Kwanini wanawake tunaojimudu tunaogopeka?

Kwanini wanawake tunaojimudu tunaogopeka?

Wanaojua hawatetereki
 

Attachments

  • 1397412609079.jpg
    1397412609079.jpg
    46.9 KB · Views: 105
Ukweli tatizo lipo kwenu hamjitambui,ukishajiweza kuliko mwanaume unataka uwe boss ndani.binafs nilishampata moja kanizdi kila kitu kuanzia elimu mpaka hela sawa tulipendana tatizo likaanza mimi nikimpigia cim mara nyingine hapokei badae anakupigia oh rory nilikua bize mpenz wangu.mimi namuelewa.yeye apige uspokee unanuniwa wiki mpaka umbembeleze.funga kazi akawa anataka mimi ndo nikaish kwake baada ya ndoa nikaona haya nimajanga

Duh nimesikitika sana! huyo hakukupenda au ni tabia yake! Hizo tabia hazina uhusiano kabisa na status ya kimaisha ya mtu! Unataka kusema wanawake wenye vipato vidogo hawanuni? Yaani wao ni ever smile?
Problem ni kwamba uki date mdada aliyevizuri kuzidi wewe una expect awe malaika, kwamba hakosei! Akikosea baaasi ni kiburi cha fedha! That's where you are very wrong!
 
we unadhani nikikwambia kitu utanisikiliza wakati we ndo mwenye hela?

Kwa nini nisikusikilize wakati tunapendana na ambacho unaniambia kina maana!
Unachotaka wewe ni kufanya upuuzi halafu kwavile mimi ni mwanamke nikusikilize tu hata kama naona unataka kunitumbukiza kwenye shimo nikubali simply bcoz you are a man!
Kwa mfano unaniambia tufanye biashara ya "sembe" tena unalazimisha nitoe hela kwenye account nikupe, au unaniambia tufanye mapenzi kinyume na maumbile, au ni mlevi kupindukia, unarudi asubuhi, au unachepuka, mwanamke yupi awezaye kubeba zigo hili?
 
Sasa Boss hiyo poverty mentality iko kwa huyu mwanamke mwenye gari au kwa mwanume asiye nalo? We unaona gari ni kama viatu lakini wenzio wakiona gari hata kama ni la serikali akili zinawaruka. It is a status symbol. Hata viatu havifanani. Vaa basi yebo yebo au R.I.O na mwenzio avae viatu vizuri (bahati mbaya sijui designers wa vitu vya kiume ukiacha kelvin clain) muwe na sifa zinazofanana halafu mpeane muda sawa wa kutongoza uone nani atawahi kufanikiwa).

Wanaume ndo waliokuwa wamezoeleka kuwa na magari ya kuwazuzulia wanawake. Sasa wanawake nao wana magari, nao wana shahada, vyeo, biashara, mali n.k. Haya mabadiliko unafikiri yamerahisisha maisha? Wanaume wamepoteza identities na wanawake pia. Nadhani umeshasikia neno "mwanaume suruali", "iron ladies" n.k. Ni vigumu mwanamke aliyejitanabaisha na "vitu vya wanaume" kuendelea kuonekana ni mwanamke yule yule. Wanawake wenye magari nao wanawazuzua vijana wasio nayo. Wanaume waoga wapo, wanajishuku kuwa wataonekana kapuku kama hawana magari na nyumba kama wanawake zao kwani uanaume wao wameuambatisha kwenye hivyo vitu. Wanawake wenye hela pia wana matatizo kama ya wanaume wenye hela. Wanafatwa na wengi kiasi kwamba hawajui nani kafata mapendo, nani kafata kulelewa. kazi yake inakuwa ngumu kuliko yule asiye navyo. Ni wanaume wanaojitambua tu wanaweza kuanzisha mahusiano mazuri na ya kudumu na wanawake wa aina hii wanaojitambua pia.

Thank you Nandera! Kula likes Mia 8
 
Mwanamke ni Mwanamke tu...
labda Paranormal activity
 
sisi tusio hata na vitanda sijui itakuwaje.....?
 
Lakini pia, mwanaume akiwa anajipanga ili kunyanyuka kwa kutegemea mgongo wa mwanamke, ni sawa na yule anayekubali tu kuishi na mwanamke akiwa amemzidi kipato, kwani hata akifanikiwa bado itaonekana kwa nguvu ya mke, kwahyo atakuwa ameshindwa kuonesha uanaume wake.
kwa hilo naomba nisikubaliane na wewe kama ni mwanamke wako amekusaidiia ukafinikiwa its ok kuliko kuendelea kumtegemea watu wanasaidiwa na wanafanikiwa na watu baki sembuse kusaidiwa na mwanamke wako nahisi hiyo ni kawaida na ndio inapaswa hivyo mtu klumjali na kumsaidia mwenza wako
 
kawaida ndani ya nyumba mwanaume ndo simba lkn ikifikia akawa kazidiwa na mwanamke Karl kipato ,elimu na mambo mengine hapo anakuwa kama mbwa koko mtu wa kupewa amri
 
Hamjimudu kuna vijidume vinawawezesha Angalia eti gari zote nzuri mwamiliki nyie mtakufa mkatubu
 
Unajua kuna sifa za mke na kuna sifa za mume ambazo zote kwa pamoja haziamuliwi na kiwango cha elimu au kipato. Biblia imesema "enyi wanaume wapendeni wake zenu kama Kristo alivyo lipenda kanisa....enyi wanawake watiini waume zenu..... sasa hapa ni wewe kujiangalia. Je, pamoja na pesa zako nyingi unaonyesha utii na unaweza kudumisha utii huo siku zote? au kwa sababu una kipato kikubwa unajiona unaweza kufanya au kusema chochote na mumeo asiweze kuhoji? Ukiwa mtii na kuonyesha kwa hakika uwezo wako wa kudumisha tabia njema za mke mwanaume mwenye akili timamu atakupenda na kukujali siku zote na hatimaye kipato chako kikubwa kitakuwa chachu ya amani kwako na mwenzako badala ya kuwa chanzo ya msongo wa mawazo.
 
Back
Top Bottom