Kafara
JF-Expert Member
- Feb 17, 2007
- 1,396
- 413
Naomba msome hii ArticleDAWASCO wamkataa Mkurugenzi wao...
2008-03-22 09:41:24
Na Mashaka Mgeta
Wafanyakazi wa Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO), wamemtaka Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wao, Bw. Alex Kaaya, wanayedai kuwa `aliwekwa` madarakani na aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, aachie ngazi kwa kushindwa kuendeleza kampuni.
ina maana utaratibu wa ajira haukufuatwa? kama haukufuatwa nadhani wanahoja ila wafuate taratibu kama walivyoshauriwa
...``Alituahidi kutupatia viwanja kwa kila mfanyakazi, kufanya mikutano kila baada ya miezi mitatu, kutuletea maisha bora ili tumudu kuwasomesha watoto wetu, hajatekeleza hayo yote,`` alisema.
kama huyu mheshimiwa aliahidi haya basi alilikoroga mwenyewe sasa umefika wakati wa kulinywa
...``Hata hivyo, Bw. Nkakatisi, aliwataka wafanyakazi hao kufuata sheria, kanuni na taratibu, ili kupata suluhu ya kero zinazowakabili.
Bw. Nkakatisi, aliyekabidhiwa risala ya wafanyakazi hao, alisema hatua yoyote itakayokuwa kinyume cha sheria, kanuni na taratibu zilizopo, itaashiria vurugu na hivyo kuwafanya wasifikie malengo yao...
SOURCE: Nipashe
imetoka kwa Nipashe 22/03/08
nadhani ni ushauri makini