Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

IMG_4761.JPG
 
KLOPP for life
Huyu apewe mkataba wa maisha kama enzi zile akina Bill shanky na Bob Pleasey na Jon Fagan
Kuondoka Liverpool hadi siku kifo kinamchukua!
Liverpool ni best team Ulaya as we speak now!
 
Actually, ni fainali niliyoitaka. Itapendeza, ili mzizi wa fitna ukatwe!!
Kwa mechi hizi za Roma, raundi hizi 2, liver wajirekebishe! Huu ni ukweli tu.
Liver walistahili kupita ila kama ulivyosema tatizo letu tuna kikosi kidogo sana na tatizo kubwa sana ni katikati, najuwa Keita nakuja ila bado tunahitaji mmoja zaidi, defender mmoja na striker mmoja wachezaji kama wa nne. tukipata midfielder mmoja anayeweza kukaa na mpira itakuwa tumemaliza maana tulio nao sio wabaya ila ni wazuri katika kukaba na kujituma. Hatuwezi kuwa Milner ndio tegemeo ila ni mzuri akiwa back up na hata captain wetu sio wa kuanza game kila mara. Naomba Liver wafanyie kazi sehemu hizo tutafika mbali.
 
Hongera yetu ila bado tuna mapungufu kwenye safu ya Ulinzi hasa upande wa Trent alexander-anord, nimechek game zote za Liverpool mipira Mingi inapitia kwa TAA, tusipo chukua taharadhari Madrid watapitia Sana kwa upande wa TAA
Ni kweli jana hakucheza vizuri lakini tukumbuke huyu bado mtoto mdogo miaka 19 tu na jana ilikuwa experiance nzuri kwake kucheza game ya ukubwa kiasi kile na zaid away. Ana future nzuri sababu sio mara nyingi kuwa na defender 19yrs kutegemewe kikosini.
 
Hongera yetu ila bado tuna mapungufu kwenye safu ya Ulinzi hasa upande wa Trent alexander-anord, nimechek game zote za Liverpool mipira Mingi inapitia kwa TAA, tusipo chukua taharadhari Madrid watapitia Sana kwa upande wa TAA


Mkuu Sio Kwamba TAA Ni mbovu ila kama utafatilia Mechi Nyingi Za Liverpool anapocheza Na Timu Kubwa Basi Upande Wetu Wa Kushoto (VVD + Robbo) unakuwa Salama Kwa Sababu Uko imara Maadui Huwa Hawashambulii Kupitia Upande Huo.

Lakini Upande Wetu Wa Kulia (TAA + Lovren) Ndiyo Unakuwa Main Target Kwa Wapinzani Wetu Na Wanaushambulia Mara Kwa Mara Kwasababu Wanajua Mlinzi Ni TAA tu! Wakifanikiwa Kumpita Yeye Basi Hana Cover yoyote Kwa Lovren hatabiriki atafanya Nini!

Kwahiyo sio Kwamba TAA Ni mbovu Wa Kukaba Bali Hule Ni mfumo maalum Wa Wapinzani wetu! Kwahiyo Hata Aje Acheze Beki Gani pale iwapo na Lovren ataendelea Kuwepo Upande hule Basi Maadui Hawataacha Kutumia Upande hule Kama Ni Njia.

Na vilevile Kumbuka Kuwa TAA Ni Majeruhi na Mechi Stoke Hakucheza wala Alikuwa Hapigi Mazoezi! Kwahiyo Jana Alijiforce tu Kwa ajili Ya Kuokoa Jahazi lakini Physical Fitness hakuwa Nayo.
 
We jamaa inaonekana liva inakuumiza sana moyo sisi wenye timu yetu matatzo yetu tunayajua au umeona kuna mtu analaumu beki zetu..embu tuache kdgo tupumue!!


Huyo Ni Mshabiki Wa Arsenal Kindakindaki!
Kinachompa Wivu na Maumivu Ni Vitu viwili!

1) Kumtoa Ndani Ya Top Four

2) Hili Ndiyo Linamuuma Zaidi Kuona Arsenal imeshiriki #CL Miaka 19 mfululizo na haikuambulia Kombe Hata Moja. Lakini anaumia Kwanini Liverpool tokea iache Kushiriki hii Ni Mara Yake Ya Kwanza Kushiri na inacheza Fainali, na Huenda ikabeba Kombe.

Kwahiyo Huyo jamaa anaumizwa na mengi na Ndiyomana Anatumia Kichaka Cha Real Madrid kuficha Wivu Wake Wa Arsenal.
 
Hongera zetu Liverpool lkn sub inatuumiza sana make naona kila match sub ikifanyika tunafungwa goli!
Mungu tusaidie hili kombe tulibebe tuwafunge midomo mavuvuzela wanaotubeza kila match


Mkuu Hapa Zaidi Ya Mara moja niliwahi Kupost Kuwa Katika Kikosi Chetu Chote Cha Wachezaji 29 tulionao, basi Kwasasahivi Wachezaji Wa Ushindani tulionao ni 11 tu!

Karius
TAA
Lovren
VVD
Robbo
Gini
Milli
Hendo
Mo
Bobby
Mane


Kwahiyo Hapo Tukifanya Sub tu Ni Kosa hususan anapotolewa Mmoja Kati ya Hao Watatu Wa Mbele Kwani Kwenye Bench hatuna Mbadala Wao.

Msimu Ujao Lazima Tupate Wachezaji 4 Wa Kuongeza Nguvu, Venginevyo Tujiandae na Kilio.
 
Actually, ni fainali niliyoitaka. Itapendeza, ili mzizi wa fitna ukatwe!!
Kwa mechi hizi za Roma, raundi hizi 2, liver wajirekebishe! Huu ni ukweli tu.


Kabla Ya Kutunyooshea sisi Vidole ulikuwa uangalie Kwenye Mechi Ya Second Leg vs Juventus, na Second Leg vs Bayern Kuwa nawewe Una Kitu Cha Kujifunza Kwani usidhani Kuwa Makocha Wa Liverpool Hawakuona ulivyocheza.

Na Jengine Uzingatie Kuwa Kwanini Mechi ya Juve ya 2nd Leg Ronaldo hakuweza Kufunga Mpaka Akapewa Penalty Ndiyo aliyofungia. Na Mechi Zote Mbili Za Bayern hakufunga wala Kupiga shot on target Hata moja? Hapo Jifunze Kitu.

Sisi Hatuna Cha Kujifunza Kwani Mechi Zote Mbili Za Roma Tunafungwa Magoli baada Ya Kufanya SUBSTITUTIONS na hilo imeliona.
Tunafanya Subs Kwasababu Bado tuna pressure Kubwa Ndani Ya [HASHTAG]#EPL[/HASHTAG] kwahiyo Tunapumzisha Washambuliaji Watu waweze kupambana Ligi Zote 2 kutokana na Kuwa Hatuna Kikosi B.

Lakini Kwenye Fainali usitegemee Kuwa Tutamtoa Mchezaji Yoyote Kati Ya Salah, Mane na Firmino Kwani Hapo Hatutakuwa na Mchezo mwengine Wowote Wa Kuhofia.
 
Wanasema GOOD OFFENSE WINS YOU MATCHES, but GOOD DEFENCE WINS YOU TITLES. There is a title on the line here buddy!!


Mkuu Kama Hujui Huo Ni Msemo Wa Manure baada Ya Kupoteza Mwelekeo Wameamua Kujifariji Kwa Kudai eti Wamemquote Ferguson! Lakini Cha Ajabu Kwenye Miaka 5 tokea Aondoke Ferguson Hawakuwahi Kuuona Msemo huu, ila Msimu Wa 2017/18 Ndiyo wameuona.

Labda nikuulize Wewe Defence Yako ina ubora gani?
 
Three front ya liver ni beki tosha kabisa ukiivuruga tu kwa sub umeruhusu mashambulizi
 
1958....madrid winner
1968 miaka 10 baadae Man u bingwa
1978.miaka 10 baadae Liver bingwa
THEN
1998 madrid bingwa
2008 miaka 10 baadae Man u bingwa
2018 miaka 10 baadae.......(jaza mwenyewe)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom