Lowassa anasafishwa!

Naomba msome hii ArticleDAWASCO wamkataa Mkurugenzi wao...

2008-03-22 09:41:24
Na Mashaka Mgeta


Wafanyakazi wa Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO), wamemtaka Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wao, Bw. Alex Kaaya, wanayedai kuwa `aliwekwa` madarakani na aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, aachie ngazi kwa kushindwa kuendeleza kampuni.

ina maana utaratibu wa ajira haukufuatwa? kama haukufuatwa nadhani wanahoja ila wafuate taratibu kama walivyoshauriwa


...``Alituahidi kutupatia viwanja kwa kila mfanyakazi, kufanya mikutano kila baada ya miezi mitatu, kutuletea maisha bora ili tumudu kuwasomesha watoto wetu, hajatekeleza hayo yote,`` alisema.

kama huyu mheshimiwa aliahidi haya basi alilikoroga mwenyewe sasa umefika wakati wa kulinywa

...``Hata hivyo, Bw. Nkakatisi, aliwataka wafanyakazi hao kufuata sheria, kanuni na taratibu, ili kupata suluhu ya kero zinazowakabili.

Bw. Nkakatisi, aliyekabidhiwa risala ya wafanyakazi hao, alisema hatua yoyote itakayokuwa kinyume cha sheria, kanuni na taratibu zilizopo, itaashiria vurugu na hivyo kuwafanya wasifikie malengo yao...

SOURCE: Nipashe
imetoka kwa Nipashe 22/03/08

nadhani ni ushauri makini
 
Kaaya,why cant you apply LOWASALISM SYSTEM?Hapo moto umekwishawaka.Na kwa taarifa yako huo moto hauzimiki tena,jiondokee mwanawane kabla hatujakuingiza katika ufisadi.Unatuletea ahadi kama za JK,wewe kwa sababu tunakumudu sio kama JK,achia hiyo nafasi mapema.
 
Kaaya,why cant you apply LOWASALISM SYSTEM?Hapo moto umekwishawaka.Na kwa taarifa yako huo moto hauzimiki tena,jiondokee mwanawane kabla hatujakuingiza katika ufisadi.Unatuletea ahadi kama za JK,wewe kwa sababu tunakumudu sio kama JK,achia hiyo nafasi mapema.
 
Mimi Sidhani kuwa kila kilichofanywa na Lowassa si sahihi,lahasha yako mambo ambayo yamefanywa ni sahihi na kwa mujibu wa sheria.Kinachopingwa hapa ni mtu ila si utaratibu kwa maana ya kuwa Waziri wa Maji kwa nafasi yake ndiye mwenye Mamlaka ya kumteua Mkurugenzi wa DAWASCO.Tatizo ni kanuni,sheria na taratibu zilizopo zaweza kutoa mwanya wa kuchagua mtu ambaye ni swahiba wa Waziri si maanishi kuwa Kaaya ni swahiba wa Waziri.

LLazima tukubali kuwa moja ya malalamiko ni kuwa Wasomi wanakua juu,ili si tatizo lakini ni kwa kiasi gani Bwana Kaaya anaintergrate watu wote ktk system.Kutobagua huyu ni msomi na huyu si msomi ndani ya DAWSCO ni lamsingi.Anachotakiwa kufanya si kunyanyapaa wasiosoma bali kuwa nao bega kwa bega ili kuweza kufikia lengo la DAWASCO.

Yako mambo mengine ambayo yanadaiwa na watumishi lakini si haki kimsingi pengine Kaaya aliyasema hayo ktk kubuild good relation with his staffs.Si mbaya na ata kama angefanikiwa basi hali ya mambo ingekuwa mswano,kwani DAWASCO hawahusiki ktk kutoa viwanja isipokuwa alikuwa anataka kufanya kama motivation kwa watumishi.

Suala la makato ya kisheria ili ni suala muhimu sana na ni wajibu kuhakikisha makato yote ya watumishi yanakwenda yanakotakiwa.Nimeshuhudia sehemu nyingi makato haya hayapelekwi ipasavyo.Kwanza wahasibu wanatakiwa kuwa makini ktk ili ili kuhakikisha kuwa malipo yanakwenda sehemu husika.

DAWASCO wanatatakiwa kujidhatiti ktk kufuatilia vyanzo vyake vya mapato na kuzuia mianya yote ya rushwa ya wafanyakazi wake jambo ambalo linaipunguzia mamlaka mapato na hii inaweza ikasaidia kulipa makato ya kisheria kwa wakati.

Kaaya anatakiwa kuwa na timu iliyokuwa adilifu ili kuweza kuongeza Imani kwa watumishi na kwa Umma.Nadhani uwajibikaji si jambo la kuepa hivyo basi ni lazima Kaaya awajibike kwa kile alicho kifanya lakini tatizo lililokubwa ni kwa kiasi gani taarifa iliyopo ni sahihi.Ili ni suala la kufanyia kazi.Na ikiwa ni KWELI ANATAKIWA AWAJIBIKE .

Nawasilisha.
 

....WANABODI..huyu kaaya hana neno ila ana onewa tu...kama tukiamua kufanya kila kitu ni siasa tutapoteza watendaji wazuri tu...

kwa nini kaaya amefikia hapo???

..vision ya kuibadili dawasa..ilihitaji wasomi ambao dawasco haikuwa nayo...asilimia 80% ya wafanyakazi aliowakuta pale walikuwa hawajafika form four....alichofanya ili reform ifanikiwe aliongea na world bank ili kupata pesaza kuwapunguza wasio kuwa na tija.....!! [makusanyo ya hawa wazee yalikuwa hayazidi milioni 600 kwa mwezi against budget ya dawasco ya milionoi 1200 kwa mwezi.. HILO KISIASA NI KOSA NAMBA MOJA,KWA KUWA TUNAPENDA KUWAFURAHISHA WATU BILA UKWELI....

aliajiri vijana wadogo wachache wenye elimu ya chuo kikuu[ndio wanaoitwa hawana uzoefu]....lakini hawa vijana kwa kushirikiana na wale wazoefu wacheche wenye elimu waliobaki wameweza kuifanya dawasco chini ya huyu kaaya ambaye hawa wazee hawamtaki kufikia makusanyo ya zaidi ya MILIONI 2,000 KWA MWEZI...

nafikiri kwa kuangalia wanaenda vema na kama watapewa ushirikiano watafanikiwa ..kumbukeni perfomance ya dawasco ya kaaaya inazidi city water mara dufu ..na tukumbuke hawa waswahili hawalipwi dolas kama city water ...makusanyo ya city water yalikuwa maximum milioni 1,000 kwa mwezi ..ikiwa na maana pamoja na kulipwa vema bado kila mwezi walikuwa wanabalkiwa na NAKISI....

TUACHE ku entertain siasa kwenye biashara...la tutaishia kufukuza watendaji wazuri..na kinachotokea ni kuwa wale wafanyakazi waliopunguzwa wanashirikiana na hawa viongozi wa TUICO kumuondoa huyu....kaaya...
 
.
.
.

``Alituahidi kutupatia viwanja kwa kila mfanyakazi, kufanya mikutano kila baada ya miezi mitatu, kutuletea maisha bora ili tumudu kuwasomesha watoto wetu, hajatekeleza hayo yote,`` alisema.


Alidai kuwa, wafanyakazi wa zamani wanalipwa mishahara duni na kunyanyaswa, wakati wasomi wasiokuwa na ujuzi wanapata uongozi na mishahara mikubwa, hivyo kuwa `vinara` wa unyanyasaji.
.

SOURCE: Nipashe
imetoka kwa Nipashe 22/03/08[/QUOTE]

....kwa kuangalia hawaka ndugu zangu mimi naona tuhuma zote zinatawaliwa na chuki walizonazo wafanyakazi wenye "UZOEFU KAZINI"..Dhidi ya wasomi......inawezekana hawaoni sababu ya mtu aliyeajiriwa pale ana MBA au BSC eng...walipwe mshahara mkubwa kuliko fundi mchundo anayeweza kufanya baadhi ya kazi za engneer..lakini nachelea kusema hizi chuki za wasomi na wasiosoma zipo kwenye karibu mashirika yote ya zamani.....kuna vijana hadi hufanyiwa uswahili na kukimbia kazi..wengine hususiwa ..lakini huwezi kutumia tuhuma za aina hii kumuondoa mtendaji!!!!

..hayo maisha bora ya kununuliwa viwanja wanayodai...miaka yote wamefanya kazi hawajanunuliwa na viongozi waliopita..saasa wanategemea huyu kiongozi awanunulie viwanja ndani ya miaka mitatu ya utendaji?!!! nadhani ni bora wakaundiwa saccos ili kama wanaweza wakopeshwe wanunue viwanja bila riba...WAKUMBUKE WAO KUNUNULIWA VIWANJA INAWEZEKANA LAKINI ITABIDI GHARAMA ILIPWE NA WATUMIAJI WA HUDUMA ...WATALAZIMIKA KUPANDISHA BILI MARADUFU..ILI WOTE WAPATE VIWANJA[ viwanja kwa wafanyakazi takribani 1,000 na bei ya kila kiwanja inakaribia 5 million.hiyo ni bilioni 5 ..yaani makusanyo yao ya miezi 3...]

hii hali ya chuki dhidi ya wasomi ndio iliyofanya benki kama crdb walipotaka kutekeleza reform zao ..wao waliondoa wafanyakzi woote wa zamani wakaajiri upya vijana wenye degree na ndipo walipoanza kupata faida...lakini as long as huko dawasco bado kuna wafanyakazi wa zamani ..hizi chuki zitaendelea ...watu hawataki kudhamini elimu za watu ...wanaona ni rahisi tu kuwa graduate!!!!
 
---Ni sababu zipi zinawapelekea viongozi walio jiuzulu kwa kashfa kujiandalia mapokezi kwenye majimbo yao? (Nina imani kuwa wanaridhia maandalizi hayo)

--- Faragha gani wanapata mioyoni mwao kwa kupigiwa vigelele na akina mama walioshika majembe ya mikononi na ndoo za maji juu ya vichwa (wengine bila hata kata), hali yaliyowapelekesha kujiuzulu ni udhalimu na shutuma za uhujumu wa Taifa?

---Ni tatizo lipi la kisaikolojia ambalo binadamu anakuwa nalo la kuweza kukubali vifijo, ndelemo na shangwe za pongezi kutoka kwa wananchi wasio na uelewo (na kama wana uelewo, basi ni sahihi kusema kuwa ni vifijo na ndelemo vya kinafiki) wa lile waliungalo mkono na kulishangilia? Kama wana uelewo, je, binadamu huyo anafarijika vipi na unafiki huo?

---Kwa kuwa mimi naona mapokezi hayo ni aibu.. je, ni nini kifanyike kuelimisha jamii hizi, yakwamba - kusherehekea kujiuzulu kwa kiongozi ni jambo la kukubalika, lakini kushereheka na kiongozi aliyejiuzulu na kumpongeza kwa vifijo na ndelemo si jambo la kukubalika?

---Kama unaona kushereheka na kiongozi aliyejiuzulu kwa kashfa ni jambo la maana au sijambo la aibu naomba unipatie maelezo. Asante.

---ifuatayo ni nakala iliyovuta hisia zangu hapo juu......

`Mapokezi ya Chenge aibu`

2008-05-10 11:37:18
Na Pendo Fundisha,PST, Mbeya


Baadhi ya wakazi wa Mbeya na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa, wamelaani mapokezi ya Mbunge wa Bariadi Magharibi, Bw. Andrew Chenge (CCM) na wanachama wake kwa madai kuwa yanakidhalilisha chama hicho na kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete.

Walisema hakuna sababu za msingi za kuwafanyia mapokezi makubwa watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, kwa kuwa kwa kufanya hivyo wanazorotesha juhudi za chama hicho na serikali katika vita yake dhidi ya ufisadi.

Mapokezi ya aina hiyo ni ya pili kufanyika baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wake baada ya kuhusishwa katika kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond iliyodaiwa kupata zabuni kwa njia ya utata.

Baada ya kujiuzulu kwake Februari mwaka huu, Bw. Lowassa alifanyiwa mapokezi makubwa jimboni kwake Monduli, mkoani Arusha.

Bw. Chenge alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu mapema mwezi uliopita, baada ya kufichuliwa kwa habari kwamba anamiliki zaidi ya Sh. Bilioni 1.2 ambazo zimehifadhiwa katika akaunti moja nje ya nchi. Fedha hizo zinadhaniwa kuwa zilipatikana kifisadi katika \'dili\' la ununuzi wa rada ghali ambayo kimsingi Tanzania ilikuwa haiihitaji.

Baada ya kujiuzulu Bw. Chenge wiki hii alikwenda jimboni kwake na kupokelewa na msafara mkubwa wa magari na wapiga kura wake wakiwemo makada wa vyama.

Wakizungumza juzi jioni walipokuwa wakiangalia taarifa za habari katika televisheni mbalimbali zilizokuwa zikionyesha mapokezi hayo yaliyohudhuriwa na baadhi ya makada wa CCM wakiwa katika makundi, walidai huo ni udhalilishaji wa chama hicho na viongozi wake.

Wakiongea na PST baadhi ya viongozi hao walidai kuwa imekuwa ni kejeli kwa serikali pale viongozi wa ngazi za juu waliokumbwa na tuhuma za ufisadi na kujiuzulu na kukimbilia katika majimbo yao kujisafisha.

``Kwa kweli wananchi, hususan wanachama wa CCM mnapaswa sasa kugeuka na kuangalia ni nini kinachofanywa na viongozi wa ngazi za juu, na si tu kujipanga katika barabara na ofisi za chama kwa ajili ya mapokezi ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Mnajidhalilisha kwa kunufaisha mafisadi na nyinyi wananchi wenye maisha duni mkizidi kupandishiwa gharama za maisha,`` alisema kiongozi mmoja.

Walisema wananchi walikuwa wakisubiri kauli ya serikali kupitia kwa Rais Kikwete dhidi ya hatua za makusudi zinazochukuliwa dhidi yao, lakini kila kukicha wanawasikia watuhumiwa wakikimbilia majimboni kwao na vyama vyao vikiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika mapokezi na kwenye mikutano ya hadhara.

Naye mwananchama wa CUF, mkazi wa kitongoji cha Majengo, Bw. Augustino Amani, alisema serikali ilipaswa kufumbua macho na kuwaeleza wananchi hatma inayochukuliwa dhidi ya watu wanaotuhumiwa na ufisadi.

Alisema kwa sasa serikali inapaswa kuwa wazi kwa wananchi na si kuwanyonya kwa kuwapandishia gharama za maisha kutokana na gharama za bidhaa hususan, mafuta, mazao ya chakula kama mahindi na kumfanya mwananchi mwenye kipato cha chini kushindwa kumudu kupanda kwa gharama hizo.
Source links: http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2008/05/10/114077.html
:http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/05/10/114093.html


SteveD.
 
Ni moja ya viashiria kuwa watanzania bado hawaelewi kitu, wanahitaji kuelimishwa. Wanasiasa kambi ya upinzani wana kazi ya ziada. Yaani Bariadi wamenishangaza kweli as kwa kujua kuna UDP wengi basi mambo yangekuwa tofauti na wangeweza kumhoji vijisenti na angeshindwa kujieleza wangempiga chini kuwa sio mbunge wao;badala ya kuwawakilisha anawaaibisha. Kazi ipo 2010
 
Ni moja ya viashiria kuwa watanzania bado hawaelewi kitu, wanahitaji kuelimishwa. Wanasiasa kambi ya upinzani wana kazi ya ziada. Yaani Bariadi wamenishangaza kweli as kwa kujua kuna UDP wengi basi mambo yangekuwa tofauti na wangeweza kumhoji vijisenti na angeshindwa kujieleza wangempiga chini kuwa sio mbunge wao;badala ya kuwawakilisha anawaaibisha. Kazi ipo 2010

Mama, nakuunga mkono kabisa....Upinzani wasipo target kuelimisha wananchi kama hao, sidhani kama maendeleo tunayoyataka yatatufikia..... hakika hii ni strong case ya kuonesha kuwa jamii zetu na pahala pengi (samahani, ngoja tu nitumie hili neno) ni ma-mbumbumbu.

I am sure, miongoni mwa wale walioenda kwenye mapokezi hayo siyo wanachama au makada wa CCM tu, lazima kulikuwa na wale neutrals......bali nafikiri walipelekeshwa kushiriki kwenye mapokezi hayo kwa imani za kimshikamano wa kiukoo, kikabila na kijamii ......na nina imani ni wengi, upinzani ought to look and capitalize on events like these.... nikiwa mtu ambaye niko neutral na vyama, i think it's right to point at such opportunity and discrepancy, i'm a strong believer wa kuongeza nguvu ya upinzani kama njia mojawapo ya kuleta sound checks and balances kwenye serikali yetu.

SteveD.
 
Ngosha,

Si umesikia Katibu Mkuu akisema ni ruksa kuandamana?

Lakini kama nilivyosema awali kwenye ile thread ya divided perspective, what is wrong huko vijijini? au ni vitisho kutoka kwa viongozi na woga wa wananchi ulioambatana na "unyonge na Umasikini" ndio unafanya Wananchi waendelee kuunga mkono "watuhumuwa" wa Uhujumu uchumi?
 
Rev. Kishoka,

Ajabu kubwa wakiandamana Machinga serikali nzima inatishia kufanyiza lakini maandamano ya kuwafariji Mafisadi yanaungwa mkono na jeshi letu...
Ebu tujiulize hicho kibali cha kuandamana kumkaribisha fisadi kilitolewa na nani ikiwa Fisadi kwa maana ya matumizi ya neno hili ni Adui wa wananchi.
Fisadi = Mhujumu uchumi
 
Rev. Kishoka,

Ajabu kubwa wakiandamana Machinga serikali nzima inatishia kufanyiza lakini maandamano ya kuwafariji Mafisadi yanaungwa mkono na jeshi letu...
Ebu tujiulize hicho kibali cha kuandamana kumkaribisha fisadi kilitolewa na nani ikiwa Fisadi kwa maana ya matumizi ya neno hili ni Adui wa wananchi.
Fisadi = Mhujumu uchumi

Tuna sirikali ambayo imeshindwa kazi iko tayari kuwadhalilisha wananchi wanaotaka kuandamana ili kudai haki ya kujiingizia kipato halali, wakati huo huo haiko tayari kuzuia mapokezi ya kishujaa ambayo hayastahili kwa fisadi aliyewafisadi Watanzania na kujipatia mabilioni ya shilingi kwa njia za haramu.
 
Mbeya residents decry grand reception for graft suspect

2008-05-10 11:00:52
By Pendo Fundisha, PST, Mbeya


Residents and leaders of different political parties in Mbeya Region have condemned the high-note receptions accorded to former Infrastucture minister Andrew Chenge by members of Chama Cha Mapinduzi (CCM) in Mwanza and Shinyanga regions as an affront to President Jakaya Kikwete`s efforts to combat corruption.

The views were aired by the residents after watching televised programmes by a number of stations of the grand receptions accorded to the former minister.

Chenge resigned last month over allegations of corruption and abuse of office.

Speaking to PST in separate interviews here, most of them said the high-note reception granted to Chenge in which both low and high cadres of CCM were involved in the two regions was a humiliation to the ruling party`s leaders who are dedicated in the fight against corruption and in exposing culprits in its rank and file.

They unreservedly blasted the current habit in which leaders suspected of corruption and abuse of office retreated to their constituencies ``to manipulate their electorate, most of whom are not very conversant with what is happening beyond their localities.``

``CCM members have to wake up and realize that the people they so much hold high in esteem are actually stabbing them behind their backs. Otherwise they will end up cheering people who are prospering through their sweat,`` said a resident, who identified himself by only one name of Mwambalaswa.

A member of the opposition party, who identified himself by a single name as Marshall, said it was absurd that people should give such grand receptions to suspects of corruption.

``It is beyond anybody`s imagination that so many people fall easy prey to manoeuvers by politicians who use their wealth to make them laughing stocks in their own constituencies,`` he said.

A member of the Civic United Front (CUF) party, Augustino Amani, said the government had to tell the people now what measures it would take against such suspects once proved to have been involved in the vice.

``The government has to tell us now on the measures it will take to punish all those implicated in amassing wealth and using their office for individual gain,`` he said.

Amani said without doing so now, the public was likely to lose confidence in the government.

He added that the government should bring down the rocketing prices of a number of domestic items and services which shot up as a result of corrupt machinations perpertrated by those in power.

SOURCE: Guardian
 
Ngosha,

Si umesikia Katibu Mkuu akisema ni ruksa kuandamana?

Lakini kama nilivyosema awali kwenye ile thread ya divided perspective, what is wrong huko vijijini? au ni vitisho kutoka kwa viongozi na woga wa wananchi ulioambatana na "unyonge na Umasikini" ndio unafanya Wananchi waendelee kuunga mkono "watuhumuwa" wa Uhujumu uchumi?

may be hao wanavijiji hawajui thamani ya hizo pesa, wanadhani ni shilingi millioni moja ndio maana wanamwona bado anafaa, wananchi bado hawajaelimika na wataendelea kuwasifia tu, ooh mbunge wetu ana magari ya kiasi kadhaa, ana majumba mangapi.....bila kujiangalia wao wanahitaji kuwa na nini kimsingi
 
tuuukubali ukweli, waliomshangilia chenge na lowasa walifanya hivyo kwa njaa zao, tunaambiwa kuwa yale magari yaliyoko kwenye msafara yanapewa mafuta toka kwenye akaunti ya vijisenti, kule bariadi kila mahali alipohutubia ngombe alichinjwa watu wakala bureee, ni mwanakijiji gani ataacha kujitokeza kupewa nyama ya bure, nyama anayokula mara moja kwa mwezi au sikukuu kama krismasi? mafisadi wamenunua nchi, wananufaika na umaskini waliowatengenezea wananchi, BADO SAFARI NI NNDEFU
 
tuuukubali ukweli, waliomshangilia chenge na lowasa walifanya hivyo kwa njaa zao, tunaambiwa kuwa yale magari yaliyoko kwenye msafara yanapewa mafuta toka kwenye akaunti ya vijisenti, kule bariadi kila mahali alipohutubia ngombe alichinjwa watu wakala bureee, ni mwanakijiji gani ataacha kujitokeza kupewa nyama ya bure, nyama anayokula mara moja kwa mwezi au sikukuu kama krismasi? mafisadi wamenunua nchi, wananufaika na umaskini waliowatengenezea wananchi, BADO SAFARI NI NNDEFU



ndo kusema vijisent ako addicted na rushwa sio...kila pahala lazima atoe vijisent au avipokee! Hao wananchi walitakiwa wamsusie hata hiyo nyama wasile ili ajue ni kiasi gani amewafedhehesha.
 
may be hao wanavijiji hawajui thamani ya hizo pesa, wanadhani ni shilingi millioni moja ndio maana wanamwona bado anafaa, wananchi bado hawajaelimika na wataendelea kuwasifia tu, ooh mbunge wetu ana magari ya kiasi kadhaa, ana majumba mangapi.....bila kujiangalia wao wanahitaji kuwa na nini kimsingi

Huko vijijini ambako ndio asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi bado tuna matatizo makubwa sana ya kuwafahamisha hawa wenzetu kuhusiana na uharamia wa hali ya juu unaofanywa na mafisadi mbali mbali akiwamo fisadi Mkapa.

Na viongozi walio madarakani nao ni dhaifu mno labda kutokana na wao kuwa mafisadi au kuwaogopa mafisadi. Kikwete angekuwa kiongozi imara asingeruhusu Chenge kwenda kwenye jimbo lake kwa kishindo, hilo lisingetokea lakini tuna picha ya Rais pale Ikulu ambaye hana uwezo wa kufanya maamuzi yoyote kwa maslahi ya nchi.
 
Huko vijijini ambako ndio asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi bado tuna matatizo makubwa sana ya kuwafahamisha hawa wenzetu kuhusiana na uharamia wa hali ya juu unaofanywa na mafisadi mbali mbali akiwamo fisadi Mkapa.
Na viongozi walio madarakani nao ni dhaifu mno labda kutokana na wao kuwa mafisadi au kuwaogopa mafisadi. Kikwete angekuwa kiongozi imara asingeruhusu Chenge kwenda kwenye jimbo lake kwa kishindo, hilo lisingetokea lakini tuna picha ya Rais pale Ikulu ambaye hana uwezo wa kufanya maamuzi yoyote kwa maslahi ya nchi.

lakini na opposition wangewaelimisha hao kwa kufanya counter attack papo kwa papo.
 
Pia tukumbuke kijadi chetu kuwa huwa tunashangilia pindi Jambazi linapokamatwa..
Aidha maandamano makubwa ya Chenge huko Bariadi ilikuwa ni pamoja na watu kutaka kumwona huyo Jambazi kama alivyoingia Idd Amin Dada mjini Mwanza mwaka 72, Umati mkubwa ulijitokeza kumwona kuliko ule uliompokea Nyerere mwenyewe na sidhani kama mkuisanyiko ule ulikuwa ni ishara ya mapenzi kwa Amin..

Who knows lakini kwa kifupi maandamano hayo ni changa la macho na dharau kubwa kwa serikali ya Kiwete.
 
Jamani ni kweli wapinzani walekeze nguvu za kuwaelimisha watu wengi vijijini lakini hata sisi pia wenye ndugu vijijini tutumie fursa hiyo kuwaelimisha ndugu zetu kuhusiana na UFISADI unaofanywa na hawa MAJAMBAZI wa CCM. Watu vijini wanafanywa kama Mazuzu yaani aibu sana.
 
Back
Top Bottom