"MORINHO ANAKARIBIA KUISHI GHETTO MOJA NA DAZ BABA"
maisha yana mafumbo mengi sana. Kuna nyakati naamini msanii aliyewahi kutamba na kundi la Daz Nunda Ndugu Daz Baba kuna mda anajiuliza Maswali mengi pasipo majibu.
Nahisi kuna nyakati anasikiliza nyimbo zake alipokuwa na kundi lake halafu anasikiliza nyimbo zake binafsi Kama "elimu dunia" na "umbo namba 8" basi anatoa machozi ya kiume mwenyewe.
Naamini haamini kama nyimbo za msanii kama dogo Aslay zinagusu hata nusu ya ubora wa nyimbo zake.
Hayo ndiyo Maisha ya mateso ya nafsi anayopitia msanii Daz Baba anapokuwa ghetto kwake. Hawezi mwambie mtu zaidi ya kutoa machozi ya kiume.
Kwanini Daz Baba amkaribishe Morinho kwenye Maisha magumu ya ghetto?
Toka mwisho wa msimu wa 2017-2018 wa Epl, mropokaji Josee Morinho amekuwa hana furaha na Maisha ya ardhi ya Carrington.
Morinho amekuwa akiilaumu bodi ya usajili waziwazi mbele ya vyombo vya habari kitu ambacho siyo utamaduni wa Manchester United. Morinho amekuwa na migogoro ya Mara kwa Mara na wachezaji muhimu wa timu Kama Pogba, Fellaini na Athony Martial.
Achana na mifumo ya kuudhi anayotumia ambayo inawakera akina Eric Cantona, Paul Scholes, Giggs, Neville na mastaa kibao waliotamba united.
Siku chache zilizopita Christian Ronaldo aliweka wazi kuwa alishindwa kwenda united kwasababu hayupo tayari kucheza Kama beki wa pembeni kitu ambacho ni kijembe kwa Morinho kwa kutumia mfumo wa kuwatumia left and right wingers kama mabeki wa pembeni.
Yapo mengi sana ambayo naamini Maisha ya Morinho hayana furaha kwasasa pale united. Anachofanya ni kukaa Mahali mwenyewe na anapokumbuka mafanikio yake ya nyuma basi huanza kuhisi kama dunia imemtenga Kama ilivyomtenga Daz Baba.
Kwenye moyo wa Morinho amechukizwa na usajili wa Liverpool FC, amechukizwa na kutokupewa hela ya kusajili mastaa aliokuwa anawataka, na Bado anachukizwa na Uwepo wa Gurdiola kwenye nyasi za etihad.
Ni Shabiki pekee wa united anayeishi Namtumbo anaweza akachukulia poah matokea ya Pre-sisson pale marekani dhidi ya Liverpool lakini siyo kwa watu Kama akina Sir Alex Ferguson.
Sishangazwi Sana na tetesi za Zinedine Zidane Ndani ya Old Trafford. Naamini Morinho kwasasa hayupo sehemu salama kwenye vikao vya bodi ya Manchester United.
Ni Shabiki pekee wa Nkasi ambaye anafurahia matokeo ya united kushinda kwa wartford au Leicester City huku zaidi ya dk 75 anacheza Mfumo wa kuzuia.
Nyakati hazidanganyi kwasasa... Daz Baba yupo ghetto akikumbuka jinsi dunia ya viwanja vya shoo za Daz Nunda ilivyomtenga... Wakati Daz Baba yupo ghetto la Dar es salaam kuna mreno kiburi yupo ghetto la jiji la Manchester akiwa anawaza Mawazo Sawa na Daz Baba.
Karibu Epl uniondolee Mawazo ya wanasiasa.

KEY THE DON.