green29
JF-Expert Member
- Jul 4, 2007
- 311
- 44
Hivi katika job description yake aliambiwa aendelee upuuzi wa ziara za kisiasa mikoani kama Lowassa?
Wazee nafikiri kwa kuwa ndio kwanza amechukua ofisi, nafikiri ziara ya utambulisho na kutangaza sera zake na mikakati yake ni muhimu japo kwa muda mfupi hivi inaweza kuwa ni mapema mno.
.
Alitakiwa akae ofisini kwanza atleast apate feedback mwenzake aliishia wapi kwenye kazi njema na kazi za richmond. All in all ngoja aende tu apigiwe makofi kidogo ili aweze ku-feel ukubwa wa mamlaka na madaraka aliyonayo.
Wizara aliyotoka inafanya tutarajie kuwa anafahamu vitu vingi sana huko mikoani. NA labda Cheo kipya kwake ni kama karandinga la kufukua maeneo yaliyomshinda akiwa waziri wa kawaida - serikali za mitaa.
Kama anafanya ziara ambazo zitakuwa productive kwa Taifa basi tumtakie safari njema tu, ila kama ni zile ziara za rangi ya kijani na nyeusi basi awe makini sana.