Kwanini Nyerere hakumkubali Lowassa?

Kwanini Nyerere hakumkubali Lowassa?

Edward Lowasa alikuwa ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya Urais mwaka 1995 na akaenguliwa kwa hoja nzito ya kutokuwa muadilifu na marehemu Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere, kwa ukweli (wala sio tuhuma) kuwa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi kwa kipindi kifupi ndani ya CCM na Serikali.Muda mfupi alikuwa ni mtumishi wa CCM, muda mfupi kama Mkurugenzi wa kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha. Mwalimu i Nyerere pamoja na kuwa na uthibitisho kuwa Lowasa ni fisadi, kwa nini hakumpeleka mahakamani . Ilikuwa ni uzushi? Au nidhamu hiyo ndio imetufikisha hapa tulipo, yaani pamoja na kujua kuwa kiongozi fulani kafuja mali za umma na tukamwacha mitani na kuwadharau walipa kodi. Na kwa upande mwingine kwa nini Lowasa mpaka sasa hivi haja kana kwamba jina lake lilichafuliwa na Nyerere kuwa kajilimbikizia mali. Kukaa kwake kimya kunaweza kutufanya kufikiri kuwa ni kweli yeye ni fisadi
 
Kwa sababu inaelekea hujui kwamba kazi ya kumfikisha mahakamani mhalifu yeyote ni ya serikali na hasa kurugenzi ya mashitaka, ni vizuri ukaambiwa kwamba Mwalimu hakuwa sehemu ya mamlaka hizo. Lakini hivi wewe ungeweza mtu anayeshangazwa na utajiri wa mtu katika utumishi wake wa muda mfupi? Suala la ufisadi wa huyu bwana halistahili kujadiliwa muda mrefu hivi kwa sababu yeye mwenyewe anajijua.
 
History has never been wrong; time will tell.

Nyerere never endorsed Kikwete, and we all know the results today. However Nyerere also endorsed Mkapa and we saw the results of that endorsement after his passing away. None of the results from the two camps were good for us, but relatively, it is possible than one of them was better.

Time will tell.
 
Kwan nyerere ni nan? Akimkataa m2 inakuwa ndio msimamo wa kumjudge m2. Acheni fikra za kizamani, lowassa ndio anastahili kupewa nchi hii , mpeni mchawi amlee mtoto km ajamkuza,huu msemo tafakari. Acheni upinzani wa kihehere, ccm hakuna anaweza kuwa rais wa ukwel km e l over

CCM Kweli hakuna anayefaa kuwa rais.Kama watanzania watamweka huyu mwizi kuwa raisi basi curse be over my dead body.Nyerere alikua mzalendo wa kweli,aliona mbali,anawafahamu vilivyo wale wenye tamaa na wazalendo wa kweli.Kwa nini mtu utumie hata mbinu chafu ili kuingia tu ikulu????? Lowassa hafai,ninyi mnaompigia kampeni huenda mmeleweshwa na utajiri wake.Mtu alie tuingiza kwenye mkataba mbovu wa richmond ambao sasa tunatakiwa kulipa mabilioni leo awe rais,hapana,hapana,no that is imposible.
 
Imani na itikadi kali juu ya siasa ya ujamaa na kujitegemea ni kirusi kilichokuwa kimeathiri kwa kiasi kikubwa mfumo wa ufahamu wa baba wa Taifa mwalimu Nyerere na, kuamini kuwa hakuna kitakachofanya nchi isonge mbele zaidi ya siasa ya ujamaa na kujitegemea. Msimamo uliosababisha chuki kwa wajasiriamali wengi waliojitolea nguvu zao halali kuongeza vipato, mmojawapo akiwa Lowassa.

Chuki ambayo iliibuka wazi wakati wa kinyang'anyiro cha kuwania urais mwaka 1995. Kwa kuwa Nyerere tayari alikuwa ameshajichagulia mtu wa kumrithisha kiti kilichokuwa kinaachwa na mzee wa ruksa. Wengine waliokuwa na nia ya kuwania kiti hicho akawaundia zengwe la kuwaangusha.

Mmoja wa wanasiasa walioathirika na propaganda hizo ni mheshimiwa LOWASSA ambaye hivi sasa mamilioni ya watanzania wanategemea ukombozi wa kweli kutoka kwake. Mwingine aliyeathiriwa na zengwe la NYERERE ni rais wa sasa Mh JM KIKWETE.

Hakuna siri kuwa MKAPA ndiye aliyekuwa chaguo la wazi la mwalimu kiasi cha kutumia kila aina ya ushawishi wake kuhakikisha kuwa LOWASSA na KIKWETE wanaanguka. Kinachosikitisha, zaidi ya miaka 15 imepita sasa bado kuna Watanzania ambao wanaamini kile kilichosemwa na NYERERE dhidi ya LOWASSA.

Propaganda ni kitu kibaya sana, mtu anaweza kuujengea hoja uongo na kuwa ukweli na, watu wakashikilia misimamo wakitetea uongo uliogeuzwa na mwana propaganda kuwa ukweli.

NYERERE alimkataa LOWASSA kwa kisingizio cha kivuli cha ubepari, kwa bahati mbaya wakati huo hakukuwa na mtu wa kumuuliza NYERERE kwa nini hakupambana na ubepari wa LOWASSA wakati wa utawala wake badala yake iwe wakati wa uchaguzi ambao unafanyika mbali na awamu yake ya uongozi? Hapa mtu makini ataamini kuwa propaganda hizo zilikuwa zinaongozwa na chuki binafsi na wala sio uzalendo.

Mtu makini ataamini kuwa NYERERE alikuwa anajua kuwa, ujasiriamali wa LOWASSA haukuwa haramu ndiyo maana hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake.

Ni wakati sasa kwa wale waliorithi habari za mapokeo dhidi ya LOWASSA na kujiaminisha kuwa ni mtu asiyefaa. Wafikirishe akili zao kwa makini na sote kwa pamoja tumuunge mkono mtu huyu iwapo atasimama kwa ajili ya kuomba nafasi ya kuliongoza Taifa hili.
 
Hongera sana mkuu kwa kusema ukweli! Tusubiri wafuasi wa NAPE.
 
Naunga mkono hoja 100%... Itikadi ya CCM si ya ujamaa na kujitegemea tena bali ni ya ujasiriamali... Lowassa anatufaa sana katika kipindi hiki kwani ni mtu pekee mwenye maamuzi ....
 
Mkuu na wewe unatumia maneno ya mtandaoni ama maneno ya yule mzee anayeitwa Kasori. Hivi kuna minutes zozote zinazosema Nyerere aliyatoa hayo maneno?
 
Lowassa ata umsafishe vipi atabaki kuwa mwizi,acha kupoteza nguvu zako bure..
Kama unabisha tafuta mtoto wa darasa la kwanza njiani kisha muulize "ivi fisadi namba moja nchi hii ni nani?"..alafu utashangaa jinsi atakavokujibu vizuri.
 
Imani na itikadi kali juu ya siasa ya ujamaa na kujitegemea ni kirusi kilichokuwa kimeathiri kwa kiasi kikubwa mfumo wa ufahamu wa baba wa Taifa mwalimu Nyerere na, kuamini kuwa hakuna kitakachofanya nchi isonge mbele zaidi ya siasa ya ujamaa na kujitegemea. Msimamo uliosababisha chuki kwa wajasiriamali wengi waliojitolea nguvu zao halali kuongeza vipato, mmojawapo akiwa Lowassa. Chuki ambayo iliibuka wazi wakati wa kinyang'anyiro cha kuwania urais mwaka 1995. Kwa kuwa Nyerere tayari alikuwa ameshajichagulia mtu wa kumrithisha kiti kilichokuwa kinaachwa na mzee wa ruksa. Wengine waliokuwa na nia ya kuwania kiti hicho akawaundia zengwe la kuwaangusha. Mmoja wa wanasiasa walioathirika na propaganda hizo ni mheshimiwa LOWASSA ambaye hivi sasa mamilioni ya watanzania wanategemea ukombozi wa kweli kutoka kwake. Mwingine aliyeathiriwa na zengwe la NYERERE ni rais wa sasa Mh JM KIKWETE. Hakuna siri kuwa MKAPA ndiye aliyekuwa chaguo la wazi la mwalimu kiasi cha kutumia kila aina ya ushawishi wake kuhakikisha kuwa LOWASSA na KIKWETE wanaanguka. Kinachosikitisha, zaidi ya miaka 15 imepita sasa bado kuna Watanzania ambao wanaamini kile kilichosemwa na NYERERE dhidi ya LOWASSA. Propaganda ni kitu kibaya sana, mtu anaweza kuujengea hoja uongo na kuwa ukweli na, watu wakashikilia misimamo wakitetea uongo uliogeuzwa na mwana propaganda kuwa ukweli. NYERERE alimkataa LOWASSA kwa kisingizio cha kivuli cha ubepari, kwa bahati mbaya wakati huo hakukuwa na mtu wa kumuuliza NYERERE kwa nini hakupambana na ubepari wa LOWASSA wakati wa utawala wake badala yake iwe wakati wa uchaguzi ambao unafanyika mbali na awamu yake ya uongozi? Hapa mtu makini ataamini kuwa propaganda hizo zilikuwa zinaongozwa na chuki binafsi na wala sio uzalendo. Mtu makini ataamini kuwa NYERERE alikuwa anajua kuwa, ujasiriamali wa LOWASSA haukuwa haramu ndiyo maana hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake. Ni wakati sasa kwa wale waliorithi habari za mapokeo dhidi ya LOWASSA na kujiaminisha kuwa ni mtu asiyefaa. Wafikirishe akili zao kwa makini na sote kwa pamoja tumuunge mkono mtu huyu iwapo atasimama kwa ajili ya kuomba nafasi ya kuliongoza Taifa hili.


