Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

Waziri wetu mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko ziarani Rukwa kwa siku saba 'kukagua' shughuli za maendeleo huko na nadhani sana sana ni kuwaona ndugu na jamaa zake baada ya kupata nafasi ya ukulu, ukubwa na uzee aliouachia Lowassa.
Sasa akiwa katika kijiji cha Kakese leo asubuhi amemtetea Edward Lowassa akisema kuwa kosa alilotenda Lowassa ni la kwanza na kwamba Waswahili husema kosa siyo kosa hadi utakapolirejea.
Pinda akizungumzia kashfa ya Richmond alisema Lowassa hapaswi kulaumiwa kwa kuwa yaliyomkuta ni miongoni mwa changamoto za uongozi na kwamba alifanya vyema kujiuzulu baada ya wanaomsaidia kuhusishwa na sakata la kampuni ya mfukoni ya Richmond ambayo ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.


kamanda,
leo hatimaye ...
 
Sasa hiyo picha maana yake nini...unaicheka comment yangu au...?

Nope Nyani!!!!!. Si unajua tena katika hizi issues za black ndivyo tulivyo huwa ninakuunga mkono kwa asilimia 100%. Wanaonivunja mbavu ni hao homo sapiens wenzangu wa huko Clayton county. Pamoja na kuishi US bado wanaendekeza mambo ya uswazi.
 
Nope Nyani!!!!!. Si unajua tena katika hizi issues za black ndivyo tulivyo huwa ninakuunga mkono kwa asilimia 100%. Wanaonivunja mbavu ni hao homo sapiens wenzangu wa huko Clayton county. Pamoja na kuishi US bado wanaendekeza mambo ya uswazi.

Gotcha!!
Nenda Jamaica au Trinidad mambo vile vile tu hakuna tofauti...
 
Well...nakubali tunaweza kurefine...lakini tatizo ni hili; nchi nyingi zilizopo Afrika kusini mwa jangwa la Sahara matatizo yake yanafana fanana. Uende Cameroon...upitie Guinea Bissau...Ghana...Nigeria....Zimbabwe....mambo yale yale tu. Juzi nimeona kwenye CNN International eti inflation ya Zimbabwe imefikia asilimia 66,000....how can this even be possible? Halafu eti chama cha Zanu-PF kimempendekeza Mugabe agombee tena...and guess what...atashinda tena na wakati huo huo Wazimbabwe wanakula panya!! Wakati wa Rhodesia mambo yalikuwa freshi...so nini kimetokea?

Natambua kwamba Waafrika wote si watu weusi but damn...we obviously got some issues....we can't run anything...

Kwani hii inayoitwa Afrika halisi (the real Africa) ilishawahi kupata uhuru? Hakuna nchi katika kundi hilo yenye uhuru! Rhodesia haikuwa nchi ya kiafrika kwa taarifa yenu, ile ilikuwa ya Ian Smith, ilikuwa nchi "binamu" ya Uingereza kama US, Australia na New Zealand. Ile "unilateral declaration of independence" ambayo Ian Smith alinakili kutoka katika ule waraka wa kina George Washington huko Marekani ilikuwa "geresha" tu, hakuwahi kutengana na Uingereza! Na South Africa pia nayo hivyohivyo, baada ya jitihada za miaka mingi za waafrika (ambazo japo wazungu walijua vita ya silaha waafrika wasingeshinda, walijua ingewanyima wazungu raha ya kutanua na mapesa ya almasi na dhahabu), wazungu wameachia utawala wa kisiasa lakini wamebaki na utawala wa kiuchumi, kwa hiyo kimsingi bado wao ni watawala. Walichojitahidi sana South Africa ni kuelewana tu kuwa sasa hivi wote (bila kujali rangi) ni raia wenye haki sawa, kwa hiyo mweusi akitawala kisiasa wakati mweupe anatawala kiuchumi, kwao ni wa-South-Africa wanatawala yote hayo!

Kuna division mpya nimeiona siku hizi ya maeneo ya dunia (naona wanasita tu kuanzisha bara jipya), nchi za Africa kaskazini ziko kwenye region inaitwa MENA (Middle East and North Africa), na iliyobaki wanasita tu kuziita Africa nyeusi (actually wapo wanaoziita "black Africa!") lakini basi "kishkaji" wanaziita Sub-Saharan Africa (hebu rudia tu jiografia uangalie kama nchi zote chini ya jangwa la Sahara ziko kundi hili, au kama hakuna nchi juu ya Sahara ambazo bado ziko kundi hili!). Hii Afrika iliyobaki, hii nyeusi hii, haijawahi kuwa huru, bado inatawaliwa na kwa remote control na wazungu, na ikileta fyoko inashughulikiwa "waziwazi" kama tunavyoona sasa Zimbabwe. Haya ya Zimbabwe yanaweza kuipata nchi yoyote inayokorofishana na "wakubwa" (kama Nyerere alivyowaita). Marehemu Prof Abdulrahman Babu aliwaita "mabeberu" huku akifundisha katika vyuo vyao (nijuavyo mimi beberu ni dume kubwa la mbuzi, sasa sijui wasomi walimaanisha nini hapa! Hadi leo tunatumia neno "ubeberu" kumaanisha "imperialism").

Kwa hiyo huku kwetu Africa nyeusi tuna matatizo makuu mawili, moja ni huo "ubeberu", na la pili lina sehemu mbili ambazo kwa pamoja naziita "in-breeding", naazima neno hili kutoka kwa rafiki yangu aliyekuwa anafundisha agriculture. Tuna in-breeding ya viongozi wabovu yaani tunaruhusu viongozi wetu walio wabovu kutuchagulia successors wao, hapohapo tuna methali zetu kuwa "mwana wa nyoka ni nyoka", "zimwi likujualo...." (hebu ziweke kwenye context, "mwana wa fisadi ni...." "fisadi akujuaye ....." nk). Kwa hiyo fisadi anatuchagulia fisadi mwenzie kwa kuwa lao moja, tunaendelea na "in-breeding" ya mafisadi. Lakini la pili, tuna "in-breeding" ya mifumo dhalimu/ovu, mfano wabunge waliopatikana kwa njia ya rushwa ndio wanaotunga sheria za nchi, unategemea sheria za aina gani kama sio zile za "takrima", kubadilisha katiba ili rais atawale milele nk? Na katika nchi kama hizo utaambiwa wanafuata utawala wa sheria, kwa kuwa kila wanachofanya ni kwa mujibu wa sheria zao hizo! Mifumo yote ya uongozi (vyama vya siasa, halmashauri za mikoa na miji), mihimili ya dola (bunge, serikali na mahakama) kote kuna "in-breeding" ya "traits" zilezile, maendeleo yatatoka wapi? Naambiwa na rafiki yangu huyo wa Agriculture kuwa kwa kila "cycle" moja ya "in-breeding", quality ya product inapungua kwa 50%, na ungefanya "cross-breeding" ingeongezeka kwa 50%!
 
JK alimleta huyu anyooshe njia lakini naona ime Pinda kama mshale na upinde wake, ndiyo kazi yenyewe hiyo ukiipata kwa kukurupuka bila tegemeo ndivyo inavyokuwa. Mwaka huu hii njia ita Pinda sana.

Pinda si alikuwa karibu na mpini wa mshale ulio Pinda?
 
JK alimleta huyu anyooshe njia lakini naona ime Pinda kama mshale na upinde wake, ndiyo kazi yenyewe hiyo ukiipata kwa kukurupuka bila tegemeo ndivyo inavyokuwa. Mwaka huu hii njia ita Pinda sana.

Pinda si alikuwa karibu na mpini wa mshale ulio Pinda?

Yuko aliyeanzisha mizengwe. Kuwa kuwa mizengwe ilishaanza wamesubiri ipite kwanza kisha watapinda, plani iko wazi, mizengwe kaianza, ikipita, pinda!
 
Yuko aliyeanzisha mizengwe. Kuwa kuwa mizengwe ilishaanza wamesubiri ipite kwanza kisha watapinda, plani iko wazi, mizengwe kaianza, ikipita, pinda!

kwa kweli hapo mmenifanya nicheke sana,hadi nimevunjika mbavu.
Lakini nilisema siku ya kwanza tu, kuwa jk ameleta zezeta lingine kwa hiyo tusitegemee mihujiza.siku zote majina ya watu uhendana na matendo yao.
 
Hivi mlitegemea kitu gani tofauti?...

Jamani mwee, hata siku moja haiwezekani serikali kupambana na rushwa hali ni serikali hiyo hiyo inayoshiriki ktk rushwa. Nani amkamate nani?
Ebu fikiria hili Kafiri (Asiyeamini Mungu) kaanzisha kanisa la makafiri wakitumia jina la Yesu kufundisha Uongovu!... Hapa wenzangu kweli mnategemea huo uongovu ni upi, kama sio haramu kuitwa halali maadam unatumia jina la Yesu. Hii ndio tahadhali alotuachia Yesu kuwa wapo mitume wa Uongo, tusije fikiria hata siku moja kuwa watakuwa na alama tofauti nasi ama tofauti na binadamu wengine...
Kifupi sikutegemea Pinda kuja na mawazo tofauti ikiwa rais mwenyewe kisha sema Lowassa hana makosa ni shujaa!... sawa na ushajaa wa Yuda alivyosifiwa na Mfalme!
 
Waziri wetu mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko ziarani Rukwa kwa siku saba 'kukagua' shughuli za maendeleo huko na nadhani sana sana ni kuwaona ndugu na jamaa zake baada ya kupata nafasi ya ukulu, ukubwa na uzee aliouachia Lowassa.
Sasa akiwa katika kijiji cha Kakese leo asubuhi amemtetea Edward Lowassa akisema kuwa kosa alilotenda Lowassa ni la kwanza na kwamba Waswahili husema kosa siyo kosa hadi utakapolirejea.
Pinda akizungumzia kashfa ya Richmond alisema Lowassa hapaswi kulaumiwa kwa kuwa yaliyomkuta ni miongoni mwa changamoto za uongozi na kwamba alifanya vyema kujiuzulu baada ya wanaomsaidia kuhusishwa na sakata la kampuni ya mfukoni ya Richmond ambayo ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.

Huyu naye hawezi kuzungumza bila kumtaja Lowassa? Badala ya kuzungumzia atafanya nini ili kuboresha maisha ya wananchi wa Rukwa na yale ya Watanzania wote na vipi atazishughulikia kashfa mbali mbali zilizoigubika SK, anataka kumtetea mtu asiyestahili kutetewa! Asipoangalia atapoteza credibility yake haraka sana na kuingizwa kwenye kundi la wasanii.
 
Kwa kauli hizi tutarajie makubwa kuliko ya kina RICHMOND !

Sipendi kuamaini kwamba Mh kamtetea mfisadi. Labda kwa maono yangu ulimi umeteleza. Au tusubiri wasaidizi wake watasema mwandishi wa habari hii amemnukuu vibaya Mh. Kama vyote hivyo havitatokea, basi nitaamini na yeye yuko kwenye mtandao wa kumuosha EL. Tukumbuke hata alipo kuwa anawashukuru wakuu wa mjengoni kwa kumkubali kuwa kilanja wao, alisema atatekeleza kwa makini yale mema yaliyofanywa na EL. On the other hand labda na hili la Richmond hewa kwake ni jema.

Kila mtu ana mtazamo wake wa maono. Ila kwa hili tumwambie mkuu wetu hapa katuchefua.
 
Sipendi kuamaini kwamba Mh kamtetea mfisadi. Labda kwa maono yangu ulimi umeteleza. Au tusubiri wasaidizi wake watasema mwandishi wa habari hii amemnukuu vibaya Mh. Kama vyote hivyo havitatokea, basi nitaamini na yeye yuko kwenye mtandao wa kumuosha EL. Tukumbuke hata alipo kuwa anawashukuru wakuu wa mjengoni kwa kumkubali kuwa kilanja wao, alisema atatekeleza kwa makini yale mema yaliyofanywa na EL. On the other hand labda na hili la Richmond hewa kwake ni jema.

Kila mtu ana mtazamo wake wa maono. Ila kwa hili tumwambie mkuu wetu hapa katuchefua.


Lunyungu aliwahi kuja na hizi habari za kumuosha mzee wa nywele nyeupe days ago na baadaye mengine yalianza kujiri .Leo unataka kuendelea kushangaa na hata baada ya Lunyungun na mambo mengine kujitokeza kwa uwazi jamani ?
 
What else is new! Dr. Watson akisema sisi mazuzu tunaanza kulialia

Hivi jamani mtu mmoja hawezi kutunukiwa tuzo ya NOBEL zaidi ya mara moja? Mi ningependekeza Dr. Watson apewe tena tuzo ya NOBEL kwa utafiti wake huo wa tofauti ya IQ ya mtu mweusi na mweupe. Yuko sahihi kabisa!
 
Waziri wetu mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko ziarani Rukwa kwa siku saba 'kukagua' shughuli za maendeleo huko na nadhani sana sana ni kuwaona ndugu na jamaa zake baada ya kupata nafasi ya ukulu, ukubwa na uzee aliouachia Lowassa.
Sasa akiwa katika kijiji cha Kakese leo asubuhi amemtetea Edward Lowassa akisema kuwa kosa alilotenda Lowassa ni la kwanza na kwamba Waswahili husema kosa siyo kosa hadi utakapolirejea.
Pinda akizungumzia kashfa ya Richmond alisema Lowassa hapaswi kulaumiwa kwa kuwa yaliyomkuta ni miongoni mwa changamoto za uongozi na kwamba alifanya vyema kujiuzulu baada ya wanaomsaidia kuhusishwa na sakata la kampuni ya mfukoni ya Richmond ambayo ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.

ZZZzzzzzzzzzzz......krrrrrrrrrr....zzzzzzzzzzzzzzzzzz, sijui hiki kitanda kind kunguni, maana naona machomwa chomwa... aaa ngoja ni lale hivo hivo


YA KENYA YANANUKIA TANZANIA.......
 
Yes...why are you surprised...? Pinda ni kiongozi mzuri sana na ni muadilifu

siku Moja niliandika hivi " haitoshi kumpima kiongozi wa juu kwa vigezo kama, ni mpole, anatoka katika familia ya kawaida..... kwangu mimi naona tunarudi pale pale waliposema tumchague kwa sababu ni " mwenzetu"

Kigezo kimoja kinatosha kwa huyu waziri Mkubwa nacho ni ,. Mwaka jana Halmashauri ngapi za wilaya zilipata hati chafu kutokana na matumizi mabay ya pesa za walipa kodi kwa mujibu CAG? Je waziri mwenye dhamana (Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa) alichukua hatua gani? Naomba majibu kwa maswali haya ya nyongeza ili niweze kukubali kuwa huyu bwana ni mwadilifu na nimwngize katika fikra for 2010.
 
Waziri wetu mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko ziarani Rukwa kwa siku saba 'kukagua' shughuli za maendeleo huko na nadhani sana sana ni kuwaona ndugu na jamaa zake baada ya kupata nafasi ya ukulu, ukubwa na uzee aliouachia Lowassa.
Sasa akiwa katika kijiji cha Kakese leo asubuhi amemtetea Edward Lowassa akisema kuwa kosa alilotenda Lowassa ni la kwanza na kwamba Waswahili husema kosa siyo kosa hadi utakapolirejea.
Pinda akizungumzia kashfa ya Richmond alisema Lowassa hapaswi kulaumiwa kwa kuwa yaliyomkuta ni miongoni mwa changamoto za uongozi na kwamba alifanya vyema kujiuzulu baada ya wanaomsaidia kuhusishwa na sakata la kampuni ya mfukoni ya Richmond ambayo ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.

Kumbuka kati ya watu ambao PINDA aliwataja mwanzoni kuwa walimjenga kisiasa ni LOWASSA. Hivyo sishangai kusikia kauli hiyo.
 
HOTUBA YA MHE. MIZENGO KAYANZA PETER PINDA (MB) – WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA WAKATI AKIFUNGUA RASMI MAFUNZO YA WAKURUGENZI WAPYA WA HALMASHAURI YALIYOFANYIKA HILUX HOTEL MOROGORO, TAREHE 13-08-2007

8. Ndugu Wakurugenzi, kwa maelezo hayo machache ni wazi kwamba majukumu mliyo nayo ni mazito. Kwa mfano majukumu yote ya Kisheria ambayo mengine sikuyataja hapa, msipoyatekeleza mnaweza kushitakiwa na kufunguliwa kesi Mahakamani. Ikithibitika Mahakamani kwamba kweli ulifanya makosa unaweza kufungwa. Madhara ya kifungo sote tunayafahamu.

Mambo yakiharibika nyie ndio watu wa kwanza kunyoshewa kidole. Tafadhalini sana tusifike huko. OWM-TAMISEMI kwa upande wake itashirikiana na nyinyi kuhakikisha kwamba mnatimiza wajibu wenu ipasavyo

10. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Ndugu Wakurugenzi, historia inaonyesha kuwa suala la utunzaji wa vitabu vya hesabu za Halmashauri nchini limekwa ni tatizo kubwa kwa muda mrefu, japokuwa hivi karibuni hali imeanza kuwa nzuri kwa mujibu wa Taarifa za Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali kwa mwaka 2004/05 na 2005/06 ikilinganishwa na miaka ya 2000 hadi 2003. Mwaka 2004/05 kati ya Halmashauri 117, Halmashauri 62 zilipata hati safi, 4 zilipata hati chafu na 51 zilipata hati zenye masharti. Mwaka 2005/06 kati ya Halmashauri 122, 52 zilipata hati safi, 4 zilipata hati chafu na 61 zilipata hati zenye masharti. Pamoja na mafanikio haya, bado kuna changamoto kubwa ya kuhakikisha kuwa Serikali inapata thamani kwa fedha zinazotolewa na kutumika katika Halmashauri kwa kuhakikisha kuwa, Halmashauri nyingi zinapata hati safi. Hii itawezekana tu iwapo Halmashauri zote zitazingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za matumizi ya fedha za Serikali. Halmshauri zenu nyingi bado ni mpya. Hivyo, napenda kuwaagiza yafuatayo:

Maneno ya kuwawajibisha wakurugenzi yamerudiwa baada ya kupewa u-PM. Alishindiwa wapi wakati akiwa TAMISEMI?
 
Kwanza Naona Ni Mapema Mno Kuanza Ziara Kabla Hata Ya Kusoma Mazingira Ya Ofisi Maana Ofisi Ni Mpya Hiyo
 
Kama Hizo Halmashauri Serikali Zimewashinda Kwanini Msizibinafsishe Maana Mnajifanya Mmejitoa Ktk Biashara Wakati Kila Mtu Anajua Ni Unafiki Wa Siasa Tu Kama Mmejitoa Ktk Biashara Nyumba Za Nhc Mnang'ang'ania Za Nini Na Yale Majengo Yaliyokuwa Yamejengwa Na Vyama Vya Ushirika Hao Washirika Wenyewe Wanafaidi Kitu Gani Kama Siyo Dhuluma Tu Na Mjue Mwisho Wenu Unakaribia Ndiyo Maana Sasa Hivi Kila Mmoja Wenu Anaonekana Kama Amechanganyikiwa
 
Hivi katika job description yake aliambiwa aendelee upuuzi wa ziara za kisiasa mikoani kama Lowassa?

Tulilalamika kuwa Lowassa na ofisi yake kazi yao ilikuwa ni kumaliza Tax payers mmoney kutembea mikoani bila sababu yoyote ya msingi

Mbona ofisi ya waziri mkuu haitoi mchanganuo wa hizi ziara?

Zina cost kiasi gani? ujumbe wake huwa ni watu wangapi? na zishaleta matunda yepi?

This is very disappointing to the max
 
Back
Top Bottom