Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

Binafsi sipingi kwamba Lowassa alikuwa mchakalikaji mzuri (alipotaka kufanya kazi).Some may even say he was Kikwete's "policy wonk" whom such mediocre figures like Sumaye and Pinda may never dream to rank as.Some may even reason that the arrogance borne out of the knowledge of his "wonkness" contributed a lot to his demise, he saw himself above reproach and indispensable to an intellectual weakling of a president.

Wala, unlike many members here, sipingi kwamba Lowassa kwa kutopewa fursa ya kujitetea hakufanyiwa haki (I recall FMES called it "the rule of politics" as opposed to "the rule of law")

Ila naona muandishi kwa kujifanya hajui bin maamuma wa cardinal rules za uandishi/ sheria, mojawapo ikiwa suala zima la paradox ya anonimity na credibility.Katika uandishi wa habari / ripoti za aina hii, the more anonymous your source is the better chance of getting more information and even quality information, even rising to the level of classified information.People simply do not want to risk exposure and easily muddy their career waters to say nothing of creating enemies.So a certain level of anonimity is allowed in journalism to protect the identity of the whistleblower.

The problem with anonimity is credibility, or to be precise lack thereof.An anonymous source commands less credibility than a named one.And perhaps as our esteemed brother pointed out, the report was as much accomplishing "the rule of politics" as it was "the rule of law"

The bottom line, at least in principle if the practicality of the matter was deemed implausible, is that Lowassa could have seized his moment in parliament and brandished a resolute, fact based (if he was really in a position to do so) counter attack aimed at self exoneration.

He did not do that, either because it did not matter to him or because he had no ammunition (facts) to fire back.

So who are you to speak for he who could not speak for himself?
 
Ifahamike wazi kuwa simtetei Lowassa

Hapo Mwanakijiji umenichanganya kidogo,maana heading inasema "mtetezi mpya wa Lowassa" at the same time unasema humtetei.

Kwa maoni yangu naona Lowassa mwenyewe alijua kuwa hakuna cha kufanya and that his only defence was to say kuwa hakutendewa haki.Lets say, for example,ile report ya Hosea,kuwa Richmond ni safi ingekuwa ndio mwisho wa haya yote.Maswali mangapi yangekuwa yameachwa bila kujibiwa? Na tukumbuke madhumuni ya ile report ya Hosea ndio ilikuwa kum-exonerate Lowassa.JK was right kusema kuwa Lowassa kakutwa na ajali ya kisiasa,kwa sababu yeye as PM alikuwa ana muda mrefu sana wa kulirekebisha hili swala,lakini yeye aliamua kutumia shortcut ya PCCB.Sasa limemtokea puani,issue inageuka na kuwa tena hakupewa muda wa kujitetea.Mpaka leo hii hajatokea hata mmoja wao ku proove kuwa hawahusiki na Richmond,zaidi ya kusema kijuujuu tu.Kama alivyosema Pundit,alipata muda bungeni baada ya report kusomwa,lakini yeye akaamua kujibu mashambulizi kama vile yeye ni amateur kwenye haya mambo.Msabaha alifanya vizuri kuliko hata yeye.

Thats my take...
 
achaneni naye huyo mmeru,

yeye si aliamua kuzira kwa vile "watu" walikuwa wanautaka uwaziri mkuu?Ina maana bila Lowassa tanzania haiwezi kwenda mbele?Mbona huyo "mwandishi maalum" hataki kuonesha mapungufu ya huyo Lowassa?Kwa hiyo anataka kutuaminisha kuwa Lowassa was, and still is, a saint?
 
Nakubaliana na watu wote wanaosema EL was a right man for kikwete, serikali atleast ilikuwa active sio kama sasa imeibiwa, hiko kama haiko lakini tunaingia kwenye maadili hatuwezi kumuacha EL madarakani hata kama amefanya madudu ya makusudi kuliibia Taifa kwa kuwa alikuwa right man kwa kikwete.

Unless EL na RA waje mbele ya watu na kuwaeleza wananchofaamu kwenye RD ndo tutaacha kutuhumu kama mafisadi, watueleze ukweli badala ya kusimamia ibara ya 15:1 ya katiba ya CCM. Watangulize masirahi ya taifa na kutumbia RD ilikuwa ya nani na Dowarns ni ya nani, hicho ndo wananchi wanataka kupata na sio kutetewa kwa maneno yasikuwa na maana.
 
Mh!

Huyu mwandishi wa hii makala anadai hamtetei EL wakati amefanya hivyo kwa nguvu kabisa! Kukumbusha aliyofanya kama sehemu ya WAJIBU wake hakufanyi hiyo kuwa utetezi wa kilichotokea!

maadamu hii makali imetoka kwen gazeti la Rai, tunaelewa nini maana yake....
 
Nimeipenda hii mada kwa sababu kuu mbili

  1. Imekuja na hoja, leaving room for discussion

  • Inatazama pande zote mbili na sio ushabiki tu! Imefikia stage ata wale safi wanaitwa mafisadi..utabaki nani?
 
Nimeipenda hii mada kwa sababu kuu mbili

  1. Imekuja na hoja, leaving room for discussion

  • Inatazama pande zote mbili na sio ushabiki tu! Imefikia stage ata wale safi wanaitwa mafisadi..utabaki nani?

Mapambano,

Ni kweli hii hoja ina room of discussion lakini zidhani kama kweli inatazama pande zote mbili za shilingi. Kwa mtizamo wangu imeletwa kwa ajili ya kumuokoa EL kisiasa. Kama kweli EL ni kibangusilo mbona alikuwa na nafasi ya kujieleza bungeni ambako media yote ilikuwa imeelekzwa lakini hakufanya hivyo zaidi ya kudai kuwa kuna watu wanakitaka cheo cha uwaziri mkuu. Kwa upande wangu bungeni jamaa alikuwa nafasi lakini hakuitumia badala yake akaenda kusemea kijijini (jimboni ) kwao amboko amezoea kuwadanganya ili wampe kura na ambako yeye ni mfalme!!!
 
Tangu nianze kupitia hii JF nimekuwa nikiridhishwa na arguments na analysis zako, lakini kwa hili la EL, kwa kweli nashindwa kukubaliana moja kwa moja.
1. Mtu kufanya mengi mazuri hakuondoi haki ya kukosolewa pale unapokosea. Ukosolewaji wako utaendana na ukubwa wa dhara ulilotenda. Hivyo EL pamoja na hayo mazuri mengi aliyofanya bado haitosha kuoverlook upotofu na uharibifu alioufanya. Issue ya umeme sidhani kama ni jambo dogo kwa watanzania na uchumi wao na maendeleo yao.

2. EL kwa nafasi yake kama mtanzania tu wa kawaida alikuwa na haki ya kushiriki zoezi la kutoa taarifa kama alikuwa nazo ili kusaidia uchunguzi uliokuwa unafanyika. Lakini kama waziri mkuu na kiongozi wa shughuli za serikali, na hasa kwa kuzingatia kumbe ni swala alilowahi kulishughulikia, alikuwa na wajibu wa kufika mbele ya kamati na kueleza alichokijua na alichokifanya. Ni mara ngapi tumeona polisi wakifanya upelelezi kwa kuomba mwenye taarifa aende polisi kutoa? Ni mara ngapi upelelezi wa polisi umesaidiwa na raia wema ambao walijitolea kwenda mbele na kusema walilojua au kuona. EL alitakiwa afanye HILO tu na si zaidi kwa nafasi mbili alizokuwa nazo. Kama raia wa kawaida wa Tanzania na kama waziri mkuu na kiongozi wa shughuli za serikali.

3. Kama kweli EL alikuwa na maelezo basi alikuwa hana budi kuyatoa kwa watanzania wote na sio tu kwa watu wa jimbo lake la uchaguzi. Ni sababu ipi kabla Mhe. Spika hajawaonya kuhusu kusema sema kwao kulikomfanya akaona watu wa Monduli ndio waliokuwa wameathirika zaidi na kujiuzulu kwake na sio watanzania wote waliostahili maelezo, kwani swala la umeme lilikuwa haliigusi Monduli peke yake. Je, ni sahihi mtu akifikiria kwamba aliwasize up watu wa Monduli na akaona watamsikiliza bila maswali na sisi wengine huenda tungeuliza au kutaka maelezo zaidi.

