Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi
Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.
Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa.
Watanzania wenzetu sijui nani katuloga. Mbona tunasahau mapema sana kiasi hiki. Hivi leo tumesahau kuwa chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini ni mfumo uliopo serikalini?
Swali dogo naomba kuuliza:
Ni waziri mkuu gani mwenye rekodi ya kipekee ya kuwa mkali zaidi tena kwa vitendo kwa watendaji wa serikali? Sio Lowassa huyu huyu aliekaa madarakani kama mtendaji mkuu wa serikali kwa muda mchache zaidi, na ndie huyu aliweka rekodi ya kuwa mkali zaidi kwa watendaji wa serikali wanaopenda kufanya kazi kwa mazoea?
Ni waziri mkuu yupi aliekuwa na uwezo wa kumwajibisha mkuu wa wilaya on the spot? Halafu leo mnasema Lowassa hajawahi kupambana na ufisadi!
Kitendo kile cha Lowassa kinaonyesha dhahiri kuwa ni kiongozi anaepambana na system nzima ambayo ndio chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini. Kwa maneno mengine Lowassa anapambana na chanzo cha ufisadi ambao ni mfumo wa utendaji wa serikali. Lowassa kawawajibisha watendaji kadhaa wa serikali kwa kipindi kifupi cha madaraka yake. Hii ni kuonyesha kuwa anakabiliana na mfumo mbaya uliopo serikalini kiasi cha kuasisi kile kinachoitwa ufisadi.
Sitaki kuamini kuwa watanzania tunapenda maneno matupu yanayoendelea kusemwa na viongozi wengi kuhusu ufisadi ilhali ufisadi unaasisiwa na ulegelege uliopo kwenye mifumo ya utendaji wa serikali. Hawa wengine wanaongea kuhusu ufisadi wamechukua hatua gani kukabiliana na ufisadi? Leo hii kuna baadhi ya watanzania ambao kuongea tu bila vitendo kunatosha kuwaridhisha. Jamani maneno bila matendo hakufai kitu.
Lowassa anaelewa vizuri sana chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini ni mifumo ya kiserikali. Na ndio maana muda mchache aliokaa madarakani kama waziri mkuu alianza kudili perpendicularly na mifumo hiyo kwa kuwawajibishwa wale waliopewa dhamani kwenye utumishi wa umma, ambao kwapo ndio mianya ya ufisadi.
HAKUNA NAMNA YA KUWEZA KUDHIBITI UFISADI NCHI HII ZAIDI YA KUKABILIANA NA MFUMO WA UTENDAJI ULIOPO SERIKALINI, JAMBO AMBALO LOWASSA TAYARI ALIANZA KULITEKELEZA!
Lowassa ana upeo mkubwa sana, na nchi anaifahamu vizuri sana ndani nje! Ni mtendaji sio muimba taarabu!
KWA WATIA NIA WOTE HAKUNA ALIYEWAHI KUPAMBANA NA UFISADI KWA MATENDO KAMA LOWASSA. KILA MTANZANIA NI SHAHIDI.
Leteni hoja nyingine sio hii ya Lowassa ya kupambana na ufisadi maana ameshapambana nao kwa matendo. Anajua chanzo kikuu cha ufisadi na ndo hapo hapo alipokomalia!
Anaesema Lowassa hajawahi kupambana na ufisadi alete pua yake hapa kwenye huu uzi. Na aseme ni kiongozi yupi ndani ya ccm aliewahi kuelewa vizuri dhana hii ya ufisadi na kuanza kuikabili kama sio Lowassa.
Mara nyingine mkiuliza maswali magumu muwe pia una uwezo wa kuelewa majibu magumu. Lowassa hapendi kuzungumzia hadharani ufisadi kwa maneno matupu kwa sababu anaelewa fika wapi kilipo chanzo kikuu cha ufisadi. Ni utendaji wa mifumo ya kiserikali ambao ndio aliokuwa anakabiliana nao kwa vitendo sio kwa porojo
Lowassa ndio mpambanaji pekee anayeweza kupambana na ufisadi kwa vitendo na sio kwa ngonjera na dhana eti tukimchague yule eti masikini mwenzetu ataweza. Acheni ushabiki kuweni realistic. We trust in Lowassa. All the best MH Lowassa
Naunga mkonyo hoja,EL alikuwa anaogopeka na watendaji wa serikali kipindi cha uwaziri mkuu wake.
