Kiongozi,wewe haujuagi kabisa kuchanganya hisia zako na facts..!
Ni kitu kigumu sana kukiona kwa mashabiki wa timu mbalimbali humu JF..!
Wengi wetu humu JF huwa tunafanya hisia zetu kuwa facts..!
Kama mshabiki kuna muda hisia lazima zikuchukue, ila uhalisia ni kitu muhimu sana kwa sababu inakuweka katika nafasi ya kukupunguzia machungu unapofungwa na timu bora zaidi yako.
Kuna vitu viko wazi, huhitaji nguvu kujua kwamba tunaongoza ligi kwa sababu za kibahati na si uwezo.
Kwangu mimi Man City ni the best EPL msimu huu, iko well balanced kila idara, kilichowakuta majeruhi ya KDB na Fernandinho ilikuwa bahati sana na tuliitumia vizuri December.
Man Utd ugomvi wa wachezaji na kocha ni bahati nyingine kwetu ilikuwa, naamini kama wangeanza na morale hii tungekuwa nao level.
The same to Chelsea, kocha kaja na mbinu mpya, watu wameisoma, kashindwa kubadilika, imeua morale kwa wachezaji sasa hivi wanapigwa tu, hiyo ni bahati nyingine pia kwetu.
Tottenham tumeachana nao points 5 tu, nao majeruhi ya key players yanawatesa, otherwise walikuwa na kikosi ambacho kina weight nzuri pia.
Liverpool tulifanya upgrade kwa VVD na Allison, partnership ya Gomez na VVD ilikuwa ni combination bora mimi kuwahi kuiona kwa beki zetu kwa zaidi ya miaka 10, bahati mbaya Gomez ni pancha mkononi.
You can see last year we had a very spectacular forward line, ilifunga magoli mengi sana, shida ilikuwa defense, this time defense imekuwa upgraded forwards hazifanyi yale ya msimu uliopita.
Now, majeruhi yameathiri defense, wafungaji wetu wameendelea kuwa butu, matokeo yake droo zimekuwa nyingi sana, unaweza kuona sasa hivi hata cleansheets hatuzisemi humu kama kipindi Gomez akiwa mzima.
Hali ilivyo sasa hivi hainipi amani kudhani eti nitashinda kirahisi game kubwa kama ya Man Utd, wakati Leicester na Westham wamenishinda, Crystal Palace anapata 3 goals.