4. Kwa kiasi fulani nakubaliana na hofu yako "Kwa utamaduni wa kumalizani tunaelekea wapi?" Hilo ni swali zuri na nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu kwani binadamu sote tuna mapungufu na hasa unapokuwa kiongozi iwe kwenye level ya familia, jamii au taifa. Ninachoamini ni kwamba familia, jamii au taifa hutoa hukumu kwa misingi fulani ambayo inakuwa inakubalika kwa uwiano mkubwa. Ndio maana kwenye jamii kuna makosa makubwa na makosa madogo. Vivyo hivyo EL amehukumiwa. Kosa alilofanya ni kubwa na limeathiri wengi na kwa kiasi kikubwa. Mbona alivyosaidia kushinikiza yule mtuhumiwa Nyari atoke jela watu hawakulalamika. Ni kwa vile liliwagusa wachache. Huenda ni wale tu waliokuwa kwenye sekta ya madini ndio waliojua athari ya msaada ule lakini wengine hatukujua au hatuathirika.

Ni mambo mengi yanafanyika ambayo si sahihi, ni mengi Mwl. Nyerere alikosea wakati wa uogozi wake, lakini hakuhukumiwa kwa ubaya kama EL. Ni nini umekosea na ni namna gani unajieleza au unajiweka ndiko saa zingine kunapelekea hukumu mbaya. EL alijiweka mahali pa (i) hakuna wa kumgusa (ii) kujipa uhalali (Sense of entitlement) ambako kulimfanya ashangae pale alipoulizwa kwani hajazoea au anaona hastahili kuulizwa na ndio maana akazira. Hiyo ni hali mbaya kweli unapokuwa kiongozi. Kiogozi ni lazima unyeyekea waliokuweka pale. Huu si ufalme, na huo nao siku hizi watu wanauliza ukifanya ujinga ujinga iwe sembuse uwaziri mkuu waliogawaiana kama njugu, ubunge ambao wengi wamepata kwa kununua?

Kufanya kwako mazuri hakukuepushi na dhahama ya kusulubiwa ukikosea. Ni kosa gani na ni adhabu ipi unastahili ndio issue itakayojadiliwa. Utendaji wako mzuri unaweza ukawa a good mitigating factor, but until we have turned everything upside down and have all the facts correct and proved ndipo hilo linaweza kuapply.
 
Let me put it very clear... mimi siyo mwandishi wa makala hiyo, nimeikopi toka Rai ya juzi! Sorry for the confusion.
 
Nakubaliana na watu wote wanaosema EL was a right man for kikwete, serikali atleast ilikuwa active sio kama sasa imeibiwa, hiko kama haiko lakini tunaingia kwenye maadili hatuwezi kumuacha EL madarakani hata kama amefanya madudu ya makusudi kuliibia Taifa kwa kuwa alikuwa right man kwa kikwete.

Unless EL na RA waje mbele ya watu na kuwaeleza wananchofaamu kwenye RD ndo tutaacha kutuhumu kama mafisadi, watueleze ukweli badala ya kusimamia ibara ya 15:1 ya katiba ya CCM. Watangulize masirahi ya taifa na kutumbia RD ilikuwa ya nani na Dowarns ni ya nani, hicho ndo wananchi wanataka kupata na sio kutetewa kwa maneno yasikuwa na maana.

What makes you think so? EL might have been the right man for Kikwete but not for this Tanzanians!

Mwanakijiji > who's mwandishi maalum - Rai?? this person could be even EL himself trying to clean up the mess! I just don't know what's wrong with us Tanzanians....we hear something and believe it with all our heart but the moment we hear something else we dont even reason we change our minds! Hivi haya tunayoandika kila kukicha ya kuwatetea watu ambao hata wenyewe hawawezi kujitetea ndio UZALENDO???

Haikuwa Lazima EL kuhojiwa na Kamati teule provided they had all the hard evidence they needed. Hata huyu EL mwenyewe analielewa hilo na ndio maana aliuchuna kimya akisubiri kuitwa mbele ya kamati teule....why couldn't he just walk over maana alisema ofisi za bunge ziko karibu sana na ofisi yake! Kamati ilikuwa open for anyone who could talk to them.....

Watetezi wa EL watakuja wengi tu lakini they wont make any substantial change unless huyo EL, na Muasia wake RA waje mbele na kuongelea kile wanachokijua kuhusiana na hili la Richmond/Dowans na hata mengine mengi waliowahi kufanya.

Huu utetezi hautoshi......
 
What makes you think so? EL might have been the right man for Kikwete but not for this Tanzanians!

Mwanakijiji > who's mwandishi maalum - Rai?? this person could be even EL himself trying to clean up the mess! I just don't know what's wrong with us Tanzanians....we hear something and believe it with all our heart but the moment we hear something else we dont even reason we change our minds! Hivi haya tunayoandika kila kukicha ya kuwatetea watu ambao hata wenyewe hawawezi kujitetea ndio UZALENDO???

