Kwanini mahusiano/ndoa nyingi hazidumu?

Kwanini mahusiano/ndoa nyingi hazidumu?

Nilitaka ni comment lakini nilivyo fika hapa nikaona hakuna umuhimu tena wakuendelea kusoma comments wala kuandika nilichotaka kuchangia.

Zaburi 133:1 tazama ilivyopendeza jinsi ndugu,wanandoa wakae pamoja na kuwa umoja.( maana yake WANANDOA ni kitu kimoja kosa la mmoja ni la wote hivyo nguzo kuu ni kuvumiliana)
Uvumilivu ndo nguzo kuu ya mahusiano ikikosekana basi ni lazima kuishia njiani
 
Tumeacha mila na desturi zetu tukachukua za magharibi hii ndio gharama yake zamani tulioa kwa kushauliwa na kuufahamu ukoo unaokusudia kuoa na tulikuwa wasikivu kwa sasa tunakutana bar.viuoni.kwenye daladala nk nani anafahamu historia ya ukoo wa mwenza tunachojua ni kutangaza ndoa miezi michache tu imevunjika
 
Uvumilivu ndo nguzo kuu ya mahusiano ikikosekana basi ni lazima kuishia njiani
Kabisa, uvumilivu siku hizi watu wanaona ni ujinga wakati ndio nguzo kuu ya mahusiano yoyote yaliyodumu... Uwa nawaangalia tu wanavyodanganyana.

Naamini kabisa hata mzazi wako tangu aanze kukulea udogoni mpaka umefika hapo alikuvumilia kwa mengi sana kam vile kula ada ya shule, kupigana ovyo,kula ganji etc... Lakini pamoja na yote hayo hakuwahi kuthubutu hata siku moja kukufukuza nyumbani kwake!

Sasa tukichukua mfano huu halafu tukajaribu kuamishia kwenye ndoa, tutaishinda mitihani mingi sana.
 
Ndoa nyingi huvunjika kwa sabab ya uwepo wa simu za mkonon.......thats all hakuna jingine
 
Kabisa, uvumilivu siku hizi watu wanaona ni ujinga wakati ndio nguzo kuu ya mahusiano yoyote yaliyodumu... Uwa nawaangalia tu wanavyodanganyana.

Naamini kabisa hata mzazi wako tangu aanze kukulea udogoni mpaka umefika hapo alikuvumilia kwa mengi sana kam vile kula ada ya shule, kupigana ovyo,kula ganji etc... Lakini pamoja na yote hayo hakuwahi kuthubutu hata siku moja kukufukuza nyumbani kwake!

Sasa tukichukua mfano huu halafu tukajaribu kuamishia kwenye ndoa, tutaishinda mitihani mingi sana.
[emoji120] [emoji120] [emoji120] ubarikiwe mkuu
 
Babu na bibi zetu mpaka Leo wapo kwenye mahusiano .. Unakuta wtu wanatimiza miaka 60 ya kuish pamoja

Lakin kizaz Chetu ndoa zmekua zikivunjika kila kukichwa...nilishuhudia mke akipewa talaka siku moja baada ya harusi

Zama hzi ndoa ikifkisha miaka 10 ujue watu wamevumiliana sana...
Je, nini kinasababsha hili janga??

1) usaliti?
2) kutokua makini wakat wa kuchagua mwenza?
3) wanandoa kutojua wajibu wao?
4) utandawazi unachangia?

Tujadiliane huu Uzi wakuu
Wewe umeoa au kuolewa ?


Ndoa zinadumu, tatizo watu mnapenda kutumia mifano ya watu wanaofeli kwenye mahusiano badala ya kujifunza kupitia ndoa zenye mafanikio.
 
Ukosekano Wa uvumilivu tu ndio sababu

Ili ndoa idumu
1: uvumilivu
2:u uvumilivu
3:uu uvumilivu
 
Babu na bibi zetu mpaka Leo wapo kwenye mahusiano .. Unakuta wtu wanatimiza miaka 60 ya kuish pamoja

Lakin kizaz Chetu ndoa zmekua zikivunjika kila kukichwa...nilishuhudia mke akipewa talaka siku moja baada ya harusi

Zama hzi ndoa ikifkisha miaka 10 ujue watu wamevumiliana sana...
Je, nini kinasababsha hili janga??

1) usaliti?
2) kutokua makini wakat wa kuchagua mwenza?
3) wanandoa kutojua wajibu wao?
4) utandawazi unachangia?

Tujadiliane huu Uzi wakuu
Siku hizi kubaini usaliti ni rahisi sana ukilinganisha na miaka. Zama hizo ndoa nyingi zilidumu siyo kwa upendo bali ukweli kufichwa kwa ustadi wa hali ya juu.
 
Habari ya leo wanajumuia wa hapa, Leo nimeona tushirikiane juu ya jambo hili. Niende moja kwa moja kwenye Mada.

Miaka ya karibuni K umekuwa nana ongezeko kubwa la ndoa zinazofungwa lakini matokeo yake asilimia kubwa ya ndoa hizo hazidumu, mpaka tunajiuliza kulikoni mbona walipendana vya kutosha imekuaje? Mbona harusi yao ilifana sana? Ndani ya mwaka mmoja wameachana sababu ni :-

1. Wanawake kufanya harakati kwenye ndoa, hapa wanawake wanafika kwenye ndoa wakiwa na akili ya kutaka haki sawa, kitu ambacho kwenye tasisi ya ndoa hakipo kabisa, mwanaume ameumbwa na amepewa mamla ya kutawala tangu pale Mwanadamu wa kwanza kuasi pale bustani ya Edeni(Mwanzo;3:16, "Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako na kuzaa kwako, utungu utazaa watoto na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala") kwahiyo maana yake ukiolewa uko chini ya utawala wa Mume, ukitaka usawa maana yake hakuna maana ya mwanamke kuolewa bali kuoa.

2. Utii; Wanawake siku hizi wamekosa utii labda kwa sababu kuna taasisi nyingi zipo kwa minajili ya kutetea haki zao, au pengine ni kutokana na Elimu waliyoipata utii umekosekana mwanamke ili adumu kwenye ndoa utii kwa mume unamhusu, kwa wakristo wale walokole wanakosa utii kwa waume zao matokeo yake wanapeleka utii kwa wachungaji wao wa kiroho, wenyewe ni mashahidi ndoa za wengi wao zimevurugika na kashfa kibao kosa ni kukosa utii( kolosai 3:18) imempasa mwanamke kumtii mume wake katika hali yeyote huo utii kwa kiingereza wametumia neno submissive yaani utii ukiwa na unyenyekevu, neno utii limesisitizwa pia waefeso 5:22-24, 1petro 3:1-2.

Mtasema mbona umeongelea wanawake tu na sio wanaune , wanawake ndo wamepewa dhamana kuijenga ndoa na ndo maana ukisoma mithal inasema mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba kwa mikono yake maana yake MWANAMKE mwerevu huijenga.

Niwatakie siku njema
 
Back
Top Bottom