Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,184
- 671
Leo ni Muungano
2008-04-26 09:18:54
Na Mhariri.
Leo ni Kumbukumbu ya Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutimiza miaka 44 ambapo sherehe hizo kitaifa, zinafanyika katika Uwanja wa zamani wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo zitakazohudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa kitaifa na wananchi ambapo pamoja na mambo mengine, atakagua gwaride lililoandaliwa na vikosi mbalimbali vya Majeshi ya Ulinzi na Usalama.
Mhariri na timu yake yote ya gazeti hili, inawatakia sikukuu njema Watanzania wote katika maadhimisho hayo muhimu ya kitaifa.
SOURCE: Nipashe
2008-04-26 09:18:54
Na Mhariri.
Leo ni Kumbukumbu ya Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutimiza miaka 44 ambapo sherehe hizo kitaifa, zinafanyika katika Uwanja wa zamani wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo zitakazohudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa kitaifa na wananchi ambapo pamoja na mambo mengine, atakagua gwaride lililoandaliwa na vikosi mbalimbali vya Majeshi ya Ulinzi na Usalama.
Mhariri na timu yake yote ya gazeti hili, inawatakia sikukuu njema Watanzania wote katika maadhimisho hayo muhimu ya kitaifa.
SOURCE: Nipashe