Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Ukumbusho mzuri sana huu
Ni vizuri ungeitaja Hiyo timu yenye wings zenye pace kubwa.tuijue .

Kama ingekuwa rahisi hivyo Liverpool kufungika,mpaka sasa kwenye ligi kafungwa mechi ngapi? Au wewe ndio unaona sana kuwa shinda makocha wote wa epl waliofungwa na Liverpool mpaka sasa?

Liverpool msimu uliopita kafungwa mechi 1 tu na man city pale etihad.timu zingine zimeshindwa kuchukua point 3 kwa Liverpool.

Usijidanganye liverpool wako vizuri,ndio timu iliyoruhusu magoli machache mpaka saizi kwenye epl.unafikiri ni kitu rahisi?
 
Clean sheet msimu uliopita azikutusaidia kuchukua ubingwa sasa hivi ni mwendo wa ushindi tu.

Liverpool ndio timu iliyoruhusu goli machache mpaka sasa hivi.

Me nauwakika unawakalisha pale anfield,ingekuwa etihadi ningekuwa na wasiwasi.
Ndhani leicester ndio wameruhusu machache sio liverpool
 
CL hamuwezi kubeba msimu huu ukweli mchungu,najua mtabisha lakini ukweli utabaki palepale kikosi mlichonacho msimu huu hakina pumzi yakutosha kufanya hivyo.

La msimu huu tutaliongelea tukishachukua kwanza tuongelee hili
IMG_9532.JPG
 
Kwa haki kabisa Ginni mnamkosea heshima sana. Kumfananisha Ginni na Captain ni kumwonea kabisa.

Mbona Ginni sio mbaya kama wengine mnavyomwona?


Naanza kumwelewa Malafyale

Gini kazidiwa statistics za chances created na Henderson msimu huu

We kiungo gani umecreate chance moja tu yaani unazidiwa hata Na holding mid(kiungo mkabaji) Fabinho
 
Ollachuga Oc ni mtu wa utani. Afu pia ana mahaba na reds japo hasemi. Kule kwao hashindi, kijiwe chake ni hapa.

Ni mtani wake King Ngwaba. Anapenda utani. Msimtenge
Hahaha huyu hatengwi ni jamaa yetu Sana tu hapa hapa...

Yeye na Southern Highland na Kimario ni Wa hapa hapa tunawaelewa Sana tu...
 
Ollachuga Oc ni mtu wa utani. Afu pia ana mahaba na reds japo hasemi. Kule kwao hashindi, kijiwe chake ni hapa.

Ni mtani wake King Ngwaba. Anapenda utani. Msimtenge

Ukitaka kuujua utani wa Ollachuga mtazame akidundwa tu, Atapita nyuzi zote kutangaza kuwa hakuna wa kuifunga Timu iliyomdunda yeye!
Lakini chakushangaza kapigwa 4 na Manure, Akapigwa tena 2 na Manure lakini hakuwahi kutangaza kuwa hakuna wa Kumfunga Manure bali hata Manure acheze na Biashara United ataishia kusema Manure anafungwa.
 
Gini kazidiwa statistics za chances created na Henderson msimu huu

We kiungo gani umecreate chance moja tu yaani unazidiwa hata Na holding mid(kiungo mkabaji) Fabinho

Mkuu naona umekomaa na GINI?

Elewa hivi! Sio kwamba sisi hapa tunamuona GINI ni Messi! But kwenye kikosi chetu kuna baadhi ya Positions tuna mchezaji mmoja mmoja tu! Kwa mfano:-

LB tuna Robbo pekee
RB tuna TAA pekee
LW tuna Mane pekee
RW tuna Salah pekee
DM tuna Fabinho pekee
CM tuna GINI pekee

Sehmu tulizokuwa tuna angalau mbadala ni:-

AM tuna Hendo na OX
CB tuna VVD, MATIP, GOMEZ na LOVREN.
FW tuna Bobby na Origi
GK tuna Alison na Adrian

Kwanini sikuwaeka hawa Lallana, Keita, Xhaqiri na Milner?
Lallana simuhesabu kuwa ni mchezaji
Keita ni injury prone kwahiyo kabla ya kupona vizuri anarudi tena kwenye injury! So, ni vigumu kurejea kwenye ubora wake.
Xhaqiri hayupo kwenye mipango ya Klopp
Milner kutokana na umri wake 34yrs ni Backup player tu.

Sasa Mkuu katika positions hizo zenye Mchezaji mmoja tu hata ulalamike basi Klopp hana la kufanya ndiyomana humu wengi wetu tunamlilia Hendo na Lovren tu kwasababu Mbadala wa hawa yupo.

Hendo vs OX
Lovren vs Matip and Gomez

Lakini GINI kuanza ni Lazima kwa sababu hana mbadala.
Tuliyemtegemea kucheza position ya GINI ni Keita tu, Lakini kwasasa kumchezesha Keita ni kujirisk kwa baada ya mechi 2 tu tutamrudisha Wodini. Tusubiri apone kwanza.

Ni sawa na wanaomponda Salah! Hata aharibu kiasi gani bado ataendelea kucheza tu coz hakuna mbadala wa kumueka benchi.

Kwahiyo kwasasa tuendelee na GINI wetu tu.
 
Gini kazidiwa statistics za chances created na Henderson msimu huu

We kiungo gani umecreate chance moja tu yaani unazidiwa hata Na holding mid(kiungo mkabaji) Fabinho

Jengine ni kwamba tuliwahi kueka mjadala hapa tukasema mbona GINI wa Timu ya Taifa ni Tofauti na Huyu wa Liverpool?

Jibu likawa ni moja tu! Wa Timu ya Taifa anachezeshwa position na Mfumo tofauti na huyu wa Liverpool.
Na ndiyomana kwenye Timu ya Taifa kama unafatili GINI kila mechi anafunga goli.

Sasa kwa Timu ya Liverpool GINI huwezi kumlinganisha na Hendo coz GINI anacheza chini kuliko Hendo.

GINI anachezeshwa kama mido ya pili kutoka chini as CM kutokea kushoto but Hendo anachezeshwa mido ya juu kutokea kulia.

Na ndoyomana GINI anafanywa kwa 100% awe Defensive Minded Midfielder.

Na huu ndiyo mfumo wetu kwa sasa GINI na FABINHO wanasaidia kudefend While Robbo and TAA ndiyo attackers.

Hendo ni created ingawa hana uwezo wa kufanya hivyo that's why tunamlilia OX aanze na Keita apone.

Mkuu GINI si mbovu kama ulivyojiaminisha but anachezeshwa na kocha aonekane hivyo unavyomuona.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom