Kwanini wanawake tunaojimudu tunaogopeka?

Kwanini wanawake tunaojimudu tunaogopeka?

tutakula kifanyio na kodi ikiisha utatumia kifanyio kuongea na baba mwenye nyumba au
sasa we si umeshasema unajiweza Ila kiukweli laiti kama wanaume tungekuwatunaweka kigezo cha ugolikipa mbele kusingekuwa na ndoa,maana wapo wamama kibao magolikipa
 
Mbona bahati kama hizi huwa hazipiti huku mtaani kwangu.

Yani mwanamke nikuogope kisa unamali huu ni udhaifu wa miaka mia moja...

Wanaume wa hivyo hawastahili sifa ya uanaume..

Mwanaume wa kweli hujiamini kwenye kila jambo.

Mwanaume asiyejua kitu kinacho control akili za mwanamke ndo utakuwa muoga kwenye jambo hilo.

Mwanamke mwenye mali zake ananifaa sana mi mwanaume bahili...
nyie ndo wale wale tunaowaita ma KB.
 
sasa we si umeshasema unajiweza Ila kiukweli laiti kama wanaume tungekuwatunaweka kigezo cha ugolikipa mbele kusingekuwa na ndoa,maana wapo wamama kibao magolikipa

kama najiweza haimanishi we ndo ukae tu kusubiri nikuleteee kila kitu chakarika ujenge heshima
hao wamama magolikpa ni haki yao maana wanafuata maagizo ya mungu
 
Baelezee bana yaani hawa wanaume wa siku hizi sijui ndo kujiona wajanja,hata wanachotakiwa kufanya hawakielewi, mapenzi yamekuwa kama biashara, kwa kuwa napendwa basi nisifanye kazi nigharimiwe tu, unashangaa mtu kila siku hana hela, kufanya kazi hataki anataka ajira za tra, tpdc, pccb, tanroad baaaaaas,hata kulima tu hawezi, mtu wa hivyo unamvumilia ili iwe nini, unamchan live akafanye kazi, hatutakula mapenzi


Maisha yatakielewesha tu!!!!!!
Tutanyooshana Marrykate:
 
Last edited by a moderator:
hahahahaha unapenda mtelemko jirani
ndo mana hupati bahati kama hizo

Ukiwa na mwanamke wa hivyo unapunguza kuhudumia kila mtu anakufa na chake,, tunakutana pale unapokuwa tumepandwa na mihemko.
 
sio wote wa aina hiyo japo ni kweli asilimia kubwa wana hizo tabia,

kwanza wengi huaminimwanamke kupata mali si nguvu yake mwenyewe (anaweza kuwa kawezeshwa na mwanaume mwingini) kwa hiyo kuhofia kuwa na mahusiano na girl wa mtu!!

pia inachangiwa na wadada wengi wenye kuweza kujimudu kuwa na tabia za kujisikia na kuwa jeuri kiasi fulani, kwa wanaume wengi hatupendi kutawaliwa au kumilikiwa kimasinyango!

nina meng ila nadhani na wengne niwape nafasi pia juu ya hili

Good day!!
 
Mwanaume anayeogopa mwanamke mwenye hela au mali jua hajiamini kabisa. Na mwanaume huyo ni yule ambaye anataka akiwa na familia basi awe ndiyo polisi!!!! Kama mnaelewana hata ule uanaume wa kujifanya wewe kijongoo unakuwa haupo kabisa!!! Cha msingi mwanaume unatakiwa ufanye kazi kwa bidii kwa kuwa hata mke awe na hela kiasia gani but ni msaidizi wako (kwa imani yangu) hivyo usimtake yeye mkeo awe ndiyo the maing provider. Hapa ndipo matatizo ya wanaume wengi yamelala maana wao wakiona mke ana earning nzuri basi wanakuwa zao ni za kupeleka kwenye unnecessary spending kama nyumba ndogo na offer za kufa mtu kwenye club!!! Tu wajinga sana.
 
kama najiweza haimanishi we ndo ukae tu kusubiri nikuleteee kila kitu chakarika ujenge heshima
hao wamama magolikpa ni haki yao maana wanafuata maagizo ya mungu

Kwahiyo nyinyi ambao siyo magolikipa,mnavunja maagizo ya Mungu!?
 
sio wote wa aina hiyo japo ni kweli asilimia kubwa wana hizo tabia,

kwanza wengi huaminimwanamke kupata mali si nguvu yake mwenyewe (anaweza kuwa kawezeshwa na mwanaume mwingini) kwa hiyo kuhofia kuwa na mahusiano na girl wa mtu!!

pia inachangiwa na wadada wengi wenye kuweza kujimudu kuwa na tabia za kujisikia na kuwa jeuri kiasi fulani, kwa wanaume wengi hatupendi kutawaliwa au kumilikiwa kimasinyango!

nina meng ila nadhani na wengne niwape nafasi pia juu ya hili

Good day!!

Ni kweli jamaa,hawa wanajiskia sana ndo mana huwa wanamegwa wanaachwa,.
 
Me ninadukuduku, Sielewi kwanini vijana wengi wa sasa wakikuona mwanamke ukishakuwa unaweza kujimudu wanakuwa wanakuogopa......
Mfano: Wakikuona una gari ye hana gari

Akikuona umepanga au una nyumba ye hana nyumba ....Basi inakuwa taabu tupu ikitokea umempenda..huwa wanahisi kama hujampenda kweli , Mwanaume akiwa na wewe atakuwa na wewe si kidhati,anakuwa na wewe huku yupo na mwingine, ye mawazo yake yanakuwa kukutumia tuu..........
Sielewi kwanini wanakuwa na fikra potofu hivi?

Mwanamke unapokuwa unajitahidi kutafuta maisha unatafuta pia ukijua utakuja kuwa na mwenzio...So mwanaume ukipendwa jiamini...ila tu jitahidi na wewe kimaisha sio uwe wa kula kulala...

tatizo huwa hamko tayari kudumu katika ndoa kwa utii, wengi wenu huwa mnakuwa wanyanyasaji wa wanaume na hufikia mahali mnawaita mwanaume suruali, mnapaswa kujitizama, wengi wenu hamna uwezo wa kuzimudu fedha na matumizi yake
 
ni kweli kabisa dada ila chanzo cha tatizo ni ninyi wenyewe wanawake/wasichana mnakuwaga na vijidharau fulani ndio maana tunaogopa kuwatongoza au kuwa nanyi kimapenzi kwa kuhofia kudharaulika, badilikeni kwanza enyi wadada ndipo nasi tutabadilika, kwa kuwa msichana akishakuwa na gari anadhani yupo peponi tayari

Me ninadukuduku, Sielewi kwanini vijana wengi wa sasa wakikuona mwanamke ukishakuwa unaweza kujimudu wanakuwa wanakuogopa......
Mfano: Wakikuona una gari ye hana gari

Akikuona umepanga au una nyumba ye hana nyumba ....Basi inakuwa taabu tupu ikitokea umempenda..huwa wanahisi kama hujampenda kweli , Mwanaume akiwa na wewe atakuwa na wewe si kidhati,anakuwa na wewe huku yupo na mwingine, ye mawazo yake yanakuwa kukutumia tuu..........
Sielewi kwanini wanakuwa na fikra potofu hivi?

Mwanamke unapokuwa unajitahidi kutafuta maisha unatafuta pia ukijua utakuja kuwa na mwenzio...So mwanaume ukipendwa jiamini...ila tu jitahidi na wewe kimaisha sio uwe wa kula kulala...
 
Back
Top Bottom