Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Nimekuelewa vzr mkuu, kama ishu ni depth ya kikosi sioni atakaemzuia Man City kutetea ubingwa, msimu ukiopita tumepoteza points nyingi katika mechi dhidi ya timu zilizo nafasi za 10 kushuka chini.
Kama tungepata zile points basi tungekuwa nafasi ya pili kwa karibu sana na Man City, shida ilikuwa ni kipa,Lovren na Matip walikuwa ktk poor form,hatukuwa na defending midfielders wa kusaidia CD,upande wa attacking hatuna shida..

Angalau kwa 70% matatizo yameshughulikiwa, bado shida atakapoumia Van Dijk hana mbadala,yafaa tuongeze CD mwingine wa kiwango cha juu, upande wa kulia ni battle kati ya Clyne na T.A.A, kushoto ni Robertson na Moreno, upande wa DM Wjinaldum na milner bado wapo..

Bado naamini tunaweza kupata ubingwa kama hatutapata injuries nyingi, kutopoteza points kwa timu ndogo.Mpinzani ni Man City tu sioni kama Man u,Arsenal,Chelsea watafanya maajabu, labda Spurs coz bado ana kikosi kizuri.
Hahaha umeongea vizuri sana ila apo mwisho ndo umeharibu.

Yani unaanzanje kirahisi tu kumtoa Chelsea au Man u kwenye mbio za ubingwa? Wewe unaona kuwa una kikosi kipana sana eeh!!

Angalia sana maan msimu uliopita hujaifunga Chelsea na Man u alikukalisha vile vile ..hao man city wanafungika tu
 
Liverpool msimu huu mtacheza mpira mzuri sana, tena kuliko timu yeyote uingereza. Lakini tatizo lipo kwenye kubeba makombe. Sidhani kama mtafanikiwa kubeba kombe hata moja kutokana na approach ya kocha wenu, ambayo inafanana sana na Pochettino wa Toti. Kwa uzuri wa kikosi chenu kwa jinsi kilivyoboreshwa, ingefaa muwe na kocha kama Antonio Conte hakika angewafaa sana.

Uyo klopp kubeba kikombe chohote apo England asahau. Kama alishindwa akiwa bundersliga basi hapo England itakuwa mtihani mgumu sana kwake.

Tutakwenda kushuhudia Liverpool ikicheza mpira mzuri sana ..pengine kama Barcelona ..lakin suala la kubeba makombe itakuwa ni shughuli pevu.

Tunza hii Komenti.


Hapo umekosea! Klopp Alipokuwa na Dortmund amebeba Makombe.....

Hapa Liverpool Kilichomfanya Asibebe Kombe Mpaka Sasa ni Kuwa alichelewa Kuiboresha Timu Katika Misimu Yake Miwili ya Mwanzo Akiamini Kuwaboresha Wachezaji Aliowakuta Wakati Walikuwa ni Mizigo na Walimcost Kwa Kila Mechi! Alifanya Ukaidi Mpaka Mwisho Akaukubali Ukweli Kuwa ili afanikiwe ni Lazima aingie Sokoni...

Kwa Msimu huu siwezi ongea Kitu kwasababu Bado Kikosi chetu sio Kipana ni Kidogo Mno ambacho Mchezaji Mmoja tu Akipata injury ni Kosa!
Ila naamini iwapo Klopp ataendelea kuiboresha Timu kama Hivi anavyofanya, Basi Mbeleni Tutakuwa na Timu Nzuri tu Ya Kuweza Kubeba Kombe.
 
Benwoodburn Kumpeleka Kwa Mkopo Kwa Timu ya Sheffield United inayocheza Championship ni Kumdumaza na Si Kumboresha.

Zipo Timu za Midtable Zinazocheza #EPL ambazo zinamtaka ni bora wampleke huko ili akapate good experience ya EPL.
 
Allison na Firmino Leo wameanza Rasmi Mazoezi pamona na Kikosi Chetu.

thumb_69442_default_news_size_5.jpeg
 
Alisson Anavaa Jezi Namba 13 na Fabinho anavaa Jezi Namba 3. Bado Wachezaji Hawa hawajapewa Official Squad numbers zao.
Hii inatokana na Wote Wawili Wanataka Namba Ambazo Tayari zinawenyewe ndani ya Kikosi Chetu.
• Fabinho anataka Namba 6 ambayo anavaa Lovren.
• Alisson anataka Namba 1 ambayo anavaa Karius.
 
