Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mimi nasema gemu ambazo zinaweza kuwa sababu ya kutunyima ubingwa ni liverpool 2-2 brighton, na leicester 1-0 liverpool hii gemu leicester walikuwa na injuries Kibao Salah na Mane waliunderperfom sana
 
Na ile everton alionyimwa na man city😃😃😃 ile point ilituumiza wote everton na liverpool.
 
Hapa sare ya Brentford na chelsea ndo zilituvuruga, sare ya Mancity ni bargain kutokana na quality yao na venue.
Mkuu nimesema hio Manchester City maana ki ukweli ile gemu tulicheza vyema tulipopigwa goli tukisawazisha tulitulia tuliiii.

YNWA
 
Na ile everton alionyimwa na man city😃😃😃 ile point ilituumiza wote everton na liverpool.
Yule refa wakishuka daraja kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 68 nakwambia watamsaka alipo ndugu yaaani itakua BIG ISHU aafu akatokea mkuu wa marefa kuwaomba msamaha Everton pale ndio kabisa alitifua mambo. Yaaani VAR hata kumshauri refa akacheki mwenyewe pale kwenye ki TV hakuna...

Lakini pia sare ya Liverpool vs Tottenham maana ile gemu mapema tu Harry Kane alitakiwa ale nyekundu ajabu nayo alibakia hata refa kwenda kwenye ki TV hakuna kisa tu Harry ni Kapteni wa England khaa double standards.

YNWA
 
Mimi nasema gemu ambazo zinaweza kuwa sababu ya kutunyima ubingwa ni liverpool 2-2 brighton, na leicester 1-0 liverpool hii gemu leicester walikuwa na injuries Kibao Salah na Mane waliunderperfom sana
Mkuu Brighton hua wakiwa na kikosi kizima wanakwenda na sisi jino kwa jino katika gemu 4 za miaka ya hivu karibuni tumeshinda 1 na wao wameshinda 1 na tumetoka sare 2 hivyo utaona wakiwa kamili hua wanatumudu vyema tu.

Leicester ile ilikua hatukua clinical maana hata Rogers mechi ile alicheza na mark shift back line ajabu walituzima safi kabisa.

YNWA
 
Gemu na aston villa bro man city ajipange, tukishinda zetu zote na huakika Captain Stiv G anatupa kombe. Sijui ni kwa nn ila nina amin ivyo
Mkuu hatuna kingine zaidi ya imani.

Hivi Uefa hawa vijana wa Unai na wapo clinical sana kwenye kaunta zao na hii highline yetu tusimame vipi pale nyuma je Konate ama Matip na pale kati aanze Keita ama Hendo na je mbele tusimame vipi Diaz, Mane na Salah ama namna gani. Kimbaya zaidi hawa Villarreal hawana nyumbani na ugenini yaaani wao wanapaki treni aafu wanameza na kumeza mashambulizi aafu kaunta moja tu kwao goli watapata duuh huyu Unai noma sanaaaa.

YNWA
 

Sisi kucheza vizuri inategemea katikati kacheza nani, hiyo mechi ya sare na Brighton kati alicheza ox, Jones na Milner na Henderson yaani viungo wengine hawakuwepo lakini hata leicester ilikuwa hivyo hivyo.
 
Gemu na aston villa bro man city ajipange, tukishinda zetu zote na huakika Captain Stiv G anatupa kombe. Sijui ni kwa nn ila nina amin ivyo
Wewe mwenyewe una game za villa ,kama Steve g anawapenda Sana ,basi akaongee na bodi ya ligi mpewe point za bure dhidi yake [emoji23][emoji23][emoji23]

Kwanza mkikaa vibaya hata yeye atawaweka ,na hata angalia sijui yeye ni Liverpool [emoji23] game ya kwanza mmepata ushindi mwembamba mbona alikaza ?

Unaonesha namna gani ni mtoto mdogo Sana kijana ,!
 
inauma kweli, sijui tutumie mbinu gani kuondoa utawala wa City, 2018/19 kombe lilikua lakwetu kabisa kuliko msimu huu ila tulufeli wapi sijui

We've to accept the truth kwamba this year ni wa Man City tayari tumezinduka tukiwa tumeshachelewa kwani gape la points tulilokuwanalo dhidi ya Man City lilikuwa ni kubwa sana.
 
Kwakweli Klopp katengeneza Timu nzuri sana lakini ukweli ni kwamba katengeneza Timu katika Kipindi kisicho sahihi cha Utawala wa Pep Guardiola.
Mpaka sasahivi mafanikio tukiyopata tulistahili zaidi ya haya.
Nahofia Pep kuwa kama Ferguson kutamba kwa almost 2 decades.
Na upo uwezekano mkubwa wa Klopp kuondoka EPL bila ya kubeba tena Kombe la EPL.

Yote maisha haya.
 
Kabisa mkuu, maana walijua kufungwa lazima wafungwe tu ila yule Dogo Gordon alitupeleka mkuu sijui aliikamia game?
 
Akili yangu inaniambia liverpool wachukua hili kombe..

Tusubiri muda useme.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…