Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Iran alijibu within hours baada ya kushambuliwa tena akifumua Radar kubwa ya Marekani middle east, akapiga kambi zote za Marekani middle east. Hakuna Taifa lililoshambulia kambi za Marekani zaidi ya Pearl Harbour miaka 85 iliyopita. Iran imeweza tena si kwa kubahatisha, ni kuilazimu USA kuomba hifuadhi Cyprus

Hapa ndipo inaonyesha hujui kinachoendelea, unahitaji msaada

Anga la Israel linalindwa na layers nyingi kuliko anga lolote duniani kwa mifumo hii, THAAD ya Marekani, PATRIOT ya Marekani, David Sling , Arrow na Iron dome. Iran ilihitaji kufumua mifumo hiyo kwanza.

Drones na makombora yalilenga ku deplete stock ya anti missile. Drone moja ina bei ya Dollar 25,000 wakati anti missile moja ina dola milioni moja. Iran ilichofanya ni ku flood the sky na kulazimisha Israel kutungua drone na makombora ya zamani kiasi cha kumaliza mfumo wa anga wa Israel

Baada ya hapo unaona Tel Aviv inapigwa kama Gaza. Kila kombora la Iran linatua eneo lolote la Israel.
Kwasasa Iran haihitaji kutumia makombora na drones nyingi kwasababu anga la Israel lipo wazi kama ilivyo middle east. Iran ilishambulia nchi zote zilizozuia makombora kutokana na somo la vita ya siku 12

Kwasasa kombora moja tu lina madhara kwasababu drones zimeufumua mfumo wa anga wa Israel.
Hakuna Taasisi yoyote ya ulinzi ya Israel iliyosimama.

Katika vita hii Israel yupo kama jina, wenye vita ni hawa; USA, UK, Australi, Netherland, Germany, France na EU ukiondoa Spain. Vita kati ya Israel na Iran ilikwisha, Iran ana deal na mkusanyiko wa Mataifa

Israel imepiga marufuku mashirika ya habari kupiga picha bila ruhusa.
Raia anayepiga picha anafungwa miaka 5.Unajua ni kwanini?

Well, umeona teknolojia ya kuficha makombora ardhini?

Iran haipigani vita kushinda inapigana ku sruvive. Iran inapigana na USA, EU na Washirika wao wa middle east
Juzi walionesha Khorramshir! wenyewe wanasema stock ya zamani imekwisha, wanaanza na mpya

Love or hate Iran, wapeni maua yao!
Ushabiki.
Unasema israel wanazui watu kutoa habari ila wewe uko namtumbo unajua kwamba inapigwa kama Gaza!

Iran kwa sasa anarusha drones na makombora kwa kuvizia, maana mwanzo alirusha kwa kupupa mara israel mara kwa waarabu wenzie, wakati anarusha kwa pupa Israel alikuwa anawinda lounchers na maghala kisha kulipua.

Irani sasa hivi anatepeta ila anatembelea kiburi cha waislamu wote duniani kwamba ni bora kufa kuliko ku surrender

Kitakwimu inaonesha makombora na drones zinazorushwa toka Iran imepungua kwa 90%
 
You constantly shy away from speaking the truth. If you can not speak honesty due to your " Mahaba" it would be better to remain silent than to mislead people. As one of the Most prominent JF Speakers, Many may assume you hold the monopoly on Truth.
Once I felt a victim to your biased posts. back then I would slide into your profile and read your posts and I felt apprehensive about what the future holds for the world. due to your incessant take on Geopolitics.
Then, I have taken my time to study pattens and it appears that you prettily alarming opinionated emotional analyst.

In other hand.
adriz Remind your children that jumping into a conversation when adults are talking is a sign of being ill-mannered. Discourage this both in your home and elsewhere.
Your English has improved exponentially. Hongera Sana....

I hope next time we meet, the edges of your brain power would pace geometrically as well....
 
Usiwape hizi taarifa, waache watafute wenyewe.....
Sijui kama wanajua watafutie wapi. Taarifa ya kendy itawasaidia sana vijana wa Kenya na Uganda wanaosoma JF. Hawa wakwetu lugha ni tatizo, kutafuta habari tatizo !
Hapa atakuja kusema chanzo chako hakiaminiki, hivyo usipoteze muda......
Sidhani kama watahoji chanzo! kwani wameelewa kilichoandikwa!

Some people will always be committed to misunderstanding you no matter how hard you explain....
Nawatetea Vijana hakuna misunderstanding kuna ignorance ya hali ya juu sana Tanzania.
Wengi wanasoma ili kujibu kilichoandikwa, hawasomi kuelewa kilichoandikwa ndio maana wanabisha tu katika mabandiko. Hawana uwezo wa ku rebuttal hoja. Ujinga umekolezwa na DINI. Yaani hawana muda wa kuangali jambo kutoka angle tofauti! huku Wayahudi kule Waarabu! hawajishughulishi hata kutafuta facts

Mfano, nimewauliza kosa la Iran ni lipi hadi ashambuliwe? Hakuna anayejibu, wapo bize, apigwe !
 
Adolf Hitler alipovamia USSR mwaka 1941 alidhani vita ingaisha wiki tatu tu, ikageuka miaka minne.

Benitho Mussolini alipovamia kisiwa cha Crete mwaka 1940 alidhani itakuwa wiki, kumbe miezi nane.

Lyndon Johnson alipeleka vikosi Vietnam mwaka 1965 wakitegemea itaisha mapema wakafika 1973.

Bill Clinton alipeleka vikosi Somalia mwaka 1993 akisema operesheni itakuwa ya saa moja, ikawa siku 1.

Siasa za dunia haziendeshwi kama MCHEZO WA UPATU, hii dunia ina mmliki wake halali na siyo USA.
Hayo huwa ni mahesabu ya mdomoni kwa watu ila field huwa wanajua kabisa hapa lolote inatokea.

Hata Putin alienda akifikiria siku tatu tu Ukrain itakuwa imeanguka ila mpaka leo mwaka wa nne ana hangaika.

Putin anaanglia faida ya miaka 50 mpaka 100 ijayo.

Hapo Iran USA atapoteza pesa lakin in long run hizo hela si kitu
 
Ushabiki.
Unasema israel wanazui watu kutoa habari ila wewe uko namtumbo unajua kwamba inapigwa kama Gaza!

Iran kwa sasa anarusha drones na makombora kwa kuvizia, maana mwanzo alirusha kwa kupupa mara israel mara kwa waarabu wenzie, wakati anarusha kwa pupa Israel alikuwa anawinda lounchers na maghala kisha kulipua.

Irani sasa hivi anatepeta ila anatembelea kiburi cha waislamu wote duniani kwamba ni bora kufa kuliko ku surrender

Kitakwimu inaonesha makombora na drones zinazorushwa toka Iran imepungua kwa 90%
Hiii chai %90 haaaaa wangepishana vikumbo kuondosha Wananchi wao Middle East!!!!!!! Iran

ndio kwanza yupo kwenye %0 . 0 ndiomana Yemen bado kanyuti kaambiwa tulia kwanza tupungeze zagazaga za miaka ileeeee..

ngoma bado Asubui sn.

Tela Aviv wanakufa kwa presha tu usiku mnene kwao.
 
Ila huyu POTUS akili zake anazijua mwenyewe. USA imepatikana term hii.
a567e261-0684-44ce-a98f-3be714b55bf1.jpg
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2022 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

Kwa hiyo ulitegemea Iran itapigwa ndani ya siku ngapi?
Iran ni nchi kubwa sana na ina jeshi kubwa (kwa idadi ya wanajeshi na silaha)
 
Boeing KC-135 siyo tu ndege, bali ni alama (A Symbol) ya nguvu ya kijeshi ya jeshi la anga la Marekani na ubunifu wa kiteknolojia. Leo hii moja imeanguka na kusababisha vifo vya askari 6, huku nyingine imepata hitilafu na kukimbilia Israel. Hitilafu zimetokea Iraq na wao wanadai ni matatizo ya kiufundi.

Hizi ndege zilitengenezwa mwaka 1955, kipindi cha utawala wa Raisi Dwight Eisenhower na mpaka leo hii zipo tu. Kiufupi hizi ndege ni vituo vya mafuta vinavyopaa (Flying Gas Station). Hizi ndege ni za kipindi cha vita baridi na zina miaka zaidi ya 60, jambo ambalo linazifanya zitumia gharama kubwa mno kwenye ukarabati (Maintenance).

Taarifa zinasema kwamba hizi ndege kwa safari moja tu hutumia zaidi ya dola za Kimarekani 11,000 ambazo ni sawa na milioni 23 hadi 24 za kitanzania. Jumla ndege zote hugharimu dola za Kimarekani bilioni 5 kwa mwaka kufanyiwa matengenezo. Miaka ya 2003 baada ya kuonekana hizi ndege ni kongwe na zitahitaji gharama kubwa kuzifanyia marekebisho ilibidi watengeneze ndege nyingine jambo ambalo halikufanikiwa mpaka leo hii. Inasemekana mbali na marekebisho mengi, hizi ndege haziwezi kuvuka 2030.

KIUFUPI SASA: Operesheni nzima ya Marekani na Israel inategemea Boeing KC-135. Ndege-vita kama F-35 zinazoshambulia, au B-2 Spirit(Ambazo zinategemewa kutumiwa hivi punde) na ndege nyingine zinazofanya shughuli za ujasusi zinategemea sana hizi Boeing KC-135 katika kufanya mashambulio. Tatizo linakuja hapa sasa:

Mosi, hizi ndege zinahitaji matengenezo makubwa ya gharama ili kuweza kuruka juu na kufanya kazi vizuri. Hii vita ikiendelea, sidhani kama Marekani atakuwa na uwezo wa kuzifanyia marekebisho ndani ya muda mfupi ndege zenye miaka zaidi ya 60, kongwe kuliko hata TANGANYIKA. Rushwa ndiyo chanzo kikubwa kufanya serikali ya Marekani ishindwe kupitisha zabuni ya kutengeneza aina nyingine ya ndege zenye uwezo wa kujaza mafuta kama KC-135. Kiufupi, kinachomkuta Marekani kipindi hiki, ndicho kilichomkuta Urusi miaka ya 90's (Zingatia the Sinking of the Kursk/Crash of Antonov A-24)ambapo ndege zake kongwe na manowari zilikuwa zinapata ajali tu kwasababu za kiufundi.