Posho imenogaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, inogile posho hiyoooooooooo,kula pesa ya white hair banaaaaaaa
 
nyerere alikuwa na wivu sana yule mzee alikuwa hataki mtu ampite
 
napigana nawe kwa asilimia 1,000 kabisa. Lowasa hawezi kuwa kiongozi mzuri hata siku moja kwa tanzania hiii, hizo propaganda zinafanywa kwa nguvu ya pesa tu. Naweza kusema, na bado ntaendelea na msimamo wangu juu hawa jamaa wawili.....mwl aliwaewa na akasema bado sana kuchukua nchi, nadhani kila mtu anaona jinsi nchi isivyotawalika kwa sasa....yanayotekea sasa ni matokeo ya tulichoambiawa. Mkapa aliicha nchi mahali ambapo sio penyeweee kabisa.....na bado tutayaona mengi sibirini
 
day light dreamin.. we dnt nid lowassa.. we dnt nid jk.. we dnt nid mizengo and we dnt nid ccm..! msemeni Nyerere bt mkae mkijua hakuwahi hata cku moja kufanya maamuzi kwa maslahi yake au familia yake au rafiki zake.. na hapo ndipo alipowaacha mbali..
 
Hivi kwanini mnaompinga Lowassa hamna hoja zaidi ya chuki tu?
 
Nyerere alikuwa binadamu, hangeweza kuwa sahihi 100% kwa kila alichosimamia. Umesema mwenyewe aliwakataa Lowasa na kikwete, miaka kumi baadaye mkawa 'mmekua' mkawapa hao watu wawili nchi, sasa je, wamem-prove wrong Nyerere?! Hao watu ambao mfumo wao wa ufahamu haujaathirika ndio ambao au wameiibia nchi hii au wanawalinda wanaoiibia! Hivi kwa nchi yenye viongozi wenye akili timamu, sahau habari za richmond/dowans, na madudu ya karibuni yote... fikiria IPTL tu... ingekuwepo hadi leo ikiukamua uchumi wa nchi hii?? Wenzenu wamejaribu kumlaumu Nyerere ili kuficha uovu wao wamechemka! Ajabu na nyie mnafuata mkondo uleule! Kajipangeni upya.
 
day light dreamin.. we dnt nid lowassa.. we dnt nid jk.. we dnt nid mizengo and we dnt nid ccm..! msemeni Nyerere bt mkae mkijua hakuwahi hata cku moja kufanya maamuzi kwa maslahi yake au familia yake au rafiki zake.. na hapo ndipo alipowaacha mbali..

daaah kweli nimeamini lowasa anamkono mkubwa saana nchini hapa, lakini ung'ang'anizi woote huo wa lowasa anataka nini hasa? kwani mheshimiwa lowasa unaamini wewe ni kiongozi pekee wa nchi hii kwanini huwezi kuwaachia wengine sababu wewe umeshachafuka. najua unanguvu ndani ya ccm na hakuna mtu wakukuzuia wewe si jk wala nape, lakini kwanini usipumzike tuu lowasa. Please mheshimiwa Lowasa achana na ndoto za uraisi wa nchi hii jikite zaidi kwenye biashara zako mkuu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom