Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Nimeelewa
Asante Malafyale kwa maelezo. Ni kweli Coutinho au mchezaji yeyote anayetegemewa na timu anatakiwa aondoke wakati aidha kuna mbadala au mwisho wa msimu. Ndio maana Hazard anasisitiza hataondoka katikati ya msimu Chelsea

Nadhani mimi mtaniona wa ajabu kidogo kutokana na hilo swala, simwoni jamaa kama msaliti isipokuwa alipigania kwenda sehemu alipoona pana maslahi kwake.

Kabla ya hiyo January jamaa aliomba kuhama mapema, that was July. Timu ikagoma kabisa na kuna bids kadhaa zilikataliwa mpaka transfer window ikafungwa. Ilipokuja nyingine timu zikafikia makubaliano jamaa akaondoka.

Wachezaji wanachukuliwa kama watumwa, tunasahau kwamba wako kazini, akiuzwa na timu tunasema ni business, akiomba kuondoka tunamwita msaliti.
 

Sometimes we tend to be selfish because of fighting for trophies.
 
kwa kocha tulie ni rahisi saana kuchuwa than any other cups ambazo ni mechi moja tu ya kuamua mshindi.

Can bet with anyone, this time around tuna shinda epl ila siyo UCL au FA
 

Sometimes we tend to be selfish because of fighting for trophies.

Ni swali tu Nauliza wakuu na wala siko kwenye point ya kuanzisha mjadala!!

"Kwa Mfano ikitokezea tukimaliza msimu huu with ZERO TROOHY ikapelekea wachezaji kuvunjika Moyo na hatimae SALAH, MANE, FIRMINO, VVD, ALISSON, GOMEZ na ROBERTSON wakadai kuondoka ili wakatafute mafanikio kwengine Kama Coutinho! Je ili tuoneshe kuwa tupo kiuwanamichezo kuliko uselfish, tunapaswa kuwauza wote na tukakusanye watoto Academy ili tutengeneze timu mpya?" Coz tukiwazuia ni uselfish!!!!

Mimi ninachojua mpira ni biashara! Na biashara haitazami Maslahi ya Mteja (Mchezaji) tu, Bali pia inaangalua Maslahi ya Tajiri (Mmiliki na Bodi ya Timu).
 

Ili ufanikiwe kibiashara hakuna kuangaliana usoni, kuoneana huruma kwa expense ya business, unapoona opportunity unaitumia.

Klabu inatakiwa ku-operate kwa maslahi yake kwanza, ya mteja baadae. Ndo maana Coutinho hakuachiwa haraka mpaka walipoona kwamba ni faida kumuuza at that point. Wangeona si sahihi wangeweza kuweka ngumu kwa sababu alikuwa na mkataba na angetakiwa kuutii.

Kwa upande wa mchezaji napo anachanga karata zake anaona huu ni wakati wa kujadili upepo anaamua kumove on, ubaya yeye hayuko kwenye upande wa maamuzi, na ndiyo maana tunaishia kumlabel majina kwa sababu mchezaji anapoomba kuondoka propaganda zinakuwa nyingi.
 
Grujic ni fundi haswa mzee sielewi kwanini JK alishindwa kumtumia
 


Mkuu usiniambie unataka turudi kwenye hii era

 

Better to be selfish 100% and lift trophies...
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…