Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Huhitaji kumsikia Lowassa akipayuka kuhusu mambo ya ufisadi;unachotakiwa kula hela ya umma halafu ukatize mbele yake uone atakachokufanya;mfano nenda jimboni kwake Monduli halaf kakwibe fedha za miradi ya maendeleo,utajuta kuzaliwa
 
Natafuta speach ya Lowassa akikemea ufisadi, na matumizi mabaya ya mali ya umma.
Natanguliza shukrani zangu za dhati. Bujibuji

Unachokitafuta ni sawa na kumtafuta Imamu (tena mwenye wake wanne) akiongoza kanisa katoliki tokea Vatican city.
 
Last edited by a moderator:
CCM watalazimisha watu wachague UKAWA, maana inaonekana chaguo lao ni kati ya Lowassa na Pinda.
 
Kwani Wapi Professor Kikwete amekemea?. Yeye Rais Mpaka akemee?. Mpe Uraisi uone mtakavyo jamba.
 
Hivi kikao cha CC ya CCM kimeamua nini kuhusu rushwa za Lowassa?
 
lAigwanani mkuu ni mla rushwa wa kuzaliwa hawez kukemea ufisadi atakataje tawi alilokalia?
 
ni vema kujua Nini maana ya Neno "Fisadi" kama linavyotumika na waswahili.Kwenye Siasa Fisadi ,ni pale mtu anapotumia Ofisi ya Umma kwa maslahi yake binafsi.

kuna tabia mbaya imezuka kwa Watanzania ya kupenda Kula maneno ya Wanasiasa haswa wakiwa pale bohari Dodoma lilipo Bunge letu tukufu,

Mtanzania ataweka kumbukumbu ya hotuba zilizoamsha hisia kwa kusheheni maneno ya kejeli na vijembe lakini hatoweka kumbukumbu ya utendaji wa Kiongozi juu ya maneno Yale Yale aliyoyasikia kwa viongozi wengine.

Mimi nawajua Viongozi waliokemea Ufisadi waziwazi lakini walipoukuta sehemu zao hawakuushughulikia zaidi tu ya kufanya reshuffle,yaani viongozi hao wanamsimamo wa wazi juu ya Ufisadi ambao kimsingi umekithiri Serikalini na maeneo yao ya kazi ila cha ajabu hawana record ya kufanya maamuzi magumu Katika hilo na kuwasimamisha kazi Hata watu wawili kwa juhudi zao binafsi

lakini pia namjua Kiongozi mwenye Record ya kuongea kidogo na kutenda sana ,Hakika hajalisha watu maneno Bali kwa matendo yake hakuishia kusema tu juu ya ufisadi Bali alionyesha nini cha kufanya kwa nafasi yake pale alipokutana nao

sasa chagua Leo Unataka speech za kukemea ufisadi ama Unataka kuona nini unatakiwa ufanye pindi unapokutana nao.
 
Nashangaa eti anataka mwizi akemee wizi. Si uchizi huu! Eti mkuu!

Lowasa, da! sijui kwanza ukitamka neno ufisadi kwake unaonekana kituko. Sikuwahi kuona akikemea bungeni, sikwahi kuona akiaddress kwenye vyombo vya habari wala sikuwahi kuona akikemea ufisadi kwenye kamati anayosimamia ya ulinzi na usalama. (Fahamu kwa kuna wabunge wengi ambao wameingia kwenye kashifa ya kula fedha za safari bila kusafiri, Kuna wabunge wanafanya fujo bungeni lakini sijawahi kusikia akitoa tamko kama mwenyekiti, kuna hatari ya vyombo vya ulinzi "kusumbua wananchi - polisi" lakini hakuna speech.

Nachojiuliza ni kwa nini kamati za Zitto zinafanya kazi inayoonekana lakini hii ya Lowasa kazi yake ni kupeleka wajumbe nje ya nchi?
 
Huhitaji kumsikia Lowassa akipayuka kuhusu mambo ya ufisadi;unachotakiwa kula hela ya umma halafu ukatize mbele yake uone atakachokufanya;mfano nenda jimboni kwake Monduli halaf kakwibe fedha za miradi ya maendeleo,utajuta kuzaliwa

Hahahahaha....nimeipenda hio!!
 
Hivi kikao cha CC ya CCM kimeamua nini kuhusu rushwa za Lowassa?


Hee!! Lowasa anatoa rushwa!!? PCCB wapo kwa ajili ya nani? ina maana akichaguliwa kuwa mkuu wa kaya ataifutilia mbali PCCB
 
Natafuta speach ya Lowassa akikemea ufisadi, na matumizi mabaya ya mali ya umma.
Natanguliza shukrani zangu za dhati. Bujibuji

mkuu, twende mbele na kurudi nyuma. kuna watu wamekuwa wazuri sana kukemea ufisadi kwenye majukwaa lakini vitendo vyao vimekuwa haviakisi wanachokihubiri asilani.

few names spring to mind but the picks of the day are BWM & JK who have been the trusted occupants of the highest office (one of them was actually christened a "mr clean"!).

tatizo si Lowasa, sote tunajua kiini cha tatizo ni nini. yes, tunajua. this is food for thought (UKAWA).

twende mbele na kurudi nyuma...
 
Last edited by a moderator:
Lowassa mnafiki fisadi papa! eti linajitetea liliamua kukaa kimya kwa maslahi ya chama chake! Utetezi wa kipuuzi kabisa.
Hatutaki Rais anayefumbia uovu utaoleteleza hasara kwa Taifa kwa sababu ya chama au mtu yeyote!
Amehusika na Richmond hana pa kuikwepa kashfa hii!
Tariffs za umeme zinatunyonga wananchi kisa alijua Richmond ni deal ila si yake! Nonsense!
 
Ameamua kujipanga kukemea hadharani wale wote wanaojihusisha na rushwa na ufisad. Amedai kuwa wanalitia aibu taifa letu.
Hiyo nimeipata kutoka kwa wapambe wa Lowassa a.k.a team Lowassa kuwa mzee wao kaamua kuja na style hiyo ya kukemea rushwa na ufisadi pengine labda inaweza kumtoa kimasomaso kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015 October.
 
Back
Top Bottom