Mkuu Ngoja nikukumbushe kitu!
Sisi tuliyaona mapema haya kwasababu tunaamini Biashara ni Asubuhi.
Kipindi Cha January Wakati Klopp Anajaribujaribu Mechi tulipinga Vikali kutoa Draw na timu zilizojichokea! Lakini Munakumbuka Mulituambiaje?
Mulituambia kuwa "Nyinyi tatizo lenu Munataka Mushinde Kila Mchezo".
Mukaendelea kutwambia kuwa "Kutoa Sare baadhi ya game si mbaya, Hata Man City atadondosha Points".
Mara Mukasisitiza "Bado tupo Pazuri".
Sasa sisi tuliokuwa tukizilalamikia draw zisizo za lazima tuliamini tokea kipindi kile kuwa uzembe tunaoufanya utatucost baadae! Na tukajua kuwa tayari tumeshapoteza nafasi.
Sasa Mkuu Mulitulaumu kuwa 'tulitaka kushinda kila mechi'... Kwanini sasahivi na nyinyi munataka kushinda kila mechi? Si tuachie tu game ya mwisho tufungwe!
Sasa tuendelee kujisifia performance tu kwa kupost Articles za watu hapa! Eti tunaeka habari Guardiola anatusifia! Alaa! Yeye achukue kombe halafu sisi tujisifie eti tumemfukuza????? Kweli sisi ni Loserfools wanaotuita hawajakosea.
Nitaona watu ni wa ajabu sana kujisifia Msimu huu tumefanya vizuri wakati tukiwa ni Zero Trophy. Coz ninachoamini Mimi ni Makombe tu kwenye mpira na si kukusanya Points nyingi.
Hata tukimaliza ligi na Points 300 kama hatuna kombe basi kazi bure! Tutabakia kuwa sisi ni Loser tu.