Kuifukuza City Water.... KUrejesha kiwanja cha Mnazi Mmoja... kukusudia kuvunja mkataba wa Richmond ?.... Lowassa ndo Jembe la Ukweli la CCM .. hakuna mwingine ...
Kwenu
gwijimimi ,
Utotole ,
h120 na wengine wachache! post hapo chini ya
LebronWade naijibu hapa kama ifuatavyo:
Japo mwandishi ameandika kama analia lakini ngoja nimjibu kiungwana zaidi.
== Sio sahihi kumfananisha mkuu wa wilaya na mwenyekiti wa kata, kumfananisha hivi ni kuonyesha dharau na kuonyesha pengine haujui vizuri mfumo wa utawala wa nchi yako. Kukusaidia ni kuwa hao viongozi ni ngazi, wajibu na madaraka tofauti sana sivyo kama unavyofikiri wewe. Ondoa hizo fikra, delete kabisa.
== Swala la kuhusu ufisadi ni dhana pana ila rahisi sana kudili nayo. Hili ni swala gumu sana, kama wewe ni mtu unaesombwa na fikra za watu kuhusu hii dhana ya ufisadi basi sio rahisi kuelewa dhana nzima ya ufisadi. Ufisadi unaanzia kwenye mifumo (system) ya utendaji serikalini na si mahala pengine. Kukabiliana na ufisadi maana yake ni kukabiliana na utendaji wa kimazoea (business as usual) na kupambana na utendaji wa kizembe. Hapo ndipo utakapokuwa umeanza vizuri kupambana na ufisadi kwa vitendo.
Usifikiri ufisadi ni ishu ya kuwasha na kuzima kibatari. Sio hivyo. Mafisadi sio mbumbu kiasi unachofikiri wewe. Wanatumia weakness ya mfumo kufanya ufisadi. Ufisadi unaasisiwa na mfumo uliopo. Kwa Lowassa kuzungumzia bayana ubaya wa mfumo wa chama chake ni kujikosesha mwenyewe bendera ya chama chake kupeperusha kwenye mbio za kugombea urais, isipokuwa anachotakiwa kufanya ni kuukabili utendaji mbovu wa serikali kwa kuanza kuwakabili watendaji wenyewe. Na kwa hili ndipo ninapomwona Lowassa is very brave. NA NDIO MAANA NASEMA KAMA UNAULIZA SWALI GUMU HAKIKISHA KUWA UNA UWEZO WA KUELEWA MAJIBU MAGUMU PIA.
== Lowassa amekuwa waziri mkuu kwa muda mfupi zaidi kuliko waziri mkuu yeyote hapa Tanzania. Kwa kipindi hicho kisichozidi miaka miwili aliweza walau kuonyesha ni Tanzania ipi tunayoitaka. Kukaa madarakani kwa miaka michache kiasi kile na kuthubutu kwa vitendo kujaribu kung'oa mizizi ya ufisadi kunamaanisha kuwa labda huko tuendako kama angeendelea kuwa waziri mkuu tungekuwa tunasikia leo kesi zizizo na idadi za kashfa ya ufisadi. Lakini kwa kutambua na kuheshimu dhana nzima ya uwajibika alijiuzulu na hapo ikawa ndio mwisho wa harakati zake za kupambana na ufisadi.
Mzee naona unachanganya dhana mbili tofauti kabisa "Kufanya kazi kwa Mazoea/Uzembe" na "Ufisadi"...
Bado unazunguka zunguka tu,bado unazungumzia yeye kuwawajibisha watendaji wadogo kama sisimizi kwa utendaji wa uzembe na sio ufisadi mkuu...Mkuu wa wilaya anatofauti gani na mwenyekiti wa kata?..Bado hakuwahi gusa ufisadi,na usilete mambo ya system hapa,amepambana na system gani par se?Yeye ni carrier ccm politician,kakulia humo humo....
Nidhibitishie kashika wezi wangapi wa ufisadi?Nipe idadi na kwenye hiyo idadi taja jina moja na kiasi cha pesa alichofisidi!Go on ,I wait!