Mhe. Kigwangalla sasa unaanza kuharibu, sikutaka kuchangia katika hoja hii hata kidogo ila kwa kuanza kutoa comment kama mtoto wa darasa la kwanza au la pili unanifanya nianze kudoubt uelewa wako na elimu yako kwa ujumla, siasa si kuongea point kuwa nitafanya 1, 2,3 la hasha ni pamoja na kuvumbua vitu vilivyofichika kama hayo uliyosema kuhusu viongozi wa CDM, pili wanasiasa wengi duniani wamefanikiwa sana kwa style ya kudai haki inayomilikiwa na wanyanganyi kama CCM, sina haja ya kutoa mifano wewe upo CCM na unajua mnachojivunia kuhusu ukombozi wa bara la Afrika, sijui kama ulikuwa bila umwangaji wa DAMU... yaani umenifanya nikuone kuwa wewe ni KILAZA WA SIASA kuliko VILAZA WOTE NILIOPATA KUWAONA.
Kama CDM wanakuandama kuhusiana na jinsi ulivyopata elimu yako, wewe toa fact kwamba siyo kweli, ni rahisi sana sina haja ya kwenda huku kama vipi wewe kaa kimya subiri kama watakwenda mahakamani.
Otherwise nakushauri uangalie jinsi gani ya kuwasaidia wana Nzega wezako na Tabora kwa ujumla, hali ya Nzega na Tabora kwa ujumla ni mbaya sana, hasa kwenye infrastructure, maji, elimu etc sehemu kubwa ya jimbo lako watu wana shida na matatizo mengi jipange kuyatatua na wala si kubishana na wa JF, wapo makini na tunaijua nchi hii ndani nje.
Nafikiri ni vizuri ukatumia pesa zako za ubunge kutafuta consultant wa kukusaidia kuwainua kiuchumi wanazenga wezako badala ya kukaa na kuidiscuss CDM.