelea na hoja yako kama watamsafisha halitakuwa jukumu lako tena lakini watanzania si wajinga tena watajua ukweli na huo utakuwa ushahidi tosha wakuwashitakia wananchi ,simamia taratibu zitto

Unasema nini???... Ina maana hujawahi kuisikia the High Court Bazaar ambapo haki huuzwa kwa mwenye dau kubwa?... Umeshawahi kumsikia mtu anaitwa Fungamtama??... Hicho kifaa kikiingia mahakamni kutetea mtu basi majaji na mahakimu wanakua kama mbwa kwa chatu...usiulize kwa nini!

Mheshimiwa Zitto with all due respect this is a wrong move, kwako kisiasa na kwa taifa kiujumla. Ni kulazimisha kumclear Lowasa na mdudu ruba Richmond. Wenye macho wameshastukia hili dili linalotaka kuchezwa. Hao majaji wenyewe lundo waliochaguliwa na JK, wengi wao kawapendekeza Lowasa halafu unataka kutuletea sijui habari gani hapa.

Kama serikali na bunge wanapingana, wananchi tuna macho ya kujua nani wasanii na nani wamefanya maamuzi kwa maslahi ya taifa kati ya bunge na serikali kwenye kashfa ya Richmond.... adhabu za wasaliti wa taifa zitakua kwenye ballot box, si majaji watatu watakao wekwa sawa ili watuchezee tena akili. NAKUSIHI ULIDROP HILI WAZO LAKO LENYE HARUFU FULANI.
 
... Tume ya Majaji itakayoundwa kwa mujibu wa Public Inquiry Act inaweza kumwelekeza DPP afungue kesi ya jinai dhidi ya mtu yeyote.
Hivi hiyo sheria imekaa sawa kweli? Maana, iwapo majaji wataamua kumwelekeza DPP kufungua kesi ina maana watakuwa wameona ushahidi usio na shaka kwa mba mtu ni mkosa. Sasa hiyo kauli yao si itakuwa hukumu moja kwa moja, kwa sababu haiyumkini majaji waelekeze kufunguliwa kwa mashtaka halafy mahakama ikamuona mtu huyo aliyeshitakiwa kuwa hana hatia
 
Kwa ufupi sana naomba kukubali kutokubaliana na baadhi ya watu katika hoja hii.
Kwanza kabisa hoja hii imechanganywa changanywa hasa kwa kuingia kwa suala la Sakina, ambalo naona kama halihusiani kabisa na hoja ya Richmond. Kama kuna hoja ingeweza kuletwa jamvini kwa mahali mwafaka ikajadiliwa kwa kuungwa mkono ama kukosolewa kwa hoja. Hii imeonyesha wazi kwani hata baadhi ya wachangiaji wameiona kama vile Sakina yumo katika operesheni safisha Lowassa. Pamoja na kuwa naweza kutofautiana na Sakina kwa mambo fulani fulani (si ya msingi), hoja ya Richmond isichanganywe naye.

Kuhusu hoja ya msingi ya Majaji na kusafisha ama kutomsafisha Lowassa, nadhani mtoa hoja ana haki kutoa maoni yake japo alipaswa kuepuka kuchanganya mada na kuegemea kwenye hisia zaidi na alipaswa kutoa mifano kama hana ushahidi wa wazi wazi. Lakini pia ameonekana kuwa mwoga maana kama si ujasiri wa Zitto kujitokeza, wengi humu JF wasingejua hadi siku ya siku kwani baadhi humu huwa hawafuatilii mambo mengi kwa wakati.

Lakini pia, sidhani kwamba Zitto anaweza kukubali kubeba gunia la misumari katika upara wake, maana Lowassa ni mzigo mzito sana kwa sasa, japo wako wanaoubeba kwa gharama kubwa, gharama ambazo zitakuwa kubwa zaidi 2010-2015, kwani wapo wanaoweza kupoteza nafasi zao kwa kupokea kazi hiyo.

Kuhusu suala la majaji, nakubaliana na wengi humu JF kwamba inawezekana kuna taratibu nzuri tu kuundwa kwa jopo hilo, lakini hoja hapa si kusafishwa ama kutosafishwa kwa Lowassa. Naamini suaa la kusafishwa kwa Lowassa, Mkapa na wengineo ni gumu sana kwa sababu nyingi sana, moja ikiwa ni "ALAMA ZA NYAKATI" kwamba. Lowassa ama Mkapa wangekuwa na umri wa Zitto, Ngeleja ama Nyalandu wangeweza kujipanga na kufanya maajabu, lakini kwa sasa Wananchi watajiuliza, kama yalipita (ya Richmond) si apumzike? Kwani hakuna Watanzania kama yeye ili na "wao wale"? maana "kila zama na walaji wake", baada ya Mkapa, akaja Lowassa, sasa ni zamu ya mwingine "kula".

Tunao utamaduni wa ajabu wa kifikra, fikra za kihalifu fikra ambazo mhalifu akiwa maendeleo "hata ya kuwanunulia bia wenzake" anasifiwa kwa kuitwa "mjanja", "ana akili sana ya kutafuta".

Nitaendelea baadaye, lakini tujadili hoja bila kutanguliza kwanza matokeo ya HOJA yenyewe kabla haijaanza kuwasilishwa ama kujadiliwa. Kwa yaliyotokea nyuma hakuna anayeweza kubeba tenga la samaki waliochina na kutembea nalo kichwani akijua majimaji yanukayo yatamvujia. Wao wenyewe (Lowassa na wenzake) hawawezi kusimama mahali kama "Tarime", "Busanda" ama "Biharamulo" na kuhutubia jukwaani ama hata kuvinjari mitaani bila ulinzi mkali. Tumuombe Mungu atunusuru, lakini Lowassa akishika nafasi ya juu ya uongozi PATAKUWA HAPATOSHI.
 
Last edited:
Huyu bwana Lowasa ana roho ngumu kama ya PAKA! unajua paka hata ukimbamiza ukutani ukadhani amekufa ukaenda kumtupa polini unajidanganya, atakupa siku moja tu baadaye utamwona huyo anakuja nyumbani na kuomba chakula kama si kuiba jikoni iwapo alikuwa na tabia ya wizi.

Lakini mimi sishangai sana kwani hii ndo tabia ya vibaka wote hata wapigwe vipi si rahisi kukiri na kuomba radhi bali ataendelea kulalama kuwa anaonewa pamoja na ushahidi kuwepo. Dawa ya kibaka ni kumchoma moto na dawa ya paka mwizi kata kichwa halafu fukia ardhini. Na huyu jamaa dawa yake ni kumpeleka mahakamani afunguliwe kesi za wizi wa mali ya umma kwani kaiba sana, na kisha kutupwa selo akanyee debe ndipo hao akina Balile waandike vizuri labda na magereza zitaangaliwa na kuboreshwa.
 
Nakusanya data nitazimwaga hapa jamvini kuhusu huyu Lowassa,Mtu amechuma kiasi hicho haridhiki naona anachotaka ni kupa nafasi ya kulipiza kisasi kwa wapinzani wake,ila asome vizuri alama za nyakati kwani ameshashutukiwa hata na JK mwenyewe alipotaka awe Rais wa kipindi kimoja tu.
 
maskini ana ugonjwa wa tamaa anahitaji maombi makali akipona atajua tatizo lake haiyumkiniki binaadamu kujilimbikizia mali kiasi chake bila kukinai na pia kutamani uongozi kiasi hiki chake he needs help for sure the man is sick
 
Nakusanya data nitazimwaga hapa jamvini kuhusu huyu Lowassa,Mtu amechuma kiasi hicho haridhiki naona anachotaka ni kupa nafasi ya kulipiza kisasi kwa wapinzani wake,ila asome vizuri alama za nyakati kwani ameshashutukiwa hata na JK mwenyewe alipotaka awe Rais wa kipindi kimoja tu.

Hii ni stahili ya zamani sana ambayo ilitumiwa na wapinzani wa Kikwete kumtisha mkapa kuwa kina kikwete wanataka kugombea urais mwaka 2000 na ilibidi Apson afanye kazi ya ziada kumwambia kuwa hao wakina meja jenaerali Ngwilizi na Mangula ni waongo wakubwa, sasa inatumika tena kumfarakanisha huyohuyo jk na lowasa watu ambao no waanga wa mchezo huohuo mchafu.

Nakumbuka jambo hilo lilipelekwea JK atangaze hadharani tena mapema kuwa anmuunga mkono mkapa ata kabbla aya kipindi cha kuchukua fomu kuanza na hivyo nachukua nafasi hii kumkumbusha JK kuwa asiwasiiklize hawa wagombanishi wanaodhania kuwa umekwisha kusahau wewe walikufanyaaje
 
Back
Top Bottom