Kwanini Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hatelezi?

Kwanini Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hatelezi?

MTU yeyeto anaeswali Na kukumbuka kupalilia makaburi ya ndugu zake Na pia afungae,huwa ni kiongozi bora mwenye utu Na kuwathamini wengine,hawezi lewa Madaraka, tofauti Na viongozi waumini wa ndumba

Sijui wa iringa hafungi au????
 
Viongozi wengi wa awamu ya tano wamekuwa wakitoa matamshi yasiyo na hekima wala busara, lakini Waziri Mkuu kwa kiasi kikubwa ameweza kuzilinda hisia zake na kudhibiti ulimi wake.

Ameweza pia kuwavumilia Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao wamekuwa wakienenda kinyume Cha maadili ikiwemo kimatamshi na Sasa mavazi.

Pamoja kulinda ulimi wake ameweza kuonyesha utumishi Bora na hata maelekezo yake yanaheshimika na kutekelezwa kuliko hata ya wale wanaotumia lugha chafu na za udhalilishaji.

Kongole Kassim Majaliwa

Ukiona hivyo ujue alishinda kwenye uchaguzi kihalali hivyo ana furaha na cheo chake na anawajali watu sio madaraka.
 
..kwa historia ya Tanganyika, ukiona Waziri Mkuu halaumiwi basi ujue hafanyi kazi yake vile inavyotakiwa na hamsaidii Raisi.

..Waziri Mkuu ndiye kiranja mkuu wa mawaziri na msimamizi wa utekelezaji wa majukumu ya serekali.

..Mtendaji mwenye majukumu hayo, lazima awe " front " muda mwingi, na ktk mazingira ya Tanganyika lazima ataangushiwa lawama nyingi.

..Fuatilieni historia ya Mawaziri Wakuu kama Mzee Kawawa, Edward Sokoine, Joseph Warioba, Cygwiyemwisi John Malecela, Frederick Sumaye, Edward Lowassa, Mizengo Pinda.

..Wote walikuwa mstari wa mbele kusimamia serekali. Na mambo yalipoharibika walibeba lawama badala ya Raisi kubeba lawama hizo.

..Suala kama la ununuzi wa korosho, awamu zilizopita Waziri Mkuu ndiyo angekuwa mstari wa mbele na siyo Raisi hata kama final say ilikuwa ni ya kwake[raisi].

..Ndiyo maana ilifika wakati watu wakaamini kwamba ukiwa Waziri Mkuu huwezi kupanda na kuwa Raisi wa Tanzania.

Cc Nguruvi3
 
Sababu ni muislam,Fanya tafit waislamu huwa Na hekima ya uongozi kuliko wakristo
Hii ni post ya pili kwenye huu Uzi kua na like nyingi.......niamini mimi waliolike sio wajinga
 
Sababu ni muislam,Fanya tafit waislamu huwa Na hekima ya uongozi kuliko wakristo
Uislamu wake unaupima kwa jina lake, 'sigda' yake, kwa kuhubiri au ? Hata Mzee Makamba, mzee Kawawa, Mzee Mwinyi, JK Kikwete na Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, wote Waislamu na wamewahi kuwa viongozi. Komando Salmin Amour na Balozi Idd Seif nao pia Waislamu. Je, kwa matumizi yao ya ulumi unawafananisha na Kassim Majaliwa?

Au miongoni mwa hao wamo ambao hawakuwa Waislamu?

Vv
 
KM ni mroma...hilo.ni jina....ila.KM amelelewa vizuri.ni kiongozi. Amepanda.ngazi hatua moja hadi nyingine..nankwenye ngazi hio hajawahi kumtukana mtu.. Namuombea maisha marefu.
 
..kwa historia ya Tanganyika, ukiona Waziri Mkuu halaumiwi basi ujue hafanyi kazi yake vile inavyotakiwa na hamsaidii Raisi.

..Waziri Mkuu ndiye kiranja mkuu wa mawaziri na msimamizi wa utekelezaji wa majukumu ya serekali.

..Mtendaji mwenye majukumu hayo, lazima awe " front " muda mwingi, na ktk mazingira ya Tanganyika lazima ataangushiwa lawama nyingi.

..Fuatilieni historia ya Mawaziri Wakuu kama Mzee Kawawa, Edward Sokoine, Joseph Warioba, Cygwiyemwisi John Malecela, Frederick Sumaye, Edward Lowassa, Mizengo Pinda.

..Wote walikuwa mstari wa mbele kusimamia serekali. Na mambo yalipoharibika walibeba lawama badala ya Raisi kubeba lawama hizo.

..Suala kama la ununuzi wa korosho, awamu zilizopita Waziri Mkuu ndiyo angekuwa mstari wa mbele na siyo Raisi hata kama final say ilikuwa ni ya kwake[raisi].
Nakubaliana nawe 100% na hatuwajawahi kuwa na Waziri Mkuu aliyejificha ficha kama Maja
Katika orodha yako yupo pia CD Msuya, ambaye kama mawaziri wakuu wengine alibeba lawama kwa niaba ya serikali. Wote walikuwa wasaidizi wazuri wa Rais Bungeni na nje

Kassim Majaliwa amekuwa waziri mkuu tofauti kabisa. Akiwa Bungeni hata pale serikali inapobanwa yeye hubaki kutazama tu na zipo nyakati kauli za mawaziri zinatia kinyaa

Huwezi kumsikia akikemea jambo au akipongeza, yaani ni ''lame duck'' PM

Jana alikuwa katika mazishi ya Mzee Mengi. Kauli za Makonda za kibaguzi na akiwa RC sehemu ya watendaji wa PM ilibidi Waziri mkuu asimame na kukemea

Waziri mkuu alikuwa kimya kana kwamba hakuna kilichotokea, aliridhia ubaguzi tu. Kimyaa

Ni afadhali Bushir Ally alikemea lakini yeye ni wa CCM siyo serikali
Maneno ya Bushir yalipaswa kusemwa na Waziri mkuu, tofauti alikuwa kimyaa akitafuta wema

Kwa mtazamo wangu, huyu Waziri mkuu hamsaidii Rais, hasaidii serikali na nchi

Ukimya wake ni kutaka kuonekana mzuri akilenga siku za baadaye kuwa mbeba bendera CCM

Lakini pia kuna element za woga. Alipo waziri mkuu hakuna attention kama alipo Bashite

Huu ni woga kwamba ukimgusa umekwenda na maji. Na woga huo hadi kwa mawaziri

Ni Waziri mkuu aliyetekeleza majukumu yake tofauti na historia ya mawaziri kuu wa Tanzania
 
Naunga mkono hoja. Mfano mwingine ni makamu wa rais Samia Suluhu. Hana mambo ya kijinga kama bosi wake!


..Mfuatilie wakati wa Bunge Maalum la Katiba ndiyo atajua misimamo yake na tabia zake.

..Huyu Mama ni mhafidhina wa CCM na si muungwana kama mnavyofikiria.
 
Sababu ni muislam,Fanya tafit waislamu huwa Na hekima ya uongozi kuliko wakristo
Wewe ni mmoja wa watu walio na uelewa mdogo.
Mungu hugawa vipawa vyake pasipo upendeleo.
Hata kwa wachina wasio na dini Mungu amechagua baadhi yao kuwa na hekima na busara za kuongoza wachina wenzao wasio na dini.
Ukisema waislam tu ndio waliojaliwa hekima na busara,maana yake inasema Mungu si mwema,kwamba Mungu ni m baguzi,kwamba Mungu hutoa kwa upendeleo,jambo ambalo sio kweli.
MUNGU NI MWEMA KILA WAKATI,NA WALA HANA UPENDELEO
 
Hapa sio ccm kukubalika. Naona udini umetamalaki ktk uzi huu.
Lkn ki ukweli jiwe katuangusha sana.
Kauli zake siyo...huyu mkuu wa Dar naye ni shida,tukirudi nyuma Mkapa naye kafanya hovyo kule Pemba,basi ili mradi majanga.
Lkn tusiogope,tunaye baba wa taifa Mwl Nyerere,kila mmoja anamkubali na kusema kweli alikuwa kiongozi wa kupigwa mfano.
Napata faraja mno kuona namna viongozi wetu wa CCM wanavyokubalika.
 
Back
Top Bottom