DOKEZO Kwanini Walimu Kilwa tunalazimishwa kubaki CWT? Wengine tunataka kuhamia CHAKUHAWATA?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Sisi baadhi ya Walimu Wilayani Kilwa tunazuiwa kujiunga katika Chama cha CHAKUHAWATA licha ya kuwa kuna wenzetu kati ya Walimu zaidi ya 300 wameshaamua kuhama kutoka CWT na kuhamia upande huo wa pili kutokana na makato makubwa ya CWT.

Kinachofanyika CWT wanaenda kwa Afisa Utumishi kuzuia Walimu wasitoke hali ambayo inachangia kuwavunja moyo Walimu katika ufanisi wa kazi kwa kuwa kwa nini watulazimishe tuendelee kubaki CWT?

Tunaomba Rais Samia Hassan Suluhu atamke neno la kuturuhusu Walimu tuende kwenye chama tunachokitaka, kwani kuna dalili za upigaji na rushwa kwa viongozi wa CWT kwa jinsi wanavyotuganda tusiondoke, wana jambo na maslahi yetu hawa, wanachama tunajua ndio maana baadhi yetu tunaamua kuhama.

Aidha, kuna mpango wa Walimu 23 waliohamia CHAKUHAWATA wanataka warudishwe tena CWT.

Jamiiforums tunaomba mtupazie sauti Kwa kuwa nyie mmekuwa sauti ya wanyonge.

Ni mimi Mwalimu kutoka Wilaya ya Kilwa Masoko Mkoa wa Lindi.
 
Kinachofanyika CWT wanaenda kwa Afisa Utumishi kuzuia Walimu wasitoke hali ambayo inachangia kuwavunja moyo Walimu katika ufanisi wa kazi kwa kuwa kwa nini watulazimishe tuendelee kubaki CWT?
Kama mmeshalijua hilo, si muandamane mwende kwa huyo afisa utumishi mpate haki yenu? Ni haki ya mtumishi kuchagua chama akipendacho.

Angalizo: mambo yakibadilika huko mnakohamia, msitushirikishe. Vumilieni au anzisheni tena chama kingine.
 
This is Divide and rule method.
CWT ilikuwa kuuuubwa ikaja na maghorofa, Mikopo, Mwalimu Benki nk nk. Mlitaka kuwa kama mhimili kwa nguvu yenu. Sasaaaa, Wenye akili wameshanusa hatari yenu, sasa mmeingia kingi mnaenda kuvurugwa mpaka mpoteane. Mpaka sasa CWT imekuwa vipande 3 na mnaendelea kugombana. Mkistuka mkoa vyama 5 mmesambaratika hamuongei lugha moja, tunaendelea kuwatawala, hakuna madaraja, mnashitakiana wenyewe kazi imeishia hapo. Kivuruge at work
 
Alafu jamani hamjui kuwa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa chama chenu akapaa juu, anatokea huku ulikokutaja? wa huko wanaogopa mauti ya chama chenu kuanzia nyumbani.
 
This is Divide and rule method.
CWT ilikuwa kuuuubwa ikaja na maghorofa, Mikopo, Mwalimu Benki nk nk. Mlitaka kuwa kama mhimili kwa nguvu yenu. Sasaaaa, Wenye akili wameshanusa hatari yenu, sasa mmeingia kingi mnaenda kuvurugwa mpaka mpoteane. Mpaka sasa CWT imekuwa vipande 3 na mnaendelea kugombana. Mkistuka mkoa vyama 5 mmesambaratika hamuongei lugha moja, tunaendelea kuwatawala, hakuna madaraja, mnashitakiana wenyewe kazi imeishia hapo. Kivuruge at work
Kwani mpaka sasa imefanya nini kikubwa cha muno kwa wanachama wake?
Kwa miundombinu iliyonayo CWT ilitakiwa isiendelee kuumiza wanachama kwa michango
lakini minaendelea kuwanyonya tuu. Imeishakuwa kama tawi la chama cha siasa hata ikifa haina madhara kwa wachangiaji,labda kwa viongozi wa chama.
 
Sisi baadhi ya Walimu Wilayani Kilwa tunazuiwa kujiunga katika Chama cha CHAKUHAWATA licha ya kuwa kuna wenzetu kati ya Walimu zaidi ya 300 wameshaamua kuhama kutoka CWT na kuhamia upande huo wa pili kutokana na makato makubwa ya CWT.

Kinachofanyika CWT wanaenda kwa Afisa Utumishi kuzuia Walimu wasitoke hali ambayo inachangia kuwavunja moyo Walimu katika ufanisi wa kazi kwa kuwa kwa nini watulazimishe tuendelee kubaki CWT?

Tunaomba Rais Samia Hassan Suluhu atamke neno la kuturuhusu Walimu tuende kwenye chama tunachokitaka, kwani kuna dalili za upigaji na rushwa kwa viongozi wa CWT kwa jinsi wanavyotuganda tusiondoke, wana jambo na maslahi yetu hawa, wanachama tunajua ndio maana baadhi yetu tunaamua kuhama.

Aidha, kuna mpango wa Walimu 23 waliohamia CHAKUHAWATA wanataka warudishwe tena CWT.

Jamiiforums tunaomba mtupazie sauti Kwa kuwa nyie mmekuwa sauti ya wanyonge.

Ni mimi Mwalimu kutoka Wilaya ya Kilwa Masoko Mkoa wa Lindi.
CWT ni kapu la mafisadi...
Hizo pesa zinachotwa na mafisiem...
 
Bora mgehamia chama cha mzee wa ubwabwa au TLP mkaifufua, hayao ma WAWAWAWAWATAAA hayatawasaidia.
 
Back
Top Bottom