Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

Waliompokea ni wapandikizwaji hili jamaa aonekane kama ni shujaa.
Ushauri wa bure kwa Lowasaa,ni kwamba ni bora akatulia kimya na kusubiri maamuzi zaidi ya watanzania. Kuendelea kuongea ni kuendelea kuwatia hasira watanzania ambao bado wanamaumivu makali na bei mbaya ya umeme. Ni vigumu kuwalazimisha watanzania waamini kile lilichosema na ndiyo maana hata maongezi yake TVT yaliondolewa hewani hili kuepusha hasira za wananchi.
Ushauri kwa CCM,itakuwa ni kosa kubwa kwa CCM kama Lowassa siku moja atasisimama na kugombea urais wa nchi hii,Mwl.Nyerere alimwona mtu huyu sio msafi toka siku nyingi. Sasa tumeyaona wenyewe,
Lowassa kaa kimya,washabiki hawa wa kupandikizwa wataendelea kukuponda
 
Nafurahi sana ninapopata watanzania ambao wanaokuja na maswali mazuri. Lowassa anakuja na mbinu nyingi sana,unajua haya mapokezi ya lowassa yalikuwa na maandalizi ya ajabu sana. Siamini kama kuna mtanzania mwenye akili timamu anayeweza kumpokea mtu ambaye ameyafanya maisha yake kuwa magumu. Miye siamini,hizi gari zilikuwa za madereva taxi zilikodiwa. Tunasubiri Raiamwema kesho
 
Nilipata kigugumizi, na kusikia mwili ukilegea niliposikia eti "Shujaa Kapokelewa kwao" nilipata nafasi kidogo ya kuangalia baadhi ya watu waliompokea kwa haraka haraka wale watu ni wa kukodishwa, kwanza haiwezekani watu wote wale wawe ni wa jimbo la Monduli, wale ni watu ambao wamenunuliwa ili kuonyesha kuwa anakubalika kwao.. Mbona sikusikia kauli ya kiongozi wa juu wa CCM akisimama jukwaani na kusema shujaa amerudi? Unajua bwana Usanii sio mahali popote kuna sehemu nyingine huwezi kucheza usanii... Ina maana hao wananchi wa Monduli wanaishi peponi? ina maana kuwa hawapati hii adhabu ya kulipa gharama kubwa ya umeme? Yes nimeshaenda Monduli mara nyingi tuu wala sijaona hayo maisha yao mazuri kiasi hicho. Barabara sio za kuridhisaha sana zaidi ya ile lami na ni kwa ajili ya TMA na sii vinginevyo? Hizo hela walizotumia kukodisha magari yote na Zulia kwa nini wasijenge machinjio ya kisasa wakaweza kuuza ng'ombe nje ya nchi? Watanzania tuache unafiki na njaa zisizokuwa na maana.. palipo na ukweli usimame ukweli sio wahariri kununuliwa kirahisi namna hii. Hivi haiwezekani vyombo vyote vya habari wakaamua kukaa kimya bila kuandika habari zake?
 
Nilipata kigugumizi, na kusikia mwili ukilegea niliposikia eti "Shujaa Kapokelewa kwao" nilipata nafasi kidogo ya kuangalia baadhi ya watu waliompokea kwa haraka haraka wale watu ni wa kukodishwa, kwanza haiwezekani watu wote wale wawe ni wa jimbo la Monduli, wale ni watu ambao wamenunuliwa ili kuonyesha kuwa anakubalika kwao.. Mbona sikusikia kauli ya kiongozi wa juu wa CCM akisimama jukwaani na kusema shujaa amerudi? Unajua bwana Usanii sio mahali popote kuna sehemu nyingine huwezi kucheza usanii... Ina maana hao wananchi wa Monduli wanaishi peponi? ina maana kuwa hawapati hii adhabu ya kulipa gharama kubwa ya umeme? Yes nimeshaenda Monduli mara nyingi tuu wala sijaona hayo maisha yao mazuri kiasi hicho. Barabara sio za kuridhisaha sana zaidi ya ile lami na ni kwa ajili ya TMA na sii vinginevyo? Hizo hela walizotumia kukodisha magari yote na Zulia kwa nini wasijenge machinjio ya kisasa wakaweza kuuza ng'ombe nje ya nchi? Watanzania tuache unafiki na njaa zisizokuwa na maana.. palipo na ukweli usimame ukweli sio wahariri kununuliwa kirahisi namna hii. Hivi haiwezekani vyombo vyote vya habari wakaamua kukaa kimya bila kuandika habari zake?

Nafikiri wengi walikuwa wanalipa fadhila kwani walifaidika wakati akiwa PM, mtu kama yule mwizi aliyetolewa mahakamani kimizengwe lazima mkono wa EL ulikuwepo
 
nafikiri ni njaa tuu inawasumbua,its OK akiamua kufight back maana ni kawaida ya wanasiasa kufanya vitu kama hivi na ninavyojua huyu jamaa hajaisha na support bado anayo kufanya hayo anayotaka.
 
Lunyungu,

Yah, nimekubaliana na wewe na naomba kwa kweli wanasheria wajitokeze tulifuatilie hili.
Kwa wale wanaodai vielelezo wasiwe na shaka. Kama tutaamua kufanya hivyo tutapata masaada na taarifa zote za wizara husika na Tanesco pamoja na kopi ya ripoti na vielelezo vyake tutavipata na swala la ku-invest muda tu. Wanasheria tunaomba msaada wenu.
 
HIVI huyu Lowassa anapata wapi ujasiri wa kifisadi namna hii?

Mbona kama vile hasikii hata sauti ya kundi kubwa la wana wa nchi (Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu) ambao walimshauri kukaa kimya ili labda historia ije imuibue, yeye hataki kusikia na anapanga kila aina ya makombora kuhakikisha kuwa anarejea serikalini na ikiwezekana kwenye kinyang'anyiro cha 2015.

Mbali na waandishi wachache wenye tamaa, wajinga wa nyakati, wasiokuwa na visheni na zaidi sana bootlickers, sasa ameamua kuwabakiza waandishi ao huko huko Arusha hadi wakachapisha gazeti.

Gazeti hilo liitwalo 'Arusha Raha Kweli' limeingia mitaani muda huu na kumkuta Kamanda mimi nikiwa nimejipumzisha na ka-bia kangu pale Hilfishers Pub mitaa ya jiji la Lusaka. Hapa kuna kibaridi kidogo.

Ilibidi nipumzishe mkono wangu kunyanyua glasi ya bia na kuanza kusoma mara nilipowasilishiwa na hawa jamaa wa kampuni ya kusafirisha vifurushi. Network bwana ni nzuri sana

Hebu sikiliza: Lead story ni:

'Lowasa ajibu mapiga na baadaye kukawa na vibwagizo kibao:
*awataja waliohusika, wamo vigogo wa serikali
* Kuna njama za kuigawa CCM
*Alia na Mwakyembe
*Madiwani Monduli wacharuka
*mahojiano yake yakatizwa ghafla TvT.

Limechapwa Dar na kiwanda cha Printech, kile kilichokuwa kinamilikiwa na kina Habari Corporation- Mtanzania, Rai, Bingwa, The African kabla ya kuwashinda na kunyang'anywa na wale waliowakopesha.

Nasikia limesambazwa nchi nzima na linauzwa 300/-, ingawa nasikia liko kwenye mikakati ya kuuzwa 200/- ili lisomwe sana.

Jamani huo ni mkakati, ambao yeye na watu wake wanadhani ni kabambe kumbe masikini ndiyo anamalizika kabisa na muda si mrefu atazimika.

Jadili hatua hii.

Ewe Mama Tanzania, twakulilia. Tutakulinda hata kwa matone ya damu.
 
Kamanda shusha majina ya wahariri hapa chini. mpango huu unaweza kuigawa nchi ikawa ya kikabila/kikanda kama Kenya.
 
HIVI huyu Lowassa anapata wapi ujasiri wa kifisadi namna hii?

Mbona kama vile hasikii hata sauti ya kundi kubwa la wana wa nchi (Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu) ambao walimshauri kukaa kimya ili labda historia ije imuibue, yeye hataki kusikia na anapanga kila aina ya makombora kuhakikisha kuwa anarejea serikalini na ikiwezekana kwenye kinyang'anyiro cha 2015.

Mbali na waandishi wachache wenye tamaa, wajinga wa nyakati, wasiokuwa na visheni na zaidi sana bootlickers, sasa ameamua kuwabakiza waandishi ao huko huko Arusha hadi wakachapisha gazeti.

Gazeti hilo liitwalo 'Arusha Raha Kweli' limeingia mitaani muda huu na kumkuta Kamanda mimi nikiwa nimejipumzisha na ka-bia kangu pale Hilfishers Pub mitaa ya jiji la Lusaka. Hapa kuna kibaridi kidogo.

Ilibidi nipumzishe mkono wangu kunyanyua glasi ya bia na kuanza kusoma mara nilipowasilishiwa na hawa jamaa wa kampuni ya kusafirisha vifurushi. Network bwana ni nzuri sana

Hebu sikiliza: Lead story ni 'Lowasa ajibu mapiga na baadaye kukawa na vibwagizo kibao: *awataja waliohusika, wamo vigogo wa serikali * Kuna njama za kuigawa CCM *Alia na Mwakyembe *Madiwani Monduli wacharuka *mahojiano yake yakatizwa ghafla TvT. Limechapwa Dar na kiwanda cha Printech, kile kilichokuwa kinamilikiwa na kina Habari Corporation- Mtanzania, Rai, Bingwa, The African kabla ya kuwashinda na kunyang'anywa na wale waliowakopesha.

Nasikia limesambazwa nchi nzima na linauzwa 300/-, ingawa nasikia liko kwenye mikakati ya kuuzwa 200/- ili lisomwe sana.

Jamani huo ni mkakati, ambao yeye na watu wake wanadhani ni kabambe kumbe masikini ndiyo anamalizika kabisa na muda si mrefu atazimika.

Jadili hatua hii.

Ewe Mama Tanzania, twakulilia. Tutakulinda hata kwa matone ya damu.

Mimi Joseph Cleophas Lunyungu Matandula wa Mademla Mnyalukolo niliwaeleza haya kabla .Haya ndiyo mambo nilisema na wako wengi sana ambao wako nyuma ya Lowasa.Mpango huu RA yumo na JK kwa mbaali lakini anaanza kushitukia ngoma .Lakini wote wamoooooooooooooooooooooo
 
JK is spineless and cannot make his mind.The sort of person who would stand in the middle of a busy road because he does not know whether to cross the road by going forward or to tun back where he is coming from.Eventually a truck or something will hit him.

Right now he cannot decide whether to distance himself from Lowassa or embrace him, dangerous indeed.
 
Lowassa ni hatari kuliko nyoka. Ashughulikiwe mapema kabla hajaleta maafa nchini. Nadhani hata ile kauli ya Ole Naiko inatoka kwenye hilo kundi la kina Lowassa. Ni mikakati michafu imeanza.
 
HIVI huyu Lowassa anapata wapi ujasiri wa kifisadi namna hii?

Mbona kama vile hasikii hata sauti ya kundi kubwa la wana wa nchi (Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu) ambao walimshauri kukaa kimya ili labda historia ije imuibue, yeye hataki kusikia na anapanga kila aina ya makombora kuhakikisha kuwa anarejea serikalini na ikiwezekana kwenye kinyang’anyiro cha 2015.

Mbali na waandishi wachache wenye tamaa, wajinga wa nyakati, wasiokuwa na visheni na zaidi sana bootlickers, sasa ameamua kuwabakiza waandishi ao huko huko Arusha hadi wakachapisha gazeti.

Gazeti hilo liitwalo 'Arusha Raha Kweli' limeingia mitaani muda huu na kumkuta Kamanda mimi nikiwa nimejipumzisha na ka-bia kangu pale Hilfishers Pub mitaa ya jiji la Lusaka. Hapa kuna kibaridi kidogo.

Ilibidi nipumzishe mkono wangu kunyanyua glasi ya bia na kuanza kusoma mara nilipowasilishiwa na hawa jamaa wa kampuni ya kusafirisha vifurushi. Network bwana ni nzuri sana

Hebu sikiliza: Lead story ni 'Lowasa ajibu mapiga na baadaye kukawa na vibwagizo kibao: *awataja waliohusika, wamo vigogo wa serikali * Kuna njama za kuigawa CCM *Alia na Mwakyembe *Madiwani Monduli wacharuka *mahojiano yake yakatizwa ghafla TvT. Limechapwa Dar na kiwanda cha Printech, kile kilichokuwa kinamilikiwa na kina Habari Corporation- Mtanzania, Rai, Bingwa, The African kabla ya kuwashinda na kunyang’anywa na wale waliowakopesha.

Nasikia limesambazwa nchi nzima na linauzwa 300/-, ingawa nasikia liko kwenye mikakati ya kuuzwa 200/- ili lisomwe sana.

Jamani huo ni mkakati, ambao yeye na watu wake wanadhani ni kabambe kumbe masikini ndiyo anamalizika kabisa na muda si mrefu atazimika.

Jadili hatua hii.

Ewe Mama Tanzania, twakulilia. Tutakulinda hata kwa matone ya damu.

WAHENGA WALISEMA, "LAKUVUNDA HALINA UBANI, NA SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA. TUTAONA MWISHO WAKE. JUST IMAGINE TULIKUWA NA PM WA AINA GANI?? AMBAYE HASHAURIKI.
 
Lowassa ni hatari kuliko nyoka. Ashughulikiwe mapema kabla hajaleta maafa nchini. Nadhani hata ile kauli ya Ole Naiko inatoka kwenye hilo kundi la kina Lowassa. Ni mikakati michafu imeanza.

..nani atamshughulikia?
 
This is totally incredible unajua Lowasa alikuwa too ambitious ati alitaka kuwa raisi baada ya JK,huu uswaiba utatupeleka pabaya as mtu anaweza bolonga ati kisa atakaempa kijiti ni mshikaji atamlinda,hopeless.
Suala la ukabila haliingii akilini wale wamonduli wamempokea kwa kishinda mhujumu uchumi ni zarau kwa watz kabisa na bunge zima.Mtu amevulunda hatma yake ni kupigwa chini sasa na kina Kara na Msabaha nao watasemaje that being the case.

Ole naiko nae mtu mzima hovyo kabisa baada ya kujibu hoja ya msingi unaanza kuropoka ati wana mpango wa kutuondoa watu wa Monduli-hopeless,tena naomba apigwe chini soon bse inaonyesha zahili jinsi alivyokuwa mhusika namba moja ktk kumsadia brother wake kuipitisha Richm.

Suala la ukabila apa halipo as ukivulunda ni kukupiga chini tuna watz wengi ambao wanaweza kutuongoza
 
Mimi sio mtaalamu wa maswala ya physcology, lakini naweza kusema kwamba ni tabia ya mwanadamu kuwa kwenye point of denial hasa mambo mazito yanapomkumba. Na maswala haya tunayaona sana nchi za dunia ya tatu, nchi ambazo democrasia ni msamiati mgumu.

Lowassa alishajua yeye na Tanzania na Tanzania na yeye, hakuwai kuwaza kwamba kuna siku ataamka na kukuta kwamba jina lake la Lowassa linafanana na ufukwe uliokumbwa na tsunami. Jina la Lowassa ni kama pesa ya Zimbabwe, huwezi kununulia hata cup of coffee.

Tatizo alilonalo Lowassa ni kutokukubaliana na reality, lakini ni vizuri kwetu sisi watanzania, mwache aweweseke eeeehhh, kisha ataanza kutaja majina ya wezi wenzie, na hapo ndio JK atakapo chukua jukumu la kumpoteza ili kulinda legency yake.

So, at the end of the day tax payer we're the winners and CCM are the loosers. Mwache anunue waandishi, akiweza anunue wanakijiji, mabalozi lakini one thing he can't is to fool all Tanzanian at once.
 
Tusubiri kuona,maana wanatumia nguvu nyingi sana kuhakikisha EL anarudi kwa kishindo na kugombea urais. Ndiyo maana anatumia sana hoja ya kujiuzuru kwa Mzee Mwinyi kwa dirisha la kuingilia. Tusubiri kuona ujio mpya wa mmasai huyu
 
Waziri wetu mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko ziarani Rukwa kwa siku saba 'kukagua' shughuli za maendeleo huko na nadhani sana sana ni kuwaona ndugu na jamaa zake baada ya kupata nafasi ya ukulu, ukubwa na uzee aliouachia Lowassa.
Sasa akiwa katika kijiji cha Kakese leo asubuhi amemtetea Edward Lowassa akisema kuwa kosa alilotenda Lowassa ni la kwanza na kwamba Waswahili husema kosa siyo kosa hadi utakapolirejea.
Pinda akizungumzia kashfa ya Richmond alisema Lowassa hapaswi kulaumiwa kwa kuwa yaliyomkuta ni miongoni mwa changamoto za uongozi na kwamba alifanya vyema kujiuzulu baada ya wanaomsaidia kuhusishwa na sakata la kampuni ya mfukoni ya Richmond ambayo ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.
 
Hawa wanao iba mitaani na kuchumwa tuna uhakika gani ni mara yao ya pili, tatu, nne ......?

Je, wanao pelekwa mahakamani wote wametenda kosa zaidi ya moja?

Ukiua mara ya kwanza, usamehewe tu kwa sababu ni mara ya kwanza?

Anyway, sielewi anamaanisha nini kwa kusema maneno hayo hapo lkn nafikiri niyakisiasa zaidi!
 
Waziri wetu mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko ziarani Rukwa kwa siku saba 'kukagua' shughuli za maendeleo huko na nadhani sana sana ni kuwaona ndugu na jamaa zake baada ya kupata nafasi ya ukulu, ukubwa na uzee aliouachia Lowassa.
Sasa akiwa katika kijiji cha Kakese leo asubuhi amemtetea Edward Lowassa akisema kuwa kosa alilotenda Lowassa ni la kwanza na kwamba Waswahili husema kosa siyo kosa hadi utakapolirejea.
Pinda akizungumzia kashfa ya Richmond alisema Lowassa hapaswi kulaumiwa kwa kuwa yaliyomkuta ni miongoni mwa changamoto za uongozi na kwamba alifanya vyema kujiuzulu baada ya wanaomsaidia kuhusishwa na sakata la kampuni ya mfukoni ya Richmond ambayo ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.

Dalili ya mvua ni mawingu
Kama wameanza kuteteana na kupeana chapuo basi maana ya ufisadi itageuzwa kuwa ni ushujaa wa kizalendo
 
Back
Top Bottom