Haikuwa Lazima EL kuhojiwa na Kamati teule provided they had all the hard evidence they needed. Hata huyu EL mwenyewe analielewa hilo na ndio maana aliuchuna kimya akisubiri kuitwa mbele ya kamati teule....why couldn't he just walk over maana alisema ofisi za bunge ziko karibu sana na ofisi yake! Kamati ilikuwa open for anyone who could talk to them.....

Watetezi wa EL watakuja wengi tu lakini they wont make any substantial change unless huyo EL, na Muasia wake RA waje mbele na kuongelea kile wanachokijua kuhusiana na hili la Richmond/Dowans na hata mengine mengi waliowahi kufanya.

Huu utetezi hautoshi......

Kuna mkakati wa magazeti ya mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata - Rostam Azizi wa kumsafisha Lowasa na kuwachafua wapinzani wake. Katika hili usishangae kuwa Lowasa na Rostam walipitia final draft kabla haijawekwa hapo kwenye gazeti la udaku la rai.
 
Jamani Nimeshasema Na Ni Mawazo Ya Wengi....sijui Mtakuja Na Mpya Gani Kumpa Tena Nafasi Kugombea Chochote..........katika Nchi Hiii...akae Kimya Aachane Na Nchi Yetuuu
 
Tatizo hasa ni njaa za waandishi ndizo zinawafanya kuwa wanafiki kwani hapo hawazungumzii nafsi zao bali matumbi yao.
 
Hata tusiposikiliza kile mwl. nyerere alisema juu ya lowassa, kiongozi gani asiyeweza hata kujitetea mwenyewe!! lakin angalia mtiririko huu wa matukio:

1.wakati mkataba tata wa buzwagi unasainiwa hotelin uk, lowasa alipitia uk akitokea paris.

2.Anahusishwa na richmond, alishindwa kuvunja mkataba kama alivyofanya kwa city water.

3.Alisafiri kwenda thailand kwa rafiki yake shinawatra eti kutafuta mvua ya kutengeneza, miezi michache baadaye rafiki yake anabainika kuwa mwizi na kuondolewa madarakani.

NI KWA NINI LOWASA KILA PALIPO NA DOSARI YEYE YUPO??? AU YUKO KARIBU NA MUHUSIKA AU KARIBU NA MAZINGIRA YANAYOLETA UTATA!

HAFAI KUWA KIONGOZI, HATA UBUNGE NI BUDI AONDOLEWE!!!
 
Hata tusiposikiliza kile mwl. nyerere alisema juu ya lowassa, kiongozi gani asiyeweza hata kujitetea mwenyewe!! lakin angalia mtiririko huu wa matukio:

1.wakati mkataba tata wa buzwagi unasainiwa hotelin uk, lowasa alipitia uk akitokea paris.

2.Anahusishwa na richmond, alishindwa kuvunja mkataba kama alivyofanya kwa city water.

3.Alisafiri kwenda thailand kwa rafiki yake shinawatra eti kutafuta mvua ya kutengeneza, miezi michache baadaye rafiki yake anabainika kuwa mwizi na kuondolewa madarakani.

NI KWA NINI LOWASA KILA PALIPO NA DOSARI YEYE YUPO??? AU YUKO KARIBU NA MUHUSIKA AU KARIBU NA MAZINGIRA YANAYOLETA UTATA!

HAFAI KUWA KIONGOZI, HATA UBUNGE NI BUDI AONDOLEWE!!!
 
Nimeipenda hii mada kwa sababu kuu mbili

  1. Imekuja na hoja, leaving room for discussion

  1. Inatazama pande zote mbili na sio ushabiki tu! Imefikia stage ata wale safi wanaitwa mafisadi..utabaki nani?

Naona ile mada yako imeunganishwa na ile ya SHY!
Kwi kwi kwi!
 
na mwandishi maalum (Rai)

WIKI hii nimesoma Habari kadhaa kupitia magazeti, na nimesikiliza nyingine kupitia redio, huku nyingine nikiziona kwa macho yangu.

Kati ya niliyoyasoma limo hili la kutaka aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ashitakiwe na wengine wanapendekeza afilisiwe.

Nimesoma hata kiongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM, akitokea huko Tanga, ameamua kusema Lowassa na mawaziri wote waliotuhumiwa wakajiuzulu wafukuzwe ndani ya chama.

Najua kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake, hivyo hawa wanaofanya hivyo wanautumia uhuru huo. Hata hivyo, nina kila sababu ya kuamini kuwa uhuru huo unapaswa kutumika vyema. Uhuru bila nidhamu unaweza kugeuka utumwa.

Fukuto, upepo na hali ya hewa tayari imechafuka. Neno ufisadi sasa limekuwa kifungua kinywa, chakula cha mchana na kinywaji wakipendacho wengi. Ni msamiati unaokua kwa kasi kubwa. Huko mitaani leo imefikia hata mwenye kumiliki line za simu mbili anaitwa fisadi.

Rais Jakaya Kikwete wakati anazungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam Februari, mwaka huu, alifafanua kwa kirefu kashfa ya Richmond. Alieleza kukerwa kwake, lakini kabla ya kuhitimisha akamtetea Lowassa. Akawambia wazee wa Dar es Salaam kuwa yaliyomkumba Lowassa ni ajali ya kisiasa.

Hii ndiyo hoja ninayotaka kuijadili leo. Msemo kuwa ‘Baniani mbaya, lakini kiatu cheke dawa’ au ‘mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni’, ndiyo msingi wa mjadala wangu.

Nilitaka kumjadili aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge, Dk. Harrison Mwakyembe, lakini pengine kwa kukaa kimya nimepata fursa ya kumfahamu, naye akapata fursa ya kukarabati kauli yake.

Mwanzo Dk. Mwakyembe alisema Richmond ni kampuni ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa na swahiba wake Rostam Aziz. Hapa ilikuwa wakati anawasilisha Ripoti ya Kamati Bungeni. Alisisitiza kuwa ilihitaji moyo wa uzalendo wa hali ya juu mtu kuwataja viongozi hawa wawili.

Hata hivyo, wakati anafanya majumuisho baada ya michango ya wabunge, Dk. Mwakyembe kidogo alibadilika. Matambo na mbwembwe japo hazikuisha, ila yalipungua. Kwa hakika alikarabati kauli yake na kusema Lowassa na Rostam hakuna popote walipotajwa na Kamati yake kuwa wamiliki wa Richmond.

Napenda kuamini kauli hii ya Mwakyembe aliyoitoa wakati wa majumuisho ndiyo yenye kusimama. Kwa kwaida wakati tupo jeshini ilikuwa tukiambiwa kuwa amri zote ni halali, ila askari anapaswa kutekeleza ya mwisho. Niazime busara hiyo, kukubaliana na kauli ya mwisho ya Dk. Mwakyembe juu ya umiliki wa Richmond.

Sasa sitajadili mkanganyiko uliotokea na kumfanya Balozi Fulgence Kazaura aikane Kamati kwa barua aliyodai kuwa hajapata kuwaeleza maneno yaliyomfanya Mwakembe na wajumbe wengine wa Kamati Teule waamini kuwa Richmond ilikuwa kampuni ya Lowassa na Rostam.

Nasema hili nalo silijadili tena, kwani Mwakyembe tayari amekwishaweka kumbukumbu sawa, ila jambo moja tu niliseme. Najiuliza na nadhani wapo wengi wenye kujiuliza juu ya mkanganyiko wa maadili hasa unapokuja utendaji wa Kamati hizi.

Kwamba nafahamu Dk. Mwakyembe ni mwanasheria aliyebobea na mwandishi mwandamizi, hapo ndipo nazidi kupata shida kidogo. Kaka yetu huyu amefundisha na anaendelea kufundisha Watanzania wengi wa rika mbalimbali.

Kwamba katika mafundisho yake amekuwa akisisitiza suala la kuaminiana na kulinda vyanzo (confidentiality and anonymity). Na kwamba Daktari huyu wa sheria anajua kuwa maneno ya mitaani wengine wanapenda kuyaita ‘ushu ushu’ (hearsays), kamwe hayawezi kusimama kama ushahidi mbele ya sheria.

Daktari wetu huyu ameamua kutunga kanuni mpya za uandishi na ushahidi mahakamani. Kwamba anonymity and confidentiality, kwake si muhimu tena na wala havina madhara kwa Kamati Teule nyingine zijazo, ikiwa ilitokea kwamba kweli aliumwa sikio. Kazaura tayari amekana kumuuma sikio, ila hili halijibiki.

Kwake daktari huyu, maneno ya mitaani anayoyaitwa kuumwa sikio, yana nguvu kuliko ushahidi wa kiapo! Namheshimu sana daktari huyu, na wala hapa simsimangi, ila najaribu kufikisha fikra zangu kwako wewe msomaji juu ya falsafa hii mpya.

Jingine ninalodhani halihitaji ujasiri kulisema ni hili la kutompa fursa ya kumhoji Waziri Mkuu, aliyejiuzulu ndugu Lowassa. Kwa hulka ya ubinadamu ni rahisi wajumbe wa kamati kujitetea, lakini hapo ndipo umimi (egoism) unathibitika.

Iwapo ningeazima maneno ya Biblia Takatifu, inasema mtende mwenzio sawa na utakavyo utendewe wewe. Na Biblia inasema kipimo hicho hicho ukitumiacho kumpimia mwenzio, ndicho kitakachotumika kukupimia haki yako mbele ya safari.

Hili nalo sipendi kulisemea sana kwani Jaji Mkuu mstaafu aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, Joseph Warioba, amelisemea vizuri. Hoja iliyotumiwa Kamati Teule kuwa ukubwa wa cheo cha Waziri Mkuu uliwazuia kumuhoji Lowassa inaacha maswali mengi.

Jaji Warioba anasema yeye akiwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, aliwahi kuhojiwa. Alikwenda mbali zaidi akafafanua kuwa hata Rais Ali Hassan Mwinyi, alipata kuhojiwa akiwa Rais.

Hapa ndipo pa kujiuliza. Ilikuwaje Kamati hii haikupata kumbukumbu hizi nyeti na kubaini kuwa kumuhoji Waziri Mkuu si jambo geni kwa Tanzania? Wapo wanaosema Kamati hii ilikuwa na ajenda ya siri, ila binafsi sipendi kuamini hivyo.

Nimesema tangu mwanzo kuwa masuala haya yamejadiliwa kwa kina na wadau mbalimbali. Ifahamike wazi kuwa simtetei Lowassa, Rostam wala Mwakyembe katika hili, ila nasimamia msingi wa hoja. Najiuliza nani msaliti kati ya Lowassa na hao waliomtenda au kutenda yaliyomfikisha alipo leo.

Hapo juu nilisema Rais Kikwete amesema yaliyompata Lowassa ni ajali ya kisiasa. Maneno ya Rais Kikwete, yanakwenda sambamba na hoja ya Dk. Ibrahim Msabaha, japo ilipuuzwa na Dk. Mwakyembe.

Msabaha alisema haya yamekwishatokea, lakini Bunge lijadili mwelekeo na hatima ya taifa siku za usoni, hasa yanapopaswa kufanywa maamuzi kwenye kipindi cha dharura.

Hoja hii wapo wenye kusema inaweza kushughulikiwa kwa kutumia utaratibu wa international shopping sawa na ilivyopendekeza TANESCO wakati wa mchakato wa kumpata mwekezaji wa umeme wa dharura.

Nasema hilo linawezekana, lakini kuna kila sababu ya kufikiria kuwa na utaratibu wa wazi jinsi ya kutatua matatizo ya kitaifa wakati wa dharura.

Ni kiongozi wa ajabu pekee, ambaye angeweza kukaa kimya kutokana na hali ya umeme ilipokuwa imefikia. Sheria ya manunuzi inataka siku 45 za kuitisha zabuni, ikiwa na maana kuwa zilihitajika siku 45 za kuitisha zabuni, huku taifa likizidi kutumbukia gizani.

Narudia, siwatetei Richmond katika hili wala yeyote awaye, ninachojadili ni hoja ya utaratibu wa kutumika wakati wa dharura utakaokubalika kwa jamii yote ya Watanzania pasipo mikwaruzano.

Watanzania tu wepesi wa kusahau mambo. Sitashangaa kukuta hata wakazi wa Kahama na Shinyanga nao wakiwa kwenye mkumbo. Lowassa aliyesifiwa kama mkombozi siku zilizopita, leo ndiye tunampiga mawe na kupendekeza asulubiwe.

Wananchi wa Kahama na Shinyanga Lowassa akiwa Waziri wa Maji na Maendeleo alidiriki kutofautiana na Wamisri kwa ajili yao kuvuta maji ya Ziwa Victoria kutoka Mwanza kwenda Kahama na Shinyanga. Ilihitaji kiongozi mwenye uwezo wa kufanya maamuzi, kitu alichofaha Lowassa na leo maji yapo Shinyanga!

Kama si Lowassa, viwanja vya mnazi mmoja vingekuwa maghorofo ya akina Baghdad. Tunajua Lowassa alivyosimama kidete bungeni mwaka 1994, na kuamuru uzio wa mabati uvunjwe uliokuwa umezungushiwa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam.

Lowassa huyu huyu alifuta umiliki wa viwanja vya tajiri mmoja anayetamba jijini Dar es Salaam, ambapo leo ndipo yamejengwa majengo ya PPF, International House na majengo mengine kadhaa.

Lowassa huyu huyu aliwafukuza nchini kampuni ya City Water mwaka 2005, waliposhindwa kutimiza masharti yaliyokuwamo kwenye mkataba. City Water walikwenda mahakamani, lakini hasilani hawakushinda kesi. Wakatakiwa kuilipa Serikali ya Tanzania sh bilioni 15.
Ni Lowassa huyu huyu aliyesimamia ujenzi wa shule za sekondari za kata. Hoja kwamba hazina walimu ni sahihi, lakini lipo swali la kujiuliza. Hivi kipi bora, kutokuwa na vyote viwili; shule na walimu au kuanza na kimoja?

Wapo wenye hoja sahihi kabisa kuwa Serikali ingeanza na kufundisha walimu kabla ya kujenga shule, lakini walimu hawa hawa iwapo wangehitimu na kukosa ajira, hoja hii hii ingegeuzwa na kudaiwa kuwa Serikali ilipaswa kujenga shule kwanza kabla ya kufundisha walimu.

Kwamba shule zinapokuwapo, kasi ya mahitaji ya walimu inakuwa na mashiko (real) badahala ya dhahania (imaginary). Hakuna safari isiyokuwa na hatua ya mwanzo.

Ni Lowassa huyu huyu aliyesimamia chakula cha njaa kikasambazwa kila tarafa, kata hadi kijiji. Ni Lowassa huyu huyu aliyepunguza foleni jijini Dar es Salaam kwa utaratibu wa njia tatu. Kwamba leo karibu barabara zote za jiji la Dar es Salaam zinapanuliwa kwa maelekezo yake.

Nimetangulia kusema kuwa kwa kipindi kirefu sikuweza kuandika makala yoyote kutokana na mazingira iliyowasilishiwa Ripoti ya Richmond. Kwamba mwanzo Dk. Mwakyembe aliamua kuwaeleza Watanzania kuwa Lowassa ni fisadi (by implication), lakini wakati wa majumuisho akakarabati kauli yake.

Hili la kukarabati kauli yake ndilo lililonifunua macho. Nikaanza kujiuliza maswali mengi. Nikajiuliza Dk. Mwakyembe alishindwa nini kutoa ufafanuzi huu kwamba Lowassa habanwi kwa ufisadi bali kwa uwajibikaji wa pamoja kama msimamizi mkuu wa shughuli za serikali, pale Lowassa alipojieleza na kufafanua alivyoonewa.

Dk. Mwakyembe alipobaini kuwa Lowassa alikuwa hajaisoma vyema ripoti hiyo kwa nini hakusimama kuweka kumbukumbu sawa kuwa hahusiki katika ufisadi bali kushindwa kwake kusimamia watendaji?

Kwamba Mwakyembe akiyajua hayo, alikaa kimya kwa siku nne mfululizo wabunge nao wakajadili hoja iliyopotoshwa, huku akijua kuwa wabunge wanajenga hoja katika dhana isiyo sahihi, hadi wakapendekeza Lowassa anyongwe, afilisiwe na matusi ya kila aina, ni aibu!

Mwakyembe alishindwa nini kusimama katikati ya mjadala na kuomba mwongozo wa Spika akafafanua hayo aliyoyasema kwenye majumuisho kwa nia ya kuepusha wabunge wasijadili hoja isiyo sahihi? Hapa kuna namna!

Lowassa ameonyesha uungwana wa hali ya juu. Yeye ameamua kujiuzulu wadhifa aliokuwanao. Ingawa jamii imekwishaamini hayo yaliyosemwa juu yake, bado anayo fursa. Alipokuwa Monduli, alieleza mchakato mzima ulivyokwenda na nani alifanya nini. Dk. Ibrahim Msabaha na Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika, hadi kesho hawajawahi kujibu hoja za Lowassa. Wanajua walichofanya.

Nimalizie makala hii, kwa kuchavusha fikra zetu. Rais Kikwete amesema yaliyomkuba Lowassa ni ajali ya kisiasa. Naamini Lowassa alipokuwa akifanya maamuzi mengi kati ya niliyoyataja hapo juu, tulimshangilia na kumsifia kama kiongozi shupavu.

Najua fika Tanzania ina kiu ya viongozi wenye kuthubutu. Viongozi wanaoweza kufikiri na wakatenda bila hofu. Lowassa ni mmoja wao. Siwezi kumsemea, natumaini yeye anayo maelezo mazuri katika hili, ila kuna kila dalili kuwa hakutendewa haki hata kabla ya Kamati Teule kuundwa. Swali ni je, utamaduni huu wa kumalizana unatupeleka wapi?
Mzee Mwanakijiji umenikuna, ingawa nimechelewa kuona taarifa yako hii nzito. Nimesoma kwa makini makala ya kumtetea Lowassa. Haisemi kipya, ni bla bla bla zile zile za akina Balile, Mhingo Rweyemamu, Manyerere na Bagenda zinazochapishwa kwenye gazeti la RAI ambalo kirefu chake ni Rostam Agency for Information na magazeti mengine mengi mapya yaliyoanzishwa na Lowassa, Karamagi na Rostam. Swali: ikiwa Lowassa aliona kaonewa, kwa nini alikimbilia kujiuzulu? Jibu jepesi ni kuwa alijua kuwa angeng'ang'ania kwenye Uwaziri Mkuu, Dk. Mwakyembe na timu yake wangelimraruararua. Vilevile nataka kujua kama Lowassa alikuwa na washauri wazuri wa sheria. Inashangaza kuwa Waziri Mkuu ambaye ni Mtawala, analilia haki ya kusikilizwa na subordinate body, yaani Kamati Teule ya Bunge. Forum yake ilikuwa Bunge ambalo hakutaka kulitumia. Lowassa ajue kuwa kadiri wapambe wake wanavyoandika makala za kumtetea kitoto-toto, ndivyo wananchi tunavyozidi kukasirika na kutamani tumfunge huyo jamaa kutokana na uroho wake wa "dili". KUNDADIDEKI! Ijabu
 
Mwandishi wa makala hii kweli ameandika kitoto.
Anampa credit mtu kwa vitu alivyotakiwa kufanya kama wajibu wake!Na alitakiwa kuwa mwema siku zote ndio yasingemkuta yaliyo mkuta.
Yeye alitaka kuwa smart kubana wengine na kuwa mkali (vizuri) ili ku win trust kwa wananchi waamini kuwa ni safi na ndio wale kiulaini (mbaya).
Ripoti ya Mwakyembe iko crystal clear sijuhi mwaandishi wa makala hii anazungusha maneno kiasi cha kunifanya nihisi katumwa na mtuhumiwa au mtuhumiwa mwenyewe akaandika.
Anadai hatetei wakati hata ukimpa mtoto wa shule ya msingi asome atasema nani mwandishi anamtetea au what is the bottom line of the story.
Ametoa reference kuwa kuna viongozi waliojiwa nyuma ,je issue zinafanana vp na je kwa kuwa walihoji huko nyuma ndio sahihi kwa siku zote za mbeleni ?kama kufanya kwao hivyo kulionyesha kuharibu uchunguzi na wao wafanye hivyo,au kila virivyo fanyika nyuma ndo good approach.
Kwani tume ilikuwa ni ya kumchunguza Waziri mkuu au kampuni ?
Mawili yaliopo kama hana maslahi na kampuni hiyo basi ni mzembe mkubwa kuipatia serikali maskini hasara na hastahiki hata ujumbe wa nyumba 10 /10.Ila ukiangalia with naked eyes hata bila microscope uhusiano wa hao viongozi na kampuni ya sasa na viongozi wao ni wazi si wazembe bali wana maslahi na kampuni.
Mwisho alikuwa na nafasi ya kujitetea hata bungeni ila hakuwa na la kujitetea .
 
Kwani kumtetea kuna kosa gani hasa ikiwa una uhakika kaonewa? Unataka ajisemee mwenyewe kwani hujui jinsi ushahidi wa second person ulivyo na nguvu kuliko wake mwenyewe?
Niliwahi kuandika na sasa naandika tena iko siku wote mtaona aibu mtakapojua kilichotokea!!!
 
Back
Top Bottom