Wana JF,
Naomba tujadili kidogo kuhusu huyu mheshimiwa Edward N Lowasa anayetaka Watanzania tumpe dhamana ya kuwa Rais.
Mimi ninavyoweza kumuelezea kwa kifupi; huyu mheshimiwa ni mtu anayejali sana makundi yote ya dini lakini tatizo kubwa ambalo analo ni kuwa muumini wa ufisadi.
Kipindi chote bungeni tangu astaafu uwaziri mkuu, sijawahi kumsikia akishiriki kutoa hoja au maoni juu ya mijadala ya ufisadi bungeni au kwenye hadhara yoyote.
Tatizo kubwa kwa sasa nchini mwetu ni usimamizi mbaya wa mali ya umma, kukithiri kwa rushwa, kubebana , madawa ya kulevya, kutojali wakulima na wafugaji, kutochukua hatua kudhibiti wizi kwenye halmashauri za wilaya, miji, manispaa na jiji, huduma duni kwenye afya, elimu na maji .
Kama tunavyojua ufisadi na rushwa vimekithiri sana tanzania.Je mheshimiwa Lowasa akiwa Rais ataweza kweli kuitokemeza au ndo itaota mizizi hadi tukome kuzaliwa tanzania na kuwa masikini wakutupwa huku yeye na team Lowasa wakizidi kujineemesha? Nawaza tu.
Mungu atupe ufahamu Watanzania na atuache ushabiki kama 2005 na tufanye maamuzi sahihi kwa ajili yetu wenyewe si kuneemesha kikundi fulani.