Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 427
KUNDI LA LOWASSA KUMNANGA MWALIMU NYERERE KABURINI AMA KWELI NGUVU ZA FEDHA HUTIA WATU UKICHAA HATA KAMA NI ZA K-ISHETANI!!!
Enyi madalali wa Mh Lowassa kwa wapiga kura wa nchi hii,
Chezea vitu vyote Tanzania hii kwa kadri utakavyoona ni vema na inafaa LAKINI unapoligusa jina la Mwalimu Nyerere kwa kujadili mizaha kama hii wenye akili hawatolumbana nawe ila walalahoi wengi wa nchi hii hujui tu ni kwa kiasi gani utakua umewatonesha moyoni mbele ya dhuluma za VITENDO VYA KIKATILI VYA MAFISADI vilivyofanya maisha yasiwe maisha tena nchi hii.
Nasema chezeeni Richmond, Dowans, endeleeni kwani mnasita kitu gani hapo; kachezeeni pia Symbioni, TANESCO, chezeeni CCM huko hata jina la Rais Kikwetekaichezeeni huko ILA wa kumnanga Mwalimu Nyerere kwa mambo ya kihayawani humu na kote kwingineko ... be warned, hilo si jina la kuuzia dagaa masokoni. Wana-Lowassa katucheeni zaidi na zaidi kifisadi WaTanzania tulio hai maana pindi utakaporusha tu ka-shilingi kwenye sakafu la kanisa au msikiti tayari WaTanzania tutakua tushasahau yote na kukimbilia haraka haraka kumfungulia mfalme Edward lango la Ikulu Magogoni akatawale!!!!!
Ni nani atakayeweza kukuzuia kitu nchi hii; endelea mkuu kachezee kila kitu, cheza, cheza tu. Hata haya matatizo lukuki ya taifa kulala gizani kila uchao sababu ya makovu ya Richmond yote ni mapambo tu tena ya kujitakia sisi wenyewe. Yale mamilioni 150,000,000/- uliotulazimisha kwa umasikini wetu kukulipa wewe kila siku iendayo kwa Mungu shauri ya ulaghai kwa TANESCO hivi sasa ndio wakati wa kuzitumia kisawasawa kila kona ya nchi hii mpaka kila mtu atakapogundua kwamba kweli kidume nchi hii Edward Lowassa wa Monduli; nunua kila kitu wala usiache wajumbe wote ndani ya CCM mikoa kwa vipapatio vya kuku na ubwabwa, kanunue na tume ya uchaguzi upya, magazeti yote kwa kazi ya fedha si ndio hizo bana! LAKINI kwa kuchezea jina la Mwalimu Nyerere kupitia kwa walevi hawa mtandaoni mkome kabisa!!!!!!!!
Naam, kwa kundi hili linaloongozwa na nguvu za fedha za ki-mashetani, waache kundi la Lowassa wamnange salama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, WaTanzania tunasubiri kwa hamu kubwa sana tu KUJA KUONA MWISHO WAKE hizi lugha chafu kama atapona mtu hapo kisiasa. Jibu ni 2015 hata CCMkirongwe vipi na fedha za MAFISADI.
Haya ndiyo matatizo ya wacheza kolokolo. Wapi hapo Nyerere amesemwa vibaya? Wapi hapo nyere amekashifiwa? Je kusema alikuwa na chuki ni kosa? Kusema alitumia propaganda ni kosa? Naona umepita mithiri ya tractor lenye jembe butu, unafyeka na kuacha magugu nyuma. Tengeneza maelezo yako yakae vyema.