Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Aliyejiuzuru Uwaziri Mkuu kwa kashfa za Richmond alizotuhumiwa bungeni Edward Lowasa, ametengeneza mtandao mkubwa kupenya ateuliwa kuwa mgombea wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kupitia CCM.

Kimsingi Lowasa ana jina kubwa lakini hana sifa au sera anazoeleza wazi atakachofanya akiwa rais kama ilivyo kwa wagombea wengi wanaowania nafasi hiyo kupitia CCM kutotuhakikishia Watanzania watabadilishaje kile tunacholalamikia serikali inayoongozwa na CCM kufumbia macho urasimu na ufisadi.
Sera tunazozisikia ni kutoka upinzani, labda kwa vile wako jukwaani wakiwaangalia wachezaji uwanjani wanaona makosa yanayofanyika kuliko Lowasa aliyoko uwanjani akiwa mchezaji hawezi kuona makosa wanayoyafanya.

Lowasa hana sera ni kujipitishapitisha na kuhudhuria mikusanyika Tanzania ya leo si ile ya kuchagua umaarufu wa mtu au umaarufu wa kujulikana, tunahitaji sera. Tanzania ya leo si ya Kitudumu Chama Cha Mapinduzi, Zidumu Fikra Sahihi Za mwenyekiti wa CCM, kila mgombea uraisi anayepitishwa na CCM kujihakikishia kuwa Rais wa Tanzania.

Tanzania ya leo hatuhitaji kujionyesha kwa kupitapita kila sehemu na kuhudhuria kila tamasha na matukio ili wapiga kura wakuone, tunahitaji uuzaji wa sera utaibadilishaje Tanzania ya leo tuwe na Tanzania tuioteayo.

Tuanataka uonyesha mapungufu kiuongozi ndani ya CCM utayashughulikiaje.Utuonyeshe kwa nini hukuweza kushughulikia matatizo hayo ulipokuwa waziri mkuu, mbunge kamati ya bunge na uongozi katika ngazi mbalimbali chamani.

Kama hayo hukuweza kuyashughulikiwa upokuwa Waziri Mkuu, Waziri, Mbunge, mwenyekiti kamati ya bunge, ngazi mbalimbali za uongozi ndani ya Chama na kuhitimishwa kwa kashfa ya Richmond hadi ukajiuzuru, utawezaji kurejesha imani kwa wananchi na kuondoa uchafu unaoendelea ndani ya serikali inayoongozwa na CCM hasa ubadhilifu wa mali ya umma?
 
Unaizungumzia Richmond pasipo kujua kiini haswa cha chimbuko lake.

Mwakipesile alichukua fomu kuutaka ubunge wa kyela..wkt huo mwakyembe naye pia alichukua..ktk kura za maoni kulitokea mtifuano mkali sana..na uhasama pia..kumbuka wkt huo Mwakipesele alikuwa mkuu wa wilaya (km sikosei) mwakyembe akashinda kura za maoni..baada ya uchaguzi mkuu..mh.Lowassa kupitia rais akamteua Mwakipesile mkuu wa mkoa wa Mbeya..ndipo Mwakyembe alipoingiwa na nyongo kwa mh.Lowassa..kwann hasimu wake kapewa cheo kikubwa..Samwel Sitta..baada ya uchaguzi alitegemea kupata uwaziri mkuu..naye akaingiwa ma nyongo..baada ya sakata la Rich kuibuka..haraka sana ikaundwa tume na Mwakyembe akapewa uenyekiti ili "amalize kazi"kabsaaa...thats why hawakumuhoji..maana walijua wakimuhoji hawatatimiza azma yao maana watapata majibu sawia..

Watu mna nyetiiiiii. Si mchezo
 
Kosa lenyewe ni kuchagua Rais aneyetoka kwenye sapoti kubwa ya aina fulani ya mtandao wenye nguvu ya pesa, kama ule wa Friends of L.

Mgombea Mtarajiwa ashasema wazi kuwa hela huwa anatoa kwa marafiki zake.

Nawahakikishieni kuwa litakuwa kosa kubwa la kujutia kumpa nchi mtu wa aina hii kwani hata yeye asipopiga hela, lakini hatakuwa na ubavu wa kuwakemea marafiki zake wenye mchango mkubwa wa yeye kuwa pale, ambao bila shaka watawekwa kwenye vyanzo vya hela na ongozi mbalimbali. Chungeni sana enyi WaTZ wenzangu, mambo mengine tufundishwe mara ngapi? Tusidanganywe na maneno yao matamu matamu kama chaguzi zilizopita.
 
Watu wamelewa pesa za lowasa mkuu sijuwi kama utaeleweka.mbaya zaidi mpaka tunaowategemea kabisa mpaka baadhi ya wabunge wamekubali tuuze nchi.ukija kwenye vyombo vya habari ndio usiseme.kilichobaki sasa ni kumuachia mungu tu.
 
Ndugai kasema tulieni bado mapema sana msiogope!!
 
Watu wanataka kuuza future yao kwa sh. Laki mbilimbili kwa fisadi mkuu.
Kataa CCM kataa fisadi mkuu.
 
Ni matusi makubwa sana kuamini kuwa watu wanamsapoti Lowassa kwa sababu wamepewa pesa. Haya matusi ni vyema mkakoma kuwatukana watanzania wenye akili zao za kupambanua uwezo wa kiongozi wanayemtaka. Watanzania wa leo si wale wa mwaka 2005. Support anayoipata Lowassa kutoka kwa wananchi si lwa sababu ya fedha, bali kwa sababu ya utendaji wake. Ifike mahali muelewe kwamba wananchi wanafahamu sakata nzima la Richmond na wahusika wakuu wa hiyo ishu na ndio maana leo hii wanamuunga mkono Lowassa.
 
Tunapojiandaa kumpeleka E.L tujue wazi tunaenda kuwaweka masikini kwenye wakati mgumu.

Team of Lowassa imejaa Matajiri na watuhumiwa wakubwa wa ufisadi hadi CCM ilitaka kuwatoa na kuwaita magamba baada ya kupiga sana.

Hapa rostam, Karamagi, Pale Mkono, na wamiliki wa migodi,

je tutegemee nini katika safari hii
1. Matajiri kukwepa kodi na masikini kulimbikizia kodi na michango ya lazima kujenga hiki na kile.

2. Ufisadi kuongezeka mara mbili, Rushwa na tenda na Zabuni za serikali kutolewa kwa upendeleo kutokana na michango wanayompatia sasa E.L

3 kila mwana tearm of lowasa kuwa na sauti na mikwala kama raisi.

4. Serikali kutelekeza wananchi na viongozi kuwa bize kugawana vitaru vya gesi, madini na kumonopolize soko la ndani.

Wafanyakazi kuli

twende na el kuelekea kwenye safar niku
 
Lowasa ameanza safari ya huzuni sasa ikulu siyo pango la mafisadi
 
Tunapojiandaa kumpeleka E.L tujue wazi tunaenda kuwaweka masikini kwenye wakati mgumu.

Team of Lowassa imejaa Matajiri na watuhumiwa wakubwa wa ufisadi hadi CCM ilitaka kuwatoa na kuwaita magamba baada ya kupiga sana.

Hapa rostam, Karamagi, Pale Mkono, na wamiliki wa migodi,

je tutegemee nini katika safari hii
1. Matajiri kukwepa kodi na masikini kulimbikizia kodi na michango ya lazima kujenga hiki na kile.

2. Ufisadi kuongezeka mara mbili, Rushwa na tenda na Zabuni za serikali kutolewa kwa upendeleo kutokana na michango wanayompatia sasa E.L

3 kila mwana tearm of lowasa kuwa na sauti na mikwala kama raisi.

4. Serikali kutelekeza wananchi na viongozi kuwa bize kugawana vitaru vya gesi, madini na kumonopolize soko la ndani.

Wafanyakazi kuli

twende na el kuelekea kwenye safar niku

Nani alikwambbia EL atakuwa Rais? ondoa hofu
 
Hawa Ccm wanatufanya watanzania ni vichaa
Juzi juzi tu kikwete aliwaambia watanzania "maisha bora kwa kila mwananchi"Tulivyo vilaza tukampa nchi
Tabu watu wameipitia kwenye utawala wa JK mungu pekee ndio shaidi
Sasa amekuja Lowassa "eti" Safari ya matumaini Hahahaha...Matumaini yapi..??
Tulikilemaa tukampa hii nchi tutaingia kwenye safari ya mateso na maumivu ya ajabu
Kuepuka hii hali ni kufanya jambo moja tu.
Kujiandikisha kwa wingi kwenye daftari la wapiga kura na baada ya hapo Kuipa Ukawa ridhaa ya kuitawala hii nchi
Ili waje warejeshe matumaini ya watanzania yaliyopotea mikononi mwa Ccm.
 
Back
Top Bottom