Pili, hizi ndege zina udhaifu mkubwa mno. Zinapojaza mafuta huwa zinaenda taratibu mno angani jambo ambalo kwa vita kama hii ya Iran, itazifanya kuwa shabaha rahisi mno. Kiusalama inabidi hizi ndege za F-35 na zingine zijazie mafuta Iraq ili zishambulie Iran. Lakini bahati mbaya, Iraq imejaa wanamgambo wa kishia ambao wanaweza kuzitungua. Ukizingatia pia kwamba itakuwa ngumu kwa hizi ndege kutua sehemu kama Saudi Arabia, UAE, Bahrain au Qatar kwasababu kambi za Marekani hazifanyi kazi kwasasa.

UKWELI NI KWAMBA, kipindi hiki Marekani ameyatimba....
WhatsApp Image 2026-03-13 at 10.58.21 AM.jpeg

648349.jpg
 
Boeing KC-135 siyo tu ndege, bali ni alama (A Symbol) ya nguvu ya kijeshi ya jeshi la anga la Marekani na ubunifu wa kiteknolojia. Leo hii moja imeanguka na kusababisha vifo vya askari 6, huku nyingine imepata hitilafu na kukimbilia Israel. Hitilafu zimetokea Iraq na wao wanadai ni matatizo ya kiufundi.

Hizi ndege zilitengenezwa mwaka 1955, kipindi cha utawala wa Raisi Dwight Eisenhower na mpaka leo hii zipo tu. Kiufupi hizi ndege ni vituo vya mafuta vinavyopaa (Flying Gas Station). Hizi ndege ni za kipindi cha vita baridi na zina miaka zaidi ya 60, jambo ambalo linazifanya zitumia gharama kubwa mno kwenye ukarabati (Maintenance).

Taarifa zinasema kwamba hizi ndege kwa safari moja tu hutumia zaidi ya dola za Kimarekani 11,000 ambazo ni sawa na milioni 23 hadi 24 za kitanzania. Jumla ndege zote hugharimu dola za Kimarekani bilioni 5 kwa mwaka kufanyiwa matengenezo. Miaka ya 2003 baada ya kuonekana hizi ndege ni kongwe na zitahitaji gharama kubwa kuzifanyia marekebisho ilibidi watengeneze ndege nyingine jambo ambalo halikufanikiwa mpaka leo hii. Inasemekana mbali na marekebisho mengi, hizi ndege haziwezi kuvuka 2030.

KIUFUPI SASA: Operesheni nzima ya Marekani na Israel inategemea Boeing KC-135. Ndege-vita kama F-35 zinazoshambulia, au B-2 Spirit(Ambazo zinategemewa kutumiwa hivi punde) na ndege nyingine zinazofanya shughuli za ujasusi zinategemea sana hizi Boeing KC-135 katika kufanya mashambulio. Tatizo linakuja hapa sasa:

Mosi, hizi ndege zinahitaji matengenezo makubwa ya gharama ili kuweza kuruka juu na kufanya kazi vizuri. Hii vita ikiendelea, sidhani kama Marekani atakuwa na uwezo wa kuzifanyia marekebisho ndani ya muda mfupi ndege zenye miaka zaidi ya 60, kongwe kuliko hata TANGANYIKA. Rushwa ndiyo chanzo kikubwa kufanya serikali ya Marekani ishindwe kupitisha zabuni ya kutengeneza aina nyingine ya ndege zenye uwezo wa kujaza mafuta kama KC-135. Kiufupi, kinachomkuta Marekani kipindi hiki, ndicho kilichomkuta Urusi miaka ya 90's (Zingatia the Sinking of the Kursk/Crash of Antonov A-24)ambapo ndege zake kongwe na manowari zilikuwa zinapata ajali tu kwasababu za kiufundi.

Pili, hizi ndege zina udhaifu mkubwa mno. Zinapojaza mafuta huwa zinaenda taratibu mno angani jambo ambalo kwa vita kama hii ya Iran, itazifanya kuwa shabaha rahisi mno. Kiusalama inabidi hizi ndege za F-35 na zingine zijazie mafuta Iraq ili zishambulie Iran. Lakini bahati mbaya, Iraq imejaa wanamgambo wa kishia ambao wanaweza kuzitungua. Ukizingatia pia kwamba itakuwa ngumu kwa hizi ndege kutua sehemu kama Saudi Arabia, UAE, Bahrain au Qatar kwasababu kambi za Marekani hazifanyi kazi kwasasa.

UKWELI NI KWAMBA, kipindi hiki Marekani ameyatimba....
View attachment 3557678

View attachment 3557679
Unajua bajeti ya ulinzi wa Marekani Kwa mwaka ukilinganisha na bajeti ya Iran na nchi zingine??
Umechagua upande ambao utakutesa sana kwenye chambuzi zako
 
Back
Top Bottom