Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.
Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.
Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.
Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Pia soma: Mbowe, wenye akili wamekuelewa. Hawa wasiokuelewa tuwaite nani?