Kwanini asisifiwe Mwananchi anayelipa kodi inayotekeleza miradi ya kitaifa?

Mawele

Member
Jul 25, 2023
30
116
kodi.PNG

Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!

Pia soma: Mbowe, wenye akili wamekuelewa. Hawa wasiokuelewa tuwaite nani?
 
Huu ni utamaduni ambao ki hualisia sio sawa kwasababu kodi zinatolewa na wananchi sio kiongozi ila cha kushangaza unakuta mradi umekamilika kwa kodi za wananchi tena wananchi wanatoa kodi zao kwa jasho na damu lakini sifa kwa mtu furani na ndio maana hao watu wanapata kiburi cha matumizi mabaya ya madaraka na maendeleo hasi katika nchi
 
Watu tukikaa tukatulia vizuri tukaacha ujinga Utakuja kugundua sisi ni watumwa wa kifikra, Ndio nyerere aliyasema haya.

Kazi ya kingozi ktk nchi ni kutatua kero za wananchi kwa kusimamia shughuli atakoyokuwa amepewa au alio iomba kulingana na nafasi yake, huku akiongozwa na katiba na sheria ya nchi

Maana yake kaaminiwa na watu wengi, kutokana na maono yake, uwezo wake, jitihada zake, akasimame badala ya watu hao/ kapewa dhamana.

Watu walio mwamini ndio wanaotoa pesa za utekelezaji wa miradi au kazi zitakazofanywa kwaajili ya kuwaletea maendeleo wananchi,

Yeye anatumika kama msimamizi na mwakilishi tu pia mshauri juu ya jambo ambalo anaweza kuona litakuwa na tija kwa jamii na kwa taifa kwa ujumla.

Sasa kuna huu ujinga wa viongozi kusema Pesa fulani ametoa kiongozi fulani ili kukamilisha mradi fulani,

Kuna kiongozi anaweza toa bilioni 3 mfukoni mwake lijengwe daraja !!

Jibu linakuwa ni gum, ni kitu ambacho ni ngumu kuwezekana, kama kiongozi yeye mwenyew mshara wake ni pesa hizo hizo za wananchi, aje atoe bilion 3 uongo ulio wazi.

Mimi sidhani kama ni Muhimu kwa viongozi kuendelea na hicho kitu,wao walitakiwa wapewe sifa kwakuwa walisimamia Miradi ilio ahidiwa na kukamilika kwa wakati, au kipinga vitendo viovu vinavyo rudisha chini uchumi wa nchi ama kuhatalisha usalam wa nchi.

NOTE; viongozi wajue zama zimebadilika, zamani watu walikuwa kwenye gunia, ila sasa hiv, watu wamo kwenye tenga, watu sasa hivi wanajua vitu vingu kuhusu viongoz, kinachowabeba ni power kwakuw wako madarakani wananchi wanakuwa hawana nguvu ya kusema
 
Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Hii ya mwashambwa.
 
Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Kodi sio malipo ya kubembelezwa au hiari ni malipo ya Lazima kwa serikali , unapongezwa vipi kwa kulipa malipo ya lazima? Wewe usipolipa Kodi ni kosa kisheria ila hakuna Sheria itakayomshitaki Rais kushindwa kufanya miradi ya maendeleo
 
Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Una point konki, lakini umeuzunguka mno mbuyu.

Nikuambie tu kwamba unachokijua ama usichokijua, hii tabia ya uchawa pamoja na kujifyetua akili hata kwa watu waheshimiwa kabisa katika jamii ni ajira inayowalipa sana wao kwa kushibisha matumbo yao.

Ni ubinafsi na uzandiki kwa uzalendo wa Taifa kwa mheshimiwa kama Waziri, Rc, Dc ama Mbunge kusimama hadharani na kusema kwa mfano: ... 'Mama katoa pesa kujenga kipande cha barabara kutoka point 'A' kwenda point 'B' na maneno mengine yenye kufanana na hayo wakati wakijua kabisa kuwa ni ya uongo mtupu.

Rais ni muajiriwa wa wananchi, ni kiongozi wa utekelezaji wa maamuzi ya Taifa, analipwa kwa kazi hiyo kama mwajiriwa yeyote mwingine wa Serikali na hana pesa hata senti 5 kuweza kuitoa mfukoni mwake kutekelezea mradi wowote hata wa kujenga choo cha shimo cha shule.

Walishaona kwamba kumsifia Rais kwa maneno ya uzandiki na unafiki wa uongo ni kumuenzi na kumfurahisha yeye ili kumfubaza mawazo yake, asiweze kuziona dosari zake katika uongozi wake na asiweze kuona watu wengine wenye sifa bobezi zenye kufaa kuweza kulitumikia taifa, kwamba wao ndiyo watu bora na wapo karibu na mama.

Na kama wako mbali, basi kwa kupaza sauti zao za kusifia, wataonekana na kusogezwa.

Kwa hiyo kama kuukemea huu uozo, tuukemee bila ya kumumunya maneno.

Kwani kumsifia Rais kwa sifa za kweli zenye kuonekana katika utekelezaji wa majukumu yake kuna ubaya gani?

Basi mwenye kusifia, akae chini achambue sifa stahiki anazopaswa kumpa kiongozi husika na siyo kumtengenezea sifa za uongo wa mchana kweupe zisizomstahili kupewa.

Na huo utaratibu mbovu kwa matumizi ya fedha za Serikali, ndiyo athari za matokeo ya mambo tunayoyaongelea sasa.

Hiyo syndicate ya wazandiki na mafisadi, hakuna anayeweza kuwakemea katika ubadhirifu wao huo kwa sababu mwenye uwezo wa kufungua kinywa na kukaripia ili kukomesha ndiye kapigwa nusu kaputi la usingizi wa sifa, kwa hiyo hawezi kuona madhila yoyote ambayo taifa linapitia kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma.
 
Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Sio Kila Kodi Inatoka Kwa Mwananchi, zingine ni Mapato ya directly ya Bandari,Utalii,Madini nk

Atasifiwa Samia Kwa kuratibu pesa kupatikana kama hivi 👇

View: https://www.instagram.com/p/C4zmB13NIBa/?igsh=NnJsNjFic3R4Mm9j
 
Kodi sio malipo ya kubembelezwa au hiari ni malipo ya Lazima kwa serikali , unapongezwa vipi kwa kulipa malipo ya lazima? Wewe usipolipa Kodi ni kosa kisheria ila hakuna Sheria itakayomshitaki Rais kushindwa kufanya miradi ya maendeleo
Sawa unalazimishwa na haubembelezwi.

Mantiki ya mtoa hoja hapa ni nani anayezistahili kupewa sifa za pesa zilizopatikana kwa nja ya kodi?

Kwani mtu akitimiza kazi zake vizuri iwe kwaku tumwa ama kujituma, hastahili pongezi?

Je pongezi zinastahili kupewa watu wenye sifa zipi?
 
Huu ni utamaduni ambao ki hualisia sio sawa kwasababu kodi zinatolewa na wananchi sio kiongozi ila cha kushangaza unakuta mradi umekamilika kwa kodi za wananchi tena wananchi wanatoa kodi zao kwa jasho na damu lakini sifa kwa mtu furani na ndio maana hao watu wanapata kiburi cha matumizi mabaya ya madaraka na maendeleo hasi katika nchi
Ni asilimia ngapi ya Kodi zinatolewa na Wananchi?
 
Sawa unalazimishwa na haubembelezwi.

Mantiki ya mtoa hoja hapa ni nani anayezistahili kupewa sifa za pesa zilizopatikana kwa nja ya kodi?

Kwani mtu akitimiza kazi zake vizuri iwe kwaku tumwa ama kujituma, hastahili pongezi?

Je pongezi zinastahili kupewa watu wenye sifa zipi?
Waliopewa dhamana ya kuhakikisha pesa zinapatikana, mfano Rais na watendaji wengine.

Nyie walipakodi mtapewa Asante ya Jumla ila Rais atatajwa Kwa jina maana aliwasimamia na mkalipa vinginevyo mungekwepa.

Hayo mengine ni ujinga na chuki zenu zinawasumbua
 
Waliopewa dhamana ya kuhakikisha kozi zinapatikana, mfano Rais na watendaji wengine.

Nyie walipakodi mtapewa Asante ya Jumla ila Rais atatajwa Kwa jina maana aliwasimamia na mkalipa vinginevyo mungekwepa.

Hayo mengine ni ujinga na chuki zenu zinawasumbua
Kwenye kujadili jambo lolote usitangulize ujuaji na kuona hoja za wengine kabla ya hitimisho kuwa ni za kijinga ama chuki.

Ujinga ama uchuki hujipembua vyenyewe kutokana na mchekecho pamoja na upembuzi wa hoja, tena havisemwi na ukivisema sijui, ujinga, upumbafu na kauli zingine kama hizo zenye kutweza wenzako ni kuharibu mjadala na inatafsiriwa kuwa ni matusi.

Labda nikuulize, ni nani aliyeithibitisha comment yako kuwa ni perfect, haina chuki ama ujinga.?

Ushaona hakimu akajihukumu?

Tuwe wastaarabu hata kwa kuigiza, haitatupunguzia chochote.
 
Kwenye kujadili jambo lolote usitangulize ujuaji na kuona hoja za wengine kabla ya hitimisho kuwa ni za kijinga ama chuki.

Ujinga ama uchuki hujipembua vyenyewe kutokana na mchekecho pamoja na upembuzi wa hoja, tena havisemwi na ukivisema sijui, ujinga, upumbafu na kauli zingine kama hizo zenye kutweza wenzako ni kuharibu mjadala na inatafsiriwa kuwa ni matusi.

Labda nikuulize, ni nani aliyeithibitisha comment yako kuwa ni perfect, haina chuki ama ujinga.?

Ushaona hakimu akajihukumu?

Tuwe wastaarabu hata kwa kuigiza, haitatupunguzia chochote.
Nchi inaendeshwa kwa hisani ya Rais
 
Kwenye kujadili jambo lolote usitangulize ujuaji na kuona hoja za wengine kabla ya hitimisho kuwa ni za kijinga ama chuki.

Ujinga ama uchuki hujipembua vyenyewe kutokana na mchekecho pamoja na upembuzi wa hoja, tena havisemwi na ukivisema sijui, ujinga, upumbafu na kauli zingine kama hizo zenye kutweza wenzako ni kuharibu mjadala na inatafsiriwa kuwa ni matusi.

Labda nikuulize, ni nani aliyeithibitisha comment yako kuwa ni perfect, haina chuki ama ujinga.?

Ushaona hakimu akajihukumu?

Tuwe wastaarabu hata kwa kuigiza, haitatupunguzia chochote.
Kitu unacholalamikia ni ujinga.Vitani Huwa hawasifiwi askari woote Bali Kiongozi wao tena Kwa jina,Je Huwa Yuko stari wa mbele wa vita? Jibu ni hapana.

So ukielewa scenario hiyo basi huwezi shangaa Rais kusifiwa.Jielimishe badala ya kuandika maelezo mengi yasiyo na msingi.
 
Back
Top Bottom