Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Au mnadhani ufisadi unaishaje hapa nchini kama sio kukabiliana na mifumo ilinayosababisha huo ufisadi? Na mfumo huo upo chini ya watendaji wa serikali na ndio maana Lowassa alidili nao vizuri sana!

mkuu mtumikie ------ ili uweze kupata ujira wako. hakuna wa kuweza badili mfumo wa kulindana ndani ya ccm kamwe hasa kama mtu huyo anatoka ndani ya ccm. kuna list kubwa ya majina mazito yameshindwa kuwajibishwa kwa sababu ya mfumo. je kina rostam,chenge, shabani gurumo , na wenguneo je lowasa anaweza kuwawajibisha pindi akiingia madarakani? huoni uwongo wa mchana kweupe.
 
Lowahasa ni kiboko ya mafisadi.
Akina Mwl.Nyerere na Sokoine ni porojo tu.
Hivi watu wengine mmeishiwa na chembe ya aibu.
 
Anaesema Lowassa hajawahi kupambana na ufisadi alete pua yake hapa kwenye huu uzi. Na aseme ni kiongozi yupi ndani ya ccm aliewahi kuelewa vizuri dhana hii ya ufisadi na kuanza kuikabili kama sio Lowassa.

Mara nyingine mkiuliza maswali magumu muwe pia una uwezo wa kuelewa majibu magumu.

mkuu mbona yeye katuhumiwa kwa ufisadi lakini bado hajajisafisha? mbona muda wote anaungwa mkono na mafisadi na hajawahi kuwatimua? usidhani watanzania wote tunatumia tumbo kufikiri.
 
Lowasa alipokuwa waziri mkuu alifanya fukuza fukuza sio kwa ajili ya kuondoa mafisadi bali kwa ajili ya kuunda tim ya mafisadi wataomlinda na kukuza ufisadi
Bila aibu kama hukuwa kwenye tim yake atakuondoa na kumuweka mtu wake.
Ni rekodi mbaya sana kwa kiobgozi wa karne hii kuwa na mtu mbaguzi na mlafi kama Lowasa.
 
Hivi ...ufisadi upi huyu mzee wa richmond alio pambana nao ??huyu angalia mafisadi wote ..ndo wanao mzunguka ....Nakumbuka ile list of shame alikuwepo alio toa Dr .Slaa pale mwembeyanga...mbona hakuenda mahakaman...huyu jamaa ni mchafu sana..hata kwa brush la chuma hatakati kabisa....mteteen ..ila najua...watanzania wanamjua vizur sana...na mkitoa hela lazima wazile kwan wanarudisha...mlicho waibia...Angalia nyie team lowasa nan msafi ?

mkuu hao wanampigania ili mkono huende kinywani. hivilowasa amewahi jisafisha? je hivi lowasa akiingia madarakani hivi anaweza washtaki kina chenge?
 
Kinachoniumiza huyu mtu kushindwa kutekeleza ahadi yake ya kuzungumzia suala la Richmond Arusha kama alivyowaahidi waandishi pale Dodoma. Tutamwaminije kwa kushindwa kwenye kadude kadogo namna hiyo? Huyu mtu si mkweli anatumia fedha nyingi kununua watu...huo ni ufisidi. Ikulu hapaendwi kwa mtindo huo...aache kununua watu...kwenye dini kanunua kila kanisa
 
hakukuwa kabisa na haja yoyote ya kujisharirisha na majibu haya.

hivi kuna waziri mkuu zaidi ya marehemu sokoine? LOWASSA NI DHAIFU, LOWASSA NI BUBU. HAWEZI KUKEMEA UFISADI KWA KUWA YEYE NDIYE FISADI MKUU NA ANAZUNGUKWA NA MAFISADI TUPU KWENYE TIMU YAKE.

pesa zimewapofusha macho sokoine alikuwa naongea na kutenda huku anaishi kwa kile akisemacho sio hawa waigizaji wakimbilia ikulu mwenyekiti wao alituambia tuwaogope kama ukoma
 
Lowassa ndio mpambanaji pekee anayeweza kupambana na ufisadi kwa vitendo na sio kwa ngonjera na dhana eti tukimchague yule eti masikini mwenzetu ataweza. Acheni ushabiki kuweni realistic. We trust in Lowassa. All the best MH Lowassa

lowasa hawezi kupambana na ufisadi kwamatendo hawezi. ni lowasa huyuhuyu anayelipwa kiinua mgongo kwa kuwa waziri mkuu mstaafu ilhali hakustaafu bali alijiuzulu. natamani watokee waandishi makini wamuulize juu ya swali hili...
 
Watanzania wenzetu sijui nani katuloga. Mbona tunasahau mapema sana kiasi hiki. Hivi leo tumesahau kuwa chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini ni mfumo uliopo serikalini?

Swali dogo naomba kuuliza:

Ni waziri mkuu gani mwenye rekodi ya kipekee ya kuwa mkali zaidi tena kwa vitendo kwa watendaji wa serikali? Sio Lowassa huyu huyu aliekaa madarakani kama mtendaji mkuu wa serikali kwa muda mchache zaidi, na ndie huyu aliweka rekodi ya kuwa mkali zaidi kwa watendaji wa serikali wanaopenda kufanya kazi kwa mazoea?

Ni waziri mkuu yupi aliekuwa na uwezo wa kumwajibisha mkuu wa wilaya on the spot? Halafu leo mnasema Lowassa hajawahi kupambana na ufisadi!

Kitendo kile cha Lowassa kinaonyesha dhahiri kuwa ni kiongozi anaepambana na system nzima ambayo ndio chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini. Kwa maneno mengine Lowassa anapambana na chanzo cha ufisadi ambao ni mfumo wa utendaji wa serikali. Lowassa kawawajibisha watendaji kadhaa wa serikali kwa kipindi kifupi cha madaraka yake. Hii ni kuonyesha kuwa anakabiliana na mfumo mbaya uliopo serikalini kiasi cha kuasisi kile kinachoitwa ufisadi.

Sitaki kuamini kuwa watanzania tunapenda maneno matupu yanayoendelea kusemwa na viongozi wengi kuhusu ufisadi ilhali ufisadi unaasisiwa na ulegelege uliopo kwenye mifumo ya utendaji wa serikali. Hawa wengine wanaongea kuhusu ufisadi wamechukua hatua gani kukabiliana na ufisadi? Leo hii kuna baadhi ya watanzania ambao kuongea tu bila vitendo kunatosha kuwaridhisha. Jamani maneno bila matendo hakufai kitu.

Lowassa anaelewa vizuri sana chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini ni mifumo ya kiserikali. Na ndio maana muda mchache aliokaa madarakani kama waziri mkuu alianza kudili perpendicularly na mifumo hiyo kwa kuwawajibishwa wale waliopewa dhamani kwenye utumishi wa umma, ambao kwapo ndio mianya ya ufisadi.

HAKUNA NAMNA YA KUWEZA KUDHIBITI UFISADI NCHI HII ZAIDI YA KUKABILIANA NA MFUMO WA UTENDAJI ULIOPO SERIKALINI, JAMBO AMBALO LOWASSA TAYARI ALIANZA KULITEKELEZA!

Lowassa ana upeo mkubwa sana, na nchi anaifahamu vizuri sana ndani nje! Ni mtendaji sio muimba taarabu!

KWA WATIA NIA WOTE HAKUNA ALIYEWAHI KUPAMBANA NA UFISADI KWA MATENDO KAMA LOWASSA. KILA MTANZANIA NI SHAHIDI.

Leteni hoja nyingine sio hii ya Lowassa ya kupambana na ufisadi maana ameshapambana nao kwa matendo. Anajua chanzo kikuu cha ufisadi na ndo hapo hapo alipokomalia!


Unfortunately au kwa makusudi tu hutaki kumuelewa mtoa mada. kuwawajibisha watendaji wa level ya dagaa si aina ya ufisadi anaouizungumzia mtoa mada na watanzania wengi. Hapa kinachoongelewa ni mapapa ya ufisadi, majoka yenye makengeza, wachota fedha ziosizo zao kutoka BoT kwa maboksi usiku, wanaopewa mazabuni ya kifisadi n.k.

Hawa siyo ma-DC au watendaji wataokuwa wakifokewa na EL wenu majukwaani akiwa ziarani iwapo atakuwa presidaa.

Tafadhali msilirahisishe kiasi hicho suala la ufisadi. Kuna mchangiaji mmoja hapo juu kasema kuna mafisadi wanaojulikana sasa hivi wanamzunguka EL katika harakati zake. nilimuona nyoka wa makengeza katika mmoja wa mkusanyiko wake. Akina Karamagi na wengine wamerudi kwa kasi. Hawa wote ni mafisadi tu, hawawezi kumshauri EL kwa mema isipokuwa kutaka kuwaibia Watanzania. Mark my words!
 
Watanzania hatudanganyiki. Lowasa hawezi kupambana na ufisadi ilhali marafiki zake wanaomuingiza Ikulu ni mafisadi wa kutupwa. Mwangalie Reginald Mengi (Fisadi Nyangumi), Rostam Aziz (fisadi Papa), Nazir Karamagi, Andrew Chenge na wengineo wengi. Lowasa asitufanye Watanzania ni wajinga. Hii karata ya ufisadi hawezi kuicheza hata iweje

mkuu lowasa hasafishiki kamwe. pamoja na kutuma misukule yake humu.
 
TeamLowassa

Mimi mtanisamehe tu,kula yangu ataipata nje ya ccm lakini ndani ya gari lile lile ambalo kwa miaka 50 halina hata dalili ya kufika ubungo stendi kuu,kwangu ni big NO.

Sikae au kuwa na shaka na utendaji wake,shida ni chombo cha usafiri anachutumia hakuna anaetaka kiendelee kutumika tena kubeba watu,kimezeeka toka enzi za munisi mwimbaji wa injiri.

Kama ccm imeonekana kuzeeka tangu miaka ya 90,na lowasa akiwa mmoja ya wanachama wake.akuwahi kisikika kokote mpaka alipokua wazari mkuu,ndo utendaji kazi wake ukaanza kuonekana.

Kwa kiswahili kingine hakua na uchungu na nchi yake cz ameona maovu mengi na akawa kimya kwa sababu ya mfumo wa mbovu wa ccm.

Watanzania tunataka kubadilisha chama na sio mwanachama kutoka chama kilekile kilichoshindwa miaka 50.NI BASI LILE LILE MADREVA WENGI.......WHY TUSITUMIE BASI JIPYA?
 
Last edited by a moderator:
Kinachoniumiza huyu mtu kushindwa kutekeleza ahadi yake ya kuzungumzia suala la Richmond Arusha kama alivyowaahidi waandishi pale Dodoma. Tutamwaminije kwa kushindwa kwenye kadude kadogo namna hiyo? Huyu mtu si mkweli anatumia fedha nyingi kununua watu...huo ni ufisidi. Ikulu hapaendwi kwa mtindo huo...aache kununua watu...kwenye dini kanunua kila kanisa

haa haa mkuu huyo jamaa anajivunia noti. kununua watu ni kawaida yake amenunua masheikh,wachungaji na hata maaskofu.pia kanunua wajumbe wa vikao vya chama chake yaani NEC na hata mkutano mkuu...
 
Au mnadhani ufisadi unaishaje hapa nchini kama sio kukabiliana na mifumo ilinayosababisha huo ufisadi? Na mfumo huo upo chini ya watendaji wa serikali na ndio maana Lowassa alidili nao vizuri sana!
Ninani aliyeiunda mifumo hiyo kama sio serikali legelege ya CCM? unataka kutofautisha Lowasa ambaye hajawahi kufanya kazi mahali pengine popote nje ya CCM na mifumo wa rushwa na ufisadi ya serikali za CCM?
 
lowasa hawezi kupambana na ufisadi kwamatendo hawezi. ni lowasa huyuhuyu anayelipwa kiinua mgongo kwa kuwa waziri mkuu mstaafu ilhali hakustaafu bali alijiuzulu. natamani watokee waandishi makini wamuulize juu ya swali hili...

