Kwanini Saudi Arabia?

Nimekuwa nikifatilia kwa miongo mingi sasa viongozi wengi madikiteta wakipinduliwa huwa wanatafuta hifadhi za kisiasa Saudi Arabia. Nitatoa mifano michache hapa


  1. Waziri mkuu wa zamani wa Pakistani Nawaz Sharif baada ya kuangushwa alikimbia Saudi Arabia
  2. Waziri mkuu wa Syria 1951 bw Ma'ruf al-Dawalibi Alikimbilia Saudia hadi alipokufa mwaka 2004
  3. Idd Amin dada raisi wa zamani wa Uganda aliyeangusha na majeshi ya Nyerere na yeye alikimbilia huko mwaka 1980 kuishi huko hadi kifo chake mwaka 2003
  4. Raisi wa zamani wa Tunisia Mh Zine el-Abidin Ben Ali naye baada ya kukimbia nchi Jan 16, 2011 amekimbilia Saudi Arabia
  5. Mzee mzima Pervez Musharraf baada ya kulazimishwa kujiuzulu naye alikimbia Saudi Arabia tangia 2008
Hii ni mifano michache ! Kwanini wanakimbilia Saudi?

Hakuna UTAWALA wa SHERIA Saudi Arabia. Wenye nchi kule ni wale waliojimilikisha uongozi wa milele. Na hawa madikteta waliokimbilia huko waliamini kuwa ni viongozi wa nchi zao milele. JK naye ana mwelekeo huo, it's just matter of muda tu naye atakimbilia huko.
 
Mfalme wa Saudia yeye huenda atakimbilia kati ya nchi hizi mbili Afghanistan ama Pakistan, si unajua hata yule kinara wa ugaidi raia wa Saudia naye yuko kati ya Afghanistan na Pakistan.

mimi nadhani hata diktetea wa ivory cost atakimbilia huko
 
Tafuta kitabuConfessions of an Economic Hit Man by John Perkins utapata jibu la swali lako na pengine mengine yanayohusiana na hayo.
 
Sababu zinazowapelekea kukimbilia Saudia ni za kiimani. Nadhani wanatambua makosa yao na kuona hakuna kwingine kwa kukimbilia na kuomba toba isipokuwa kwenye miji mitukufu ya Maka na Madina. Inshallah, Mungu atawasamehe makosa yao.
 
Sijali atakwenda wapi but I wish aachie nchi hata leo naamini nchi imemshinda ndio maana yuko kama hayopo. Ni tatizo iwapo kiongozi mkubwa wa nchi watu wako hawa-feel uwepo wako, it means even if you die none will ever remeber you, SAD
 
Sidhani kama ni dhambi kumpokea kiongozi yoyote anaeomba hifadhi ya kisiasa kama vile Nawaz Shariff alikuwa kiongozi wa kuchaguliwa kidemokrasia na wananchi wake lakini aliempindua Musharaf na yeye baada ya kufukuzwa lakushangaza amepokelewa na Uingereza na kupewa hifadhi!

Mbona huzishangai nchi za Magharibi zinapowapokea vigogo wengi waliotoroka kwao kama vile Oscar Kambona toka Tanzania,Haile Selase wa Ethiopia, Sultani Jamshid bin Abdullah Al Said wa Zanzibar aliekimbilia Uingereza, Dikteta Shah wa Iran aliekimbilia Uingereza, Dikteta Augustino Pinochet wa Chile alikimbilia Uingereza na hata hapa kwetu Tanzania tulishawapokea madikteta waliopinduliwa kwao mfano: ni Milton Obote wa Uganda!

Sasa unaishangaa Saudia ambayo imempokea Zain Abi Din Ali wa Tunisia baada ya Ufaransa kukataa kumpokea wakati alikuwa ni kimpenzi mkubwa wa Ufaransa!

Picha hizi ni baadhi ya viongozi waliokimbilia Uingereza tujikumbushe:

View attachment 20812 Oscar Kambona View attachment 20810 SULTAN WA MWISHO ZANZIBAR JAMSHID



View attachment 20808 DIKTETA AUGUSTINO PINOCHET WA CHILE



View attachment 20811 MILTON OBOTE WA UGANDA HUYU ALIPOKELEWA NA JULIUS K: NYERERE


View attachment 20809 HAILE SELASI MUNGU WA RASTAFARI WA ABBYSINIA

Wote hawa walikimbilia Uingereza mbona hushangai unaishangaa Saudia?


Mkuu umesahau huyu Obote na Nyerere ni walele, ndi maana akakaribishwa Bongo. Umesahau tulivyolishwa unga wa ndele na siasa za chuki juu ya Idd Amini? Hebu kawaulize Waganda wenyewe kuwa Idd Amini alikuwaje, watakuambia. Dikteta ni vile wakubwa wanavyokudefine, mfano Gadaf alikuwa dikteta lkn baada ya kuwa kibaraka wa Marekani amegeuka kuhubiriwa kama rais wa mfano kwa bara la Afrika.
 
Back
Top Bottom