Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Tajiri msomi vp tena?
Kocha kama huyo ni wa kumpa budget anayoitaka au mchezaj anaemtaka, ni aina ya kocha ambae ukiwajibika ataifanya timu iwe na heshima milele, madrid ni team kubwa na ina heshima kwasababu ya historia yake
 
Kocha kama huyo ni wa kumpa budget anayoitaka au mchezaj anaemtaka, ni aina ya kocha ambae ukiwajibika ataifanya timu iwe na heshima milele, madrid ni team kubwa na ina heshima kwasababu ya historia yake
Ahaa kumbe unamaanisha matajiri wanamshushia hazi sio?

Onel aliondoka Aston vila kisa hataki mchezaji auzwe matajiri wakauza akawachia tim yao mpka leo inasua sua.

Kloop angekua na tamaa kama Morinho msimu huu angekaa kwa masharti ya kujazia kikosi tena apendao.

Kloop ana mapenzi na Liverpoolfc tujivunie hilo.

Yani kumbe hata hawa mil.kumi ni mpaka tuuze kuna kusajili kweli hapo?
Huku tunapiga kelele tu kumbe hata mia hajapewa.

Kazi ipo
 
nimekupata mkuu
 

Tusitumie corona kama sababu, wengine wanaosajili hawajakutana na corona?

Na ukiangalia ndani ya seasons mbili, 2018/19 na hii ya 2019/20 Liverpool haijafanya usajili wowote wa kuumiza kichwa wakati imetengeneza hela nzuri sana.

Tutafute sababu nyingine.
 
Well said kaka... Hilo la effect za corona alitaja kipindi fulani Klopp pindi Timo alivyokwenda Chelsea, alizungumza pia la kulipa mishahara maana ndogo kama sikosei alikua anadai £200,000/= kwa wiki sasa hio peke ingeleta instability kwenye timu maana moja ya nguzo kuu ya kujenga harmony kwenye timu ni kua mfumo wa mshahara rafiki means kua rewarded kutokana na kazi kazi nk...

Ukiangalia kwa umakini ni kama vile lazima tuuze ili tununue aisee ndio maana hakuna amsha amsha kama kwa wengine... Naona Wilson atakua wa pili kuuzwa na kwa bei ya £15m sio mbaya soko hili..hivyo muda wowote utaona Jamaal anatua..

Muda utasema ndugu tuwe na subira kwa Klopp anaweza hata asinunue huyu yaani..

YNWA
 

Mimi nachoona, matajiri wamekaza kutoa mpunga, na inabidi Klopp awape backup ya visingizio.

Timu imefika Final UEFA 2018, imechukua UEFA 2019 (hapo ni almost £160m zimetengenezwa), imekuwa moja ya top earners EPL kwa 2018, 2019 now 2020.

Ukiangalia net spent (player purchases vs sales) tuko below £100m, kwa nini tusisajili?

Tulifurahi sana kupata dili la Nike na tukawa tunashangilia sana kwamba it is time wachezaji wakubwa watakuja kwa sababu tutakuwa na uwezo wa kuwalipa.

So, what is the difference na NB kama tunaogopa kuchukua mchezaji kisa mshahara?

Jamani, tusije kufanya kama alichofanya Wenger na invincibles yake.
 

Hizi hoja za Instability kwenye Timu kwasababu ya Mishahara zilishapitwa na Wakati!
Mbona Lallana walikuwa Wakimlipa £120K kwa kukaa kwenye Benchi tu huku wakina Mane wanaojituma na kuleta mafanikio wanalipwa £90M?
 
Ukweli usiofichika ni kwamba Klopp aliwataka Auba, Pulisic, Werner, Fekir na Coutinho lakini Matajiri (FSG) wamegoma kutoa!
Nadhani wanafidia yale matumizi yao waliyofanya kwa VVD, Alisson, Fabinho na Keita.

Wamemuuza Solanke na Danny Ings kwa hela nzuri tu lakini hawakuzitumia kusajili mpaka leo.

Hapa tusubiri U16 asajiliwe tuambiwe anajenga Future.
 
Net spend for the last 2 windows haifiki hata £10m tumenunua Taikumi, Sepp ,bei ya Elliot ni mpaka tribunal..

After selling and buying players we have spent around £92.4million for the last 5 years that the cash the owners had to top up since in many businesses we have done we have sold first and buy later....

Hivyo we are loaded with lots of cash from Tv right, UCL, EPL, ticket sales, wadhamini and the like..

Edwards works away from the media hivyo its likely hatutajua nini kinaedelea maana hata the gossip zilizopo sio concrete enough..

Hilo la Nike let's wait and see how thier effect in making us competitive in the market will help.. Maana hawa hua hawana masihara sokoni ili kuuza jerzy..

Dirisha linafungwo early October hivyo kwa sasa ni kula 🍿 🍿 🍿🍿🍿...

YNWA
 
Hizi hoja za Instability kwenye Timu kwasababu ya Mishahara zilishapitwa na Wakati!
Mbona Lallana walikuwa Wakimlipa £120K kwa kukaa kwenye Benchi tu huku wakina Mane wanaonituma na kuleta mafanikio wanalipwa £90M?
Mkuu kufanya kazi na hawa FSG itakua pasua aisee maana hata mimi binafsi nadhani pale Klopp hakutaka kusema aminyimwa pesa za kumnasa Timo akaleta hayo maneno ya covid na salary..

Ikukmbukwe Timo kuanzia January ilikua aidha atue Bayern ama Liverpool yaani hakuna mahala Chelsea walikua wanaonekana ghafla tu covid hioo na FSG wakapata sababu ya kutomnunua..

FSG kwenye mishahara ni majipu aisee sina uhakika kama Gini amesaini nyongeza kwa mambo hayo hayo.. Na hata akina Mane wakipewa ofa nono kwingine tutaisoma namba... Mpira nowadays ni pesq hakuna kingine yale mapenzi ya akina Steve ni nadra sana ukutane nayo..

Muda utasema kama kweli Klopp alivyosema kikosi alichonacho kinamtosha ilikua kweli ama la..

YNWA
 
For the last 5 years Manchester City's net spend is some £505.6million and Manchester United's is £378.9million na bado jamaa dirisha hili wameingia sokoni mazima regardless ya effect za corona ama kuuza wachezaji walionao..

Huku sisi net spend yetu ikiwa £92.4m for the past 5 years..

Ki ukweli Klopp alitakiwa all his target apewe tu aidha ni Kalidou, Timo, Kai, Sanco nk maana hizo ela zipo kabisa..

YNWA
 
Wana kop. Klopp tunambebesha mzigo mzito he deserves alot of congrats kwa mafanikio makubwa aliyotuletea kwa bajeti finyu ya usajili.

Kama nilivyotangulia kusema siku mbili zilizopita klopp anawabeba fsg na kuwatetea kwa sababu ambazo inahitaji ufikirivu angavu kuona sio sababu yenye mashiko. Ukiangalia target zake na zote zinashindikana sababu ni pesa kutolewa na fsg ila klopp huja kuto sababu za kutetea ili kumantain hali shwari ndani ya klabu.

Bado nina imani na klopp na edward kununua established player ni ishu hivyo wanalazimika kufanya scouting ya kina sana ya wachezaji ambao sio established.


Tungekua na kina mansour under klopp watu wangesaliti amri.
YNWA.
 
Net spend for the last 5 years..
Ipo hivi kwa miaka mitano iliyopita tumenunua wachezaji kwa 470.9m na kwa miaka mitano iliyopita tumeuza wachezaji kwa £378.5m hivyo ukitoa tulichouza na tulichotumia kununua utaona wamiliki ama klabu waliongezea £92.4m...

Je kwa washindani wetu hali iko vipi kwa miaka 5 iliyopita..
Manchester City wamenunua wachezaji wa £818. 5m na wameuza wachezaji £312.9m hivyo wenye timu ama timu waliongezea £505.6m..

Manchester United wamenunua wachezaji kwa £611. 1m na wameuza wachezaji kwa £232.2m na wenye timu ama klabu ikaongezea £378. 9m..

Chelsea wamenunua wachezaji wa £656.9m na wameuza wachezaji kwa £523.6m hivyo wenye timu ama klabu ikaongeza £133.2m

Arsenal wamenunua wachezaji wa £443.1m na wameuza wachezaji kwa £192.4m huku wenye timu ama klabu ikaongezea £249.0m..

Kwa ufupi Klopp na FSG kwa hio misimu mitano wametumia net spend per season ya £18.8m(£92.4m÷ 5years) ambayo ni minimal ukilinganisha na washindani wetu..

YNWA
 
Origi ni shujaa wa the best night ever at anfield..
Wewe unamchukuliaje poa?..

Mpira Una Royalty na loyalty..sio mahesabu Tu kama kampuni...
Sijawahi kuamini bahati katika mpira
Origi sio kwamba anajua mpira anabebwa na bahati hawezi kucheza mechi sita na kufunga magoli hata katika mechi nne akijitahidi sana ni mechi moja ama mbili
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…