Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

Amekuwa akitamba... anajiamini nini hasa huyu baba?

...... lakini baba huyu toka atoke amekuwa kwenye media hata kuliko alipokuwepo kwenye power, kulikoni? Kwani wa kuamua awe kiongozi au asiwe ni nani yeye au sisi wananchi?

Huyu ameshindwa kuijibu akiwa madarakani, sasa ataweza vipi kuijibu akiwa nje? It is about time mtu mzima amwambie wazi kuwa we do not miss him, na kwamba as a nation wa are just doing fine!
Mkuu naona GARI lako umelifunga si kwa funguo tu,bali na Kofuli juu yake kabisaa!! safi sana.
 
Na bado nazidi kuamini kuwa kitendo cha kutokuhojiwa na kamati kilipangwa, pengine hata kina Mwakyembe hawakujua kuwa wanaingizwa mkenge waliposhauriwa ama walipoamua kutokumhoji Lowassa. Huyo aliyepanga na kufanikisha hili ni tactician hasa aliyefuzu intelligensia ya kifisadi!

Hapo hata mimi ndipo pananifikirisha sana...nadhani ni eneo la kufanyia kazi. Was it by mere chance or by real choice?
 
Hapo hata mimi ndipo pananifikirisha sana...nadhani ni eneo la kufanyia kazi. Was it by mere chance or by real choice?

Mazingira ya sasa yanaashiria kuwa the intended end was to whitewash Lowassa after the scandal na hivyo means ya kufikia lengo hilo ni kuhakikisha hahojiwi na kamati ili aendelee kupata ukumbi wa kueleza upande wake akiwa free and unchallenged (hakika nani anaye-challenge wahutubiaji kwenye mikutano ya hadhara?). Jimboni kwake kesharejesha imani, na with time ata-reclaim all his territories in a triumphant comeback!
 
Ndugu zangu wa JF, hii ni breaking news: Sasa imethibitika kuwa yule waziri wetu mkuu ambaye aliamua kuachia ngazi kwa kuhusika; iwe moja kwa moja au vingevyo, anatarajia kurejea serikalini kwa nguvu zote na kwamba ameanza kujifananisha na alhaj Ali Hassan Mwinyi, yule rais wetu wa awamu ya pili.

Lowassa kasema atarejea kwa nguvu zote na hakika wabaya wake watakiona cha mtema kuni. Nadhani ana uhakika huo na habari zinasema ameshamueleza Kikwete, kumbukeni ni shwahiba wake mkubwa na ni jicho lake- elewa hajaomba ametaka. Na atapewa.

Miongoni mwa mikakati ya kurejea kwenye serikali ni eti kuhakikisha kuwa nia yake ya kuiongoza Tanzania inafanikiwa kwa njia yoyote ile. Kumbuka amekuwa na nia hiy siku zote mara baada ya kuingia kwenye siasa baada ya kuwa amechuma fedha nyingi kutoka AICC na maeneo mengine, ikiwemo kipato kikubwa kutoka kwenye nyumba zake nyingi Dar na Arusha ambazo zote ziko kwenye prime areas.

Endapo atakosa nafasi hiyo, amemuandaa mtu ambaye Kamanda wenu ameanza kumtafuta ili kuzungumza naye na baadaye kuweka maelezo yake JF.

Waandishi wa habari ni miongoni mwa watu waliotengewa fedha nyingi kwa kazi hiyo. Miongoni mwa mikakati ya awali ni kugeuza mwelekeo wa kumtengeneza Lowassa rais wa mwaka 2015 na kumsafisha kwanza kwa kutumia magazeti ya Mtanzania, Rai, The African, Tazama na huenda fedha hizo zikapenyezwa kwenye vyombo vingene.

Haya kazi kwenu wana JF- huenda tukampata Rais Lowassa, rais Rostam au Rais Msabaha miaka michache ijayo.

Tuinusuru Tanzania yetu kwa nguvu zote.


Sikatai anaweza kuwa Rais kama tu ataiue JF na wana JF wake.

Unajua fedha inaweza kufanya mengi na mengi makuu.
Namkaribisha kwa mikono miwili alete watu wake hapa JF wajenge hoja za kumsafisha Lowassa.

Kabla ya 2010 ni kweli tutaona mengi na mengi mazuri.

Nimewahi kusikia watu wakifanya MONEY LAUNDERING lakini sijawahi sikia tajiri yeyote akifanya HUMAN LAUNDERING( Lowassa laundering).

kama ata under go plastic suggery na kuja na jina jipya ni kweli tunaweza katwa maboya tukamchagua.

Tukishindwa hapa JF tuna njia nyingine binafsi za kusitisha tamaa yake.
 
Huyu Jamaa inabidi asaidiwe msione ajabu akazimia gafla siku atakaposhindwa kujitoa katka hili
 
Lowassa asitumie neno kutohojiwa kwamba ndiyo asili ya yeye kuonewa na kuachia ngazi.

Nafikiri huuni muda mwafaka wa kuweka vithibi vyote vya kamati hadharani ili tuende sambamba na MH Mamvi.

Mbona alipodai kwamba kamati ile ya kuchunguza mambo ya Reginand Mengi na yule muhindi imekula Rushwa, kamati likuja juu nakutaka ahojiwe lakini Spika aliiomba kamati isimuhoji kutokana na cheo chake wa uwaziri mkuu na yeye Lowassa jambo hilo leo hii halipigii kelele hata kidogo?

Spika alipo agiza asihojiwe kwa sababu ya cheo chake aliona Rungu lake la uwaziri mkuu linafanya kazi yake baraa baraa,
kwamba watu wanamwogopa hawana cha kumfanya.
Unaona!? Kamati imeshindwa kunihoji. mimi ndo dume lao, rais mtarajiwa.
Lakini kamati ya Dr mwakyembe ilipoacha kumhoji pengine kwa kutumia busara ile ile ya Spika, na wabunge wa SISIEMU kupania kutompa back up, ndipo sasa anaona anawe kwa kutumia hoja ambayo awali aliiona inamjenga.

Lowassa na genge lake watatawala tu kama miili ya wengi wetu itakuwa viwiliwili visivyo na Roho sivyo kazi ipo.
 
This guy is a looser, and he need reality check. Kama ulikuwa unajua sakata la Net Group why didn't you came back to the public and mention the whole scum?

I believe kwamba ataka kujishauwa tuu kama hajafanya huu wizi wote, lakini one thing i found interesting ni hiyo confidence yake. Kwa miaka mingi sana Watanzania tumekuwa undervalued kwamba we're stupid, what Lowassa forgot is we're in 21 century. No one, i mean no one will even gave him ujumbe wa nyumba kumi. CCM wameosha mapungufu kwa kuwafuga wezi hawa, yes i called them wezi. Karamangi, Lowassa and Msabaha supposed to be in Segerea au Ukonga at this moment.

Lowassa is in state of denial, lakini one of this days atakubali kwamba the fight is over, and his days are numbered. One thing i can assure you guys, there is one day this people will face justice. They will provides answers for many questions that many Tanzania have for years. There families will understand the down side of injustice. That day will come, sooner or later.
 
Kuna kitu EL anajichanganya hapa (au ana malengo fulani?), kwamba yeye kama WM ALISHAURI serikali (TANESCO?) ivunje mkataba na Richmond baada ya kuona (kutamabua/kuhisi?) kwamba kampuni ile ni ya kitapeli.

WM alipaswa kuelekeza kwamba mkataba (ambao ni zao la utapeli) uvunjwe ( WM anawaelekeza walio chini yake na si kuwashauri - nikosolewe ikiwa ni tofauti)!

Je, EL anataka kutuambia kwamba alimshauri mkuu wake kisha akapuuzwa au aliwaelekeza watu wa chini yake kisha wakampuuza? Kama alipuuzwa alifanya au alihisi nini?

Tafadhali Mhe. EL fikiria njia nyingine ya kurejea kwenye chati, hii unayotumia haifanyi kazi na imepitwa na wakati, it might work in Monduli but beyond that, forget about it. Usijifananishe na Mzee Mwinyi au wengine.

Au itatimia ile ndoto ya JKN (RIP) kwamba angependa kuwe na CCM mbili? Yaani CCM MAFISADI (japo haitatamkwa hadharani) na CCM WAZALENDO?
 
Kabla ya kurudi serikalini atuambie ni nani anahusika na RDC,sababu kila mtu anasem ahusiki na pesa za RIchmond ina maana wanamjua mhusika wa richmond,mie namuomba Lowassa au msabaha au Karamagi atuelezee,na hao waandishi wa habari waende wakamuulize maswali haya .
 
Lowassa asitumie neno kutohojiwa kwamba ndiyo asili ya yeye kuonewa na kuachia ngazi.
Hoja hii si amefundishwa na Mwanakijji?nakumbuka makala ya mwanakijiji aliyoitoa kesho yake kuelezea suala la Lowasssa kuanguka mara ya Pili.alkiongelea suala la Lowasaa kutohojiwa ..ila MZee Mwanakijiji naomba umhoji this week akuelezee ni nani anahusika na dili la RDC kama yeye hakuhusika ,na lazima awe anajua sababu aliishauri kamati iwastose kwa sababu ni kampuni Tapeli.

Mie nadhani Lowassa ni kioo cha Mtu Mpole wa kucheka cheka
 
Juzi Mh. Mbunge wa Monduli aliongea na wapiga kura wake, kama sio wapandikizwa, pamoja na mbwembwe nyingi za msafara na maokezi makubwa inayodaiwa hayajawahi kutokea, pia tulimsikia akiwaambia hao wapiga kura wake kwamba yeye sio mfisadi wala hajala rushwa ya Richmond, hakuishia hapo, anadai ameangushwa na watendaji wake, to me it seems as if hana utetezi of which sidhani kama kuna Mtz ane hitaji kusikia Lowasa akiji tetea. Ushauri wa BURE KWAKE ni kumwambia Lowasa NYAMAZA TUMEKUSIKIA. Umekeuwa Pm yamekushinda chunga mdomo wako.

THE PAST HAS GONE, USILAZIMISHE WATU WAENDELEE KUWA NA HASIRA NA WEWE.
 
TUTAWARUSHA KWENYE FORUM ZOTE HAO WAANDISHI NA MAGAZETI YAO NA WAKIFANYA HIVYO TUTACOPY MAKALA ZAO NAKUWAONYESHA MABOSS WAO ILI WAFUTWE KAZI NA KWA KUPOKEA RUSHWA MAANA WATAKUWA WAMEKUWA MAADUI ZETU..
 
Hwshima mbele wakuu!
Natumai wengi wetu tumesoma magazeti ya jana,na labda tumekua makini kufuatilia habari za lowassa jana kwa umakini,katika mtanzania ya jana,Deo Balile,kaindika habari ambayo iko very sensitional,haiko kimaadili kabisaaaa!kaandika very unprofesional,sasa naamini kuwa nayeye kahongwa,yumo kundini,zaidi,zaidi tafuteni hilo gazeti.
 
Jamani,mnakumbuka kulikua na mahojiano ya lowassa kwenye TVT,jmosi iliyopita?na nikwanini yalikatizwa ghafla tu baada ya kujielezea kwake?
Tafadhali mwenye taarifa atuelezee jamani.
 
sIKU AKIREJEA SERIKALINI ETI KAMA RAI MJUE KABISA HAKUNA TZ YENYE AMANI TENA KUTAKUWA KAMA ELDORET KULE KENYA.hAO WAANDISHI WALOHONGWA NDIO TUMEANZA KUWAONA NA SIE HATUWEZI KUKUBALI KUWA RAIS YEYE LOWASA NI MPAKA WATZ TUAMUE WENYEWE.Jamanieee ccm si wamnyang'anye uanachama aache kukisumbua chama na hao akina RA PIA.Ataishia kusema kaonewa kwann hakwenda kuwaeleza kamati ukweli alioujua yeye kama waziri mkuu?Sitaki kusikia kabisa etii kamati haikunihoji.
 
Huyu jamaa akirudi madarakani kwa njia yoyote lazima tukubali kuitwa wajinga. Sasa hivi Tanzania inaendelea kuilipa kampuni hewa mamilioni ya pesa yeye anapeta tu, na uwaziri mkuu wake has proved to be one of the lowest and absurd in the history of Tanzania, nani atamruhusu kuwa President wetu? Au ataanza spin nyingine!!
 
Hoja hii si amefundishwa na Mwanakijji?nakumbuka makala ya mwanakijiji aliyoitoa kesho yake kuelezea suala la Lowasssa kuanguka mara ya Pili.alkiongelea suala la Lowasaa kutohojiwa ..ila MZee Mwanakijiji naomba umhoji this week akuelezee ni nani anahusika na dili la RDC kama yeye hakuhusika ,na lazima awe anajua sababu aliishauri kamati iwastose kwa sababu ni kampuni Tapeli.

Mie nadhani Lowassa ni kioo cha Mtu Mpole wa kucheka cheka

Mkuu Gembe kuna makala ya jana ya Ansbert Ngurumo inayoelekea huko , na naibadika hapa chini. I salute Ngurumo, he can real call a spade a spade.

YALIYOTOKEA yametokea, lakini baadhi yetu bado tunapata shida kutenganisha majina haya mawili – Jakaya Kikwete na Edward Lowassa.

Na kama tungeweza kuhoji, labda kifalsafa kidogo, tungependa kujua Kikwete na Lowassa watakuwa watu wa namna gani miaka 2000 ijayo!

Ni wazi, kama mimi na wewe, watakuwa wametoweka katika uso wa dunia, lakini kazi zao na majina yao vitabaki kuwatangaza kwa mema au mabaya waliyowatendea Watanzania.

Nataka kuamini kwamba, kwa vyovyote watakavyokuwa wanafahamika, hawatakuwa wametenganishwa litakapokuwa linajadiliwa suala la historia ya uongozi na utawala wa Tanzania.

Zipo sababu zaidi ya 1,000. Hadi sasa, chache tu ndizo zinajadiliwa. Na hatutaacha kuwajadili hadi hapo tutakapohakikisha kuwa historia imeandikwa kikamilifu, bila kupotoshwa, kuhusu athari za umoja, urafiki, uswahiba na ‘usanii’ wa Kikwete na Lowassa.

Kwa baadhi yetu tunaowafahamu kiasi wawili hawa, si makosa makubwa kusema kwamba, kisiasa, Lowassa ni kioo cha Kikwete.

Ni vigumu kumshangilia au kumzomea Lowassa ukamuacha Kikwete. Ndivyo walivyojiunda, ndivyo walivyokuwa na ndivyo wanavyoishi.

Mojawapo ya mambo ambayo yamesemwa sana kuhusu maswahiba hawa, ni jinsi Lowassa alivyopandikiza wazo la urais kichwani na moyoni mwa Kikwete kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 1995.

Labda hatutakubaliana wote kuhusu hili, lakini sehemu ya ukweli ni kwamba, ndoto ya urais ilianzia kwa Lowassa. Akamwendea rafiki yake na wakawa na mjadala unaofanana hivi:

EL: Jakaya, nataka kuweka jina kugombea urais kipindi hiki. Na wewe weka jina tujaribu.

JK: Tutaweza lakini? Mbona mimi bado ni mchanga kisiasa?

EL: Si tuweke tu majina? Kwani hata tukikosa tuna hasara gani? Uchanga maana yake nini? Kwani urais unasomewa?...

Wanaokumbuka mchakato wa kugombea urais mwaka 1995, mwishoni mwa awamu ya Mzee Ali Hassan Mwinyi, watakubaliana nami kwamba baada ya Augustine Mrema, jina la Lowassa lilikuwa linavuma kama lilivyokuwa la John Magufuli katika awamu ya Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Lowassa alikuwa na mtandao wa makada vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliomuunga mkono nchi nzima. Alikuwa akiungwa mkono na baadhi ya wanahabari mahiri waliokuwa wakijua anachofanya.

Tulimsikia na kumsoma sana Lowassa katika vyombo vya habari; akizuia hili, akiruhusu lile, akivunja hili na kujenga lile, alipokuwa Waziri wa Nyumba na Makazi.

Hapana shaka kwamba Lowassa ndiye muasisi halisi wa dhana ya mtandao wa Kikwete tunaozungumzia leo; na ndiye amekuwa ‘baba’ na mratibu mkuu wa mtandao huo.

Yawezekana pale alipomwendea Kikwete na kumshauri waweke majina, moyoni mwake aliamini kwamba Kikwete – wakati huo akiwa Waziri wa Fedha - angekuwa msindikizaji tu. Kumbe yeye ndiye alikuwa anaanza safari ya kumsindikiza Kikwete!

Ghafla wakakubaliana, wakachukua fomu ‘kusindikizana.’ Wakala yamini; kwamba atakayedondoka amuunge mkono mwenzake. Na atakayefanikiwa kuwa rais, amteue mwingine kuwa waziri mkuu.

Baadaye kidogo wawili hao wakaitwa ‘Boyz II Men’, wakachukua na kurejesha fomu kwa mbwembwe. Kwa bahati mbaya yao (wakati huo), ndoto yao ilizimwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwanza alimzuia Lowassa kugombea - kwa sababu alizojua. Lakini Lowassa ndiye alikuwa na wafuasi wengi walioandaliwa (mtandao). Katika kujitoa, Lowassa akawaomba wafuasi wake wamuunge mkono Kikwete.

Ndivyo Kikwete alivyopata nguvu ya ghafla na ya ajabu hadi akawa miongoni mwa ‘Tatu Bora’ – Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na Cleopa Msuya. Ndivyo alivyochomoza na kudiriki kuwashinda wenzake.

Mwalimu Nyerere, kama alivyofanya kwa Lowassa, akamzuia pia Kikwete, kwa staili ya kiungwana zaidi.

Baada ya yote tunayoshuhudia chini ya uongozi wa Kikwete sasa, napata shida kuelewa Kikwete aliyegombea ghafla mwaka 1995 angeongozaje nchi hii! Kama baada ya maandalizi ya miaka 10, mambo yenyewe ndiyo haya tunayoshuhudia leo, nadiriki kusema kwamba katika hili, Mwalimu Nyerere alikuwa sahihi sana kuweka vizuizi vyake.

Maana tukizingatia Tanzania ya Mzee Mwinyi ilipoishia, na Mzee Mkapa alipoitoa na kuifikisha kwa miaka 10; tukipalinganisha na ujanja ujanja na usanii unaofanyika sasa katika miaka miwili tu ya utawala wa Kikwete, baadhi yetu tunachelea kusema kwamba Watanzania tulifanya makosa kukifungua kile ambacho kilifungwa na Mwalimu Nyerere.

Na hapa ndipo ulipo ushindi wa Lowassa dhidi ya Nyerere. Mtandao wa Lowassa haukufa. Ukageuka na kuwa mtandao wa Kikwete.

Siku alipokataliwa na Nyerere, ndiyo siku mtandao huo ulianza upya kazi ya kumsimika Kikwete kwa wananchi. Wapambe walitumia mbinu nyingi, hata kutuongopea eti ‘Mwalimu Nyerere alimwambia Kikwete asubiri hadi Mkapa amalize ngwe yake, ili akue kidogo na apate uzoefu.’

Baada ya miaka 10 mfululizo, Kikwete akajipenyeza kwa kila kada ya Watanzania – wanasiasa wenzake, vijana wa itikadi zote, viongozi wa dini, wanahabari, wafanyabiashara wakubwa na wadogo, wasanii wa fani zote, kina mama na hata watoto. Bahati mbaya, wote hawa hawakumjua vizuri. Lakini walimpenda na kumshabikia, hata kabla yeye hajajitokeza rasmi hadharani kutangaza nia yake ya kuutaka urais.

Ni jambo lililo wazi kwamba kazi ya kueneza mtandao huu haikufanywa na Kikwete mwenyewe. Nguzo zake kuu zimekuwa mbili - Rostam Aziz (Mbunge wa Igunga) na Edward Lowassa. Wengine wote waliunganishwa na hawa.

Lowassa ni mmoja wa mawaziri wa Mkapa aliyezunguka sana nchi nzima, akifanya kazi ya kujenga mtandao huo sambamba na kazi za wizara aliyosimamia ya Maji na Mifugo (bila Rais Mkapa kujua)! Baadaye, nguvu hiyo hiyo ndiyo ilitumika kumng’oa Pius Msekwa katika uspika wa Bunge na kumweka Samwel Sitta.

Katika muda wote huo, Rostam amebaki kuwa mwanamkakati mkuu, mfadhili na mtafutaji wa pesa za kampeni kutoka vyanzo vya ndani na nje ya nchi. Lowassa ndiye alikuwa kamanda mkuu, akisaidiwa na vijana wenye nafasi na ushawishi ndani ya CCM, waliohangaika mchana na usiku kuongeza nguvu na kukamilisha kazi ya ‘kumuuza’ Kikwete kwa wana CCM na Watanzania, hadi akawa rais.

Kikwete mwenyewe hakuonekana kuhangaika. Hata hivyo, yeye alikuwa na mbinu yake moja (kuu) aliyoitumia kuonekana mwenzetu, mtu wa watu. Haitatajwa katika makala hii, kwani si mahali pake.

Na bila kujua, Rais Mkapa akamweka Kikwete katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa miaka 10 mfululizo; akawa mbali na umma. Akamweka mbali na migogoro na misiguano ya moja kwa moja na wananchi. Akamweka mbali na kashfa za kila siku zilizowagusa mawaziri wengine. Watu wasiofuatilia wakadhani Kikwete ni dhahabu!

Si lengo langu kusimulia kila hatua iliyochukuliwa na wanamtandao kumpatia Kikwete urais. Mengi yanajulikana, na mengine yatajulikana baadaye.

Lakini napenda kusisitiza kwamba, inawezekana sana kwamba bila jitihada binafsi za Lowassa na wenzake, Kikwete asingeupata urais. Na ndiyo maana hata alipokwishaupata, licha ya shinikizo kutoka kwa baadhi ya wakongwe ndani ya CCM kwamba asimteue Lowassa kuwa waziri mkuu, Kikwete alikaidi, akamteua.

Alikuwa anajua anachofanya. Alikuwa na sababu za msingi na za muda mrefu. Alimwamini sana. Ndoto yao iliyozimwa na Nyerere, ilikuwa imetimia baada ya miaka 11 hivi ya maandalizi.

Sina shaka kwamba katika miaka miwili iliyopita, Kikwete na Lowassa wamekuwa wakikumbushana ndoto yao hiyo na jitihada zilizowafikisha hapo walipo. Bila shaka, Kikwete hakutarajia kwamba Lowassa angejiuzulu kirahisi hivyo, tena wakati huu.

Wala hakuwa na nia ya kumfukuza kazi – kwa sababu yoyote. Kikwete huyu huyu ‘anayeogopa’ kumuengua Andrew Chenge (licha ya kashfa zote za wazi zinazomwandama), asingeweza kupata ujasiri wa kumuondoa Lowassa. Hakuwa nao.

Ndiyo maana hata Chenge mwenyewe alipohojiwa na wanahabari kuhusu kurudishwa kwake katika baraza, aliwaambia waandishi: “Kamuulize rais, ndiye anajua kwanini ameniteua!”

Kwa maneno mengine, Chenge anasema rais anajua ‘makosa yangu, lakini ni mimi ninayeweza kuyasimamia ili serikali isianguke.’

Ndiyo maana pia katika mojawapo ya makala zangu, wiki mbili zilizopita, nilisema aliyevunja Baraza la Mawaziri si Kikwete bali Lowassa, ingawa kimantiki na kikatiba ni kazi ya rais kuvunja baraza.

Licha ya sifa alizopewa wakati anagombea nafasi hiyo, Kikwete ni mzito na mgumu wa kuchukua hatua kali na ngumu. Watu wengine wanamuita rais mwoga, mpenda sifa. Mifano miwili inaweza kutusaidia kusisitiza hili.

Alisubiri Gavana wa Benki Kuu, Daudi Ballali ajiuzulu ndipo akatangaza kuwa ‘amemfukuza kazi.’ Amesubiri Waziri Mkuu Edward Lowassa ajizulu ndipo akatangaza kuvunja Baraza la Mawaziri.

Anaogopa kukosea na kulaumiwa. Na hata akikosea, anataka wengine ndio waonekane wakosaji, walaumiwe. Wao wawajibike, mwenyewe asifiwe! Ndiyo maana mwanablogu na mwanahabari mwenzangu, Reginald Simon Miruko, wiki hii amediriki kusema wazi:

“Niaminivyo ni kwamba JK hawezi kuchinja hata kuku! Akichinja, anataka damu iwamwagikie wengine.”

Tukilitazama sakata la Richmond, tunaweza kukubaliana na Reginald, kwani ndivyo Kikwete alivyomfanyia Lowassa. Wafuatiliaji wa mambo wanajua, kama nilivyodokeza katika makala zangu wiki mbili zilizopita, kwamba huwezi kuzungumzia kashfa ya Richmond bila kuwataja Kikwete, Rostam na Lowassa. Kila mmoja alihusika katika hatua kadhaa.

Tutakubaliana na Reginald kwamba ingawa taifa zima linamtazama Lowassa kama fisadi mkuu katika mradi huo, ukweli ni kwamba yeye alitumwa kazi akaitekeleza.

Yawezekana Kamati ya Bunge iliuona mkono wa rais katika Richmond, ikaogopa kwenda mbele zaidi. Lakini ilijua ni rahisi kumtikisa waziri mkuu kuliko rais. Ikaamua iishie kwa waziri mkuu.

Yawezekana ndiyo maana haikumuhoji Lowassa. Maana kama Lowassa angehojiwa, angesema anachokijua – walau nje ya kiapo – kwamba baada ya uamuzi wa kikao rasmi cha Baraza la Mawaziri, rais alipata ‘ndoto mpya’ kuhusu Richmond, na akaagiza mchakato uende kwa kasi mpya; na akampa kazi ya kufanya: “Hakikisha unasimamia hili hadi linafanikiwa. Sitaki visingizio.”

Katika nchi zetu zenye katiba legelege, zinazotawaliwa na maagizo ya rais na utii wa wadogo kwa wakubwa, ambapo viongozi wanaona bora kumtii rais kuliko kuitii jamhuri, jambo hili linawezekana sana. Ndivyo mawaziri wetu wanavyotenda kazi zao; na ndiyo maana tunakwama.

Na hili ndilo kosa kuu la Lowassa. Ndiyo! Alikuwa anatii amri na maagizo ya mkubwa wake. Lakini je, hakuona kuwa yamepinda?

Akiwa mshauri wake mkuu, alimweleza hatari zinazoweza kutokea kutokana na ‘shinikizo’ hilo? Kama Kikwete alishauriwa akakataa, akang’ang’ana lazima Richmond ipate tenda hiyo, kwa nini Lowassa hakujiuzulu pale pale?

Yawezekana wote wawili walidhani mambo haya yangepita tu kwa sababu Watanzania ni wapole, watiifu, wapenda ‘amani’ na hawafuatilii mambo. Hata wakifuatilia hawahoji! Hata wakihoji, hawachukui hatua.

Walidhani yataibuka baada ya miaka 10 ya utawala wao, kama ilivyokuwa ya Mkapa na wenzake, wao wakishastaafu na kulindwa! Walikosea.

Najua jinsi Lowassa anavyofadhaika sasa kwa suala hili. Anajutia kosa lake na la mkubwa wake. Anaona ametoswa. Anabebeshwa udhaifu na ufisadi wote wa Kikwete, Rostam na wengine waliohusika na Richmond.

Nafika mahali namwonea huruma Lowassa; maana tofauti na kauli ya Reginald, zamu hii Kikwete alijaribu kuchinja kuku (Richmond), lakini damu yake imemmwagikia Lowassa.

Na bahati mbaya ni kwamba, sasa Watanzania hawamtazami mchinjaji, bali yule mwenye damu! Sijui kwanini Kikwete hakukubali kubeba lawama za uamuzi wake mwenyewe.

Ndiyo! Akubali, atuombe radhi; kuliko kuendelea kuishi katika uongo unaoviringishwa kwenye ‘ufisadi wa Lowassa.’

Lowassa alikwishajiuzulu, wala asingemrejesha. Lakini wanaojua mwenendo wa sakata hili, walitarajia kwamba hotuba ya Rais Kikwete kwa wazee wa Dar es Salaam, wiki iliyopita, ingekuwa ya maungamo yake kwa taifa.

Hiyo ndiyo ilikuwa fursa ya rais kutuambia ushiriki wake na ukweli anaoujua. Tulitarajia akiri makosa (kwani naye ni binadamu), na aahidi kujisahihisha yeye na serikali yake. Tungemsamehe. Na tungeelewa maana ya kauli yake kuhusu ‘ajali ya kisiasa’ iliyomkumba Lowassa.

Kama nilivyosema wiki iliyopita, si sahihi kwa Kikwete kusema tu kwamba Lowassa alifanya kazi kwa uzalendo, uadilifu na umakini mkubwa sana, huku akijua kwamba wananchi wanamzomea mtu huyo huyo na kumuita fisadi.

Ni wazi, wanaofahamu mchakato mzima na mwenendo wa uongozi chini ya Kikwete na Lowassa, wanajua fika kwamba unapomuita Lowassa fisadi, unamzungumzia Kikwete pia.

Sababu ni moja. Kama ilivyosemwa huko nyuma, Lowassa ndiye amekuwa mkono wa kulia wa Kikwete kwa muda mrefu. Sasa kama mkono umekatwa, mwenye kilema ni mwenye mkono.

Kwa maoni yangu, suala la Richmond halijaisha. Na haliwezi kuisha na Lowassa, hasa kama rais mwenyewe anajaribu, lakini anaogopa kulizungumzia.

Na kama anataka kumtetea na kumlilia Lowassa, na kuonekana muungwana, aseme ukweli kwamba ndiye alimtuma kuibeba Richmond.

Tayari Lowassa amechafuka, amejichafua na amechafuliwa. Mtu pekee anayeweza kumsafisha ni yule yule aliyeshiriki kumchafua - swahiba aliyembeba kwa zaidi ya miaka 10 – Kikwete!

Sisi wengine tukimtazama Lowassa katika hali aliyomo leo, tunamuona Kikwete halisi. Naamini hata Kikwete mwenyewe hahitaji kioo kujitazama sura na haiba yake halisi. Amtazame Lowassa!

Source: http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/2/24/makala4.php
 
Mystery surrounds Lowassa interview on State television
By Polycarp Machira
THE CITIZEN

The Tanzania Broadcasting Corporation (TBS) on Saturday night cut short an interview with former Prime Minister that was being aired on TVT.

While inside sources said they believed that the State-owned TV station was ordered to suspend the programme, leaving viewers in a state of confusion, TBC managing director Tido Mhando strongly refuted the claims in a telephone interview with The Citizen yesterday.

He said there was no truth in reports that TBC had implemented �orders from above, but was at pains to explain exactly what caused the programme to be cut short.

Mr Mhando added that the programme aired on Saturday was just a section of TVT�s exclusive interview with Mr Lowassa, adding that nobody ordered that the show be taken off air.

�I called the producer immediately the programme ended, asking why it had not gone to its conclusion it seems that the programme was inadvertently cut short.

The TBC boss dismissed claims that the corporation was grappling with State interference in its duties.

How could people even have such thoughts? We don't experience any interference in our work. No one exerts pressure on us to broadcast or not to air anything, he added.

Mr Mhando said TBC enjoyed cordial relations with government officials, saying no one obstructed them in their work, contrary to the belief that its radio and television programmes were censored.

He added that TVT planned to run a programme on Mr Lowassa�s two-year tenure as Prime Minister. Mr Mhando could not, however, explain why the TV station had decided to air the programme detailing the former prime minister�s successes in the post he held from December 2005.

Mr Lowassa spoke during his interview with TVT about issues that transpired within the ruling party, leading to his resignation.

It was not also clear why Saturday�s interview coincided with Mr Lowassa�s trip to his constituency where he was accorded a hero�s welcome, with his motorcade having dozens of vehicles.

Mr Lowassa has been featuring prominently in a section of the local media since he resigned after he was implicated in the irregular awarding of a tender to generate emergency power to Richmond Development Company (RDC) in 2006.

The parliamentary committee that investigated the tender process concluded in its report tabled in Parliament in Dodoma earlier this month that the Prime Minister�s Office influenced the awarding of the tender to RDC, which was neither qualified nor capable of undertaking the task.

On Saturday, Mr Lowassa received a red-carpet reception in his Monduli constituency in Arusha Region before addressing a well-attended public rally during which he denied any wrongdoing in the Richmond controversy.

He insisted that he decided to resign in order to save the ruling CCM and its government from imminent collapse after being rocked by the Richmond report.

Mr Lowassa for the first time revealed that his wife, Regina, was the only person he consulted before tendering his resignation to President Jakaya Kikwete.

I asked my wife whether she was ready for my resignation�she also asked me if I was ready�nobody else knew if I was going to resign, Mr Lowassa said.

His resignation prompted President Kikwete to dissolve the Cabinet and appoint a new line-up in its place. Mr Lowassa was succeeded by Mr Mizengo Pinda, who was Minister of State in the Prime Minister's Office responsible for regional administration and local governments.
 
This might be one of the worst things i've ever thought a man could ever do! Hivi huyu EL anafikiria sisi watanzania ni watu wa aina gani? Nadhani hajui ni kiasi gani watu wameteseka bila kujua sababu za mateso yao mpaka pale waliposikia suala la RDC na mengineyo...
Money can do a lot ila Lowassa doesn't know one thing that leadership is not about revenge. If he has enemies of which i'm sure he has a lot then with his attitude i assure him of failure...ALL your hopes will disappear in thin air!!

Someone had written him a letter telling him SILENCE CAN NEVER BE MISQUOTED BUT ONLY MISINTERPRETED... EL you better read this letter again...
 
Back
Top Bottom