Hii ni sehemu ya uozo ambao lazima uondolewe. I'm sory kwa uovu huu hata kikwete hayuko salama. Mtu ambaye genge lake wanamsifia eti ni tajiri kumbe anapokea malipo haram ya waziri mkuu mstaafu wakati aling'olewa na kashfa chafu ya ufisadi wa Richmond?? Kama ni kweli hat a hizi ngonjera za kuwa ni tajiri zitakuwa uongo. Hizo fedha anazogawa kumbe ni fedha haram tu. Tajiri gani anayelipwa malipo asiyostahili kutoka kwa hazina ya watanzania maskini. Nimechoshwa zaidi.
 
Mimi mtanisamehe tu,kula yangu ataipata nje ya ccm lakini ndani ya gari lile lile ambalo kwa miaka 50 halina hata dalili ya kufika ubungo stendi kuu,kwangu ni big NO.Sikae au kuwa na shaka na utendaji wake,shida ni chombo cha usafiri anachutumia hakuna anaetaka kiendelee kutumika tena kubeba watu,kimezeeka toka enzi za munisi mwimbaji wa injiri.Kama ccm imeonekana kuzeeka tangu miaka ya 90,na lowasa akiwa mmoja ya wanachama wake.akuwahi kisikika kokote mpaka alipokua wazari mkuu,ndo utendaji kazi wake ukaanza kuonekana.Kwa kiswahili kingine hakua na uchungu na nchi yake cz ameona maovu mengi na akawa kimya kwa sababu ya mfumo wa mbovu wa ccm.Watanzania tunataka kubadilisha chama na sio mwanachama kutoka chama kilekile kilichoshindwa miaka 50.NI BASI LILE LILE MADREVA WENGI.......WHY TUSITUMIE BASI JIPYA?

mkuu huo ndo ukweli wenyewe..
 
Hii ni sehemu ya uozo ambao lazima uondolewe. I'm sory kwa uovu huu hata kikwete hayuko salama. Mtu ambaye genge lake wanamsifia eti ni tajiri kumbe anapokea malipo haram ya waziri mkuu mstaafu wakati aling'olewa na kashfa chafu ya ufisadi wa Richmond?? Kama ni kweli hat a hizi ngonjera za kuwa ni tajiri zitakuwa uongo. Hizo fedha anazogawa kumbe ni fedha haram tu. Tajiri gani anayelipwa malipo asiyostahili kutoka kwa hazina ya watanzania maskini. Nimechoshwa zaidi.

mkuu hii nchi yetu imeoza inahitaji kusafishwa. tabaka kubwa la viongozi wa juu ni waharibifu wa mali za umma. nashangaa wabunge wetu wanashindwa kuhoji mambo ya msingi kama hayo. hakuna aliyemsafi ndani ya ccm kamwe.
 
Anaesema Lowassa hajawahi kupambana na ufisadi alete pua yake hapa kwenye huu uzi. Na aseme ni kiongozi yupi ndani ya ccm aliewahi kuelewa vizuri dhana hii ya ufisadi na kuanza kuikabili kama sio Lowassa.

Mara nyingine mkiuliza maswali magumu muwe pia una uwezo wa kuelewa majibu magumu.

Nakubali kweli kuwa Lowasa alishawahi kupambana na ufisadi haswa ufisadi wa kuuza mnazi mmoja na suala la city water. Lakini hajawahi hata robo kufikia rekodi iliyowekwa na Sokoine ambaye naye alikaa madarakani kwa kipindi kifupi sana.

Pili, Lowasa wakati mwingine anafanya maamuzi kwa kukurupuka ndiyo maana watendaji walimdharau na sii kumuogopa kama wengi wanavyodhani maana mambo mengi anachimba mikwara bila kutafuta ukweli kama alivyoumbuliwa na yule mkuu wa wilaya kama sikosei ya Nyamagana. Pia issue ya richmond wakati walioko chini yake wanakubali kuwa utaratibu haukufuatwa, yeye anang'ang'ania kuwa tatizo ni uwaziri mkuu. Msabaha na Karamagi waliokuwa kwenye sekta hiyo walikubali kuwa richmond ni tatizo. Ikumbukwe kuwa Ni Serikali ililiomba bunge mara ya kwanza kuwa hiyo issue ifanyiwe uchunguzi na vyombo vya serikali. Serikali chini ya Lowasa ikaenda kujisafisha badala ya kuwabaini waliosababisha matatizo.
 
Back
Top Bottom