MWANALUGALI
JF-Expert Member
- Feb 1, 2010
- 601
- 34
Mi binafsi sijakubaliana na kundi lolote kupotosha ukweli au kumuunga mkono yeyote lakini ni lazima nisema ukweli ninao ujua hata kama wewe hautaniunga mkono. Sioni kosa alilofanya Edo mpaka asulubiwe kiasi hiki!! Makosa mengi mnayomtwisha Edo binafsi ni makosa ya kimfumo yanayo paswa kubebwa na chama cha Magamba kama taasisi. Ujanja wao wa kutaka kujivua gamba hauwezekaniki wala kukubalika, hawawezi kumgeuzia kibao mtu mmoja au wawili kwa kusingizia kuwa Nyerere alimkataa. Chama chao kinaweza kujitakasa (kujivua gamba) kwa kuachia madaraka na kuitisha uchaguzi huru chini ya tume huru ya uchaguzi, vinginevyo ni heri ya huyu huyu Lowasa kuliko hawa waliopo wanao onekana kupwaya kila idara.Ndio kundi la LOWASA mlivyokubaliana kuupotosha ukweli ili kuchanganya facts. Bahati mbaya facts are very stuborn things, they will remain facts, whether you like them or not. Na watu wanaomatter wote wanaujua huo ukweli, so keep on kujipa moyo huku kwenye keyboard.
Wakitaka kushikiria hoja ya waliokataliwa na Nyerere, watakuwa wanajivua nguo hadharani maana waliokataliwaa kwenye chama chao ni wengi akiwemo Kikwete, Lowasa, Sitta, Msekwa, Malecela nk. Hivyo kwa hoja ya kukataliwa na Nyerere, basi hata CCM ya sasa ilikataliwa na Nyerere kwa kuwa imeisha toka kwenye misingi yake ya kuchukia Ufisadi na kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi.