Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mwenyekiti wa Liverpool, Tom Werner, amethibitisha kuwa majira ya joto yenye shughuli nyingi tayari yameanza kwa mabingwa wa Ligi Kuu ya England, huku wakiwa kwenye mazungumzo ya uhamisho wa rekodi wa Florian Wirtz na wakikaribia kukamilisha dili la mchezaji mwenzake wa Bayer Leverkusen, Jeremie Frimpong.


Liverpool ndio wanaoongoza katika kumsajili Wirtz baada ya nyota huyo kukataa kujiunga na Bayern Munich huku Manchester City wakijiondoa katika mbio hizo. Mazungumzo kuhusu ada ya uhamisho yameanza na Leverkusen, ambao wanataka pauni milioni 126 kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani. Ada hiyo itavunja rekodi ya usajili ya Liverpool ya pauni milioni 85 waliomlipa Benfica kwa ajili ya Darwin Núñez mwaka 2022. Hata hivyo, Liverpool wanatarajia kufanikisha dili hilo kwa kulipa kiasi kidogo cha awali kisha kuongeza malipo kulingana na mafanikio ya mchezaji.


Kampuni ya Fenway Sports Group, wamiliki wa Liverpool, walitumia kiasi kidogo cha pesa msimu wa kwanza wa kocha Arne Slot, wakisajili tu Federico Chiesa kutoka Juventus kwa dili ambalo linaweza kufikia pauni milioni 12, na kipa wa Valencia, Giorgi Mamardashvili kwa pauni milioni 29. Sasa klabu ipo katika nafasi ya kutumia fedha nyingi, na kuna matumaini makubwa ndani ya Anfield kuwa Wirtz na Frimpong — ambaye ana kipengele cha kuachwa kwa pauni milioni 30 — wanaweza kusajiliwa mapema katika dirisha la uhamisho.


Werner alipoulizwa kama anatarajia dirisha la usajili kuwa na shughuli nyingi kwa mabingwa wapya hao, alisema: “Tayari ni shughuli tupu.” Aliongeza kuwa anatarajia kikosi kuwa imara zaidi msimu ujao. “Tunaendelea. Kushinda hachoshi. Tunawajibika kwa mashabiki wetu wote kuirejesha timu iliyobora zaidi msimu ujao.”


Wirtz, ambaye anaweza kucheza katika nafasi tofauti za ushambuliaji, ni miongoni mwa wachezaji wanaowaniwa zaidi barani Ulaya na inaelezwa kuwa amevutiwa na mipango ya Liverpool. Mkurugenzi wa michezo wa Leverkusen, Simon Rolfes, amethibitisha Liverpool kumtaka mchezaji huyo, akisema:
“Kuna nia ya dhahiri kutoka Liverpool, hilo ni wazi, lakini kwa sasa hakuna hatua nyingine zaidi.”


Frimpong tayari amepita vipimo vya afya Liverpool na uhamisho wa beki huyo wa kulia, ambaye ni rafiki wa karibu wa Wirtz, unatarajiwa kuthibitishwa pindi dirisha la uhamisho litakapofunguliwa rasmi Jumapili. Beki wa kushoto wa Bournemouth, Milos Kerkez, pia ni moja ya malengo ya Liverpool.


Slot amesema itakuwa vyema iwapo wachezaji wapya watakuwa tayari mapema kabla ya maandalizi ya msimu mpya kuanza Julai 8. Kocha huyo wa Liverpool alisema Jumapili:
“Klabu hii haianzi shughuli za usajili leo wala kuanzia leo. Kazi kubwa imefanyika tayari nyuma ya pazia msimu huu kutambua malengo yetu na kujaribu kuwasajili. Nina imani kuwa tukielekeza kwa mchezaji sahihi, tutajaribu kumsajili. Ila tuone kama na lini hilo litatokea, maana kwa sasa ninafurahia kikosi tulichonacho.”


Bajeti ya usajili ya Liverpool inatarajiwa kuongezeka kutokana na wachezaji wanaotarajiwa kuuzwa. Núñez, Chiesa, Caoimhin Kelleher, Kostas Tsimikas na Ben Doak ni miongoni mwa wanaoweza kuondoka majira haya ya joto.


Bado kuna sintofahamu kuhusu mustakabali wa muda mrefu wa Ibrahima Konaté katika klabu hiyo. Beki huyo muhimu atakuwa anaingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Liverpool msimu huu na anakiri kuwa hakuna maendeleo makubwa katika mazungumzo ya mkataba mpya. Konaté alithibitisha:
“Maendeleo? Sio sana. Wakala wangu alikutana na klabu wiki iliyopita lakini sijui nini kitatokea. Siwezi kusema aliniambia nini lakini tusubiri tuone.”


Wakati huo huo, Virgil van Dijk amefichua kuwa ilikuwa ni wazo lake kutunukiwa kombe la Ligi Kuu na aliyekuwa nahodha na beki wa Liverpool, Alan Hansen. Hansen mwenye umri wa miaka 69 alikuwa mgonjwa mahututi msimu uliopita wa joto na alipokelewa kwa shangwe kubwa alipokabidhi kombe mbele ya mashabiki wa Kop akiwa na Van Dijk.


Nahodha huyo wa Liverpool alisema:
“Nilikuwa na dhamira ya kuhakikisha kuwa yeye ndiye atakayenikabidhi kombe. Nimefurahi ilivyotimia. Pia nina furaha kuwa Mark na Jo [McVeigh] kutoka taasisi ya Owen McVeigh Foundation, ambao nimefanya nao kazi kwa miaka kadhaa, waliweza pia kushiriki.”


“Alan Hansen ni mmoja wa mabeki bora kabisa waliowahi kuchezea klabu hii. Nilishawahi kukutana naye na kuzungumza kidogo. Nimefurahi kumuona akiwa na afya nzuri sasa. Nilifurahishwa sana kuona naye pia alikuwepo mbele ya Kop kwa sababu alistahili sana.
 

🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥ni mwendo wa kusherekea haikua rahisi 🤣🤣🤣

YNWA
 

Parade ya nguvu sana...
Jiji la Liverpool Jana lilikua ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️ ♥️
Big up kwa mashabiki wote wa Liverpool humu JF baada ya mateso mengi sana ya Kipara hatimae msimu huu tumeupata ubingwa wa 20 💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾😂😂💪🏾💪🏾

YNWA
 
But konate ni zaidi ya asset pale

His rapid transition na interceptions zinatubeba sana…. He covered a lot for Minjino
Konate ni pure talent na ndio maana anakomaa hata mkataba mpya klabu impe pesa za kueleweka. Ishu yangu kwake ni kuumia mara kwa mara ... Konate sidhani kama kuna msimu EPL alitupa gemu 30 ...klabu impe mkataba mpya na hapo hapo wasajili msaidizi mwenye umri 19 mpaka 23 hivi ili aww sub ya Konate au VVD...

Kipaji kikubwa Cha Konate ni kusoma mchezo aisee hio ni next level.

YNWA
 
1000045498.jpg

Champions again 🤓🤓🤓🤓🤓🤓
OllaChuga Oc Uingereza yote ni Red mwamba karejea kileleni.

YNWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom