Kwanini watu wanaipenda pombe?

Kwanini watu wanaipenda pombe?

Hiyo savana na sminorff ulikuwa unajaribu hadharani kabisa? Wewe piga whiskey tu beer ushavuka aisee😆
Savanna ni kama maji, Sminorff niliona kama tujuice kabisa tutamu sana na zote huwa najaribu mapema kabla hawajajaa nakaa Counter kuna Vidada nafahamiana navyo nakaambia chukua tu hii niwekee kwa glass weekend hii najaribu Brutal mamaee
 
Pombe tokea nilipoiacha ni miaka mingi sana
Karibu mkuu!
1761078768510.png
 
Wakuu habari

Naomba kufahamu katia unywaji wa pombe kali au bia,

Issue ya ladha, relaxation na mood ile ya kuhis vibe fulani, ndio vinawaletea mumkali?

Ladha gani mnayoipenda kwa bia na pombe kali.

For user only🔥
 
HIZI BAR AU NIGHT CLUBS ZENYE CASINO ZA KIKUBWA , SI AJABU UKIONA MWANAMKE ANAPIGWA PUMBU MBELE YA WATU LIVE BILA CHENGA .
 
Savanna ni kama maji, Sminorff niliona kama tujuice kabisa tutamu sana na zote huwa najaribu mapema kabla hawajajaa nakaa Counter kuna Vidada nafahamiana navyo nakaambia chukua tu hii niwekee kwa glass weekend hii najaribu Brutal mamaee
Hizi achana nazo zisije kubadilisha hormones zako bure🤣🤣 utamaliza crate nakwambia!
 
Hujui kitu kwenye mambo ya pombe nimekupa LIFE BAN..

NIWEKE WAZI MIMI NISINGE KUNYWA POMBE MAANA MPAKA NAMALIZA CHUO KIKUU SIKUWAI KUNYWA..

MIMI NAKUNYWA RESPONSIBLE TENA JIONI BAADA YA KAZI NAFANYA RECREATIONAL KWA KUNYWA KONYAGIIII NDOGO MOJA NA MIX NA TONIC WATER SIZIDISHI THEN NAENDA ZANGU NYUMBANII KUJUMUIKA NA FAMILIA..

POMBE HUFANYA NIWE VERY HIGH KIAKILI , MAWAZO,UTENDAJI, BUSARA NA HATA KUPANGA MADILI YA MAISHA NA BIASHARA..

SISI WENGINE POMBE ZIPO KWENYE UKOO BABA ENGINEER MPAKA KASTAAFU HAJAWAI KUHARIBU KAZI KUGOMBANA AU KUSHINDWA KULEA FAMILIA TUNAKULA, LALA, SOMA VIZURI WATOTO WOTEEEEEEE

KILA MTOTO ALI MJENGEA NYUMBA YAKE NA ALIKUA ANAKUNYWA KILA SIKU..ASIPO KUNYWA ALISEMA HAPATI USINGIZII..

KWA SASA AGE GO HANYWI KABISA USHAUR WA KITABIBU YUPO ANAKULA PENSION WANAINJOI NA MKEWE MPAKA MUDA HUU SO POMBE ZIPO NA WAPO WANAO ZIMUDU

UKIONA HUWEZI POMBE ACHANA NAZO MAANA SIO KILA KICHWA KINA UWEZO WA KUMUDU ALCOHOL

Umeandika na wamekuelewa bro . Sina shaka kwenye Hilo.

Binafsi nakunywa pombe ili nirelax. Nipate muda wa kufuatilia ishu 2 tatu kwa simu. Nipate akili ya ziada.
(Stimulate brain activities).
Nimepunguza mabia sikuhizi. Na kama Nikinywa katkat ya wiki bas jua kuna mpira au kuna kikao muhim na mtu.
Ila ijumaa & jmosi najiloweka kabisa.

Kwangu Ladha ina matters a lot.
pia matokeo baada ya kunywa bia (hangover)
Ndio maana nakunywa Castle lite au castle lager.
Hata nikipiga 15+ naamka sina hangover. Nikila nikioga nakuwa mpya.

Ila mapombe makal au bia nyingne Siziwezi. nitamka na mawenge. Na hiyo sipend kabisa.
 
Maranyingi nikinywa kesho yake huwa nakuwa mtu wa majuto sana , najutia kupoteza pesa , mwili unakuwa katika hali ya uchovu , nakosa hamu ya kula ., kesi zinakuwa nyingi mara oooh et nimemtukana huyu.au yule .... mbaya zaidi nakuwa katika hali ya wasiwasi majuto na kujiona sina heshima ..... na kila nikijiapiza kuiacha baada ya muda najikuta nairudia .... pia huwa nikimuona mtu kalewa huwa namuona kama hajitambui , kichaa na mtu siyekuwa na heshima ... kiufupu pombe ni mbayaaaa..... pombe ni mbayaaaaa SANAAAA
 
Maranyingi nikinywa kesho yake huwa nakuwa mtu wa majuto sana , najutia kupoteza pesa , mwili unakuwa katika hali ya uchovu , nakosa hamu ya kula ., kesi zinakuwa nyingi mara oooh et nimemtukana huyu.au yule .... mbaya zaidi nakuwa katika hali ya wasiwasi majuto na kujiona sina heshima ..... na kila nikijiapiza kuiacha baada ya muda najikuta nairudia .... pia huwa nikimuona mtu kalewa huwa namuona kama hajitambui , kichaa na mtu siyekuwa na heshima ... kiufupu pombe ni mbayaaaa..... pombe ni mbayaaaaa SANAAAA
We pombe huiwezi, achana nayo.. ukiona unakunywa pombe na ujinga unakuanza achana nazo kabisa.
 
Wakuu habari

Naomba kufahamu katia unywaji wa pombe kali au bia,

Issue ya ladha, relaxation na mood ile ya kuhis vibe fulani, ndio vinawaletea mumkali?

Ladha gani mnayoipenda kwa bia na pombe kali.

For user only🔥
Pombe sio nzuri, wengi tuliotumbukia kwenye mtego huu kwa sehemu kubwa ni pear pressure, adolescent quriosity na mass propaganda kuwa unywaji wa pombe unaambatana na best moments, vibe na ujasiri which in deed is a day time lie.
Pombe zimeleta madhara mengi kwa watu kuliko hata wahusika wanavyoweza kukiri. Pombe ina uhusiano wa moja kwa moja na matumizi mabaya ya pesa, ngono zembe, utendaji duni kazini na kuvunjika kwa familia.
Ni muhimu kuukabili ukweli kuwa unywaji wa pombe ni tatizo ambalo kama tusipolipatia suluhu kwa wakati litazalisha majanga mengi tuendako.
 
Pombe sio nzuri, wengi tuliotumbukia kwenye mtego huu kwa sehemu kubwa ni pear pressure, adolescent quriosity na mass propaganda kuwa unywaji wa pombe unaambatana na best moments, vibe na ujasiri which in deed is a day time lie.
Pombe zimeleta madhara mengi kwa watu kuliko hata wahusika wanavyoweza kukiri. Pombe ina uhusiano wa moja kwa moja na matumizi mabaya ya pesa, ngono zembe, utendaji duni kazini na kuvunjika kwa familia.
Ni muhimu kuukabili ukweli kuwa unywaji wa pombe ni tatizo ambalo kama tusipolipatia suluhu kwa wakati litazalisha majanga mengi tuendako.
Sawa, lakini kwanini tena watu wakiwa na stress wanatafuta hiyo pombe na kunywa ata wakiwa faragha?
 
Sawa, lakini kwanini tena watu wakiwa na stress wanatafuta hiyo pombe na kunywa ata wakiwa faragha?
Sababu kubwa ni dependency, alcohol is addictive.
Unapokunywa pombe, mara moja kiasi cha dopamine huongezeka katika ubongo wako, hiki ndicho kinachokufanya ujisikie furaha na mwenye kujiamini. Ukitumia pombe kwa muda mrefu, ubongo wako unatengeneza utegemezi wa pombe kupata dopamine, hali hii ndio huzaa alcohol dependency
 
Sababu kubwa ni dependency, alcohol is addictive.
Unapokunywa pombe, mara moja kiasi cha dopamine huongezeka katika ubongo wako, hiki ndicho kinachokufanya ujisikie furaha na mwenye kujiamini. Ukitumia pombe kwa muda mrefu, ubongo wako unatengeneza utegemezi wa pombe kupata dopamine, hali hii ndio huzaa alcohol dependency
Duhh hatari! Na kujiengua bila kutamani kurudi ata kama ni mwaka inawezekana kweli? Mi niliacha aisee cha ajabu nmepata tamaa ya ajabu sielewi na ni ghafla tu😟
 
Kufunga mwezi mzima au kwa lugha nyingine kuweza kujizuia mwezi mzima.

Baada ya kuumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhani ilikuwa mwaka 2014 kama sijakosea nikaona ujinga kurudi kwenye mapombe.

Na mimi sikuwa mlevi kivile, nilikuwa napiga piga za afya.
Jambo jema sana mkuu.
 
Duhh hatari! Na kujiengua bila kutamani kurudi ata kama ni mwaka inawezekana kweli? Mi niliacha aisee cha ajabu nmepata tamaa ya ajabu sielewi na ni ghafla tu😟
Hii changamoto inawapata wengi, lakini its worth your efforts. Ukiweza kujizuia kwa muda, ubongo wako utaanza kurudi kwenye hali yake ya awali taratibu.
 
Back
Top Bottom