Alisson Anavaa Jezi Namba 13 na Fabinho anavaa Jezi Namba 3. Bado Wachezaji Hawa hawajapewa Official Squad numbers zao.
Hii inatokana na Wote Wawili Wanataka Namba Ambazo Tayari zinawenyewe ndani ya Kikosi Chetu.
• Fabinho anataka Namba 6 ambayo anavaa Lovren.
• Alisson anataka Namba 1 ambayo anavaa Karius.
Hapo patamu but Waprove kuwa hizo namba zinawafaha. Nampa hazina Tija hata avae namba 99 Kama ni bora ni bora tu.
 
Maneno Kuntu Kutoka Kwa Liverpudlian Micky Quinn:

"It would be a case of world domination for the Reds if they offloaded Dejan Lovren".

“I’m excited now for this coming season,”

“Don’t forget we got Virgil van Dijk in in January, so he’s bedded in now".

“We’ve got goals up front, a midfield to die for, Trent at right-back and Robertson at left-back, and a goalkeeper at last!".

“Dejan Lovren is the weakest link. If they got a centre-back to partner Van Dijk, then I think it would be world domination for Liverpool Football Club.”
 
Ben Woodburn Tayari ameshajiunga na Sheffield United inayocheza Championship Kwa Mkopo Wa Msimu Mmoja Wa 2018/19.
Natumai dogo atajiendeleza Vizuri tu.
 
Hawa Dortmund Wanataka Kutuchezea Mchezo Kama Waliotuchezea RB Leipzig Kwa Naby K8...

Christian Pulisic amebakisha Miaka 2 tu Katika Mkataba wake na Dortmund! Ikifika Next season atabakia na 1year jambo ambalo litashusha thamani na Dortmund watalazimika Kumuuza ili asiondoke bure.

Sasa iwapo Chelsea hawatamnunua mana Yake ni Kwamba Dortmund wanataka Watuuzie sasahivi ili kulinda thamani Yake halafu abakie palepale Kwa Dortmund Kama Tulivyofanyiwa Kwa K8 Mpaka Next season ndiyo atue Kwenye timu yetu.
 
Liverpool msimu huu mtacheza mpira mzuri sana, tena kuliko timu yeyote uingereza. Lakini tatizo lipo kwenye kubeba makombe. Sidhani kama mtafanikiwa kubeba kombe hata moja kutokana na approach ya kocha wenu, ambayo inafanana sana na Pochettino wa Toti. Kwa uzuri wa kikosi chenu kwa jinsi kilivyoboreshwa, ingefaa muwe na kocha kama Antonio Conte hakika angewafaa sana.

Uyo klopp kubeba kikombe chohote apo England asahau. Kama alishindwa akiwa bundersliga basi hapo England itakuwa mtihani mgumu sana kwake.

Tutakwenda kushuhudia Liverpool ikicheza mpira mzuri sana ..pengine kama Barcelona ..lakin suala la kubeba makombe itakuwa ni shughuli pevu.

Tunza hii Komenti.
mkuu ujeremani alibeba sana tu tena na kikosi cha kuungaunga...England ni kungumu sana
Naamimi msimuu atafanya kweli na kombe tunalihitaji sana la EPL...
 
Hawa Dortmund Wanataka Kutuchezea Mchezo Kama Waliotuchezea RB Leipzig Kwa Naby K8...

Christian Pulisic amebakisha Miaka 2 tu Katika Mkataba wake na Dortmund! Ikifika Next season atabakia na 1year jambo ambalo litashusha thamani na Dortmund watalazimika Kumuuza ili asiondoke bure.

Sasa iwapo Chelsea hawatamnunua mana Yake ni Kwamba Dortmund wanataka Watuuzie sasahivi ili kulinda thamani Yake halafu abakie palepale Kwa Dortmund Kama Tulivyofanyiwa Kwa K8 Mpaka Next season ndiyo atue Kwenye timu yetu.
mkuu hio imekaa poa anunuliwe abaki pale aje msimu ujao kuliko kumkosa kabisa, ndogo kipaji kipo
 
Ikiwa Liverpool itafanikiwa Kuwa-Offload Ings, Origi, Marcovic na Mignolet nadhani tutakuwa tumeshafanya Biashara Nzuri tu.
 
Cristian Pulisic

LIVERPOOL wanataka kurudia mpango walioufanya kwa staa wao mpya wa kimataifa wa Guinea, Naby Keita kwa kumnasa kiungo mahiri wa Borussia Dortmund, Christian Pulisic na kisha kumwacha klabuni hapo mpaka mwakani.

Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp alifanya hivyo kwa Keita msimu uliopita na yupo tayari kurudia tena kwa Pulisic ambaye ni mmoja kati ya mastaa wanaotamba katika Ligi Kuu ya Ujerumani Bundesliga na amekuwa akitakiwa na klabu mbalimbali.
 
Tottenham wanamuuza Toby
Huyu beki namkubali pale nyuma na angeanza na VVD
Sielewi why hatumchukui
Lovren ndio weakest link pale nyuma
Ningekuwa Klopp ningemchukua Musa Dembele pia


Bei Yake ndiyo imekuwa Kikwazo! Ninadhani tu..
 
"MORINHO ANAKARIBIA KUISHI GHETTO MOJA NA DAZ BABA"

maisha yana mafumbo mengi sana. Kuna nyakati naamini msanii aliyewahi kutamba na kundi la Daz Nunda Ndugu Daz Baba kuna mda anajiuliza Maswali mengi pasipo majibu.
Nahisi kuna nyakati anasikiliza nyimbo zake alipokuwa na kundi lake halafu anasikiliza nyimbo zake binafsi Kama "elimu dunia" na "umbo namba 8" basi anatoa machozi ya kiume mwenyewe.
Naamini haamini kama nyimbo za msanii kama dogo Aslay zinagusu hata nusu ya ubora wa nyimbo zake.
Hayo ndiyo Maisha ya mateso ya nafsi anayopitia msanii Daz Baba anapokuwa ghetto kwake. Hawezi mwambie mtu zaidi ya kutoa machozi ya kiume.

Kwanini Daz Baba amkaribishe Morinho kwenye Maisha magumu ya ghetto?

Toka mwisho wa msimu wa 2017-2018 wa Epl, mropokaji Josee Morinho amekuwa hana furaha na Maisha ya ardhi ya Carrington.
Morinho amekuwa akiilaumu bodi ya usajili waziwazi mbele ya vyombo vya habari kitu ambacho siyo utamaduni wa Manchester United. Morinho amekuwa na migogoro ya Mara kwa Mara na wachezaji muhimu wa timu Kama Pogba, Fellaini na Athony Martial.

Achana na mifumo ya kuudhi anayotumia ambayo inawakera akina Eric Cantona, Paul Scholes, Giggs, Neville na mastaa kibao waliotamba united.
Siku chache zilizopita Christian Ronaldo aliweka wazi kuwa alishindwa kwenda united kwasababu hayupo tayari kucheza Kama beki wa pembeni kitu ambacho ni kijembe kwa Morinho kwa kutumia mfumo wa kuwatumia left and right wingers kama mabeki wa pembeni.

Yapo mengi sana ambayo naamini Maisha ya Morinho hayana furaha kwasasa pale united. Anachofanya ni kukaa Mahali mwenyewe na anapokumbuka mafanikio yake ya nyuma basi huanza kuhisi kama dunia imemtenga Kama ilivyomtenga Daz Baba.
Kwenye moyo wa Morinho amechukizwa na usajili wa Liverpool FC, amechukizwa na kutokupewa hela ya kusajili mastaa aliokuwa anawataka, na Bado anachukizwa na Uwepo wa Gurdiola kwenye nyasi za etihad.

Ni Shabiki pekee wa united anayeishi Namtumbo anaweza akachukulia poah matokea ya Pre-sisson pale marekani dhidi ya Liverpool lakini siyo kwa watu Kama akina Sir Alex Ferguson.
Sishangazwi Sana na tetesi za Zinedine Zidane Ndani ya Old Trafford. Naamini Morinho kwasasa hayupo sehemu salama kwenye vikao vya bodi ya Manchester United.

Ni Shabiki pekee wa Nkasi ambaye anafurahia matokeo ya united kushinda kwa wartford au Leicester City huku zaidi ya dk 75 anacheza Mfumo wa kuzuia.

Nyakati hazidanganyi kwasasa... Daz Baba yupo ghetto akikumbuka jinsi dunia ya viwanja vya shoo za Daz Nunda ilivyomtenga... Wakati Daz Baba yupo ghetto la Dar es salaam kuna mreno kiburi yupo ghetto la jiji la Manchester akiwa anawaza Mawazo Sawa na Daz Baba.

Karibu Epl uniondolee Mawazo ya wanasiasa.

KEY THE DON.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom