BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
- Thread starter
- #181
Je, ilikuwaje kila mara wabunge walipohoji mkataba wa Richmond ulikuwa unawazuia wasifanye hivyo!? Ulikuwa unafanya hivyo kwa maslahi ya Tanzania, CCM au wewe mwenyewe? Hili la Netgroup Problems Watanzania wengi tulilijua tangu mwanzo. Kampuni ambayo ilikuwa inashughulikia kuuza stationery na ambayo haijui lolote kuhusiana umeme kwenda kupewa management ya shirika kubwa kama TANESCO ilikuwa ni ufisadi wa hali ya juu, lakini wakati huo hatukukusikia kusema chochote kupinga uamuzi huo, kwani ni dhambi kuwa upande mmoja na wananchi katika kupinga maamuzi yasiyo na maslahi kwa wananchi?
Watanzania wengi wakiwemo wafanyakazi wa TANESCO tulilipinga kwa kila hali hadi ikabidi waingizwe TANESCO wakiongozwa na FFU na mtutu wa bunduki, na hatima ya makaburu hao kupewa management ya TANESCO tunaijua pamoja na kulipwa mabilioni ya pesa ambazo hawakustahili.
Posted Date::2/23/2008
Lowassa ajitetea kutopata chochote kutoka Richmond
*Asema ni mkewe pekee aliyejua kuwa atajiuzulu
*Askofu Laizer akataza Wamasai kuitwa Richmond
Na Daniel Mjema, Arusha
Mwananchi
Watanzania wengi wakiwemo wafanyakazi wa TANESCO tulilipinga kwa kila hali hadi ikabidi waingizwe TANESCO wakiongozwa na FFU na mtutu wa bunduki, na hatima ya makaburu hao kupewa management ya TANESCO tunaijua pamoja na kulipwa mabilioni ya pesa ambazo hawakustahili.
Posted Date::2/23/2008
Lowassa ajitetea kutopata chochote kutoka Richmond
*Asema ni mkewe pekee aliyejua kuwa atajiuzulu
*Askofu Laizer akataza Wamasai kuitwa Richmond
Na Daniel Mjema, Arusha
Mwananchi
WAZIRI Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa jana alipokelewa kama shujaa katika uwanja mdogo wa Arusha na katika Jimbo lake la Monduli huku msafara wake ukikadiriwa kuwa na magari zaidi ya 100.
Akihutubia katika mkutano wa hadhara jimboni kwake, Lowassa alisema jana kuwa, alikuwa amesubiri kwa hamu na kwa muda mrefu siku hiyo ili aeleze kile anachokifahamu kuhusu kampuni ya Richmond Devolopment iliyomfanya ajiuzulu.
Siku nilipoamua kujiuzulu nilimuuliza mke wangu uko tayari? Na yeye akaniuliza na wewe uko tayari?Niwaambie ukweli hakuna mtu mwingine zaidi ya mke wangu aliyekuwa anajua nakwenda kujiuzulu, alisema Lowassa.
Akizungumzia suala la Richmond, Lowassa alisema ukame wa mwaka 2006 ulifanya taifa kuwa na tatizo la umeme. Kutokana na tatizo hilo, serikali iliamua kutafuta mitambo ya dharura.
Wakati Serikali ikifanya hivyo, wataalamu wakamuarifu kuwa liko tatizo la kupata mitambo hiyo kwa sababu mingi ya mitambo hiyo ilikuwa ikipelekwa nchini Iraki.
Ikumbukwe kuwa Net Group Solutions wakati huo walikuwa wameomba kuongezewa muda wa kuendelea kuliendesha shirika la umeme TANESCO wakakataliwa hivyo wakawa na usongo na Serikali, alisema na kuongeza;
"Tulivyokazana kuwaambia waagize mitambo hiyo, wao walikuwa wanapiga chenga ili ionekane kuwa bila wao isingewezekana kupata mitambo hiyo hapa tukagundua kuwa wanatuhujumu.
Lowassa alifichua kuwa, ndani ya Net Group Solutions kulikuwepo na baadhi ya mabosi wa kampuni hiyo ambao nao walikuwa na nia ya kuagiza mitambo hiyo kwa maslahi yao jambo ambalo yeye alilishitukia.
Waziri Mkuu huyo aliyejiuzulu alisema, hapo ndipo walipoamua kuachana na TANESCO na kuamua kutumia timu ya wataalamu wa Serikali wakiongozwa na Mwanasheria mkuu wa Serikali Johnson Mwanyika.
Alisema baada ya kupatikana kwa kampuni ya Richmond alianza kusikia minongono huku vyombo vya habari vikiandka juu ya kuwepo kwa matatizo katika mchakato mzima wa kuipata kampuni hiyo.
Nikaanza kusikia minongono nikamwita Waziri mwenye dhamana(Hakumtaja kwa jina) nikamuuliza mbona naanza kusikia harufu mbaya kuhusu Richmond lakini Waziri akanihakikishia kila kitu kiko sawa, alisema.
Kadri siku zilivyozidi kelele juu ya Richmond zikazidi hivyo akaamua kuwaita wakubwa wote serikalini wakiongozwa na katibu mkuu kiongozi, Philemon Luhanjo na kuwambia waangalie uwezekano wa kuvunja mkataba huo.
Lowassa alijitetea kuwa, wakubwa hao wakaomba awape muda wa saa moja kupitia vipengele vya mkataba huo na baada ya hapo walikuja na maneno kuwa isingewezekana kuvunja mkataba huo kwani serikali ingepata hasara.
Lakini mimi niliwauliza mbona tumevunja mkataba na City water wakaniambia aah mzee achana na hilo jambo kwa sababu liko mahakamani, hii ndio hali halisi ya mkataba wa Richmond,"alisema Lowassa.
Alisema binafsi amekubali kuwajibika kwa makosa ya walio chini yake lakini alirejea kauli yake kuwa kamati teule ya Bunge haikumtendea haki kwa kutomhoji kwani anaamini kama ingemhoji isingeandika taarifa kama ile.
"Niliona nisipoachia ngazi hali ya mambo katika chama changu ingekuwa mbaya. Napenda niweke jambo hili sawa kuwa sikuwajibika kwa sababu nilipata chochote Richmond.
Lowassa aliwataka wananchi wa Jimbo la Monduli kutembea kifua mbele, huku wakitambua kuwa yeye hajawahi kupokea rushwa wala hana mpango wa kufanya hivyo bali amewajibika kwa makosa ya walio chini yake.
Kwa upande wake, Askofu wa Dayosisi ya mkoani Arusha ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT), Thomas Laizer alitumia nafasi huyo kuwapiga vijembe wale wanaodhihaki kujiuzulu kwa Lowassa.
Ukuni ulioko kwenye kona usiucheke ukuni ulioko jikoni ukiungua kwa sababu nao unasubiri kuungua,alisema Askofu Laizer bila kufafanua lakini akashangiliwa na mamia kwa maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Hata hivyo baada ya kijembe hicho ndipo Askofu Laizer alipotoa kauli yeye utata akitaka kila mtu abebe mzigo wake na akakemea tabia iliyoibuka hivi sasa ambapo kila Mmasai anayeonekana mjini anaitwa Richmond.
Kuhusu ufisadi na rushwa sisi hatujui kilichotokea lakini kama ni ufisadi basi tunaungana na Rais Jakaya Kikwete kupita vita rushwa kejeli dhidi ya wamasai kuitwa Rinchmond haifai kila mtu anabeba mzigo wake, alisema.
Lowassa aliwasili katika uwanja mdogo wa ndege wa Mjini Arusha saa 6:51 mchana na kulakiwa na viongozi mbalimbali wa chama cha mapinduzi(CCM) na wale wa kidini pamoja na umati mkubwa wa wananchi.
Katika eneo hilo la uwanja, makundi ya vijana,wanawake na wanaume wakiwa wamebeba mabango mbalimbali ya kumkaribisha Lowassa huku mengine yakimtambulisha kama Shujaa wa karne.
Baadhi ya mabango hayo yalisomeka Shujaa wetu umeonyesha mfano usife moyo, Tupo pamoja nawe, Wana Monduli tunakuamini na Mheshimiwa Lowassa wewe ni Mbunge wetu 2005-2025.
Mara baada ya kusalimiana na baadhi ya viongozi na wananchi waliojitokeza kumlaki uwanjani hapo, Lowassa alipakia katika gari aina ya Toyota Landcruiser likiwa limewekewa ngao ya jadi mbele ya namba za usajili za gari hilo.
Msafara wa Lowassa ambao haujawahi kuonekana kutokana na wingi wa magari na wananchi ulianzia katika uwanja huo wa ndege huku magari yakifunga barabara ya Arusha-Monduli yakitembea pande zote mbili za barabara.
Hii ilifanya magari yaliyokuwa yakitokea Babati, Hanang, Mto wa Mbu, Karatu na mikoa mingine kwenda Arusha yanayotumia barabara hiyo kujikuta yakiegeshwa pembeni ya barabara ili kupisha msafara huo.
Alipofika Jimboni kwake alikwenda moja kwa moja hadi nyumbani kwake na kupumzika kwa muda kisha alikwenda katika eneo aliloandaliwa kuhutubia huku akiwa ametandikiwa zulia jekundu kama viongozi wa kitaifa.